TANESCO: Heri ya Sikukuu ya Pasaka

TANESCO: Heri ya Sikukuu ya Pasaka

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dkt. Tito E. Mwinuka kwa Niaba ya Bodi ya Wakurugenzi, Menejimenti na Wafanyakazi wa TANESCO anawatakia nyote Heri ya Sikukuu ya Pasaka.

Aidha, anawasihi Wateja na Umma kuwa waangalifu na kuwa mbali na miundombinu ya umeme hasa katika kipindi hiki cha mvua, na kutoa Taarifa kwa TANESCO mara inapotokea hitilafu.
View attachment 496739
IWE SIKUKUU YA HERI NA FURAHA KWETU SOTE
Swali langu namba 67 vipi ? Tunahitaji majibu wakazi wa huku.
 
Nawatakia heri nyote.
Tanesco iko vizuri zaidi na zaidi. Niwatie moyo msikatishwe tamaa na maneno ya wapinga maendeleo wanaoibuka kila uchwao. Kwa sisi tulioishi tangu enzi za vibatari tunajua Shirika hili limetoka wapi kwani tumeshuhudia mabadiliko makubwa sana na mengi kwa vipindi tofauti. Niwaambie tu kila zama zina changamoto zake na ninyi sasa ni wakati wenu hivyo msikwazwe na wanaowazushia na kutafuta huko mitandaoni kuwapunguzia kasi yenu.

Tuendelee kujenga nchi yetu.
Nawapenda nyote
 
Huku DSM ILALA, Ulongoni kwenda Bangulo mmeweka nguzo za umeme na umeme upo ila umepita barabarani tu bila kuunganishwa kwa watumiaji. Sasa hiyo si biashara kichaa, umeme upo ila humuunganishi kwa wateja!!! Kwani yamekuwa mapambo ya barabara. Inaudhi kweli. Ukifuatulia utasikia tuna order za siku nyingi nyie subirini tu.
 
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dkt. Tito E. Mwinuka kwa Niaba ya Bodi ya Wakurugenzi, Menejimenti na Wafanyakazi wa TANESCO anawatakia nyote Heri ya Sikukuu ya Pasaka.

Aidha, anawasihi Wateja na Umma kuwa waangalifu na kuwa mbali na miundombinu ya umeme hasa katika kipindi hiki cha mvua, na kutoa Taarifa kwa TANESCO mara inapotokea hitilafu.
View attachment 496739
IWE SIKUKUU YA HERI NA FURAHA KWETU SOTE
Ahsante sana mkuu, ila sisi wananchi wa mtaa wa oysterbay hatujaunganishwa na umeme, tumeenda tanesco wilaya bila majibu yakueleweka, mara tukaambiwa tujiorodheshe,tukajiorezesha hafi kufikia idadi ya watu 30,baadae tunaambiwa hatupo kwenye mpango, akajitokeza miongoni mwetu wa kvuta nguzo sita,baadae wakasema hatuwezi kupeleka kwa mtu mmoja, duu hadi tumechoka
 
Ahsante sana mkuu, ila sisi wananchi wa mtaa wa oysterbay hatujaunganishwa na umeme, tumeenda tanesco wilaya bila majibu yakueleweka, mara tukaambiwa tujiorodheshe,tukajiorezesha hafi kufikia idadi ya watu 30,baadae tunaambiwa hatupo kwenye mpango, akajitokeza miongoni mwetu wa kvuta nguzo sita,baadae wakasema hatuwezi kupeleka kwa mtu mmoja, duu hadi tumechoka
Mkoa.....
wilaya.....
osterbay karibu na nin.....
namba ya simu

Tunaomba taarifa hizo

Sent from my SM-J200H using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom