MGOGOHALISI
JF-Expert Member
- Apr 16, 2011
- 4,510
- 6,607
Kama nilivyoandika hapo juu ni bora waziri wa nishati ukatengue kauli ya kuunganisha umeme kwa 27,000. Maana wanachi wengi hasa wenye umbali wa kuhitaji nguzo moja ama mbili sasa hivi hawahudumiwi kabisa. Ukitaka kupata control number unaambiwa ulipie angalau laki moja kwa kila nguzo na hiyo laki moja kwa kila nguzo haiingii serikalini.
Bei elekezi ya 27,000 imegeuka mwanya mpya wa kuomba rushwa kwenye ofisi za Tanesco. Hata nguzo walizosambaza mitaani wameziacha chini zinaliwa na mchwa mara baada ya kupewa bei hiyo elekezi.
Nashauri waziri wa nishati utembelee kule Dodoma mathalani maeneo ya Chidachi, Makulu, Mkonze, Miganga n.k. Kule utakuta nyumba nyingi zimekamilika lakini hazijaunganishwa na umeme wa Tanesco. Wenye kuweza wameamua kuweka Solar ili maisha yaendelee.
Bei elekezi ya 27,000 imegeuka mwanya mpya wa kuomba rushwa kwenye ofisi za Tanesco. Hata nguzo walizosambaza mitaani wameziacha chini zinaliwa na mchwa mara baada ya kupewa bei hiyo elekezi.
Nashauri waziri wa nishati utembelee kule Dodoma mathalani maeneo ya Chidachi, Makulu, Mkonze, Miganga n.k. Kule utakuta nyumba nyingi zimekamilika lakini hazijaunganishwa na umeme wa Tanesco. Wenye kuweza wameamua kuweka Solar ili maisha yaendelee.