TANESCO: Heri ya Sikukuu ya Pasaka

TANESCO: Heri ya Sikukuu ya Pasaka

Heri ya Pasaka kwenu pia. Hongereni kwa jitihada zenu pamoja na kuwa mnafanya kazi katika mazingira magumu sana yanayosababishwa na mikataba ya kifisadi.

Msikae kimya kuhusu kuendesha shirika kwa hasara kubwa inayosababishwa na TANESCO kununua unit moja ya umeme kwa shilingi 544 na kuuza unit hiyo moja kwa shilingi 279.

Hili ni la kushughulikia haraka ipasavyo ili kuhakikisha uwepo wa TANESCO kwa miaka mingi ijayo vinginevyo mtapotea katika anga za Tanzania na hivyo kuzuka vikampuni uchwara ambavyo vitatulangua sana Watanzania na umeme kuwa wa bei kubw sana na hivyo Watanzania wengi kushindwa kumudu gharama kubwa.

Pia muangalie uwezekano wa kujikita kwenye umeme wa jua ambao bila shaka unaweza kushusha sana gharama zenu za uendeshaji kwa kiasi kikubwa.

I hope to see you on this forum every now and then to share your ideas with your fellow Tanzanians and also to learn from us.

Happy Easter Sunday.
hili wazo zuri sana lazma [HASHTAG]#tanesco[/HASHTAG] wataipokea tu jinsi walivyojipanga..
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mbona mmeng'ang'ana kutaka namba za simu za watoa taarifa maeneo yaliyokatika umeme? Mtu kataja hadi eneo bado mnataka namba yake....!!
BTW.. kuna uzi nilianzisha hapa siku kadhaa nikilalamikia TANESCO Mbagala. Kupitia uzi huu naomba nipatiwe majibu ya sababu ya kukatika umeme mara kwa mara hasa maeneo ya Barabara ya Charambe kuelekea Mvuti. Kwa leo umeme upo tangu jana haujakatika ila nina shaka hali itarudi kama zamani.

Asante!
Kuna miradi mikubwa inayofanyika ya uboreshaji Huduma ya umeme Jijini Dar es Salaam, Vituo vya kupoza na kusambaza umeme vya Mbagala na Kurasini vinapata umeme wa msongo wa kilovolti 33, kutokana na ongezeko la Watu na shughuli za Kiuchumi maeneo ya Mbagala, Kigamboni na Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani, kumepelekea upatikanaji wa umeme kwenye maeneo hayo kuwa na matatizo kidogo kwani vituo vinavyosambaza umeme kwenye maeneo hayo kuzidiwa
ndio maana Serikali kupitia TANESCO inaviboresha vituo hvyo vya Kupoza na Kusambaza Umeme kwa kuviongezea uwezo mkubwa wa Kilovoti 132. Maboresho hayo yanategemewa kukamilika mwaka huu hivyo kuondoa tatizo la umeme kuwa mdogo na kukatika katika kwa umeme maeneo hayo.

TANESCO inawaomba Wananchi kwa ujumla, kuwa wavumilivu wakati juhudi za kukamilisha Miradi ya uboreshaji umeme
zikiwa zinakaribia kukamilika.
 
Hapa Moshi mmekata umeme tukiwa kanisani misa inaendelea.

Narudi nyumbani soweto baada ya misa hakuna umeme nyumbani hapa SOWETO, WIRELESS
Niko wireless pia mnara wa voda
 
Habari Tanesco,
Kuna mradi wenu chini ya REA unapitia Kinondo/Malolo kuja Mabwepande Viwanja vya Manispaa Block 14,Mlitutangazia mtaleta umeme mwezi wa pili mpaka sasa tunaenda mwezi wa tano hatujapata wakazi wa huku,nguzo zimeishia njiani ni kama nguzo 7 zifike kwenye makazi mmeachia hapo hapo,naomba majibu ni lini mtatufikishia umeme huku Block 14 viwanja vya Manispaa ya kinondoni Mabwepande?
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dkt. Tito E. Mwinuka kwa Niaba ya Bodi ya Wakurugenzi, Menejimenti na Wafanyakazi wa TANESCO anawatakia nyote Heri ya Sikukuu ya Pasaka.

Aidha, anawasihi Wateja na Umma kuwa waangalifu na kuwa mbali na miundombinu ya umeme hasa katika kipindi hiki cha mvua, na kutoa Taarifa kwa TANESCO mara inapotokea hitilafu.
View attachment 496739
IWE SIKUKUU YA HERI NA FURAHA KWETU SOTE
 
TANESCO wilaya mpya ya Busega mnakuja lini? Tunahitaji huduma yenu sana. Nipo karibu na jengo jipya la Halmashauri.
 
Tanesco sisi huku Mbezi Beach hatuna Umeme tokea asbh
 
Kuna miradi mikubwa inayofanyika ya uboreshaji Huduma ya umeme Jijini Dar es Salaam, Vituo vya kupoza na kusambaza umeme vya Mbagala na Kurasini vinapata umeme wa msongo wa kilovolti 33, kutokana na ongezeko la Watu na shughuli za Kiuchumi maeneo ya Mbagala, Kigamboni na Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani, kumepelekea upatikanaji wa umeme kwenye maeneo hayo kuwa na matatizo kidogo kwani vituo vinavyosambaza umeme kwenye maeneo hayo kuzidiwa
ndio maana Serikali kupitia TANESCO inaviboresha vituo hvyo vya Kupoza na Kusambaza Umeme kwa kuviongezea uwezo mkubwa wa Kilovoti 132. Maboresho hayo yanategemewa kukamilika mwaka huu hivyo kuondoa tatizo la umeme kuwa mdogo na kukatika katika kwa umeme maeneo hayo.

TANESCO inawaomba Wananchi kwa ujumla, kuwa wavumilivu wakati juhudi za kukamilisha Miradi ya uboreshaji umeme
zikiwa zinakaribia kukamilika.
Bila taarifa kwa Umma na kwa njia rahisi itakayowafikia wengi ni bure na mtalaumiwa sana tu.
 
TANESCO njooni mchukue nguzo moja jirani na kwangu kuna nguzo mmeweka lkn haina kitu, imewekwa kimakosa. Tulio jirani na nguzo hiyo wote tuna umeme kutoka nguzo zingine. Nguzo ipo inanyeshewa.

Nipo Mbezi barabara ya Goba, karibu na Njiapanda ya TEGETA, opp na CORNERSTONE BAR.
Mkuu wewe una nguzo za ziada wakati huku sisi tunazitafutaaaa!!! Hahaaaaa watakuwa wamekusikia, tanesco wenyewe. Mimi niko mkuranga mkoa wa pwani!!yaani nimelipia toka january kila siku subiri mwezi ujao
 
Mkuu wewe una nguzo za ziada wakati huku sisi tunazitafutaaaa!!! Hahaaaaa watakuwa wamekusikia, tanesco wenyewe. Mimi niko mkuranga mkoa wa pwani!!yaani nimelipia toka january kila siku subiri mwezi ujao
Hapana hii nguzo sio yangu na wala sijailipia Mimi. Sijui TANESCO waliiletaje hapa, ipo pembeni ya barabara! Waje tu kuichukua.
 
Mbona mmeng'ang'ana kutaka namba za simu za watoa taarifa maeneo yaliyokatika umeme? Mtu kataja hadi eneo bado mnataka namba yake....!!
BTW.. kuna uzi nilianzisha hapa siku kadhaa nikilalamikia TANESCO Mbagala. Kupitia uzi huu naomba nipatiwe majibu ya sababu ya kukatika umeme mara kwa mara hasa maeneo ya Barabara ya Charambe kuelekea Mvuti. Kwa leo umeme upo tangu jana haujakatika ila nina shaka hali itarudi kama zamani.

Asante!
Namba za simu za mameneja wa Wilaya (116) wa TANESCO kwa kila Mkoa
 
Tanesco wazee wa fiksi kalamazooo.....

OvA
 
Back
Top Bottom