Mangi flani hivi
JF-Expert Member
- Jan 2, 2016
- 2,026
- 3,100
- Thread starter
- #21
Mzigo upo unadondokq tu... Haukati hauongezeki.
Acheni mvua itiririke ili mwaka kesho tusipate shida ya mahitaji ya vyakula, kwa wale waishio mabondeni ni lazima wapate majanga kwani kila mara huambiwa wahame lakini hawaelewi.Salam wakuu,
Mpaka naandika bandiko hili Muda huu, mvua kali sana bado inashuka eneo la Tanga mjini na vijana vyake. Ni mvua ambayo Kama ikiendelea kupiga namna hii non-stop basi Kesho tutegemee mengine kwenye front pages. Haijakata tangu saa9 usiku wa kuamkia leo na hapa bado inapiga.
Maafa (ambayo hayadhibitishwa na mamlaka rasmi):
1. Mtu mmoja amoteza maisha eneo la kange baada ya kusombwa na maji
2. Nyumba tatu zimebomoka
3. Barabara ya makorora imafungwa na mamlaka ya jiji kuepusha maafa. (Hii imedhibitishwa)
Waungwana sala zenu zinahitajika kwa wana Tanga. Hii mvua tunayoiomba tunaomba iwe na kiasi...
Amen.
UPDATES:
Barabara ya kuelekea kasera imefungwa na hivyo waliopo eneo Hilo ni Kama wapo kisiwani. Ninavyoandika hapa, wanamaji na polisi wamefika kuwapa pole wahanga ambao wapo upande wa pili wa barabara, (walikuwa wanatoka mjini kwenda kasera). Na wamekwama. Kwa hesabu ya haraka hawapungui watu Mia mbili. Ni janga
Wakazi wa Sahare beach wako mbioni kufutwa kwenye ramani ya tanga ikiwa mvua hii itapiga kwa masaa mengine manne mfululizo kuanzia sasa.
Maeneo korofi Kama kwanjeka na mikanjuni Kesho watahitaji usafiri mbadala kutoka makwao. Sala zenu waungwana.
Umeme umekatika.... Kwa Hali ilivyo Nadhani kuna nguzo itakuwa imeanguka. Tusubiri tamko.
Acheni mvua itiririke ili mwaka kesho tusipate shida ya mahitaji ya vyakula, kwa wale waishio mabondeni ni lazima wapate majanga kwani kila mara huambiwa wahame lakini hawaelewi.
Tena ulivyouliza ndo imeongezeka Mara mbili yake.Wakuu poleni,bado inanyesha?
Mkuu upo kipande gani....??? Sahare mpaka usagara hakuna mawasiliano ya barabara.Dah! Yaani kumaliza kupost tu Mzigo umerudi
Mkuu nilisema ikipiga masaa manne non stop hapo sahare beach lazima kueleweke. Polemic asee.Tumeshakua isolated.. Ni kama kisiwa..hii Barbara ya Tanga beach haipitiki..naona baadhi ya watu wakihaha kuhamisha vitu..nyumba zimezingirwa na maji..nashuhudia Jirani yangu hapa akitoa msaada wa malazi kwa mama mmoja..bado ni usiku mwingi tuendelee kuomba ipungue.
Nipo Chumbageni nduguMkuu upo kipande gani....??? Sahare mpaka usagara hakuna mawasiliano ya barabara.
Chumvini waombe Mungu bahari isitapike.... Maana watakutana na uono chumbani.Vip maeneo ya chumvini hali ikoje?
Barabara ya kuelekea kasera imefungwa na hivyo waliopo eneo Hilo ni Kama wapo kisiwani. Ninavyoandika hapa, wanamaji na polisi wamefika kuwapa pole wahanga ambao wapo upande wa pili wa barabara,
Waambieni viongozi wa dini waombe mungu mvua iache.kama walivyoomba mvua inyeshe.Kaka Niko donge mwisho hapa mpaka najiuliza hii ni mvua ya aina gani inagonga non stop..mbaya zaidi bora ingekua ndogo ni mvua kubwa sana..jamani mtuombee
Tunawaombea sanaKaka Niko donge mwisho hapa mpaka najiuliza hii ni mvua ya aina gani inagonga non stop..mbaya zaidi bora ingekua ndogo ni mvua kubwa sana..jamani mtuombee
Tuombe Mungu aepushe hayo. itabidi asubuhi niwapigie sim jamaa niwajulie haliChumvini waombe Mungu bahari isitapike.... Maana watakutana na uono chumbani.
Jamani watu wa Tanga poleni sana. Hapo ndio nyumbani nilipozaliwa na kukulia.Vipi maji hayajaa Amboni kwenye mapango? Hii itazuia wale wanaojificha huko au?