KERO Tanesco Mkoa wa Kinondoni Kusini- Kimara/Kibamba

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

mimimkweli

New Member
Mar 24, 2010
1
0
Tangu mwaka huu 2025 umeanza TANESCO wamekuwa na huduma mbaya ndani ya Mkoa huu wa kwao wa kiutendaji (KINONDONI SOUTH) hasa njia ya umeme ya kutoa huduma kuanzia Kimara mpaka Kibamba.

Umeme Kila siku unakatika katika ndani ya muda mfupi na wakati mwingine kukatwa kwa muda mrefu kwa maelekezo kuwa wanarekebisha miundombinu lakini tatizo haliishi.

Taarifa hii iwafikie viongozi wa TANESCO na SERIKALI kwa ujumla. Mijadala ya kwenye kundi la WhatsApp la Tanesco inatosha kuelezea tatizo hili.

Yafaa kupatiwa utatuzi wa uhakika wa mara moja.
Tunaomba watuletee majibu ya uhakika kwani Hali ni mbaya na shughuli za kiuchumi zinasimama.

Kiukweli shirika limekuwa likihujumu uchumi wa watu binafsi na SERIKALI. Tunaomba utatuzi wa mapema.

Pia soma: KERO - TANESCO mnakata umeme kuanzia Kimara mpaka Mbezi kwa zaidi ya masaa 12 kila siku bila ya kutoa taarifa yoyote ile ya kueleweka
 
aisee daily wanakata umeme, leo hii pia wameshaukata.

Jana waliukata saa 4 asubuhi wameurudisha saa 6 usiku.
 
si bora huko wanakata mara moja huku kimara wanakata umeme baada ya lisaa wanaurudisha wanakata tena wanarudisha yaani wamefanya kama kamchezo nahisi kuna mtoto watakua wamemuachia achezee umeme … tanesco acheni huo utoto mnatuunguzia vitu vyetu siku ya 3 leo mnafanya huo mchezo
 
si bora huko wanakata mara moja huku kimara wanakata umeme baada ya lisaa wanaurudisha wanakata tena wanarudisha yaani wamefanya kama kamchezo nahisi kuna mtoto watakua wamemuachia achezee umeme … tanesco acheni huo utoto mnatuunguzia vitu vyetu siku ya 3 leo mnafanya huo mchezo
jana nilipita hapo kimara waliukata saa 4 asubuhi wamekuja kuurudisha saa 5 usiku
 
Back
Top Bottom