Mkuu
Mentor, nimejikuta nikurudi kuisoma hii story kwa mara nyingine ili kujipa tafakuli kidogo juu ya maudhui yake. Hakika nimeipenda, ijapokuwa hakika hiki ni kisa cha kutunga kwa kadri ninavyoamini mimi lakini ukweli unabaki ya kwamba mambo kama hayo na hata zaidi yapo katika jamii zetu na jamii zenyewe ndio sisi wanadamu. Kumbe basi kama sio mimi, wewe basi kisa kama hiki kilishamkuta yule na huenda siku moja kinaweza kutokea kwangu ama wewe.
Sisi binadamu tumejaliwa uwezo wa kusahau mambo mazuri ama mabaya yanayotupata hapa duniani na hivyo kufanya tuzidi kusonga mbele na maisha ya wakati huo haijalishi ni magumu ama mazuri. Katika hili inabidi kwa wale tunaomwamini Mungu tuzidi kumshukuru yeye kwa huo uwezo wake anaotukilimia sisi waja wake maana vinginevyo huo mzigo tu wa mawazo ungeweza kuwa chanzo cha moja kwa moja kujongea mauti haijalishi ni mauti ya namna gani.
Nikurudi kwenye mada ya msingi, hakika inanikumbusha kuwa mimi kweli ni mkosefu, lakini je pale ninapogundua kuwa nimekosa natakiwa nifanye nini? Mkuu
Mentor pamoja na kuwa alikuwa na mtu wake
Sue (Suzana), kama alivyomtaja mwenyewe bila kuwa specific kama alikuwa mke ama mchumba ama mpenzi, lakini alipokutana na
Aneth anajikuta akiingia katika lindi la mapenzi ya ghafla huenda kutokana na urembo wa Aneth lakini pia kutokana na mazungumzo ya wawili hao. Hapo hakika ni issue ambayo huwakuta watu wengi na hasa sisi wanaume, ila tu huwa tunatofautiana tu jinsi ya ku take action baada ya tukio la kwanza. Kuna wengine hutafakari sana na mwisho wa siku huishia kughairi, lakini wengine hawajipi muda wa tafakari, yeye anachofanya ni kutenda kadri ya mapenzi ya mwili. Nadhani hiki ndicho alichofanya mtoa mada. Kumbe basi kuna haja ya kujipa tafakari ili moyo uweze kukusaidia katika maamuzi, nadhani kwa kufanya hivyo huenda nafasi ya
Sue wake ingeza kuchukuwa nafasi na kuachana na mrembo
Aneth.
Lakini ndio hivyo tena mtoa mada ametenda kadri ya hitaji la mwili, ndio hicho hutukuta wengi lakini anajikuta tena akitumia vipimo vya macho (Visual inspection) kuamua kuwa mrembo
Anethhawezi kuwa na ugonjwa wowote ambao ni hatari kwa maisha ya mtoa mada hasa ugonjwa usio na kinga wala tiba wa UKIMWI. Hakika hili nalo ni kosa la pili ambalo sisi binadamu tumekuwa tukilifanya tena mara nyingi na tukiwa na akili timamu. Kumbe basi mwandisi/mtoa mada anatuasa tubadilike, maana tunamuona mwishoni baada ya kusikia habari ambazo ziko kinyume na alivyokuwa akiamini anamua kutafuta njia mbadala ili aweze kupima, jambo ambala hakufanikiwa pia kutokana na upande wa pili kuwa na hakika pasipo shaka juu ya maambukizi ya ugojwa wa UKIMWI.
Aidha pia katika kutekeleza tendo la ngono mtoa mada atuonesha ni kwa jinsi gani walivyokuwa makini kutumia kinga (Kondomu) ili kuepuka utungaji wa mimba tu. Hakika hapa mtoa mada wamevaa uhusika unaoingaza jamii pana yetu sisi. Hivi ndivyo tulivyo katika maisha yetu ya kila siku ndani na nje ya familia zetu. Kumbe basi mtoa mada hapa napo anatupa tahadhari ili tuweze kubadilika. Anatutahadharisha hayo yote kwa lengo la kutuokoa kutokana na majanga mbalimbali ya hii dunia maana kwake yeye anasema yuko
on the way to Heaven on earth, kumbe yeye already yuko
Ablessed, na hivyo kazi ina[MENTION]BAK[/MENTION] kwetu.
Aidha pia pamoja na hayo makosa yote ambayo binadamu yoyote bila kujali jinsia yake anaweza kujikuta ameyatenda hapa duniani kama inavyojionesha kwa mtoa mada, bado anatuasa kujipa tafakuri na kutokata tamaa, maana mwanzoni yeye alijua tayari naye ni mwathirika, lakini pasipo hata kuchukua hatua ya kupata vipimo sahihi, na hivyo kujikuta katika lindi la mawazo, mara
SUE wake, kiwanja nk, jambo linalomfanya kupungua uzito kwa kasi ya ajabu. Kumbe basi anatuasa tuchukue hatua ya kufanya vipimo sahihi na kuepukana na vipimo vya macho.
Lakini mwisho ya yote mtoa mada anatuasa tuwe waaminifu kwa wenza wetu ili kuepuka matatitizo kama hayo na kwa kufanya hivyo itampendeza Mungu na katika yeye tutapata kibali.
CC
ladyfurahia,
Paloma,
Himidini,
Ablessed, [MENTION]Chritine Ibrahimu[/MENTION] na wengine wote.