Tamthiliya: Challenge Made - Sehemu ya 1

Tamthiliya: Challenge Made - Sehemu ya 1

TAMTHILIA: ZAWADI.

MWANDISHI: WINIFRIDA FRANCIS THOBIAS

SEHEMU YA : 12 $ 13.

WHATSAPP NO :0746115688.

Baada ya kupona kwa Mfalme, Zawadi alikumbuka ahadi aliyoiweka kwa moja kati ya afsa usalama aliyekuwa chini ya john John na hapo ndo alianza kuwaza kwasababu siku zote Zawadi anapotoa ahadi huwa anatimiza, lakini kwa ahadi aliyoitoa kwa John John ilikuwa ikimpa mashaka sana lakini hakuwa na jinsi kwani giza lilipoingia Zawadi alienda katika eneo ambalo ndo amekuwa akikutana na afisa yule wa usalama ambae yupo chini ya John John lakini ajabu safari hii John John ndo alikuwepo yeye mwenyewe katika eneo lile. Zawadi alishangaa sana lakini hakuwa na haki ya kuhoji hayo yote, alichofanya ni alimwambia tunaweza kwenda sasa mana baba yangu ameshapona ni muda wa mimi kuitimiza ahadi yangu. Lakini John John akamwambia huwezi kwenda popote Zawadi kwasababu kazi yako utaifanyia hapahapa, zawadi alishtuka sana na akamuuliza John John "ni kwanjia gani ntaweza kufanya kazi hiyo hapa kwetu ?' John John akamwambia zawadi cha kwanza inakubidi ujalibu kuwa hadithia vitu vizuri ambavyo wewe umekutana navyo kule, lakini pia waelezee jinsi watu wakule wanavyo jali na kuwathamini watu wengine ili tuone kama watabadili fikra zao na kutaka kuishi na wenzao . Zawadi alikubaliana na John John na kweli siku iliyofuata zawadi alipoulizwa na Mfalme juu ya yeye kutekwa yeye alielezea Uzuri tu alio kutana nao kule alipopelekwa na kuwasifia sana watu wakule lakini Mfalme akamwambia ' inawezekana watu hao kwao nipazuri sana lakini mioyo yao ni michafu zaidi kwasababu kama wangekuwa ni watu wazuri kwanini wakuteke inabidi uache tu habari hizo Zawadi mana pengine watu wakijua wanaweza hata kuku tenga.
Zawadi aliyasikiliza sana maneno ya baba yake na hapo ndo aligundua kweli ni ngumu kubadilisha ufahamu wa watu wao na baada ya zawadi kugundua hilo alimwambia John John juu ya msimamo wa baba yake lakini John John alimshawishi angalau atafute watu wakumuunga mkono juu ya jambo hilo ili iwe ngumu kwa watu wanaotaka kumpinga.
Kweli Zawadi akaanza kuwashawishi watu wanao mzunguka hasahasa vijana kama yeye, lakini vijana hao walimchukulia yeye kama msaliti na kusambaza taarifa za kuwa zawadi anampango mbaya na watu wa Ufalme wa Wetu kwa sababu amekuwa akiwashawishi watu kuweza kumuamini na kuwaamini wageni walio mteka yeye, jambo lililo wafanya watu kuweza kumtenga na kumuona mbaya na wala hajali kuhusu wao yeye anachojali ni wageni hao na sio watu wake.
Mfalme alijisikia vibaya sana aliposikia Uvumi huo kuhusu Zawadi, na hapo ndo akamwambia zawadi ' kitendo cha mimi kukukataza wewe kuacha kuendelea kuongelea habari za watu usio wajua vizuri ulikichukuliaje, kwasababu nikama vile unajali sana kuhusu hao zaidi yetu na ndio maana unajalibu sana kuwashawishi watu ili wawakubali watu waliokuteka na wawapende kama unavyo wapenda wewe lakini mimi hujaniweka wazi kabisa lengo lako ninini juu ya watu hao. Lakini pia kama walikuachia kwa masharti niambie tu ili tujue jinsi gani tunatimiza sharti lao na si kuwatumia watu wako kwa faida yao.
Zawadi alijisikia vibaya na kuona hayo yote yanayo mtokea ni kwasababu ya John John kama si yeye baba yake asingethubutu kuongea maneno makali hivyo juu ya binti yake, hivyo zawadi alienda moja kwa moja mpaka wanapo kutana na John John na baada tu ya John John kufika mahala hapo zawadi alimwambia sipo tayari kushirikiana na nyie kwasababu kila nnavyojiweka karibu na nyie napata tabu tu zaidi.
John John alichukia sana kwasababu aligundua kuna baadhi ya maadui wakubwa tu nchini wamekuwa wakienda kujificha katika maeneo yao jambo ambalo ni hatari sana kwa nchi hasa pale ambapo baadhi ya watu wa Zawadi wakiungana na makundi hayo.
Lakini upande wapili zawadi baada ya kurudi katika ufalme alibakia kuwa mpweke sana kwasababu kila mtu katika ufalme wa Wetu alikuwa akimchukia yeye kwa kampeni alizo kuwa akiwafanyia watu wa mjini. John John na yeye baada ya kuona mambo yanazidi kuwa magumu, na magaidi wanazidi kuingia katika kisiwa kile na kutoka kila siku alijua kabisa jambo hilo litakuwa shida kubwa baadae hivyo alicho kifanya alitafuta nyumba moja kubwa sana na kuanza kuwateka watu wa ufalme wa Wetu kidogokidogo na kuwaweka katika nyumba hiyooo na kuwapa elimu zaidi juu ya mambo mbalimbali waliyo kuwa hawayajui. Kilasiku watu walipokuwa wakitekwa lawama zote alikuwa akipewa zawadi jambo lililo mfanya zawadi akose marafiki lakini pia kutengwa na familia yake nzima yaani Mfalme, Malkia na watu waliokuwa wamesalia katika Ufalme huo wa wetu. Zawadi alipoona kila siku watu wake mwenyewe wana mtenga alienda katika eneo ambalo mara nyingi watu wa john John huwa wanakaa hapo , lakini kwa bahatimbaya sio John John wala watu wake walikuwa wakipatikana katika eneo hilo na kibaya zaidi aliporudi katika ufalme siku hiyo watu wote walikuwa wametekwa kama wengine, lakini chaajabu kunawatu tofauti na wafanyakazi wa John John walikuwa wakiwatafuta watu wa ufalme huo na kwambali aliwasikia wakiwa wanakili juu ya mpango wao wa kuwachukua watu wao na kuwatumia watu hao kuigeuka nnchi yao, na hapo ndo zawadi aligundua kuwa ni vizuri watu wake kuondoka katika eneo lile na wala hata hakujisikia mnyonge tena kama awali bali alichukua maamuzi ya kujilengesha kwa majambazi wale na kweli wakaingia katika mpango wake na wakamteka na baada ya muda kidogo wote wakampenda na kumuamini zawadi kwa kila jambo na zawadi akapewa cheo cha usimamizi wa eneo lile na alipoona watu wapale hawamtilii tena mashaka alienda tena kujalibu kukaa katika eneo lile la baharini na kwabahati nzuri siku hiyo John John alikuwepo na alipomuona zawadi alimkumbatia na kumwambia inabidi twende wote kwasababu mahali hapa sio salama tena, lakini zawadi akamwambia John John usijali kabisa mimi nitakuwa katika eneo hili kukusaidia kuwakamata hawa majambazi kwasababu wanavyo onekana ni watu hatari sana na bila ya kuwa waangalizi jambo lolote baya laweza tokea, bora mimi wamenielewa ntaendelea kuwa nao mpaka mtakapo wakamata. John John hakutaka kuniacha pale Zawadi lakini kwakuwa zawadi aliomba sana John John ilimbidi aondoke japo kiukweli alionekana ameanza kuvutiwa sana na zawadi kwasababu jinsi alivyokuwa anawasiwasi na alivyo mkumbatia haikuonyesha kuwa ni wasiwasi wakawaida kwani alikuwa na Shahuku sana ya kumuona zawadi lakini upendo uliakisi kwa namna ambavyo alimuangalia zawadi aliweka wazi juu ya hisia zake kwa zawadi.
Zawadi alifurahi sana kuona angalau John John anaonyesha kumjali sana kwani binafsi awali alihisi kuwa John John aliwachukua watu wote nakuamua kumtelekeza yeye kwa makusudi jambo ambalo sio kweli kwani John John anamjali sana na kumthamini na ndio maana bila kujali alirudi tena kisiwani kwaajili yake tu lakini pia akampa na nafasi ya upendeleo ya yeye kuweza kusikia sauti za wazazi wake kupitia simu jambo lililo mfanya Zawadi afurahi sana.
Sikumoja wakati zawadi akielekea zake kulala katika himaya hiyo ya majambazi , moja kati ya jambazi aliwatuma watu wake, wakaenda kumteka zawadi na kisha wakampeleka kwake na yeye akambaka Zawadi bila huruma, jambo lililo pelekea mkuu wa majambazi hao kumuua jambazi yule kwani yeye pamoja nakuwa ni jambazi ila alikuwa akimchukulia zawadi kama dada yake wakike hivyo hakufurahishwa na kitu kile kilicho tokea. lakini pia baada ya zawadi kubakwa Zawadi alitawaliwa sana na hasira kiasi cha kuamua kuwauza majambazi hao kwa muda mfupi na kweli baada ya muda wa miezi sita zawadi akaongea na mmoja wa maafisa wale wa Usalama wa Taifa na kumpa taarifa zote kuhusu majambazi hao na jinsi ya kuweza kuvamia himaya yao John John alishangaa kwanini Zawadi hakutaka kukutana na yeye, lakini hakujali sana kwani alihisi zawadi hakutaka tu kumsumbua, lakini baada ya mfanyakazi wake kukutana na zawadi aliporudi kwa bosi wake alibakia kumuonea huruma tu John John kwa alicho kiona kwa Zawadi, lakini John John alipo muona afisa wake amerudi na hana raha alimuuliza 'zawadi yuko sawa?" Na afisa huyo alimjibu ndio yupo sawa lakini, John John alishtuka sana na kumwambia malizia lakini ninini, na ndipo afisa huyo akamwambia muheshimiwa zawadi ni mjamzito kwasasa na mimba yake ni kubwa. John John alishtuka sana na kukosa nguvu hata za kusimama kisha akamwambia afisa huyo amekwambia ni ya nani? Afisa huyo alimjibu tu kuwa kweli ni mjamzito lakini hataki kuongelea kuhusu mimba yake kabisa . John John alichukia sana na kumtuma afisa wake apeleke habari makao makuu ili wakavamie haraka.
Kweli baada ya muda watu walijipanga na kwenda kuvamia eneo hilo na kumkamata mkuu wa majambazi hao pamoja na watu wake na kisha wakaingizwa kwenye boti kupelekwa mjini kuhukumiwa kwa ujambazi wao, lakini baada ya boti ya waalifu hao kuondoka boti iliyofuata ilikuwa niya maafisa pamoja na zawadi , lakini chaajabu Zawadi aligoma kuingia kwenye boti hiyo na kuwaambia nyie mnaweza kwenda tu hakikisheni wanaadhibiwa wale ni watu hatari sana. John John alipata hasira sana na kumuuliza 'hivi wewe huelewi maana ya twende au, unataka tufanyejee tukufunge pingu ndo utaungana na sisi au vip . Zawadi alimwambia hapana nyie nendeni mimi ntaishi hapa na sitasababisha matatizo yoyote niaminini. Lakini mmoja kati ya maafisa usalama akamwambia zawadi twende kwani huniamini c tulisha ongea lakini zawadi alimwambi nimebadili mawazo , john akamwambia Zawadi kwani wewe upoje, kati yetu hakuna alie kwambia uwe na mahusiano na majambazi haya sasa wamekupa mimba wanaenda jela sisi tupo hapa tu kukusaidia unatuona wajinga hutaki kuongozana na sisi kwanini lakini unafanya hivyo.
zawadi alijisikia vibaya kwa maneno makali yaliyotoka katika kinywa cha john john na hapo ndo zawadi alikimbilia msituni ili kurudi katika himaya yao ili akakae huko huko ambako watu hawata muhukumu kwalolote lile lililotokea maishani mwake, John John alishangazwa sana na tabia ya Zawadi lakini kwasababu alikuwa na hasira nae juu ya mimba aliyokuwa ameibeba aliwaambia maafisa usalama tuondokeni lakini moja kati ya maafisa hao aliomba kubakia pale na zawadi lakini John John aliwaambia ni amri wote tunaondoka na kweli wakaondoka na kumuacha Zawadi pale. Zawadi alikuwa ni binti jasiri kwaaina flani hivi ya kutisha kwasababu aliishi katika msitu bila hata kuhofia kitu chochote japo alikuwa akishinda kulia na kulala kulia kila alipokuwa akiliangalia tumbo lake.
Sikumoja wakati John John alipoenda kumuhoji jambazi mkuu, jambazi huyo alimuuliza kwanza hali ya zawadi, lakini yeye alimwambia kabakia kule mliko mkuta awali. jambazi huyo alichukukia sana na kumwambia John John nyie hamna huruma kabisa nyie mnamuacha binti wawatu kule na nimjamzito pamoja na yeye kumisaidia, lakini John alimwambia hatukumtuma akafanye umalaya kule ilikuwa ni kufanya kazi tu ya nyie kukamatwa. jambazi huyo akamkaba shingo John John na baada ya watu kuja kumtoa mikono jambazi yule shingoni maw John John , jambazi huyo akamwambia John John hata sikumoja usimtukane zawadi kwasababu ntaakuua unamuita malaya wakati kama sio yeye kujitoa kumisaidia nyie kutukamata sisi, leo angekewa hajabakwa na kupata ile mimba lakini kwasababu yenu yote yametokea halafu mnamlaumu, mashetani wakubwa nyie. mtu hakuwa analala pamoja na mimba yake , anafanya kazi ngumu yote nyie mfanikiwe halafu leo kwenu hana thamani, kweli nimeamini nyie ni watu wabaya sana msio faaa kabisa hata kuwa na rafiki kama Zawadi.
John John alishtuka sana baada ya kusikia maneno hayo na hapo ndo akatoa amri jambazi huyo aingizwe gerezani kisha akamfuata afisa aliyekuwa karibu sana na zawadi kimawasiliano kisha akamwambia niambie kila kitu kuhusu mimba ya Zawadi, na hapo ndo afisa huyo alimwambia John John kweli zawadi alibakwa na aliembaka aliuliwa na jambazi tulie mkamata kwasababu yeye siku zote anamchukulia Zawadi kama dada kwake.
wakati John John anagundua hilo zawadi akampigia simu afisa huyo huku analia akimpa taarifa juu ya kuumwa kwake....

USIKOSE SEHEMU YA 14 $15
Well done!! Kitu inazidi kunoga John John, anatatizo la wivu anaona Kama kawahiwa flani ivi
 
TAMTHILIA : ZAWADI.

MWANDISHI: WINIFRIDA FRANCIS THOBIAS

SEHEMU : 14 $ 15

WHATSAPP NO: 0746115688.

baada ya john John kugundua ya kuwa Zawadi anaumwa, haraka alifanya mpango wakumpata daktari na kuanza safari ya kwenda kumsaidia Zawadi, lakini kwabahati mbaya walichelewa kwani walimkuta zawadi ameshajifungua tena akiwa mwenyewe na mtoto yuko pembeni analia wakati yeye amepoteza fahamu kutokana na kutokwa damu nyingi wakati wa kujifungua. haraka Daktari alimsafisha mtoto nakumbeba, John John na yeye akambeba zawadi na kuanza rasmi safari yao ya kutoka kisiwani na kwenda mjini kumpeleka zawadi hospitalini, walipofika hospitalini zawadi alipata matibabu na baada ya muda zawadi alipata nafuu, na alipo amka alimuuliza Daktari aliyekuwa akimuhudumia ' samahani wewe ninani, na hapa nime fikaje mana nakumbuka mara ya mwisho nilikuwa kwetu'. Daktari akamwambia kweli mara ya mwisho ulikuwa kwenu , na sisi tulikuja kukuchukua kwasababu ulimpigia simu moja kati ya maafisa wetu ukaomba msaada kwani muda wako wa kujifungua ulikuwa ushafika na hapo ndio mimi na John John tukakufuata kwalengo la kuja kukusaidia wakati wa kujifungua lakini kwa bahati nzuri tukakukuta umesha jifungua na mtoto wako alikuwa salama. Shida ilikuwa kwako kwani tulikukuta umepoteza fahamu na kukuhudumia kwapele ilikuwa ngumu kwasababu ulihitaji huduma bora zaidi na uangalizi wa hali ya juu na ndio maana mimi pamoja na John John tulikuchukua na kukuleta hapa.
Zawadi aliwaambia Daktari natumaini wazazi wangu hawajui kuhusu mimi Daktari. lakini Daktari akamwambia Zawadi utatusamehe kwasababu kwa hali tuliyo kukuta nayo kule, hakukuwa na jinsi yeyote ya kuepuka kuwaambia wazazi wako ukweli, hivyo John John aliwaambia na hivi sasa wako karibu kufika hospitalini pamoja na John John. Zawadi alimbeba mtoto na kumwambia Daktari yeyote atakae kuulizia mwambie mimi nimetoroka na mwanangu. Kabla Daktari hajamjibu sauti ya mtu kutoka mlango ilisikika ikimwambia zawadi lakini hujatoroka bado na tumefika. Zawadi alipogeuka nyuma kuangalia ninani aliye kuwa pale na ndipo alipomuona Mfalme na Malkia mbele ya macho yake, na palepale wakamkumbatia na kumwambia pole binti yetu kwa yote uliyo yapitia, wala usijifiche na mtoto wako eti kwasababu ulibwakwa kwani kwapamoja tutamlea kwa upendo atakuwa na siku moja mwanao atakuja kukusaidia jivunie yeye wala usimtenge na ulimwengu. Zawadi akilia sana na kumwambia Malkia pamoja na Mfalme ya kuwa Kamwe siwezi kumtenga kijana wangu nitamlea vizuri atakuwa na heshima na adabu lakini pia atakuwa mtoto anayetenda matendo mema sitaruhusu afe kama baba yake bali atakufa kama shujaa.
John John alitabasamu baada ya kuona ujasiri wa zawadi , lakini pia akampa taarifa Zawadi ya kuwa rais nataka kumuona na nimuhimu sana kwayeye kwenda iliakapate kuimba msaada juu ya mahitaji yote ambayo watu wake watahitaji kwasasa. Malkia na Mfalme walimwambia Zawadi na kabla hujaenda huko inabidi ukakutane na watu wako ili ujue wanahitaji nini, na baada ya hapo unaweza tu kwenda na kupeleka mahitaj hayoo kwa muheshimiwa rais. Zawadi alishangaa sana na kumuangalia john John kisha akawauliza Malkia pamoja na Mfalme mmewezaje kumuelewa John John kwaharaka hivyo kwasababu mnajua kilakitu kuhusu huku tayari kwannavyo waona. Malkia akamwambia Zawadi ni Mwaka sasa binti yangu tumejifunza mambo mengi sana kwasasa na tunatamani kufidia ualifu wote walioufanya mababu zetu juu ya ndugu zetu wenyewe bila ya wao kujua na hata hivyo kunataarifa mpya natamani kukwambia binti angu, Zawadi akamuuliza ni taarifa gani mama ,"ukweli ni kuwa Zawadi sisi kwasasa tunajua kusoma na kuandika lakini pia watoto wote wameanzishwa hule chini ya usimamizi wa John John akiongozwa na serikali.
Zawadi alimuangalia sana John John nakumwambia asante san, japo mimi nimefundishwa hayo yote na kaka yangu japo ni jambazi ila nampenda sana na natumaini ipo siku mtampa nafasi ya kutoka nnje akiwa kabadilika tabia. John John alimuangalia sana Zawadi na kumwambia sio dhambi kumpenda jambazi unaweza kumsubiria ukipenda, lakini Zawadi akamwambia tatizo sijui utamuachia lini mana unahasira nae sana. John John alimwambia zawadi ungemficha basi siku ile na ukabakia nae kulekule kisiwani si ni raha sana kumuona. Zawadi alicheka sana na kumwambia John John mbona kama unachuki sana na mimi lakini John John akamwambia kiasi tu. Mfalme aliingilia katikati ya ugomvi wao kwakuwaambia mtoto amelala na msipo acha kelele zenu ndo ataamka na asilale tena, kisha Malkia na Mfalme wakatoka nnje ya chumba alichopo zawadi huku wakiwa wanacheka kwasababu waligundua kuwa John John amesha mpenda binti yao zawadi na anawivu na kila kitu hata visivyo kuwa na maana. Lakini wakati John John amekaa katika chumba kile na zawadi na wote wakiwa kimya huku wakiangaliana kwa hasira Daktari aliingia na kumwambia zawadi ya kuwa mtoto anaitwa nani ? Zawadi akamuuliza Daktari chagua tu wewe unaweza kumuita John au jina lako pia sio mbaya. John John alimuangalia Zawadi lakini hakuongea chochote na ghafla aliingia afisa ambae ni rafiki wa karibu sana na Zawadi na alipo ingia tu alimuangalia mtoto na zawadi moja kwa moja bila kugeuka nyuma hivyo hakujua kuwa bosi wake yuko pale. Daktari aliuliza kwahiyo nikamuandikishe mtoto kwajina la john, afisa alimuuliza zawadi kwani umempa jina la john mtoto . Zawadi akamwambia mi nimemwambia Daktari achague jina la John au la kwake mwenyewe ampe mwanangu. afisa alicheka sana na alipo geuka alimuona bosi wake John John na hapo ndo zawadi akamuuliza kwani we unaonaje au nikosa pia kumuita mwanangu John . afisa alimwambia itapendeza sana akiitwa John John John , zawadi alicheka akijua ni utani wa kawaida lakini John John aliwauliza kwani mimi ndio baba wa mtoto mpeni majina ya baba yake lakini zawadi akamwambia nilikuwa nakutania tu mbona unaonekana kuchukia? John John hakumjibu Zawadi alichofanya aliondoka eneo lile na Daktari akamuuliza zawadi 'kwahiyo aitwe John?' lakini zawadi alimwambia hapana kisha akamuuliza rafiki yake yule afisa unaitwa nani kwani , afisa akawambia naotwa elius Steven na zawadi akamwambia Daktari basi mwanangu aitwe Steven lakin elius akamwambia bora aitwe Jofrey elius Steven, mimi nikae kama baba yake kwasababu baba ake hatumjui jina. Zawadi alifurahi sana na kumshukuru elius kisha akamwambia Daktari kamsajili kwa majina hayoo. Daktari alienda na kujaza kadi y mtoto ili waweze kuruhusiwa wakiwa na kadi hiyooo. Baada ya usajili Daktari alirudi hodini ili kumpa Zawadi kadi ya mtoto lakini mlangoni alikutana na John John na alimpa taarifa zawadi anavaa hivyo Daktari huyo alimpa John John kadi ya mtoto na baada ya dakika chache Zawadi alitoka pamoja na mtoto na safari ya kumpeleka zawadi katika nyumba ambayo watu wote waliotoka katika Ufalme wa Wetu wanaishi hapo , Nabaa ya kufika mahali hapo watu walifurahi sana baada ya kumuona Zawadi na mwanae, kisha wakamuomba msamaha Zawadi kwasababu mara ya mwisho walimuacha kisiwani wakiwa na kinyongo nae , kwani walihisi kuwa anawageuka wote kwasababu ya John John. lakini zawadi aliwaambia yeye amewasamehe na hawakufanya kosa pia kutilia mashaka matendo yake kwa sababu pale ndo nyumbani kwao hivyo anapotokea mtu wa kuwashawishi waache kuishi kwao na waende kwa watu wasio wajua lazima wawe vile. Mtu mmoja akamwambia Zawadi wewe una moyo wakitofauti sana lakini pia wewe ni muelewa kwasababu pamoja na sisi kuwa wabaya kwako siku zote unatuelewa sana nakupenda sana Zawadi wetu. Zawadi alimsogelea mtu yule na kumbusu kisha akamwambia nakupenda pia wewe na kila mtu hapa. Lakini mtu mwengine akasema Zawadi unamiaka ishirini kwa sasa lakini du kama mzee vile kwa majukumu unayobeba, zawadi akamwambia toka ujue kuhesabu sasa, akamjibu na hesabu hadi Nyota. Watu walicheka sana kwa furaha huku machozi yakiwamwagika jambo lililo mfanya john John kumwaga machozi kwa sababu kweli wao wanaishi vizuri zaidi ya maisha waliyo kuwa wanaishi wakina Zawadi awali lakini chaajabu wakina Zawadi wanaelewana hata wanapokoseana, na maisha yanaendelea tena kwa furaha wakati huo huku walipo wao John John mtu akikosewa na mtu anakuchukulia uadui kabisa na mwingine anapokukosea anasahau kabisa kuna kuomba msamaha.
Zawadi aliwaambia sasa tunalia nini, tufute machozi na tupange sasa kesho naenda kumwambia ni rais . Watu walimwambia Zawadi angalau ungepumzika kwanza, lakini zawadi aliwaambia ntapumzika pale sisi tutakapo kuwa nauhakika wakuishi na kuendesha maisha yetu bila ya tabu yeyote.
Watu walifurahi sana na moja kati ya watu hao alimwambia Zawadi mi naona sio vibaya kama tutaendelea kuishi kule kwetu wakati serikali ikiendelea kutufanyia mabadiliko kule, lakini mwingine alimwambia Zawadi baadhi ya watoto hapa uwaoni kwasababu wanaenda shule jambo ambalo kule kwetu ni ngumu kwa watoto kupata elimu kwasababu hakuna shule, lakini mwingine akamwambia Zawadi hatuwezi kuitegemea serikali kwakila kitu tunahitaji na Sisi kufanya kazi kuziendesha familia zetu hatuja zoea kukaa tu muda wote .
Zawadi aliwaambia sawa mimi nimewasikia wote na hio kesho nikifanikiwa kukutana na rais nitahakikisha hoja zene wotee zinamfikia. Basi wote walikubaliana wakaendelea na shughuli zao za kila siku na John John nayeye aliondoka na kuelekea nyumbani kwake. Lakini alipofika aligundua kuwa ameondoka na kadi ya mtoto wa zawadi na alichofanya alichukua kadi ile nakuiweka juu ya redio yake na kumjulisha Zawadi kwa ujumbe mfupi kwanjia ya simu kuwa kadi ya mtoto wake yupo nayo. Zawadi akamjibu sawa kesho mpe baba wa mtoto ataileta mana wewe unaonekana hutaki kuja kabisa huku ni kazi tu ndo inakufanya ulazimike kuja karibu yetu na ndio maana kila mara tu unakasirika unapo niona usijali hivi karibuni tutakuwa mbali kabisa na macho yako na kazi yako itakuwa imeisha na Sisi, utapata kazi mpya kwa watu utakaovutiwa nao . John John aliusoma ujumbe wa zawadi lakini hakuweza kumjibu chochote na alibakia tu kujiuliza 'hivi ni kweli Zawadi hajui kama na mpenda au anafanya kusudi?"
John John aliamua tu bora alale mana kuchart na zawadi kunamfanya apate hasira tu. Lakini wakati John John yupo usingizini alikumbuka zawadi alimwambia kadi ya mtoto ampe baba wa mtoto na hapo ndo usingizi wote ulikata na kisha John John akawasha taa na kuuchukua kadi ya mtoto ili ajue huyo baba wa mtoto anaetakiwa kumpa kadi ninani?

USIKOSE SEHEMU YA 16 NA 17
 
Hapa zawadi alipofikia anataka kunigombanisha na boss ananipaje mtoto kienyeji hivi? Ila boss wangu nae akili Hana anamnunia mrembo wakati anamuhitaji mpuuzi kweli huyu
 
Back
Top Bottom