Nimekuwa natembelea maeneo mbalimbali katika nch yetu na ukweli nchi iko kwenye mgao mkali wa umeme, mfano mkoani Morogoro maeneo ya chuo kikuu cha Jordan umeme unarudi jioni, jijini Dar hali ni hiyo hiyo.
Mgao huu unatokana na ukata mkubwa unaolikumba shirika la Tanesco, wameshindwa kabisa kununua mafuta ya kutosha kulisha mitambo ya kukodi.
Jambo la ajabu usalama wa taifa wamekuwa wakizunguka mikoani na kuwachukua wafanyakazi wa TANESCO wale walioko kwenye manejimenti kwa kuwalisha viapo kuwa wasitoe siri za mgao, kwa upande wa kilimanajro viapo hivyo vilifanyika katika hostel inayomilikiwa na kkt iitwayo uhuru hostel, na hapa dsm maeneo ya ikulu.
Naomba wabunge mwambieni Prof. Muhongo aache unafiki na uongo uliokubuhu kwani ukweli ni kuwa nchi iko gizani, na yeye yuko busy kudanganya kuwa hakuna mgao na kutetea wezi wa escrow.