TANESCO: Rationing is back!

TANESCO: Rationing is back!

nakumbuka kauli ya Mh. mbowe alimwambia waziri mkuu bado sijaridhika nahuo mpango wadharura kwasababu kila mara mnasema ivo ivo, pinda akamwambia siusubiri tushidwe ndoutuulize.
sasa swali linakuja wame shidwa tayari namgao ndohuo unaanza soon, PINDA UTAMWAMBIA NINI MBOWE?

Mkuu huko kwenu utaanza? Sisi tunao kwa wastani wa mwezi na nusu hadi miwili sasa
 
Inawezekana hii ni mbinu ya MAGAMBA ili wananchi wasipate fursa ya kufuatilia yale yanayojiri huko Arumeru. Iweje sasa wanadai Aggreko wamezima mitambo ilhal Mkurugenzi wa TANESCO alisema awali (sio zaidi ya wiki moja imepita) kuwa kinachotokea sasa ni matokeo ya mkataba ulioingiwa na NET GROUP pamoja na uchakavu wa mitambo na sio mgawo kama watu wanavyohisi.

Hizi kauli tata zinazotolewa na viongozi wetu zinaashiria nini kwa mustakabali wa taifa letu?
Walikuwa wanatania mkuu
 
Hata tukibadilisha uongozi wote pale bado hali itakuwa hivi hivi kama tusipobadilisha mbinu za kibiashara za shirika hili na kuondoa siasa kwenye utendaji wake.

Kwa hali ilivyo pale Tanesco, siasa ni nyingi kuliko... Labda tutafute majibu ya maswali haya machache ili tujue hali halisi ilivyo. Hv ilikuwa ni viable kupeleka umeme mabwepande kwenye mahema? Kama jibu ni hapana ile distribution line imegharamiwa na nani au gharama zake zitarudi vp na kwa kipindi gani? The same apply kwa kawawa, kule madale enzi hizo.

Mbona Tanesco wanalazimishwa kujenga hizo line lakin serikali haiwalipi? Mbona taasisi za serikali na wizara zake hazilipi bili zao wakati budget ya matumizi hayo wanatengewa?
Wanatudanganya kwa ruzuku wanazolipatia shirika hili kumbe hata haifiki robo ya madeni yao.

Ndo maana nikasema jk akifanya timua timua kwenye tanesco nae inaweza ikamhusu
 
Agizo hilo ni feki halina mshiko maana halikuangalia source ya tatizo,tatizo si William mhando,tatizo ni serikali ya magamba kutokuwa na mipango mkakati wa kuimarisha sekta hii ya Umeme,tangu awamu ya kwamza mabwawa ya maji yalipotengenezwa hakuna serikali zilizofuata kuweka mipango ya kuimarisha sekta hii!
 
mhando tanesco2.jpg

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), William Mhando,


Midraji Ibrahim

MKURUGENZI Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), William Mhando, amesema ingawa suala la kupatiwa umeme lipo kwenye stahili za mkataba wake, hawezi kubishana na uamuzi wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) wa kuondoa jenereta nyumbani kwake.

Akizungumza kufuatia agizo la POAC kuondoa jenereta hiyo nyumbani kwake jana, ili aonje uchungu wa kukatika kwa umeme, Mhando alisema alishtushwa na hatua hiyo kwa sababu ni suala la mkataba, lakini hawezi kubishana na kamati.

“Mkataba ninao jana (juzi) nilishtuka kuhusu agizo hilo kwa sababu niliajiriwa na bodi na mwenyekiti wangu alikuwapo tutakaa tuangalie, lakini siwezi kupingana na maagizo ya kamati,” alisema Mhando.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa wa Bodi ya Tanesco, Jenerali mstaafu Robert Mboma, alisema watatii agizo la POAC la kuondoa jenereta la dharura lililopo nyumbani kwa mkurugenzi huyo.

“Tumeagizwa na kamati tutaangalia jinsi ya kulitekeleza agizo hilo la kuondoa jenereta, tupeni siku tatu au nne hivi mtaona,” alisema Jenerali Mboma.

Alipoulizwa kama kuondoa jenereta hiyo haitakuwa kinyume na mkataba wa ajira unaoonyesha stahili za mkurugenzi huyo, Mboma alisema: “ Unadhani tutafanya nini kama tumeagizwa tuiondoe, hatuna jinsi hata kama kuna mkataba sisi tutatekeleza tuliyoagizwa.”

Mhando alisema suala la kukatika kwa umeme unaondelea hivi sasa, halisababishwi na menejimenti bali inatokana na kutokuwapo kwa uwekezaji muda mrefu kwenye shirika hilo, baada ya kuwekwa chini ya Shirika la Kubinafsisha na Kuuza Mashirika ya Umma (PSRC).

“Tangu mwaka 1999 hadi 2007 hakuna uwekezaji uliofanywa kwa Tanesco baada ya shirika kuwekwa chini ya PSRC, kwa hiyo kukatika kwa umeme kunaokoonekana hivi sasa ni matokeo ya ubinafsishaji uliolengwa,” alisema.

Mkurugenzi huyo alisema kukatika kwa umeme kunatokana na uchakavu wa miundombinu, lakini siyo kuzidiwa na kwenye uzalishaji kwa sababu hivi sasa wanazalisha Megawati 782.51 ilhali mahitaji ni Megawati 772.15.

“Mfano pale City Center (katikati ya jiji), tulikuwa na transfoma mbili zote zimetumika zaidi ya miaka 30, Februari mwaka huu zimeharibika, tumeagiza kutoka Uturuki na sasa zimefika Dubai, tatizo ni miundombinu imechakaa,” alisema.

Kuhusu Aggreko na Symbion Dodoma kuzima mitambo yao, Mhando alikiri kuwa hatua hiyo inatokana na deni ambalo linafikia Sh62 bilioni na kwamba, IPTL imepunguza uzalishaji kutoka Megawati 100 hadi 50. Aggreko inadai Sh58 bilioni na Symbion Dodoma Sh4 bilioni.

“Mgawo kwa maana ya uwezo wa kuzalisha hatuna, ila hii kukatikakatika kwa sababu ya transfoma hiyo ipo. Tupo kwenye hatua mbalimbali za kukarabati miundombinu hiyo na baada ya kipindi tatizo hilo litatoweka,” alisema.

Mhando alisema hivi sasa wamepata dola 85 milioni za Marekani kwa ajili ya Dar es Salaam, Euro 25 milioni kutoka Finland na Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) imetoa dola 40 milioni za Marekani.

Juzi, Mwenyekiti wa POAC, Zitto Kabwe, alisema lazima jenereta lililoweka nyumbani kwa mkurugenzi huyo liondolewe kwa sababu linatumia mafuta ya Serikali.

CHANZO: Mkurugenzi Tanesco asikitishwa uamuzi wa POAC

Mkuki kwa Nguruwe kwa Binadamu ni mchungu. Mkuu itabidi na wewe uonje Machungu ya Umeme wa Mgao.

mamilioni haya kibao yanayokopwa kila kucha na tenesco kutoka taasisi kibao cha nchi za ulaya zitalipwaje jamani ??
Ni hatari sana kwa mkurugenzi kuanza kujifikiria yeye kwanza huku wateja wanaompa chakula wakiwa hawana uwezo wa kupata umeme. mtu mbinafsi san huyu.
 
Pia mimi nashauri haya:

1. Waziri wa elimu naye aondolewe kwenye pay roll kama miezi miwili hivi ili ajue adha ya walimu wanaoondolewa kwenye pay roll kiuzembe halafu wanapata usumbufu mkubwa kurudishwa

Watoto wake AU Wajukuu lazima waandikishwe shule za kata
 
Source Majira

Kumbe tunaendelea kuganganywa kuwa mitambo ni michakavu ndo maana kuta kukatika katika kwa umeme kumbe ni madeni yanayowafanya washindwe kuzalisha umeme hasa unaozalishwa na kampuni ya Aggreco (samahani kama nitakuwa nimekosea kuiandika) kuidai tanesco zaidi ya billion 300/=

hiyo imebainishwa na mwenyekiti wa kamati ya nishati na madini mh January Makamba hapo Jana

Watanzania tunaisaidiaje tanesco kuibanafsisha tena au kuongezewa tena bei mpya

Wakuu hii issue ya tanesco imeshakuwa kama tamsilia ya isidingo the need!
 
nakumbuka kauli ya Mh. mbowe alimwambia waziri mkuu bado sijaridhika nahuo mpango wadharura kwasababu kila mara mnasema ivo ivo, pinda akamwambia siusubiri tushidwe ndoutuulize.
sasa swali linakuja wame shidwa tayari namgao ndohuo unaanza soon, PINDA UTAMWAMBIA NINI MBOWE?

Walipitisha bajeti kwa mbwembwe kama madereva wa bodaboda!This mzee wa megawats na Mzee mapete hamtoki ngoja session zianze!
 
Ningekuwa mimi mdo rais natimua viongozi wote wa tanesco na kuweka uongozi mpya.haiwezekani shirika ambalo halina mpinzani na linalotoa huduma inayotakiwa kila mahali lijiendeshe kihasa.tanesco wakikusanya tu madeni wanayodai matatizo yameisha Its a shame

Rais naye ajitimue kazi tufanye uchaguzi upya.
 
We are great thinkers let us think deeply, kwa maoni yangu mkurugenzi wa TANESCO wanamwonea. Yeye angekuwa ni chanzo cha tatizo ningekubaliana na hatua hiyo ya kukatika mara kwa mara kwa umeme. Namkubali Zitto lakini kwa hili kachemsha. Je, Mhando akienda kushitaki mahakamani kuwa mkataba wake wa kazi umekiukwa itakuwaje. Nafikiri ni bora wakaadhibiwa wale walioifikisha TANESCO hapa ilipo.
 
mhando tanesco2.jpg

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), William Mhando,


Midraji Ibrahim

MKURUGENZI Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), William Mhando, amesema ingawa suala la kupatiwa umeme lipo kwenye stahili za mkataba wake, hawezi kubishana na uamuzi wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) wa kuondoa jenereta nyumbani kwake.

Akizungumza kufuatia agizo la POAC kuondoa jenereta hiyo nyumbani kwake jana, ili aonje uchungu wa kukatika kwa umeme, Mhando alisema alishtushwa na hatua hiyo kwa sababu ni suala la mkataba, lakini hawezi kubishana na kamati.

“Mkataba ninao jana (juzi) nilishtuka kuhusu agizo hilo kwa sababu niliajiriwa na bodi na mwenyekiti wangu alikuwapo tutakaa tuangalie, lakini siwezi kupingana na maagizo ya kamati,” alisema Mhando.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa wa Bodi ya Tanesco, Jenerali mstaafu Robert Mboma, alisema watatii agizo la POAC la kuondoa jenereta la dharura lililopo nyumbani kwa mkurugenzi huyo.

“Tumeagizwa na kamati tutaangalia jinsi ya kulitekeleza agizo hilo la kuondoa jenereta, tupeni siku tatu au nne hivi mtaona,” alisema Jenerali Mboma.

Alipoulizwa kama kuondoa jenereta hiyo haitakuwa kinyume na mkataba wa ajira unaoonyesha stahili za mkurugenzi huyo, Mboma alisema: “ Unadhani tutafanya nini kama tumeagizwa tuiondoe, hatuna jinsi hata kama kuna mkataba sisi tutatekeleza tuliyoagizwa.”

Mhando alisema suala la kukatika kwa umeme unaondelea hivi sasa, halisababishwi na menejimenti bali inatokana na kutokuwapo kwa uwekezaji muda mrefu kwenye shirika hilo, baada ya kuwekwa chini ya Shirika la Kubinafsisha na Kuuza Mashirika ya Umma (PSRC).

“Tangu mwaka 1999 hadi 2007 hakuna uwekezaji uliofanywa kwa Tanesco baada ya shirika kuwekwa chini ya PSRC, kwa hiyo kukatika kwa umeme kunaokoonekana hivi sasa ni matokeo ya ubinafsishaji uliolengwa,” alisema.

Mkurugenzi huyo alisema kukatika kwa umeme kunatokana na uchakavu wa miundombinu, lakini siyo kuzidiwa na kwenye uzalishaji kwa sababu hivi sasa wanazalisha Megawati 782.51 ilhali mahitaji ni Megawati 772.15.

“Mfano pale City Center (katikati ya jiji), tulikuwa na transfoma mbili zote zimetumika zaidi ya miaka 30, Februari mwaka huu zimeharibika, tumeagiza kutoka Uturuki na sasa zimefika Dubai, tatizo ni miundombinu imechakaa,” alisema.

Kuhusu Aggreko na Symbion Dodoma kuzima mitambo yao, Mhando alikiri kuwa hatua hiyo inatokana na deni ambalo linafikia Sh62 bilioni na kwamba, IPTL imepunguza uzalishaji kutoka Megawati 100 hadi 50. Aggreko inadai Sh58 bilioni na Symbion Dodoma Sh4 bilioni.

“Mgawo kwa maana ya uwezo wa kuzalisha hatuna, ila hii kukatikakatika kwa sababu ya transfoma hiyo ipo. Tupo kwenye hatua mbalimbali za kukarabati miundombinu hiyo na baada ya kipindi tatizo hilo litatoweka,” alisema.

Mhando alisema hivi sasa wamepata dola 85 milioni za Marekani kwa ajili ya Dar es Salaam, Euro 25 milioni kutoka Finland na Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) imetoa dola 40 milioni za Marekani.

Juzi, Mwenyekiti wa POAC, Zitto Kabwe, alisema lazima jenereta lililoweka nyumbani kwa mkurugenzi huyo liondolewe kwa sababu linatumia mafuta ya Serikali.

CHANZO: Mkurugenzi Tanesco asikitishwa uamuzi wa POAC

Mkuki kwa Nguruwe kwa Binadamu ni mchungu. Mkuu itabidi na wewe uonje Machungu ya Umeme wa Mgao.

Mhando hizi story wananchi wamezichoka kila siku visingizio hivyo hivyo.
Mytake.
Mhando atawashtaki tanesco kwa kukiuka mkataba na atashinda kesi la ruling itailazimisha tanesco kumlipa hiyo damage.This country bwanaa!
 
Karibu gizani Kaka mkubwa, ili na wewe uonje uchungu wa kukatika kwa umeme mara kwa mara!
Tunajua una uwezo wa kureplace mara tu litakapo ondolewa, lakini utatumia mshahara wako kulihudumia ili uweze kutukumbuka sisi wanyoge!
 
Inawezekana hii ni mbinu ya MAGAMBA ili wananchi wasipate fursa ya kufuatilia yale yanayojiri huko Arumeru. Iweje sasa wanadai Aggreko wamezima mitambo ilhal Mkurugenzi wa TANESCO alisema awali (sio zaidi ya wiki moja imepita) kuwa kinachotokea sasa ni matokeo ya mkataba ulioingiwa na NET GROUP pamoja na uchakavu wa mitambo na sio mgawo kama watu wanavyohisi.

Hizi kauli tata zinazotolewa na viongozi wetu zinaashiria nini kwa mustakabali wa taifa letu?

Mbinu chafu??? Hakuna kitu kama hicho, kwani uchaguzi wa arumeru usipozungumziwa nini kitatokea? Kura zitapigwa na ccm lazima iangukie pua.

Suala hapa ni serikali dhaifu na viongozi waongo. Watuambie bajeti ya 1.2trillion ya umeme wa dharura na ile mipango iliyotangazwa na Pinda bungeni imeyeyukia wapi? Tungependa kuona rais na serikali yake inawajibika haraka. Nchi imeanza kuingia kwenye tatizo la mgao, na kwa hali ilivyo tatizo litakuwa kubwa zaidi ya ilivyokuwa mwaka jana. Kuna haja gani ya kuendelea kuiacha serikali hii iendelee kudidimiza uchumi wa nchi?
 
wapendwa,

binafsi nawashangaa wote mliojadili hapa, namshangaa mkurugenzi wa tanesco na pia mwenyekiti wake wa bodi!

kwani POAC ina mamlaka gani ya kuiamuru tanesco jambo lolote? mnajua maana ya separation of powers? hiyo POAC si ni ya upande wa uwakilishi (bunge) na tanesco upande wa utekelezaji (serikali). hebu tutafakari tena hapo!

ili kuwafunza adabu watu wavivu wa kufikiri, nashauri hilo generator likishaondona hapo, siku umeme ukikatika kwake tu, aende mahakamani mara moja, ili tujue kuwa bunge ni wasimamizi tu wa seriklali na hawawezi na wala hawana haki wala mamlaka yoyote ya "KUAGIZA' moja kwa moja lolote na likatendeka huko serikalini kwa mujibu wa katiba na sheria zetu.

kwa kweli zito na kamati yake walichemka, ila hawa watakaotekeleza watakuwa wamechemka zaidi!

mbarikiwe sana wapendwa

Glory to God!
 
Hapo hakuna atakachopoteza sana sana ni kumwonea tu! Kwa nini wasimguse hata Waziri mwenye dhamana na Katibu mkuu wa wizara ya NM? Hapa naona jamaa wanamwandalia mazingira ya kujilipa mamilioni.
 
Hata tukibadilisha uongozi wote pale bado hali itakuwa hivi hivi kama tusipobadilisha mbinu za kibiashara za shirika hili na kuondoa siasa kwenye utendaji wake.

Kwa hali ilivyo pale Tanesco, siasa ni nyingi kuliko... Labda tutafute majibu ya maswali haya machache ili tujue hali halisi ilivyo. Hv ilikuwa ni viable kupeleka umeme mabwepande kwenye mahema? Kama jibu ni hapana ile distribution line imegharamiwa na nani au gharama zake zitarudi vp na kwa kipindi gani? The same apply kwa kawawa, kule madale enzi hizo.

Mbona Tanesco wanalazimishwa kujenga hizo line lakin serikali haiwalipi? Mbona taasisi za serikali na wizara zake hazilipi bili zao wakati budget ya matumizi hayo wanatengewa?
Wanatudanganya kwa ruzuku wanazolipatia shirika hili kumbe hata haifiki robo ya madeni yao.

Mkuu hata shambani kwa Sumaye kiluvywa ilipelekwa 11kva nani alilipia gharama hizi kule ulongoni Gongo la mboto kwenye wakazi zaidi ya elfu tatu umeme hakuna na watu tushalipa gharama za kuletea umeme haujaletwa mpaka tumeenda mahakamani ,

Rais dhaifu,hata viongozi wa mashirika watakuwa dhaifu wiki iliyopita Prof.Mbwete alikaririwa akisema wameingia mkataba na Mwizi wahela za OPEN UNIV.arudishe taratibu kama Rais alivyoingia mkataba na wezi wa EPA.
 
Kila siku TANESCO inadaiwa, pamoja na kupandisha bei ya umeme bado inadaiwa. Kama wameshaonesha kushindwa ni kwa nini tusitumie njia mbadala? Say, yaruhusiwe makampuni binafsi kuuza umeme kwa watumiaji!

Mkuu mimi naamini nchi hii bado ina watu wazuri wanaoweza kuongoza. Pia nafahamu kwamba huko TANESCO kuna viongozi wazuri tu tatizo ni siasa mkuu. Hivi kwa nini Dr. Idrissa aliondoka? Jibu ni kuingiliwa kisiasa. TANESCO ni shamba la bibi kila mtu anataka aingilie. Wanauziwa umeme bei aghari hawatengenezi faida! Watu wanakula kwenye mafuta ya kuendeshea mitambo ya IPTL! Mambo ni mengi.
 
Bora yajitokeze makampun mengine ya kuzalisha umeme.na Tanesco wabakie kumiliki nyaya na nguzo wao ndio wawe wanapiga servirse.

Iwe kama makampuni ya simu ingawa kila kampuni linamatatizo yake lakini siku zinasonga wakizingua tigo unawapiga chini unaweka voda wakizingua voda unahamia air tel nao wakileta magumashi yuleee zantel safari com na ttcl nao watakusubiri tu.

Lakini kwa hawa tanesco wanatuzingua sana kwanza bei zao ziko juu ukiachana na bei huduma ndiyo hizo magumashi mara washa mara zima
 
Back
Top Bottom