winnie9999
Member
- Nov 27, 2021
- 65
- 102
TAMTHILIYA: CHALLENGE MADE.
SEHEMU: 1
MUANDISHI: WINIFRIDA THOBIAS.
Usiku wa saa tano katika hospitali moja iliyopo nnje kidogo ya jiji la dar es salaam alionekana mwanamke mmoja aliyekuwa akijalibu kutoka kwa siri hospitalini hapo huku akiwa ni mjamzito wa mimba ya kama miezi nane,tisa au saba hivi.
Mwanamke huyo alikuwa akitoka taratibu sana katika hospitali hiyo huku akiwa anaogopa sana. Geti la hospitali hiyo lilikuwa mbali kidogo na jengo la maabara pamoja na hodi za wagonjwa hali iliyo pelekea mama huyo kuwakwepa walinzi wengi walio kuwa windo usiku huo katika sehemu mbalimbali ndani ya hospitali hiyo ilikuweza kufika Getini.
Lakini kwa bahati mbaya kabla ya mwanamke huyo kufanikiwa kufika getini moja kati ya madaktari wa zamu aligundua Ndani ya hodi ya wakinamama kuna mwanamama mmoja hayupo na bila ya kupoteze muda Daktari huyo alienda kuwajulisha watu waliokuwa katika chumba cha CCTV iliwaweze kumtafuta mwanamama huyo kutumia camera kabla hajatoka nnje ya hospitali kwani itakuwa hatari zaidi kwa mmiliki wa hospitali hiyo aliye fahamika kwa jina la Jackbosi.
Wafanya kazi wote wa hospitali hiyoo waliogopa sana kwani bosi wao pia atawauwa kama mwanamke huyo atafanikiwa kutoka nnje ya hospitali hiyo kwasababu mambo yaliyokuwa ya kiendelea katika hospitali hiyo ni yasiri sana na haipaswi kutolewa nnje ya eneo la hospitalini. Mkuu wa ulinzi aliamuru ulinzi uongezeke katika maeneo yote ya hospitalini haswa eneo la Getini.
Baada tu ya mwanamke huyo kuona ghafla ulinzi unaongezeka sana sehemu za Getini na pande mbalimbali za hospitalini aligundua kuwa tayari walinzi na madaktari Wameshagundua kuwa yeye anajaribu kutoroka na Kutokana na ulinzi ulivyo kuwa umeongezeke ilikuwa ni ngumu sana kwa mwanamke huyo kutoroka usiku huo hivyo aliamua kurudi ndani kwakupitia njia za siri za hospitali hiyo bila ya mtu yeyote kumuona .'kwaufupi tu nikuwa mwanamke huyo alionekana kuijua hospitali hiyo vizuri kuliko mtu yeyote alie kuwepo katika hospitali hiyoo'.
Walinzi walimtafuta sana mwanamke huyo lakini hawakuweza kumpata kwani hawakujua mwanamke huyo amejificha upande gani, madaktari waliogopa sana hivyo waliamua kumjulisha bosi wao Jack Bosi juu ya jambo lililotokea la kutoroka kwa mwanamke huyo, Jack bosi alishtuka sana na hasira zilimtawala kwa uzembe uliofanywa na walinzi pamoja na madaktari waliokuwa chini yake na bila ya kupoteza muda alianza safari ya kuelekea hospitalini huku akiongozwa na walinzi wake kutoka nyumbani kwake Masaki kuelekea katika hospitali yake ya siri baada tu ya Jackbosi kufika alianza kwa kuwagombeza vikali sana Madaktari pamoja na Walinzi wazamu wa usiku huo na kutokana na hasira ilivyo mtawala kwa wakati huo aliwapiga walinzi Wake watano risasi za miguu na bila ya huruma aliwaamuru walinzi hao wasimame kama hamna kilichotokea.
Jack bosi aliwapa masaa matatu walinzi wake Mwanamke huyo awe amepatikana kisha yeye na baadhi ya madaktari pamoja na walinzi wake walielekea katika hodi zakinamama wengine na kuwatoa wote n'je mida ya saa nane usiku na kuanza kuwatesa vikali na kuwaahidi kifo kama hawata sema mahali ambapo mwanamke huyo ameenda.
Wakati ambapo walinzi walikuwa wakiendelea kumtafuta mwanamama huyo na Jack Bosi nayeye aliendelea kuwataabisha Wakinamama wengine bila kujali wakinamama hao wamechoka na muda wowote watatakiwa kujifungua .
Baada ya mateso kuwa yamezidi kwa kinamama hao aliyekuwa kiranja wakinamama hao ambaye alifahamika kwa jina la Abi alichoka na mateso yaliyo kuwa yakiendelea hivyo alimwambia Jack Bosi aliyekuwa akipanga mipango ya kutoroka kwa grace ni jasmin jambo ambalo halikuwa la kweli kwani Abi aliamua kumsingizia jasmini kwasababu jasmini alikua akipendwa na kila mtu kuliko hata yeye ambaye ndo kiranja wakina mama hao , kwani alihisi sikumoja jasmini atachukua nafasi yake ya ukiranja.
Jack bosi baada ya kusikia hivyo kutoka kwa Abi ya kuwa jasmini ndo alipanga mipango ya grace kutoroka aliamuru haraka sana jasmini asogezwe miguuni mwake na wakinamama wengine wote wasogezwe pembeni kisha alianza kumpa mateso makali jasmini lakini jasmini hakuweza kusema chochote kwani hakuwa anajua lolote kuhusu grace kwani nikweli jasmini alikuwa rafiki wa grace lakini grace hakuwa tayari kumshirikisha mtu katika mambo yake ya hatari aliyo kuwa akiyafanya, Lakini kwasababu Jack Bosi alikuwa akimuamini sana Abi aliamua kumuua jasmini palepale na ujauzito wake baada ya kuona haongei chochote kuhusu grace alipoelekea.
Lakini wakati huohuo walinzi walirudi na kumwambia hawakumuona mwanamke huyo hospitali nzima isipokuwa kuna chumba kimoja kimefungwa na kunasauti ya mtu inasikika katika chumba hicho lakini tumeshindwa kukiifungua kwasababu kimefungwa kwa kufuri napia kinaonekana ni chumba cha siri sana kwasababu mlango wake ulikuwa umefunikwa kwa pazia jeusi .
Jack Bosi aliamuru wakinamama waongezewe ulinzi pia aliwaambia walinzi wake ya kuwa 'huyo mwanamke msimuite tena mwanamke jina lake ni grace' kisha akawaambia walinzi wake haya twendeni ikiwezekana hicho chumba kikavunjwe ili tuweze kujua huyo grace ni nani hasa'.
Jack Bosi pamoja na walinzi wake walielekea eneo ambalo mlango huo upo na kuamuru walinzi wauvunje haraka kwani yeye pia hakuwa anajua kunachumba cha siri hospitalini hapo ila hakuonyesha kuwa hajui chochote kuhusu chumba hicho mbele ya walinzi wake kwani alikuwa na Shauku ya kuweza kumjua vizuri mwanamke huyo anayejua mambo mengi kuliko hata yeye , walinzi walihangaika sana kuuvunja mlango huo lakini ilichukua muda kufanikiwa kuuvunja mlango kwani mlango huo ulitengenezwa kwa uimara sana.
Lakini baada ya kama lisaa hivi walinzi walifanikiwa kufungua mlango na wote waliokuwa katika eneo hilo walimuona grace akiwa ameshashikwa na uchungu na tayari chupa la uzazi limeisha pasuka tayari kwa mtoto kutoka na chaajabu zaidi ni kuwa grace alikuwa amefanana kilakitu na Jackbosi .
End
SEHEMU: 1
MUANDISHI: WINIFRIDA THOBIAS.
Usiku wa saa tano katika hospitali moja iliyopo nnje kidogo ya jiji la dar es salaam alionekana mwanamke mmoja aliyekuwa akijalibu kutoka kwa siri hospitalini hapo huku akiwa ni mjamzito wa mimba ya kama miezi nane,tisa au saba hivi.
Mwanamke huyo alikuwa akitoka taratibu sana katika hospitali hiyo huku akiwa anaogopa sana. Geti la hospitali hiyo lilikuwa mbali kidogo na jengo la maabara pamoja na hodi za wagonjwa hali iliyo pelekea mama huyo kuwakwepa walinzi wengi walio kuwa windo usiku huo katika sehemu mbalimbali ndani ya hospitali hiyo ilikuweza kufika Getini.
Lakini kwa bahati mbaya kabla ya mwanamke huyo kufanikiwa kufika getini moja kati ya madaktari wa zamu aligundua Ndani ya hodi ya wakinamama kuna mwanamama mmoja hayupo na bila ya kupoteze muda Daktari huyo alienda kuwajulisha watu waliokuwa katika chumba cha CCTV iliwaweze kumtafuta mwanamama huyo kutumia camera kabla hajatoka nnje ya hospitali kwani itakuwa hatari zaidi kwa mmiliki wa hospitali hiyo aliye fahamika kwa jina la Jackbosi.
Wafanya kazi wote wa hospitali hiyoo waliogopa sana kwani bosi wao pia atawauwa kama mwanamke huyo atafanikiwa kutoka nnje ya hospitali hiyo kwasababu mambo yaliyokuwa ya kiendelea katika hospitali hiyo ni yasiri sana na haipaswi kutolewa nnje ya eneo la hospitalini. Mkuu wa ulinzi aliamuru ulinzi uongezeke katika maeneo yote ya hospitalini haswa eneo la Getini.
Baada tu ya mwanamke huyo kuona ghafla ulinzi unaongezeka sana sehemu za Getini na pande mbalimbali za hospitalini aligundua kuwa tayari walinzi na madaktari Wameshagundua kuwa yeye anajaribu kutoroka na Kutokana na ulinzi ulivyo kuwa umeongezeke ilikuwa ni ngumu sana kwa mwanamke huyo kutoroka usiku huo hivyo aliamua kurudi ndani kwakupitia njia za siri za hospitali hiyo bila ya mtu yeyote kumuona .'kwaufupi tu nikuwa mwanamke huyo alionekana kuijua hospitali hiyo vizuri kuliko mtu yeyote alie kuwepo katika hospitali hiyoo'.
Walinzi walimtafuta sana mwanamke huyo lakini hawakuweza kumpata kwani hawakujua mwanamke huyo amejificha upande gani, madaktari waliogopa sana hivyo waliamua kumjulisha bosi wao Jack Bosi juu ya jambo lililotokea la kutoroka kwa mwanamke huyo, Jack bosi alishtuka sana na hasira zilimtawala kwa uzembe uliofanywa na walinzi pamoja na madaktari waliokuwa chini yake na bila ya kupoteza muda alianza safari ya kuelekea hospitalini huku akiongozwa na walinzi wake kutoka nyumbani kwake Masaki kuelekea katika hospitali yake ya siri baada tu ya Jackbosi kufika alianza kwa kuwagombeza vikali sana Madaktari pamoja na Walinzi wazamu wa usiku huo na kutokana na hasira ilivyo mtawala kwa wakati huo aliwapiga walinzi Wake watano risasi za miguu na bila ya huruma aliwaamuru walinzi hao wasimame kama hamna kilichotokea.
Jack bosi aliwapa masaa matatu walinzi wake Mwanamke huyo awe amepatikana kisha yeye na baadhi ya madaktari pamoja na walinzi wake walielekea katika hodi zakinamama wengine na kuwatoa wote n'je mida ya saa nane usiku na kuanza kuwatesa vikali na kuwaahidi kifo kama hawata sema mahali ambapo mwanamke huyo ameenda.
Wakati ambapo walinzi walikuwa wakiendelea kumtafuta mwanamama huyo na Jack Bosi nayeye aliendelea kuwataabisha Wakinamama wengine bila kujali wakinamama hao wamechoka na muda wowote watatakiwa kujifungua .
Baada ya mateso kuwa yamezidi kwa kinamama hao aliyekuwa kiranja wakinamama hao ambaye alifahamika kwa jina la Abi alichoka na mateso yaliyo kuwa yakiendelea hivyo alimwambia Jack Bosi aliyekuwa akipanga mipango ya kutoroka kwa grace ni jasmin jambo ambalo halikuwa la kweli kwani Abi aliamua kumsingizia jasmini kwasababu jasmini alikua akipendwa na kila mtu kuliko hata yeye ambaye ndo kiranja wakina mama hao , kwani alihisi sikumoja jasmini atachukua nafasi yake ya ukiranja.
Jack bosi baada ya kusikia hivyo kutoka kwa Abi ya kuwa jasmini ndo alipanga mipango ya grace kutoroka aliamuru haraka sana jasmini asogezwe miguuni mwake na wakinamama wengine wote wasogezwe pembeni kisha alianza kumpa mateso makali jasmini lakini jasmini hakuweza kusema chochote kwani hakuwa anajua lolote kuhusu grace kwani nikweli jasmini alikuwa rafiki wa grace lakini grace hakuwa tayari kumshirikisha mtu katika mambo yake ya hatari aliyo kuwa akiyafanya, Lakini kwasababu Jack Bosi alikuwa akimuamini sana Abi aliamua kumuua jasmini palepale na ujauzito wake baada ya kuona haongei chochote kuhusu grace alipoelekea.
Lakini wakati huohuo walinzi walirudi na kumwambia hawakumuona mwanamke huyo hospitali nzima isipokuwa kuna chumba kimoja kimefungwa na kunasauti ya mtu inasikika katika chumba hicho lakini tumeshindwa kukiifungua kwasababu kimefungwa kwa kufuri napia kinaonekana ni chumba cha siri sana kwasababu mlango wake ulikuwa umefunikwa kwa pazia jeusi .
Jack Bosi aliamuru wakinamama waongezewe ulinzi pia aliwaambia walinzi wake ya kuwa 'huyo mwanamke msimuite tena mwanamke jina lake ni grace' kisha akawaambia walinzi wake haya twendeni ikiwezekana hicho chumba kikavunjwe ili tuweze kujua huyo grace ni nani hasa'.
Jack Bosi pamoja na walinzi wake walielekea eneo ambalo mlango huo upo na kuamuru walinzi wauvunje haraka kwani yeye pia hakuwa anajua kunachumba cha siri hospitalini hapo ila hakuonyesha kuwa hajui chochote kuhusu chumba hicho mbele ya walinzi wake kwani alikuwa na Shauku ya kuweza kumjua vizuri mwanamke huyo anayejua mambo mengi kuliko hata yeye , walinzi walihangaika sana kuuvunja mlango huo lakini ilichukua muda kufanikiwa kuuvunja mlango kwani mlango huo ulitengenezwa kwa uimara sana.
Lakini baada ya kama lisaa hivi walinzi walifanikiwa kufungua mlango na wote waliokuwa katika eneo hilo walimuona grace akiwa ameshashikwa na uchungu na tayari chupa la uzazi limeisha pasuka tayari kwa mtoto kutoka na chaajabu zaidi ni kuwa grace alikuwa amefanana kilakitu na Jackbosi .
End