Nilipata habari kwamba mtumiaji wa umeme anayetumia unit chini ya 70 anapaswa kubadirishiwa tariff. Nikaenda ofisi za TANESCO kwa ajili ya kubadilishiwa. Kwanza mapokezi hayakuwa mazuri kwani walinipotezea muda.
Huduma ya kutolewa ndani ya dakika 15 niliipata kwa zaidi ya saa moja, kujaza fomu tu. Muhudumu ananiambia eti network iko slow. Network ilikuwa inahusika vipi kwenye kujaza fomu iliyoko mezani?
Baada ya kujaza fomu niliambiwa niondoke wao watalishughulikia suala langu. Hadi naandika hapa sijajulishwa lolote na nimeamua kuendelea kutumia utaratibu wa zamani. TANESCO kumbuka kuwa TTCL iko hivi kwa sababu zamani wahudumu wake walijifanya miungu watu.
Baada ya kuruhusu sekta binafsi kutoa huduma ya mawasiliano hakuna mtu wa kuwabembeleza tena TTCL. Ni kwanini mnashindwa kujifunza kutokana na makosa yalotendwa na taasisi kama ya kwenu?
Leo hii nawapigia simu wanaendelea kunipa kauli za hovyo hovyo! Hakika mmenikera. Eti mtu anatumia line ya huduma kwa wateja lakini anakuwa na kauli chafu
UPDATES:
Tutor B said;
NATAMANI TANESCO WAWE KAMA TTCL
Mwaka jana Nov. 2018 nilienda ofisi za Tanesco wilaya ya Ilemela ili kubadilishiwa matumizi ya umeme kwa sababu natumia chini ya Unit 60 kwa mwezi.
Kwa ujumla huduma zilikuwa mbovu sana kana kwamba wana kisa na mimi. Nilijaza fomu then nikaambiwa nikitaka kuweka umeme tena sitatumiwa token hadi pale nitakaorudi ofisini kwao. Nikakubali na kuondoka.
Hadi naandika hapa nimeishaweka tena umeme na sijaona badiliko lolote.
Udhaifu wao:
Kwanza; Wanafanya kazi kwa kujisikia kwa sababu hawajapata mshindani. Nawashauri wajifunze kwa kile kilichotokea kwa kampuni ya simu pale makampuni ya simu za mkononi yalipoanza kutoa huduma.
Pili; wanauza nguzo wakati nguzo ni mali yao. Iweje wamuuzie mteja nguzo alafu waitumie kwa ajili ya wateja wengine pasipo kumfidia yule alouziwa nguzo?
Sipendi kuandika mengi ila kwa ujumla huduma za Tanesco ni hovyo kabisa kwa sababu hawana mshindani.