TANESCO itafutiwe mshindani wa kibiashara?

TANESCO itafutiwe mshindani wa kibiashara?

Kwa niaba yangu binafsi, familia na kijiji ninachokihudumu naunga mkono hoja mkuu, ligawanye hili lidubwana linaloitwa tanesco, 2/3 ya wafanyakazi piga chini, bakisha engineers tu, idara nyengine zote TANESCO ni waste of space, wawekezaji waitwe waje kuinvest kuanzia kwenye uzalishaji mpaka ugavi, kimsingi kuwe na angalao Matanesco matano. Hapa kijijini kwangu Daslama hihiiii, wanawanchi washalipia service line huu Sasa mwez wa 5 twasubiri eti nguzo hamna "PATHETIC EXCUSE, FROM PATHETIC COMPANY.
 
Kila kitu kinaonekana kuwa ccm inahudumia wananchi unataka mfano gani au unaona inawahudumia nyumbu serengeti?
Ukiniuliza swala la nyumbu Serengeti unakosea.
Mimi nimesema twende kwa mifano, tuangalie sekta ya afya, maji, elimu, kilimo na uchumi.
Utatoa mifano yako kuonesha jinsi chama/ serikali inavyohudumia wananchi katika sekta hizo na mimi nitaonesha ni kwa vipi chama/ serikali kinaua hizo sekta.

Kama upo tayari tuanze
 
Ukiniuliza swala la nyumbu Serengeti unakosea.
Mimi nimesema twende kwa mifano, tuangalie sekta ya afya, maji, elimu, kilimo na uchumi.
Utatoa mifano yako kuonesha jinsi chama/ serikali inavyohudumia wananchi katika sekta hizo na mimi nitaonesha ni kwa vipi chama/ serikali kinaua hizo sekta.

Kama upo tayari tuanze
Hakijaua sekta yoyote kwa sababu chenyewe ndiyo imeanzisha hizo sector toka walivyochukua nchi kwa wakoloni na wakazifikisha hapa japo sio kwa kiwango cha kuridhisha. Ukisema wameua ni kama walizikuta kwa chadema zikiwa imara wakazimalizia.
 
Hakijaua sekta yoyote kwa sababu chenyewe ndiyo imeanzisha
Hizo sekta zimerithiwa kutoka kwa wakoloni mpaka miaka ya 70 Tanzania tulikua tunatumia mtaala wa mkoloni.
hizo sector toka walivyochukua nchi kwa wakoloni na wakazifikisha hapa japo sio kwa kiwango cha kuridhisha.
Viwango tunaweza kuvipima huku mijini vijijini hakuna hata huduma ambayo unaweza kusema kua hii ipo ila si kwa kiwango cha kuridhisha, Singida wamesotea maji muda mkubwa sana sekta binafsi zimejitahidi mno kujenga visima mpaka mbunge akaamua kutumia alichonacho.
Ukisema wameua ni kama walizikuta kwa chadema zikiwa imara wakazimalizia.
Naona hauna mifano dhahiri, ukiingiza CDM katika hiki tunachoongea mimi na wewe hauoni kama ni tatizo ikiwa hata haujui kama mimi ni CDM ama la?
 
Hizo sekta zimerithiwa kutoka kwa wakoloni mpaka miaka ya 70 Tanzania tulikua tunatumia mtaala wa mkoloni.

Viwango tunaweza kuvipima huku mijini vijijini hakuna hata huduma ambayo unaweza kusema kua hii ipo ila si kwa kiwango cha kuridhisha, Singida wamesotea maji muda mkubwa sana sekta binafsi zimejitahidi mno kujenga visima mpaka mbunge akaamua kutumia alichonacho.
Naona hauna mifano dhahiri, ukiingiza CDM katika hiki tunachoongea mimi na wewe hauoni kama ni tatizo ikiwa hata haujui kama mimi ni CDM ama la?
Natolea mfano wa chadema sio kwa sab wewe ni chadema la asha bali ni kwa sab chadema ni chama kikuu cha upinzani
 
Phillipo Bukililo ,

..kwanza tukate mirija yote inayoinyonya damu Tanesco.

..mirija hiyo ni mikataba ya kifisadi baina ya Tanesco na makampuni kama iptl.

..baada ya hapo tutakuwa na nafasi nzuri zaidi ya kuijadili hii hoja yako.

..nimesema haya kwa kuheshimu hoja yako. Ila mimi binafsi napendelea Tanesco iwe na monopoly ktk sekta ya umeme.

.. Natamani Tanesco iwe multinational iweze kutoka Tz na kuwekeza ktk nchi jirani.
Mkuu, hizi issue za mara IPTL mara Harbinder Singh mara PAP mara sijui nini...kwa kweli zinaboa sana
 
Usijidanganye. Hata sasa hivi kunaushindani kwenye kuzalisha umeme. Tatizo ni mikataba yakifisadi ambayo Tanesco imeingizwa na viongozi wa serekali. Na swala la usambazaji ni inefficiency kuwa na makampuni mawili ya kusambaza umeme. Kwana vitu kama national grid ni swala la national security huwezi kuachia makamupuni binafsi kama PAP kuendesha. Sana sana wanaweza ku privataze local distribution kama mkoa kwa mkoa. Nigeria wamefanya hivyo lakini haija saidia. Kwakifupi huwezi kuwa na option ya kupata umeme kutoka makampuni mawili tofaiti kwenye mji mmoja. Hoyo inawezekana kwenye Telco services lakini sio umeme. Sana sana kama bongo wangekua na sheria nzuru basi ingewezekana kipata makampuni yanakuja kukuwekea solar panel kwenye paa zanyumba bila kuzinunua ila unakua unalipia umeme kwa mwezi. Tatizo la hio option ni CAPEX na inaitaji serekali labda iweke tax exemption na sheria za kuweza kuingia na wateja mkataba wa miaka kama kumi. Pia kuna wizi pia.
Mkuu, very local mindset. Nchi zenye uchumi mkubwa kuna wasambazaji na wazalishaji kibao wa umeme. Wewe bado una mawazo yale yale ya national grid. Wewe ni mjamaa kindakindaki.
 
Mkuu, very local mindset. Nchi zenye uchumi mkubwa kuna wasambazaji na wazalishaji kibao wa umeme. Wewe bado una mawazo yale yale ya national grid. Wewe ni mjamaa kindakindaki.

Nakubali kunawazalishaji wengi kwenye nchi nyingi. Ila kwenye usambazaji ndio naona minimun ni inefficient na zaidi makampuni binafsi huwa yanachelewesha uboreshaji wa miundombinu. Sasa nipe jina la kampuni binafsi zinazofanya vizuri katika usambazaji umeme china au marekani maana hayo ndio mataifa yenye uchumi mkubwa duniani alafu ulinganishe na SOE za china.

50d601bfa3586bf20d28584b0a62e302.jpg
 
Nakubali kunawazalishaji wengi kwenye nchi nyingi. Ila kwenye usambazaji ndio naona minimun ni inefficient na zaidi makampuni binafsi huwa yanachelewesha uboreshaji wa miundombinu. Sasa nipe jina la kampuni binafsi zinazofanya vizuri katika usambazaji umeme china au marekani maana hayo ndio mataifa yenye uchumi mkubwa duniani alafu ulinganishe na SOE za china.

50d601bfa3586bf20d28584b0a62e302.jpg
Mkuu pamoja na matatizo yanayoweza kuwepo kwa makampuni binafsi lakini wingi wa makampuni hayo kwa njia moja au nyingine utaondoa kujisahau kwa namna yoyote ile kwa TANESCO. Siasa zimechangia sana katika kukwamisha ufanisi wa TANESCO, wakiongezeka wengine itakuwepo heshima katika uzalishaji na usambazaji. Na ndicho kitu ambacho mwananchi anakitaka.
 
Ndio hivyo Mkuu, hebu vuta picha kama tungekuwa na kampuni moja ya usafirishaji, si watu wangepangiwa siku na muda wa kufanya safari zao?.....Si ingechochea umasikini sana?


Kuna maeneo kadhaa siku za nyuma abiria walikuwa wanapigwa makofi na wahudumu wa mabasi kwa makosa yao wenyewe wahudumu

Ndicho kinachotokea Tanesco sasa
 
Mkuu pamoja na matatizo yanayoweza kuwepo kwa makampuni binafsi lakini wingi wa makampuni hayo kwa njia moja au nyingine utaondoa kujisahau kwa namna yoyote ile kwa TANESCO.


Mikataba yao ya ajira itazamwe upya ikiwezekana wale watu wa usambazaji walipwe kwa idadi ya wateja watakaowahudumia
 
January Makamba aliwahi kuelezea in detail hii issue ngoja nitafute thread
 
Habari zenu guys!

Hili shirika tokea limeanzishwa sijawahi kusikia likipata mshindani , nahisi ndio maana huduma zao ni mbovu na wanafanya kazi kwa mazoea kwa sababu wapo peke yao, kama ttcl ilipata washindani na sasa tunaheshimiana kwa nini Tanesco hana mpinzani kutoka sekta binafsi?
 
Kwakweli....nimewahi nafasi najua ina wenyewe hii.
 
Ni nchi gani ambayo Ina makampuni independent ya umeme ambayo si mali ya serikali kwa namna moja au nyingine?

Biashara ya ufuaji umeme, popote duniani, ni huria ila sababu ya gharama kubwa za kuendesha inabaki kuwa a Monopoly market. Hata nchi zenye umeme wa uhakika sio kwamba zina ushindani bali wamewekeza heavily kwenye mashirikia yao.

Hakuna nchi hata moja, narudia, hata moja yenye ushindani kwenye mambo ya umeme Kama ilivyo kwenye masoko mengine.

So, TZ kama nchi zinginge, hakutakuwa na ushindani kwenye ufuaji na usambazaji umeme.
 
Elimu yetu hovyo inazalisha wataalam wasiokidhi wanashindwa kubuni na kuendeleza tasisi hucka
 
Back
Top Bottom