Tanesco New Slogan!!

Tanesco New Slogan!!

JS

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2009
Posts
2,064
Reaction score
506
Wadau wa JF,

Kwa kweli hili suala la mgao wa umeme TENA nchi nzima limenisikitisha sana. TANESCO sucks big time na uongozi wake wote. Iweje watangaze umeme utakuwa historia halaf ndani ya miezi michache tunapata habari ya MGAO mwingine utakaozidi masaa 12??

Kwani hawajui hasara inayokumba nchi nzima katika suala zima la MAPATO umeme ukikosekana??? Na hao wawekezaji tunaopaswa kuwaencourage waje kuwekeza, watakuja kweli kwa hali hii???

Katika pitapita zangu nimepata slogan mpya kutokana na shida hii ya umeme. Mhe. JK alitoa slogan ya UKIMWI kwamba TZ bila ukimwi inawezekana. Kuhusu UMEME inageuzwa inakuwa hivi, TZ BILA UMEME HAIWEZEKANI KABISA kuishi na kufanya biashara na kufanya kazi yoyote inayohusu maendeleo. Natamani angeliona tatizo hili JK kwa undani zaidi kama ambavyo aliona tatizo la ukimwi.

Ninaanza kuchoka na nchi yangu hii. I wish i wasnt born here at times or not born at all nisione mambo haya!!!!!!!!!
icon9.gif
icon9.gif
 
Kwa hiyo Raisi wetu kwenye hio slogan ya UKIMWI amefanikiwa?
 
Sisy JS, jipe moyo utashinda tu, usijistress sana u will end with nothing hii ndio bongo tambarare yetu, kaza buti twende.
 
Kwa hiyo Raisi wetu kwenye hio slogan ya UKIMWI amefanikiwa?

Atleast ameweza kutengeneza awareness kwa watu na wadau husika. Ngoja nikuambie Nguli, ile ya ukimwi si alisema mwenyewe JK kwa hiyo ikapewa uzito zaidi. kwa hiyo na ya umeme akisema itapewa uzito.
 
Kwa hiyo Raisi wetu kwenye hio slogan ya UKIMWI amefanikiwa?
Hiyo slogan ya ukimwi imegeuzwa kuwa madili ya watu kujineemesha.
Na kuhusu mashirika ya umma(SU) na ofisi ya serikali zote hali ni mbaya sana.Sahizi rushwa, wizi na uhujumu unafanywa na wafanyakazi wenyewe.Kwanza wanasema mishahara haitoshi na pili wana-revenge rushwa inayofanywa na wakubwa(RICHMOND).
Haya mapambano sijui ya kushitaki mawaziri ni kama yamechochea zaidi uhujumu.Hali ni mbaya sana na matokeo yake ndio haya ya uzorotaji wa huduma muhimu.
Na hii ni cha mtoto tu,huko tunaendea tutakaa miezi kadhaa bila umeme.
Kama unaweza Js wahi tu ughaibuni.
 
Atleast ameweza kutengeneza awareness kwa watu na wadau husika. Ngoja nikuambie Nguli, ile ya ukimwi si alisema mwenyewe JK kwa hiyo ikapewa uzito zaidi. kwa hiyo na ya umeme akisema itapewa uzito.
JS mdogo wangu,Suala la Umeme ni tofauti na ukimwi.
Halihitaji awareness linahitaji DECISIONS( DANGEROUS DECISIONS)
 
Stiegler's Gorge....how I wish that will happen....potential is there for 2500Mw and we need only 900Mw...shida pale hapatatoa 10% ndio maana wakubwa wanang'ang'ania hayo maumeme ya dharura...rushwa tupu
 
JS mdogo wangu,Suala la Umeme ni tofauti na ukimwi.
Halihitaji awareness linahitaji DECISIONS( DANGEROUS DECISIONS)


Basi somebody should make hiyo dangerous decision haraka.
 
Hivi kwani humu hamna mtu anayefanya kazi TANESCO atueleze ukweli wa mambo?

Iweje mashine zote ziharibike kwa pamoja? Hakuna regular maintenance ya mashine?
 
Tanesco wanapaswa kubadilisha slogan yake kuwa "
Tanesco: we frustrate the economy"

Wajasiriamali na biashara nyingi zinakufaa kwa sababu ya Tanesco, tunahitaji kampuni nyingine ya uzalishaji na usambazaji wa umeme
 
umeme bongo ni luxury service, tulipoambiwa tufunge mikanda ni pamoja na kuukosa huo umeme, si mliambiwa chanzo ni Dk. Rashid , sasa hayupo tutafute sababu zingine za kijifariji ili siku zisonge, wabongo hawataki umeme, wakipewa sababu tu za kuukosa wana thumb up, tumeambiwa kuna Major repair tusharidhika!!
 
JS mdogo wangu,Suala la Umeme ni tofauti na ukimwi.
Halihitaji awareness linahitaji DECISIONS( DANGEROUS DECISIONS)
Hapa nimekugongea kale kakitu! tunahitaji maamuzi ya hatari, sio magumu!!
 
Tanesco wanapaswa kubadilisha slogan yake kuwa "
Tanesco: we frustrate the economy"

Wajasiriamali na biashara nyingi zinakufaa kwa sababu ya Tanesco, tunahitaji kampuni nyingine ya uzalishaji na usambazaji wa umeme
TANESCO wana matatizo yao ynayochangia hali hii,lakini matatizo makubwa yapo Serikalini(siasa tena za kimaslahi binafsi zimezidi)
 
Tanesco wanapaswa kubadilisha slogan yake kuwa "
Tanesco: we frustrate the economy"

Wajasiriamali na biashara nyingi zinakufaa kwa sababu ya Tanesco, tunahitaji kampuni nyingine ya uzalishaji na usambazaji wa umeme
Imagine hapa nilipo umeme unarudi usiku, lakini ndipo ilipo workshop yangu ya kuchana mbao, wafanyakazi wanacheza pooltable na draft, mwisho wa mwezi natakiwa kuwalipa.

uwezo wa kununua generator kwa 16 - 20M sina, na hata nikinunua operation cost zitanitoa sokoni, na zinaweza kunirudisha kijijini kabisa.
 
Tatizo ni kuwa tutampata wapi mtu kama huyo?mwenye moyo wa kijeshijeshi.

Mie hapa Charity............natamani ingekuwa rahisi kihivyo. NAenda kutafuta kazi TANESCO nichape kazi hakuna kulala nipate cheo haraka nilianzishe
 
umeme bongo ni luxury service, tulipoambiwa tufunge mikanda ni pamoja na kuukosa huo umeme, si mliambiwa chanzo ni Dk. Rashid , sasa hayupo tutafute sababu zingine za kijifariji ili siku zisonge, wabongo hawataki umeme, wakipewa sababu tu za kuukosa wana thumb up, tumeambiwa kuna Major repair tusharidhika!!

Songoro unaonaje tukianzisha mass demonstration kuhusu hili suala???? Tuanzie hapa JF
 
Back
Top Bottom