TANESCO: Rationing is back!

TANESCO: Rationing is back!

Nadhani vitu ambavyo vimeanziwa na Herufi "T" vina laana/matatizo maana kadri siku zinavyokwenda majina ya T yamekuwa kero.Mfano TIGO na TANESCO bila kumsahau baba mwenye nyumba wao TANZANIA.Tuungane kuiondoa herufi T kwenye ALPHABET
 
Kama kweli Mkataba wa William Mhando unasema kwamba atapatiwa umeme wa GENERATOR na sio kutoka kwenye GRID ya TAIFA. Basi nchi hii tuna matatizo makubwa and solution of power rationing in this country is a far fetched idea!

Usemi wa CHARITY BEGINS AT HOME has no any meaning to Tanzanians! No wonder waziri wa ELIMU anapeleka mtoto wake OPRIVATE school, Waziri wa viwanda biashara na masoko, fenicha katika ofisa yake zote ni za kutoka Germany, Waziri wa Kilimo hajawahi kunywa/kununua chai, kahawa, sukari ya Tanzania. the list goes on
 
Tanesco itangaze muflisi ufungwe halafu tujipange upya.

Nchi ina gas kibao lakini mitambo ya kuzalisha umeme mingi inatumia mafuta.

Nilitegemea mitambo ya kuzalisha umeme nchi nzima ingefungwa huko huko Songo songo.
 
Nadhani vitu ambavyo vimeanziwa na Herufi "T" vina matatizo maana kadri siku zinavyokwenda majina ya T yamekuwa kero.Mfano TIGO na TANESCO bila kumsahau baba mwenye nyumba wao TANZANIA.Tuungane kuiondoa herufi T kwenye ALPHABET
 
Generator halitoki hapo mtaniambia, ni siasa tu hapo zinachezwa! Kama kawaida solution ya matatizo mengi ya nchi yetu tunadhani tutayamaliza kwa kuendekeza siasa kila sehemu.
 
Mkuu mimi naamini nchi hii bado ina watu wazuri wanaoweza kuongoza. Pia nafahamu kwamba huko TANESCO kuna viongozi wazuri tu tatizo ni siasa mkuu. Hivi kwa nini Dr. Idrissa aliondoka? Jibu ni kuingiliwa kisiasa. TANESCO ni shamba la bibi kila mtu anataka aingilie. Wanauziwa umeme bei aghari hawatengenezi faida! Watu wanakula kwenye mafuta ya kuendeshea mitambo ya IPTL! Mambo ni mengi.

well said mkuu kimbunga unajua key issue hapa ni moja HAWA JAMAA HAWA THE SO CALLED MAFISADI WAKALAMU kwenye energy sector huku wameona kuna loophole tena kwenye PROCUREMENT ya mitambo na vitendea kazi vya nishati ya umeme .... NISHATI YA UMEME NI DILI KUBWA SANA NA KWA KUTAMBUA HILO WENZETU WAMEONA MWANYA HAPO WANAKULA TU BILA HURUMA ... WANAJUA TENA WANAJUA YA KWAMBA EMERGENCY BACK UP POWER - HIYO DHARURA DHARURA HIYO SIO SULUHU NA KIUHALISIA UWEZI KUENDESHA UCHUMI KWA DHARURA UMEME NI MOYO WA UCHUMI HALAFU KILA SIKU UMEME NI DHARURA KWELI... ISSUE KUBWA HAPA NI KWAMBA WANAJUA WANAPATA SANA PESA KWA HIZI DHARURA .....NDIO MAANA PROJECT KUBWA ZA UMEME ZIMEBAKI MAKARATASINI TU ....
SULUHISHO LA KUDUMU SIO KUISAKAMA TANESCO MARA SIJUI ALETWE COMPETITOR MARA MANAGEMENT MBOVU
SULULU NI KUWA NA VIPAUMBELE TUKUBALI KWA UMEME NI MOYO WA UCHUMI TUWEKEZE KWENYE MIRADI MIKUBWA YA UMEME ... WAKATI MWINGINE TUACHANE NA POROJO NA KUDANGANYA WATU HAPA
 
Nimekuwa nikifuatilia yaliyojiri kikao cha kamati ya nishati na tanesco. Mhe Zitto alithubutu kutoa agizo standby generator liondolewe nyumbani kwa wiliam mhando ili naye ajue adha ya umeme.naungana nae mia kwa mia viongozi wetu wamejifanya miungu watu hawajui hata tone la uchungu wa matatizo yanayowakabili watu walio chini yao.

Pia mimi nashauri haya:

1. Waziri wa elimu naye aondolewe kwenye pay roll kama miezi miwili hivi ili ajue adha ya walimu wanaoondolewa kwenye pay roll kiuzembe halafu wanapata usumbufu mkubwa kurudishwa
2. Ikulu wakatiwe maji ili wajue adha ya maji mawilayani kama Bariadi, Meatu nk

Katika hili ninaipongeza kamati ya POAC, kwani viongozi wengi wa serikali na mashirika ya umma wamejisahau sana kiasi kwamba matatizo ya wananchi hayawahusu. Nadhani huu uwe ni mwanzo tu na kamati nyengine nazo ziige mfano huu kwa wale wote wasiowajibika ipasavyo.

Katika muktadha huo huo nadhani POAC wasishie kwa mkurugenzi mkuu pekee, bali waende mbele zaidi na kwa wakurugenzi wengine kama wa Thermo Generation, Hydro generation, CFO, Human Resources, Transmission e.t.c

mhando tanesco2.jpg

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), William Mhando,


"Mfano pale City Center (katikati ya jiji), tulikuwa na transfoma mbili zote zimetumika zaidi ya miaka 30, Februari mwaka huu zimeharibika, tumeagiza kutoka Uturuki na sasa zimefika Dubai, tatizo ni miundombinu imechakaa," alisema.

Kama wangekuwa makini katika kutenda kazi zao wangetambua kwamba hizo transformer za city centre zimeshachoka na kununua nyengine mapema kwa ajili ya kufanya replacement. Kusubiri hadi zimeshindwa kufanya kazi na sasa imepelekea wananchi kuingia gizani ni dalili za uzembe na kutokuwajibika, na kimsingi kama ingewezekana wao(Tanesco) walitakiwa kuingizwa kwenye mgao hadi transformer zitakapokuwa zimefungwa na mgao umekwisha.
 
tukiacha siasa tukija kwenye sheria, kamati ya bunge inavunja sheria. Kama umeme wa jenereta ni sehemu ya stahili kwenye mkataba wa ajira baina ya Tanesco na bwana Mhando, kuondoa kwa namna yoyote isiyo na makubaliano baina ya pande mbili katika mkataba huo (Tanesco vs Mhando) ni uvunjifu wa mkataba kisheria. Mhando kama mwajiriwa yoyote katika nchi hii anayo haki. Sehemu ya haki hiyo imo ndani ya mkataba wake wa ajira na sehemu nyingine ipo katika sheria ya ajira na mahusiano kazini (sheria na 6/2004), na sehemu nyingine ipo ktk sheria ya mikataba (2002, sura ya 345) vitu vyote hivyo vitatu vinalinda haki zake kisheria. Tunaposhabikia haki zake kuvunjwa, tunashabikia haki za mwajiriwa awaye yeyote yule kuvunjwa. Mboma naye ni mbumbumbu wa sheria. Anashindwa kujua kua hata kamati ya bunge haipo juu ya sheria. Unatakiwa utii only lawful order. Ndiyo maana hata sheria ya ajira na mahusiano kazini na. 6/2004 inahesabu kuwa ni usitishaji wa ajira usio wa haki endapo mwajiri atamfukuza kazi mwajiriwa aliyekaidi amri isiyo halali. Amri ya POAC si halali kisheria.
Ushauri wangu: POAC na serikali kwa ujumla vitatue tatizo la umeme kisayansi zaidi badala ya kisiasa kwa kudhulumu haki ya kisheria ya mwajiriwa mmoja. Mhando amesema tatizo la umeme lipo wapi. Mkimwondolea jenereta miundombinu itaacha kuwa chakavu ghafla na kuwa mipya? Hayo madeni yatajilipa kwa kuwa tu Mkurugenzi naye analala kizani? Let us think out of box.
 
Umeliona hili Mkuu eeh.. Nimeshangazwa sana na kauli hiyo ya wabunge.. Kwanza wana mandate hiyo ya kuingilia mipangilio ya hw tanesco wanapeana privileges..? Au ndo yale ya taasisi na viongozi kutojua mipaka yao ya kazi..? Halafu itatatua vipi tatizo lililopo la umeme..? Kwa nini wasiseme mpaka lile la pale Ikulu litolewe nalo..? Wakati umefika sasa kwa hawa viongozi kuacha kutoa kauli za kisiasa.. political stunts hazitasaidia...

Hilo la kuondoa Jenereta amesema tu, amemuagiza nani akatoe,Mhando hawezi kulitoa, sio fundi (ni CEO). Ana mechanism gani ya kuhakikisha kuwa linatolewa.
 
Hivi ile trilion na kitu ilitolewa bungeni ili wabunge wapitishe bajeti ya wizara ikisemekana ni ya kufanya hali ya umeme iwe ya uhakika imeenda wapi vile
 
Hii ni hatari kwelikweli! nchi inachezewa kama kichwa cha mwendawazimu.
Hivi kweli nchi hii kuna kiongozi anayeweza kutoa maamuzi kwa maslahi ya taifa?
Huyo jk akili yake ilishagota ukingoni siku nyingi, anasubiri tu miaka yake mitatu iishe, alishawahakikishia watanzania mwaka gani ule, kwamba kufikia desemba yake tatizo la umeme litakuwa ni historia, akiulizwa leo hatua ipi ilichukuliwa atajibu nini?
 
We are great thinkers let us think deeply, kwa maoni yangu mkurugenzi wa TANESCO wanamwonea. Yeye angekuwa ni chanzo cha tatizo ningekubaliana na hatua hiyo ya kukatika mara kwa mara kwa umeme. Namkubali Zitto lakini kwa hili kachemsha. Je, Mhando akienda kushitaki mahakamani kuwa mkataba wake wa kazi umekiukwa itakuwaje. Nafikiri ni bora wakaadhibiwa wale walioifikisha TANESCO hapa ilipo.

Mkuu umenena sasa tuchukulie agizo lao limetekelezwa je ndio shida ya umeme imeisha?
 
Says Aggreko has withdrawn 100MW from grid over 230bn/-

The Tanzania Electric Supply Company Limited (Tanesco) has officially announced a countrywide power rationing following withdrawal of 100 megawatts from the national grid by Aggreko to press for payment of over 230bn/- debt.

Tanesco officials who were summonded by the Parliamentary Parastatal Organisations Committee (POAC) said Aggreko had switched off its generators and was awaiting payment.

For his part Tanesco Executive Director William Mhando admitted to the committee that the power shedding has started officially following the switching off of the Agrekko power plant. No further details of the load shedding were forthcoming from the officials, but POAC has directed the government through the Ministry of Energy and Minerals to provide Tanesco with 408bn/- to settle the bill.

POAC Chairman
Zitto Kabwe also ordered Tanesco to make sure that power generators at the Independent Tanzania Power Limited (IPTL) are switched off in May this year, and that a generator currently being used by Mhando at his residence is removed. The fuel bill for the generator is reportedly being paid for by the company.

Zitto said that the order to take out the generator at the residence of Tanesco CEO must be implemented from today and applied to other officers using generators whose cost was being covered by the company.

The committee said such expenditures should be stopped as they contributed to more costs.

Zitto told journalists in Dar es Salaam that after going through the company accounts, committee members discovered that Tanecso was facing serious financial problems due to expenditure for purchasing power from private firms.

He said Tanesco incurred a loss of 64bn/- in 2010 due to power purchases from IPTL, a situation experienced in the past four years. He added: “It is better we stop buying power from private sources”.

Giving the statistics of the losses, Zitto said in 2007 the power firm suffered a loss of 69bn/-, while in 2008 the figure went down to 21bn/-. In 2009 Tanesco lost 43bn/- rising to 47bn/- in 2010.

He said Tanesco should now start producing power from its own generators instead of the current system where it purchases electricity from private companies and distributes to its customers.

He explained that Tanesco revenue per year was 466bn/- but the cost of purchasing power from private companies and distributing it to customers was 492bn/-, a loss of 25bn/-.

He also pointed out that Tanesco incurred loss each year from the power it purchased from Songas despite the fact that the gas being used to generate power was being produced in the country.

A week a go Tanzania Electric Supply Company attributed the current power cuts in the country to system failures, saying it requires 1.3trn/- to overhaul its worn out production, transmission and distribution infrastructure.

The reaction followed a study by the World Bank and Twaweza which showed that there were more frequent power cuts recently, which lasted longer.

Most of the interviewees in the study said that power cuts occur more frequently and last longer. They said power outages would typically last more than six hours (40.6 percent) compared to only one in four in the 2010 survey (25.5 percent).

Mhando clarified that the country’s current power generation stands at 718MW while the demand is estimated at between 600MW and 829MW per day.

He gave an example whereby Kihansi dam was generating 100MW, Kidatu 160MW, Mtera 40MW, Pangani 15MW, Hale 5MW and Nyumba ya Mungu 2.6MW.

He said the energy produced from other sources were as follows, Songas 142MW, Ubungo gas plant 102MW, Independent Power Tanzania Limited (IPTL) 60MW, Tegeta gas plant 42MW and Symbion 60MW.



Hii kitu haiwezi kwisha ikiwa watu wanaofaidika na utengenezwaji wa huu umeme wa dharura ndiyo hao hao wenye nguvu na ushawishi katika maamuzi ya hii sekta ya nishati hapa Tanzania.

umeme wa dharura unawapa watu hela katika kusupply mafuta, hizi generators na kwa sababu bei ya umeme ni kitu kigumu kuwa determined jamaa wanapanga tu bei zao na tanesco haina jinsi inabidi ilipe. Wahusika wote kuanzia hawa wawekezaji IPTL, Songas, Symbion na wanasiasa wahandamizi katika sekta na nje ya sekta wananufaika na hii migao yaI umeme isiyokwisha.

Hamna kitu katika taifa hili kinachoonyesha wazi wazi ubinafsi uliokithiri wa hawa viongozi wetu zaidi ya hili la umeme.
 
Mchungaji Zachary Kakobe alishamuonja Ngeleja kuwa nchi haitaweza ondokana na tatizo la mgao wa umeme mpaka Ngeleja aende akatubu na kuomba msamaha kwa Mchumnaji Kakobe.
Ngeleja alionyesha jeuri na dharau kubwa kwa Kakobe wakati ule wa swala la upitishaji wa nguzo kubwa za umeme pale Mwenge karibu na Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship.
Ngeleja alidhani ni utani, sasa nchi inapata taabu ya umeme kwa sababu yake.
 
William Ngeleja ni janga la kitaifa. Sijui kwa nini JK anaendelea kumkumbatia mtu ambaye ameshindwa kabisa kuongoza wizara yake. Toka nchi imepata uhuru haijapata tokea waziri ameshindwa kiutendaji kama Ngeleja. Sijui atahadithia nini watoto na wajukuu zake kwani miaka yote ya uongozi wake umeme wa mgao, madini yanaporwa na wazungu bila kodi, mafuta yanachakachuliwa na wauzaji wanaiamulia serikali cha kufanya. Kikwete watose hawa washkaji zako kina Ngeleja kwani mzigo uliompa ameshindwa kuubeba...

To be fair, waziri tunamlaumu sana lakini haya ni matatizo yaliyotengenezwa miaka 50 iliyopita. Huwezi kupata short term solutions kutoka kwa Ngeleja utake usitake. Tumlaumu kama hapo alipo hana longterm plan ya kutatua tatizo hili! Jiulize ni kwa nini reli ya kati haitengenzwi (kwa ajili ya usafirishaji wa mafuta), kwa nini hatutengenezi mabwawa mapya. Utakuta kuna matatizo makubwa zaidi kwenye hii sekta
 
Mchungaji Zachary Kakobe alishamuonja Ngeleja kuwa nchi haitaweza ondokana na tatizo la mgao wa umeme mpaka Ngeleja aende akatubu na kuomba msamaha kwa Mchumnaji Kakobe.
Ngeleja alionyesha jeuri na dharau kubwa kwa Kakobe wakati ule wa swala la upitishaji wa nguzo kubwa za umeme pale Mwenge karibu na Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship.
Ngeleja alidhani ni utani, sasa nchi inapata taabu ya umeme kwa sababu yake.

Duh.. Kwa hiyo Mkuu unataka kutuambia shida yote hii ya umeme itaisha pindi Ngeleja akienda kuomba radhi kwa Kakobe..? Wewe mwenyewe unaamini hivyo au unataka kutuaminisha sie tu humu jamvini..?
 
dili za majenereta zikiisha everything wil be history. Tatizo la umeme haliwezi kuisha kamwe kwa style hii. Mi naona Tanesco wanazimazima umeme tena city centre ili watu wapige kelele kama hivi then agreko walipwe ili watu wachukue chao. ni uhuni tu hakuna chochote. Tanzania hii ni aibu kuu. Na anaemtetea Mhando ni mbavu tu. hivi akichukuliwa machinga muuza viatu bar akaambiwa aagize mita za luku toka september mpaka leo march angekuwa bado hajazileta tu? huu ni u**nge kabisa.
 
Back
Top Bottom