TANESCO kwanini mnafurahia kututesa Watanzania?

TANESCO kwanini mnafurahia kututesa Watanzania?

Keynez

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2007
Posts
3,718
Reaction score
6,772
Mmeshindwa kutupa umeme wa uhakika tunawaangalia tu.

Sasa mmeshindwa kuja na ratiba rasmi ya huo mgao wenu ili hata mtu apangilie ratiba yake ya siku maana shughuli nyingi bila umeme haziendi?

Sasa mnakata umeme saa 2 usiku weekend, mnataka twende wapi muda huu?

Hivi furaha yenu ni kuona watanzania tunateseka au?
 
Sisi huku ratiba ni ya usiku tu, mchana empty. Inaanzia saa 12 jioni mpaka saa 3 asubuhi.
 
Bado wana chuma wakisha tosheka umeme utakaa sawa. Mimi najiuliza hivi huyu mtanzania aliyekopa Akawekeza kwenye biashara ya kuuza bidhaa za vitoweo Ameweka stock Yake kwenye freezer Alafu umeme imekua tahabu Anafidiwa na nani?

Je! Waliomkopesha fedha watamsamehe fedha Alizo poteza kwa kukosa Umeme wa uhakika?


Jamani SERIKALI ya mama. Mjitafakari sana. Kama mtaendelea kuwaamimi hawa wataalam wa tanesko mtaharibu kabisa uchumi wa wananchi.
 
Pigo kwenye nishati ni pigo ndoige. Ndio maana hata Russia anapiga miundombinu ya umeme na gesi ya Ukraine. Hata siye tunachakazwa mbaya. EFD hazitumiki kisa hakuna umeme, hospital watu hawapimwi kisa umeme, viwanda havizalishi kisa umeme, n.k
 
CCM wana raha sana kuongoza pimbi ingekuwa nchiiii nyingine tungekuwa kwenye uongozi wa mpitoo...tunasubiri uchaguzi.
 
Pigo kwenye nishati ni pigo ndoige. Ndo maana hata Russia anapiga miundombinu ya umeme na gesi ya Ukraine. Hata siye tunachakazwa mbaya. Efd hazitumiki kisa hakuna umeme, hospital watu hawapimwi kisa umeme, viwanda havizalishi kisa umeme, n.k
Na hapo tunajivunia amani na utulivu tuko na hali hii.
 
Jamani yule jamaa aliposema tutamkumbuka alikuwa anamaanisha mambo kama haya. Wakati wake mgao wa umeme ulipungua sana, tukawa tunapata umeme 95%, tukasahu kabisa huu ujinga wa mgao; alichoambulia toka kwetu ni matusi na dhihaki. Ngoja tuonje joto ya jiwe ili fahamu ziturudie tujue kuappriciate tunapofanyiwa mambo mazuri.
 
Hivi Watanzania tumeshindwa hata kuorganise njia ya kuonyesha kutoridhishwa kwetu na huu mgao? Huu ukimya una maana gani?

Tumeshindwa hata kuorganise simu moja ya wiki ambayo wote tutagoma kutumia umeme kwa masaa 24, uwepo usiwepo tunaiweka nchi gizani kwa masaa 24. Unajua ni impact kiasi gani hata kitu kama hicho kikifanyika hata kama kutakuwa na watakaoamua kutoshiriki? Mabadiliko ya kweli yanaanzaga kama mzaha tu.
 
Mmeshindwa kutupa umeme wa uhakika tunawaangalia tu.

Sasa mmeshindwa kuja na ratiba rasmi ya huo mgao wenu ili hata mtu apangilie ratiba yake ya siku maana shughuli nyingi bila umeme haziendi?

Sasa mnakata umeme saa 2 usiku weekend, mnataka twende wapi muda huu?

Hivi furaha yenu ni kuona watanzania tunateseka au?
Imagine [emoji18]
 
Hivi Watanzania tumeshindwa hata kuorganise njia ya kuonyesha kutoridhishwa kwetu na huu mgao? Huu ukimya una maana gani?

Tumeshindwa hata kuorganise simu moja ya wiki ambayo wote tutagoma kutumia umeme kwa masaa 24, uwepo usiwepo tunaiweka nchi gizani kwa masaa 24. Unajua ni impact kiasi gani hata kitu kama hicho kikifanyika hata kama kutakuwa na watakaoamua kutoshiriki? Mabadiliko ya kweli yanaanzaga kama mzaha tu.
Hii Nchi Ina Misukule binadamu wa kawaida hawawezi kuwa wapumbavu Kwa kuvumilia ujinga kiasi hiki ingekuwa nchi za wenzetu tungeona maandamano, viongozi hawajielewi waandishi wa habari ndio hawajielewi ilitakiwa Kila Kona media mripoti hii changamoto Kwa kuwasiliana na watu Moja Kwa Moja kuona wameathirika vipi na mgao ispokuwa mpo tu kuripoti PhD Shame on you
 
Hali ya upatikanaji umeme imekuwa hoi bin taaban na unaweza kuona namna watu walivyo desperate kushindwa kufanya shughuli zao zinazowaingizia vipato, jamani kama hii nchi imewashinda kuongoza ondokeni tu wala hakuna atakayewakejeli kwa uamuzi wa kuwa wakweli kwa nafsi zenu ili waje wengine wenye majawabu na hizi changamoto za miaka nenda rudi zinazowasibu hawa wananchi amabo wamejikuta wamezaliwa na kuishi Tanzania, ni hayo tu kwa leo...​
 
Hii Nchi Ina Misukule binadamu wa kawaida hawawezi kuwa wapumbavu Kwa kuvumilia ujinga kiasi hiki ingekuwa nchi za wenzetu tungeona maandamano, viongozi hawajielewi waandishi wa habari ndio hawajielewi ilitakiwa Kila Kona media mripoti hii changamoto Kwa kuwasiliana na watu Moja Kwa Moja kuona wameathirika vipi na mgao ispokuwa mpo tu kuripoti PhD Shame on you
Tatizo ni kila penye watz wawili basi mmoja ni shushushu, yaani ukianzisha tu kusema dakika si nyingi umenyakwa
 
Huku kwetu 12 kamili jioni wameondoka nao saa 6 kasoro usiku ndiyo wamerudisha hapa ndiyo simu zetu tumacharge maana hatujui hiyo kesho, yaani nchi hii kama inajiongoza wenyewe popote ni njia.
 
Hawa jamaa ni shida
IMG-20221203-WA0010.jpg
 
Hivi Watanzania tumeshindwa hata kuorganise njia ya kuonyesha kutoridhishwa kwetu na huu mgao? Huu ukimya una maana gani?

Tumeshindwa hata kuorganise simu moja ya wiki ambayo wote tutagoma kutumia umeme kwa masaa 24, uwepo usiwepo tunaiweka nchi gizani kwa masaa 24. Unajua ni impact kiasi gani hata kitu kama hicho kikifanyika hata kama kutakuwa na watakaoamua kutoshiriki? Mabadiliko ya kweli yanaanzaga kama mzaha tu.
Ni Wacha he watakuelewa
Hilo linchi ujinga ni mwingi sana na unathaminiwa
 
Tatizo ni kila penye watz wawili basi mmoja ni shushushu, yaani ukianzisha tu kusema dakika si nyingi umenyakwa
Tuache visingizio vya woga. Kama ni kuogopa kupigwa virungu, kuna njia bunifu za kuonyesha kutoridhishwa kwenu. Mgomo baridi kama niliosema hapo juu ni njia mojawapo ila kuna njia nyingi zisizohusisha kuingia barabarani na ziko very effective.

Itafika wakati watakanusha kuwa hakuna mgao ingawa utakuwepo unaendelea. Jana kuna sehemu nimeona mtu anasema TANESCO hawatoi ratiba kwa sababu hakuna mgao, can you imagine? Na kweli baadae bila uthibitisho wa kimaandishi hauwezi kusema mgao ulikuwepo, kwa hiyo inawezekana kabisa ni mkakati maalum. Ndiyo kama hawa wanaosema kipindi cha Magufuli umeme haukuwa unakatika wakati si kweli.
 
Back
Top Bottom