Tamthiliya: Challenge Made - Sehemu ya 1

Tamthiliya: Challenge Made - Sehemu ya 1

TAMTHILIA : CHALLENGE MADE.
MUANDISHI : WINIFRIDA FRANCIS THOBIAS.
SEHEMU: 15 $ 16.
WHATSAPP : 0746115688.
Grace alihamia rasmi nyumbani kwa Mr.kivuli na Jackbosi alihamia nyumbani kwa grace . grace alimkabidhi Jackbosi kampuni na biashara zote za familia na kumwambia kila kitu ni cha kwetu na sio cha kwangu tu , kwasababu utafutaji wa baba haukuwa kwaajili ya binti mmoja tu bali binti zake wote wawili yaani grace na Jack ndio maana hata kampuni aliita Graja. mimi naenda kwa Mr.kivuli kutafuta uhuru wako mdogo wangu pamoja na mimi na watu wote wanaoteseka kwaajili ya Mr.kivuli na pia kila mtu ajue kuwa wewe ndio Jack mtoto wa mzee wetu Steven na mimi ndio dada yako na Mrs.kivuli ndo mama yetu, kwasababu amekupenda wewe kama mwanae mimi sina tatizo nae kabisa kwasababu furaha yako mdogo wangu ndo ya dada yako kumbuka hilo . Grace alipoondaka Jackbosi alianza rasmi kusimamia kampuni na kwakuwa yeye alisoma biashara alipofika tu hatua ya kwanza alifuta project zote ambazo hazina faida na kupunguza wafanyakazi wasio kuwa na ulazima na kila mfanyakazi aliyekuwa anamfukuza alimlipa fedha za kujikimu Siku hiyohiyo aliyoondoka.
Mr.kivuli yeye hakuweza kujua hata kama pale nyumbani wanaishi na grace kwani hakuwahi kukaa na Jackbosi muda mrefu kiasi cha kujua huyu ni grace na huyu ni Jackbosi.
Baada ya wiki moja rasmi wakinamama wale walio saini mkataba na Mr.kivuli walienda kuanza kazi na Mr.kivuli aliwagawanya katika kila biashara zake akaweka mwanamama mmoja. Kwasiku za mwanzoni kila mwanamama alisimamia vizuri wafanyakazi waliokuwa chini yake lakini hawakuruhusu kabisa mtu yeyote kuona sura zao pamoja na kazi nzuri waliyofanya. Kwabahati nzuri Ade alibahatisha kufanya kazi katika eneo ambalo ndo madawa ya kulevya yanapotengenezwa na james lakini pia huyohuyo james ndo alikuwa kiongozi wa eneo hilo kwa upande wa utengenezaji. Lakini kwabahati nzuri pia Ade aligundua hakuna madawa yaliyo toka nnje ya eneo lile kwani ilikuwa ni ngumu kwao kusambaza amigo kwani James ni mgeni alihitaji mwenyeji kwanza iliasome ramani na ndio maana Ade akaajiliwa ili aandae mpango wa madawa hayo kusafirishwa nnje ya nchi na kusambazwa kwa watumiaji wadogowadogo.
Upande wa grace yeye alijiweka karibu sana na Mr.kivuli na kumfanya amuamini sana kiasi cha yeye kumruhusu kuingia katika chumba ambacho kinanyaraka na karatasi mbalimbali za mikataba yake pamoja na viongozi wa siri ambao walikuwa kwenye mtandao wa Mr.kivuli.
taratibu Mr kivuli alimuamini grace kuwa ni Jackbosi na wafanyakazi alio waajili na baada tu ya wote kupata imani ya Mr.kivuli walipanga Siku ili wakutane wapange mpango wa mwisho wa kumuangusha sasa Mr.kivuli , ambae wao waliamini ndie kiongozi wa biashara zote hizo chafu. Walipo kutana siku hiyo watu walishangaa sana kuona kumbe grace na yeye anateam ya viongozi wa kubwa wa nchi ambao wao ni waaaminifu na wanaopenda nchi yao kiasi cha kujitolea kuungana na grace pamoja na Mrs.kivuli ili waweze kupata uhuru wa nnchi na vijana kwa ujumla kwasababu biashara haramu za Mr.kivuli ziliwalejenga zaidi vijana. kwapamoja walikubaliana kwanza kabisa kuteketeza biashara zote zinazo mhusu Mr.kivuli.
kisha kupata nyaraka za watu wanaoshirikiana nae ili kuweza kuwatishia waweze kutoa ushahidi juu yake ili ahukumiwe, halafu bila ya wao kujua wakati wanatoa ushahidi ndio watakuwa wamejiangamiza pia. wakinamama wanaofanya kazi katika vituo vya Mr.kivuli walipanga mipango ya kuweza kuteketeza sehemu hizo, na baadhi ya wafanyakazi wa Mr.kivuli waliamua kuwasaidia kwani hata wao hawakufurahia kufanya kazi katika biashara zake lakini yeye aliwalazimisha na kuwatishia kuteketeza ndugu zao kama watakataa na hio ndio sababu ya wao kufanya nae kazi hivyo walivyogundua kuna mtu anahitaji kumteketeza Mr.kivuli waliungana nae kwani walikuwa wamesha choka na wanahitaji uhuru wao .
Basi siku moja wakati Mr.kivuli yupo katika Tafrija na wafanyakazi wake mtu mmoja alimtumia ujumbe afungue WhatsApp kuna zawadi yake na Mr kivuli alipofungua aliona jinsi biashara zake zinavyo teketea kwa moto na pia aliwaona wale wakinamama walio vaa maski wakiwaongoza wachomaji wa biashara hizo. Mr.kivuli alipokuwa akijiuliza ni wakina nani hasa hawa wakinamama na kwanini wanafanya hivi wakati niliwaajili na kuwapa pesa nzuri tu, palepale kwenye video wakinamama walivua maski huku wakimcheka sana Mr.kivuli kisha kwapamoja wakamwambia Mr.kivuli wewe ni binadamu tu na kama ulihisi wewe ni mungu bhasi ulikosea sana kwani toka mwanzo ulipaswa kujua wewe ni binadamu tu. Kisha wakinamama kwa pamoja wakavaa maski na kuondoka katika eneo lile .
Mr.kivuli akawagawanya wafanyakazi waliokuwepo katika Tafrija hiyo haraka ili waende sehemu mbalimbali za biashara zake kwani alihisi pengine labda ni utani tu na mambo ya kuedit ili kumkatisha tamaa yeye.
Lakini baada ya muda mchache mfanyakazi wa kwanza alipofika eneo la tukio alimpigia bosi wake video call kumuonyesha kuwa kweli moto umewaka na hakuna jinsi ya kuokoa chochote, baada ya taarifa hizo grace na Mrs.kivuli waliwaambia wageni wote waondoke Tafrija imeghairishwa kisha wakaiingia ndani pamoja na Mr.Kivuli,
wote walikuwa wamekaa kwenye kochi kusubiri taarifa mpya kutoka kwa wafanyakazi walioenda kuangalia maeneo yaliyo bakia na baada ya muda kidogo James alimpigia simu Mr.kivuli na kumpataarifa ya kuwa biashara zote zimeteketea kilichobakia ni majivu tu hakuna cha zaidi.
Hapohapo Mr.kivuli alianguka kwa presha, ndani ya wiki moja alikuwa akiamka analia ntakuwa masikini mimi kisha anazimia, madaktari walijalibu kumuhudumia kwa kadiri walivyoweza na kweli hali yakuzimia zimia ikapotea kabisa na madaktari waka ahidi siku inayo fuata watamruhusu Mr.kivuli. Wakati Mr.kivuli anaugulia hospitali grace alichukua nyaraka zote za siri nakuzificha lakini pia akayapa taarifa mabenki yote aliyokopa kuwa Mr.kivuli kafirisika na hivi karibuni atatoroka hivyo mabenki yote yakaungana na Siku iliyofuata wakati Mrs.kivuli na grace wanamchukua Mr.kivuli kumpeleka nyumbani Mr.kivuli alipofika nnje ya hospitali akaona kulikuwa na mnada wa live kwenye tv uliokuwa ukionyesha jinsi nyumba, magari na mali nyingine za Mr.kivuli zinavyo pigwa mnada na hapo ndo Mr.kivuli alianguka tena na kurudi hodini.
Lakini upande wa Jackbosi bila kumpa taarifa mtu yeyote aliongea na Daktari bingwa wa nchizannje wamasuala ya ubongo na kumueleza afya za wakina mama wote waliochanganyikiwa na akamuelezea pia kuhusu chip walizonazo na Daktari alimpa taarifa Jackbosi anauwezo wakuwasaidia kwasababu upasuaji wao una asilimia sabini na tano za wao kuishi , baada ya jibu hilo Jackbosi alimuuliza Daktari anahitaji kiasi gani lakini Daktari akamwambia nataka wapone tu kwasababu kwa stori uliyo ni hadithia kuhusu wao mimi pia ni muathirika, kwani nililetwa huku kutolewa viungo tu lakini moja kati ya madaktari aliniokoa na kunisomesha mpaka sasa mimi ni Daktari bingwa na nafanya hivi kwaajili ya watu wote walio uwawa kwa amri ya Mr.kivuli kwani sisi ni ndugu tulikua pamoja na kupendana sana kama si yeye naamini tungekuwa pamoja mpaka sasa . wakati grace anammaliza Mr.kivuli taratibu kwa Jackbosi nayeye Daktari aliwasili jijini dar es salaam na kuwafanyia upasuaji wakinamama wote na akafanikiwa kutoa chip kwa wakinamama wote na wote wakatoka katika upasuaji salama lakini pia akaanza kumtibu Steven taratibu taratibu na kweli nafuu ilianza kuonekana.
Mr.kivuli alipo amka kwenye mshtuko wa safari hii alimwambia ukweli wote grace akijua ni Jackbosi kuhusu biashara alizo fanya , Mr.kivuli bila kujua grace alikuwa anamrekodi kwa kamera aliyokuwa ameivaa kama kifungo katika shati lake lakini kikubwa zaidi alimpa siri ambayo hata grace alikuwa hajui kuwa yeye sio bosi wa hizo biashara bosi wake alikuwa ni mstaafu mmoja wa Udaktari ambae anaduka dogo tu la madawa la kuizugia serikari na pia akawaambia mtaa alipo ili wakamwambie anahitaji msaada wake lakini kwa bahati mbaya grace ,Mrs.kivuli pamoja na wakinamama walipoelekea mahali ambapo Daktari huyo yupo walikuta msiba kwani Daktari huyo alijinyonga baada ya kujua mambo yameharibika ili familia yake isimchukulie yeye ni jambazi na kweli japo wakina grace waliwaambia ndugu zake ukweli wa mzee huyo lakini ndugu hawakuamini kwani hawaku wahi kuona dalili yeyote kwa mzee huyo ya kuonyesha anafanya biashara hiyooo.
Wakina grace waliona hamna haja ya kuwalazimisha watu, kwanza kashajiadhibu mwenyewe na kwaupande mwingine bado Mr.kivuli ndo hatari zaidi kuachiwa huru kwani yeye ndo alikuwa mpangaji mkuu na msimamizi wa biashara hizo hivyo akiwa huru mambo yataharibika hivyo grace pamoja na Mrs.kivuli walimua kumfungulia mashtaka Mr.kivuli kwa kujihusisha na biashara za madawa, na viungo vya binadamu mashtaka ya madawa yalipelekea james kukamatwa .
wakati Mr.kivuli yupo hospitalini alishangaa kwenye tv kuona mkewe na grace wamemshitaki yeye tena bila woga hapo ndo Mr.kivuli akili alimjia akavua nguo za hospitalini na kutoroka hivyo polisi walipo kuwa wakimtafuta hospitalini ili akamjibu mashtaka Hawakumpata.
grace nae alimwambia Mrs.kivuli asiwe na wasiwasi kwani Mr.kivuli hana pakwenda chaumuhimu ni kuwalaghai washirika wake , na kweli grace akakutana na washirika mbalimbali wa mr.kivuli na kuwaonyesha ushahidi wa kuwamaliza kama hawatatoa ushahidi dhidi ya Mr.kivuli na kweli washirika wake wote baada ya kuona ushahidi huo hawakuwa na jinsi walikuwa tayari kusimama mahakamani kama mashahidi . Usiku mmoja polisI walipo kuwa katika windo walimuona Mr kivuli akiwa amepitiwa na usingizi chini ya gari la kubeba mataka na hapohapo wakamkamata na baada ya mwezi kesi ilipelekwa mahakamani na mashahidi wa kwanza walikuwa ni wakinamama waliokuwa na grace hospitalini ambao ushahidi wao ulikataliwa kwani mahakama ilishindwa kuamini kua kweli Mr.kivuli anapandikiza mbegu kwa wakinamama kwani wao watoto walikuwa ni wawanaume zao ambao wanadai wameuwawa na Mr.kivuli, hivyo mahakama ili mwambia grace atafute ushahidi mwingine. grace akawashawishi viongozi walioshirikiana nae na kweli waliwasili mahakamani na kutoa ushahidi lakini baada ya grace kutoa ushahidi mwingine wa video ambayo ilikuwa inaonyesha hadi wao walikuwa pamoja na Mr.kivuli mahakama ili kataa kuwaamini pia kwani waliamini grace kuwatishia kwani ni ngumu mtuhumiwa kutoa ushahidi wa kujizulu bila sababu za msingi hivyo hakimu aliomba utulivu mahakamani na kumwambia grace kama hana ushahidi wa kueleweka kesi itafungwa mana hapangilii ushahidi hivyo Mr.kivuli atahukumiwa kwa makosa yenye ushahidi tu na makosa yenye ushahidi yalikuwa madogodogo tu ambayo anaweza epuka kwa faini tu .
grace alichoka kwani alikuwa hajui atapatia wapi ushahidi mwingine wakuwafanya Mr.kivuli na wenzake wasitoke jela kabisa lakini ghafla hakimu kabla hajatamka hukumu Jackbosi aliingia akiwa na wakinamama wale walio kuwa wamechanganyikiwa tena wakiwa wazima pamoja na Steven na Daktari yule ambae ni ushahidi tosha wa suala la upandikizaji wa mbegu kwani yeye pia mamayake alipandikizwa tu mbegu hivyo yeye hamjui hata baba yake zaidi ya mama yake, lakini pia anajua hadi hospitali wanayotolewagwa vijana hao viungo baada ya kutolewa nchini na Mr.kivuli.
hakimu alimuuliza wewe ni nani na Jackbosi alimwambia muheshimiwa hakimu mimi naitwa jack Steven ila maarufu kama Jackbosi na hawa unao waona mbele yako ni waathirika waliotokana na huyo Mr.kivuli yaani namaanisha baba yangu mlezi.
Mr kivuli alishangaa sana kwani aliyekuwa akimuhisi kama Jackbosi ni grace lakini pia alijua ni ngumu kupona tena kwa ushahidi aliokuwa nao Jackbosi hivyo alimwambia muheshimiwa hakimu inatosha , kwasasa naomba tu nafasi ya kuongea kidogo, muheshimiwa hakimu akampa Mr.kivuli nafasi aliyo itaka na Mr kivuli kwanza akakubali shutuma zake na kumwambia hakimu hata hawa viongozi kweli wanahusika na taratibu akawageukia viongozi wale pamoja na wafanya biashara wakubwa tu na wengine ni viongozi hadi wa dining ambao alikuwa wanaoshirikiana nao kisha akawaambia wakubwa Inatosha hakuna njia ya kutoka tena na wote wakainamisha vichwa chini kwa aibu . Mr kivuli akamuomba hakimu tena nafasi ya kuongea japo kidogo na hakimu alimpa tena nafasi, Mr.kivuli akasema nashukuru sana wote nyie mlioshirikiana kuhakikisha leo najuta kwa ubinafsi na tamaa zilizo kuwa zina niandama, lakini pia nashukuru kwani nyie mmenifundisha kuwa changamoto zinaweza kujenga usipo jali ujenzi huo utachukua muda gani, mimi umaskini tu ulinifanya nikaogopa kabisa kupambana nikashawishiwa na Daktari john ambae ni marehemu kwasasa nakwapamoja bila kujali tukatumia uhai wawatu wengine kama pesa kwetu, mpaka sasahivi najiuliza kama umaskini tu umenifanya nikawa mtu mbaya hivi je ingekuwa ndugu zangu ndo wamepitia waliyo yapitia ndugu zenu sijui nchi yangu leo ingekuwa inapambana na mtu wa namna gani, kisha mr.kivuli akatoa bunduki aliyokuwa ameificha na kuisalimisha kwa askari wakaribu yake kisha akasema nilitamani mambo ya kiwa magumu nijipige risasi nifie mbali ili aibu isinipate lakini nimegundua hata nijikatekate vipande kama nyama cwezi lipa madhambi niliyo tenda hivyo muheshimiwa hakimu naomba nipe adhabu itakayo wafanya watu waogope kabisa kufikilia kufanya nilicho kifanya mimi. kisha Mr.kivuli akamwambia Jackbosi ahsante sana wewe pamoja na dada yako grace kwa mlicho kifanya pamoja na mke wangu kaeni mkijua sijawachukia wala sinakinyongo na nyie nisameheni sana kama inawezekana na nawapenda sana kuanzia sasa kwani mmenifundisha upendo ananguvu kiasi gani . Baada ya maneno hayo Mr.kivuli alihukumiwa kunyongwa pamoja na washirika wake wote.
grace aliendelea kuwa Daktari na kumlea mwanae, lakini pia Jackbosi aliolewa na Daktari yule na alipata watoto wake wawili , wakinamama waliendelea nashughuli zao kwa wale waliokuwa na taaruma zao na wengine waliajiliwa katika kampuni ya Graja chini ya usimamizi wa mwenyekiti Jack steven
MWISHO.
ubarikiwe

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
TAMTHILIA: ZAWADI .

MUANDISHI: WINIFRIDA FRANCI THOBIAS.

SEHEMU YA: 1.

WHATSAPP NO: 0746115688.

Sophia ni binti ambaye hakubahatika kulelewa na wazazi wake wote wawili kwasababu mama yake alifariki siku aliyo mzaa Sophia. Hivyo Sophia alilelewa na baba yake ambaye anafahamika kwa jina la Mzee Ali kuanzia siku ambayo mama yake alimleta duniani. Sophia alipofikisha umri wa miaka kumi na tisa baba yake aligundua binti yake alikuwa mjamzito na hakuwa ameolewa wala kuwa na mchumba rasmi anaetambulika nyumbani jambo ambalo mzee Ali alilichukulia kama dharau na hapo ndo akachukua maamuzi magumu ya kumfukuza sophia ili aende kwa mwanaume aliyempa mimba japo ilikuwa ikimuuma sana mzee Ali lakini hakuwa na njia nyingine zaidi ya kumfukuza ili sophia ajifunze . Sophia alipofukuzwa na baba yake alienda moja kwa moja kwa mpenzi wake Joseph ambae ndo muhusika wa mimba hiyo na kumueleza yote yaliyomkuta baada ya baba yake kugundua yeye ni mjamzito. Josefu alimpenda sana sophia na hakupenda kumuona Sophia akisononeka hivyo akamchukua na kwenda nae kwa wazazi wake. Walipofika nyumbani kwakina Joseph sophia aliwasalimia wazazi wake na Joseph lakini hawakuitika kwani walikuwa na Shauku ya kujua kuna tatizo gani kwanza. Joseph aliwaambia wazazi wake ya kuwa huyu binti anaitwa Sophia na Sophia ni mjamzito na baba yake amemfukuza , naombeni msaada wenu kwani ujauzito Alio ubeba sophia ni wakwangu japo pia natambua mimi na Sophia tulichofanya ni kosa ila naomba mtusamehe. Mama na baba yake Joseph walimwambia Joseph ndio umetenda kosa na kwakosa ulotenda hatuwezi na sisi pia kukupokea kwasababu hicho mlicho fanya ni dharau hivyo chamsingi kwasasa na wewe chukua vitu vyako vyote na uondoke hapa nyumbani hatutaki kukuona kabisa kwani umeshakuwa na humu ndani hatuwezi lea baba,mama na mtoto wao . Joseph aliwaomba sana wazazi wake angalau wamsaidie Sophia tu na yeye kwakuwa anamaliza chuo mwaka wa mwisho akimaliza tu atajipanga na kumchukua sophia pamoja na mwanae. Mama yake Joseph alimwambia Joseph mwanangu kama ulijua kuna kujipanga usingempa Huyu chokolaa mimba, binti asiejua hata kusoma angalau hata ungekuwa umempa mimba msomi kama wewe ningempokea mana najua angetusaidia lakinini Huyu chokolaa hana cha kunisaidia hivyo naomba muondoke haraka machoni mwetu. Josefu alijalibu sana kuomba msaada kwa wazazi wake hadi kwakupiga magoti huku machozi ya kimmwagika lakini wazazi wake hawakuwa tayari kumpokea Sophia. Sophia akamwambia Joseph basi sasa inatosha ! ,nakushukuru kwani umejaribu sana kunipambania mimi pamoja na mtoto wako , lakini inakubidi kukubali kuwa mama yako na baba yako hawapo tayari kuishi na chokolaa nisiejua kuandika hata jina langu hivyo usijali mimi nitapambana Joseph kwaajili ya mtoto wetu na nitahakikisha mwanangu anajua na kusoma ili siku moja asije ishia kutukanwa kama mama yake lakini pia usijali unaweza kukaa kwenu tu sitakuchukia na mwanao sitamficha kabisa kuhusiana na baba yake kwasababu unajalibu sana kumpigania . Josefu alimwambia Sophia kama nihivyo tunaondoka wote kwasababu hata ukiniacha hapa sitaishi kwa amani kabisa. pia baba na mama napenda tu kuwaambia japo hamumtaki Sophia ila mnapaswa kujua mtoto atakae zaliwa na Sophia ni mjukuuu wenu haijalishi mama yake yupoje lakini pia wazazazi wangu mtoto akinyea mkono hauwezi kukata kiganja bali utakiosha tu na maisha yataendelea , Naombeni mnisamehe sana mama pamoja na baba kwakosa nililotenda . Baada ya joseph kusema hayo yeye pamoja na Sophia wakaanza safari yao rasmi ya kuondoka kijijini hapo na kwenda mjini kuanza maisha yao mapya kwani hakuna mtu aliyekuwa akiwahitaji tena. Maisha ya Sophia na Joseph yalikuwa magumu sana hivyo walipanga chumba cha bei rahisi ili waweze kupata pesa kidogo kwaajili ya chakula cha sikuchache wakati Joseph akihangaika kutafuta kazi. Joseph mara kwa mara hakuonekana mwenye furaha kila alipo kuwa akimuangalia Sophia kwani aliamini yeye ndo sababu ya maisha magumu anayo yapitia sophia na Sophia pia aligundua hilo mapema tu na kumwambia Joseph inabidi ujitahidi kupunguza mawazo kwani hata hayo magorofa unayo yaona yanapendezesha mji hayakubandikwa tu bali kunamchanganyiko wa vifaa mbalimbali lakini pia na nguvu ya binadamu na kutokana na ushirikiano wa vitu vyoote hivyo ndo mana mimi na wewe leo tunayaona yamesimama, hivyo huu sio muda wa wewe kujiona Mkosaji kwani wote tumekua sababu ya maisha haya tunayoishi kwasasa na huu ndo muda wa wewe na mimi kusimama ilikutengeneza maisha mazuri kwaajili ya mtoto wetu au tuandae majuto na yeye akija ajute kama sisi.. Joseph alijikuta akimuangalia sana Sophia na akizidi kumpenda mara dufu zaidi kwani alikuwa ni binti mdogo lakini alikuwa na mawazo ya kusimama baada ya kuanguka nasio kusubiri mtu aje amshike mkono ndo aamke, pamoja nakuwa hana elimu lakini alikuwa na mawazo ya mbali kushinda hata hao wasomi walio wazunguka. kuanzia siku hiyo Joseph alikaza moyo na yeye pamoja na Sophia wakapambana mchana na usiku kuhakikisha maisha yao yanakuwa bora na sio magumu siku zote bila hata kujali aina ya kazi wanayo fanya. Baada ya mwaka mmoja na nusu Sophia alikuwa tayari ameshajìfungua na alibahatika kupata mtoto wakike ambaye Joseph alimpa jina la Zawadi , maisha yao kwa ujumla yalikuwa mazuri sana kwani joseph alibahatika kupata kazi katika shule ya secondary iliyokuwa ikimilikiwa na mtu binafsi na yeye alikuwa mwalimu wa masomo ya sayansi pekee katika shule hiyo hivyo alilipwa mshahara mzuri sana. muda ulienda sana miaka mitano ikapita na hatimaye binti yao zawadi Alianza daraja la kwanza na Sophia pamoja na Joseph walibahatika kuwa na duka la vifaa vya umeme ambalo Sophia ndo alikuwa akilisimamia. Siku moja Joseph alimuomba Sophia Amuandae zawadi ili akamnunulie vifaa vya shule na Sophia alifanya hivyo alimuandaa zawadi kisha Joseph na zawadi wakamuaga Sophia na kuondoka kuelekea kununua vifaa vya shule vya zawadi . Baada ya muda kidogo Sophia aliisikia simu yake ikiwa inaita na alipo angalia aligundua ni mumewe ndo anapiga lakini cha ajabu alipo pokea simu aliiambiwa anahitajika hospitalini mumewake alipata Ajali mbaya sana. Sophia alifunga tu mlango wanyumbani kwake bila kujali amevaa nini moja kwa moja alielekea katika hospitali aliyokuwa ameelekezwa lakini alipofika hospitalini hakupata angalau bahati yakuongea na mumewe kwani Joseph alikuwa ameshafariki na alipoulizia kuhusu mtoto akaambiwa mtoto hakuonekana katika eneo lile labda mtoto atakuwa amepotelea majini kwani gari iliangukia pembeni ya bahari.

USIKOSE SEHEMU YA PILI .
 
TAMTHILIA: ZAWADI.

MUANDISHI :WINIFRIDA FRANCIS THOBIAS.

SEHEMU : 2 $3.

WHATSAPP NO: 0746115688

kifo cha Joseph na kupotea kwa binti yake Zawadi kili mzoofisha sana Sophia kiasi cha yeye kushindwa kutoa maamuzi ya kuupumzisha mwili wa mume wake ndani ya wiki nzima mpaka pale ambapo rafiki yake Sophia ambae ni Elizabeth alipo mwambia unapaswa kukubaliana na ukweli ya kuwa mumewe ameshafariki na hata binti yako pia kwani ni ngumu kwa mwanao kupona katika kina kirefu cha maji ukizingatia ni binti mdogo wa miaka sita tu. Sophia hakuwa najinsi aliweka saini kwenye makaratasi ya hospitalini na kuuchukua mwili wa mumewe na kisha aliandaa majeneza mawili ambayo moja uliifadhiwa mwili wa mumewe na lingine alihifadhi vitu vya binti yake kama ishara ya kumpunzisha binti yake kwani mwili wa zawadi ulitafutwa sana lakini hauku patikana jambo lililomfanya Sophia aamini kuwa binti yake hayupo tena duniani. Maziko yalifanyika ya mumewe pamoja na binti yake lakini upande wapili maji yalimsukuma zawadi mpaka mbele ya macho ya mwanamke mmoja mrembo aliyekuwa akiyachezea maji pembeni ya bahari na mwanamke huyo alishangaa sana kumuona binti mdogo aliyekuwa pembeni ya bahari akiwa amepoteza fahamu, mwanamke huyo alimchukua Zawadi na kumpeleka mpaka katika jengo la kifalme ambapo yeye ndo alikuwa akiishi hapo kama malkia, kisha akawaita madaktari wote wa ufalme huo waweze kumuhudumia binti huyo kwani mwanamke huyo alitokea kuvutiwa sana na binti huyo bila hata kujua ametokea wap .
Na kwaupande wa pili hali ya Sophia ilikuwa mbaya kiasi cha yeye kuanza kuchanganyikiwa kutokana na msongo wa mawazo yaliomtawala, hali iliyo mfanya rafiki ake mpendwa Sophia kumpeleka Sophia katika hospitali moja ya akili na kufunga biashara zake zote pamoja na nyumba ya Sophia.
Upande wa ufalme Malkia yule aliye mchukua zawadi baada ya kuona madaktari wanajalibu sana kumsaidia zawadi lakini hamna mafanikio yeyote ya kupona kwake aliamua kufunga safari moja kwa moja mpaka katika makazi ya Mfalme na kumuelezea kila kitu kuhusu binti aliye muokota pembeni ya bahari , Mfalme alimwambia malkia twende tukamuone binti huyo na chaajabu Mfalme alipo kutanisha tu macho yake na zawadi moyo wake ulipata amani na kutokea kumpenda sana zawadi na hapo ndo alipo wakusanya wazee wa ufalme wa Wetu iliwaweze kutoa ushauri kama kuna njia nyingine yeyote ya wao kuweza kumponya binti huyo kwani amekuwa akipokea matibabu lakini hakuweza kufungua macho yake.
mzee mmoja alimfahamisha Mfalme kwanza inabidi binti huyo asomwe Nyota ndo afanyiwe matibabu na Mfalme alikubali lakini msoma Nyota kila alipojalibu kusoma Nyota ya zawadi alishindwa lakini alitokea kumpenda tu jinsi anavyoonekana na hapo ndo akawaambia wazee wengine pamoja na Mfalme binti huyu ni mejalibu sana kumsoma Nyota lakini imekuwa tofauti kwani Nyota yake sio rahisi kusoma, mzee mmoja aliye fahamika kwajina la Mzee Togwa alisimama na kuwaambia wazee wengine ni ngumu sana kuishi na mtoto ambaye hata Nyota yake ni ngumu kusoma nani ajuae huyu binti atakuja kuleta majanga gani katika ufalme huu, wazee wengine waliungana nae na kupinga suala la binti huyo kusaidiwa na wengine walitoa Wazo la zawadi kuuliwa kabisa, Malkia na Mfalme hawakuwa tayari kuona zawadi anauliwa hivyo aliwaomba wazee wengine wawape muda wa siku mbili kama binti huyo hata amka bhasi atawauwa.
upande wa pili Sophia aliendelea kupokea matibabu lakini hakuweza kuonyesha unafuu wowote wa kupona jambo lililo mfanya Elizabeth kuamua kuwatafuta ndugu wa Sophia, iliwajalibu kuwanae karibu pengine itakuwa nafuu ya yeye kupona haraka . Elizabethi alifunga safari na kuelekea kijiji ambacho Sophia pamoja na Joseph walizaliwa na alipofika moja kwa moja aliomba kuelekezwa mahali mwenyekiti alipo na kweli alielekezwa na alipofika kwamwenyekiti alimuelezea kila kitu lakini mwenyekiti alimpa taarifa Elizabeth kuwa baba yake na Sophia amefariki na hivi sasa ni wewe umekuja hapa ndo umenisubirisha lakini nilikua naelekea kwake kwani muda wa Mazishi yake ndo huu. Elizabeth alimuomba mwenyekiti ahifadhi begi lake ofisini kwake ili nayeye akahudhulie mazishi ya mzee Ali na baada ya hapo ataongea na ndugu wa Sophia kama watamuelewa aende nao katika hospitali aliyo kuwa amelazwa sophia.
Mfalme nae alihangaika sana kuweza kutafuta suluhisho la kuweza kumuokoa zawadi kwani hakutaka kuona zawadi anauwawa na hapo ndo aliwaomba madaktari wakaongee hata na mizimu ili tu zawadi aamke lakini haiku saidia kitu kwani wazee waliwakataza wao kwenda kuabudu mizimu kwamtu ambae hawamjui hata ametokea wapi. malkia alimwambia Mfalme wamtafute mganga ambae ataweza kumponya zawadi kwasababu wazee wote hawakuwa tayari kuona zawadi anaombewa kwenye mizimu yao ikiwa hata Nyota yake tu ni ngumu kusomeka. Mfalme alifanyia kazi ushauri wa mkewe akamtafuta mganga mmoja mkubwa sana katika ufalme wa Wetu na usiku wasiku hiyo ya kwanza kati ya siku mbili walizoomba mganga huyo aliingia katika ufalme kwasiri na moja kwa moja akapelekwa katika chumba alichokuwa amelazwa zawadi , baada ya mganga huyo kuingia katika chumba icho alimpa heshima Mfalme pamoja na malkia kisha akaomba ruhusa ya kumkagua zawadi na Mfalme alimruhusu lakini chaajabu mganga alipofika tu katika sehemu ambayo zawadi amelala midomo yake ilitabasamu sana na alipo jalibu kusoma Nyota ya zawadi hakupata chochote zaidi ya mganga huyo kuanza kucheka jambo ambalo liliwashangaza watu wote waliokuwa katika eneo lile kwani moja kati ya sifa za mganga huyo ni kwamba hajawahi kucheka kabisa mbele za watu yaani hakuna mtu anajua kuwa mganga huyo anachekaga au la ! na kwakuwa Mfalme analijua hilo alihisi mganga huyo anadharau kazi aliyo pewa hivyo aliwaambia walinzi wamtoe mganga huyo kwani anaonekana hayupo tayari kufanya kazi. lakini mganga alimwambia Mfalme ya kuwa ' Mfalme wangu ni ngumu sana kukutana na uso wa binti huyu na kujizuia kuwa na furaha au kumpenda kwani uso wake unakibali hakuna mtu ataweza kuona uso wa huyu binti halafu akamchukia lakini pia nimejalibu sana kusoma Nyota yake lakini haisomeki ila kama kweli kupona kwake ni muhimu bhasi anahitajika kuombewa na watu wote katika ufalme huu wa wetu yaani asiwepo yeyote atakae kosekana katika maombi hayo na hapo ndo yeye atapona'. mfalme alimwambia mganga kuwa watu hawawezi kuwa tayari kwani wazee wote wa jadi hawako tayari kuungana na sisi kuhakikisha binti huyu anapona, mganga alicheka sana na kumwambia Mfalme tumia uso wa binti huyu mbele ya macho ya kila mtu na hakuna yeyote atakae ruhusu kifo chake kisha mganga akampaheshima mfalme na walinzi wakamtoa kwa siri kama alivyo ingia kwa siri.
Baada ya mazishi ya mzee Ali Elizabeth alikaa na ndugu zake Sophia na kuwaeleza hali anayopitia Sophia lakini hakuna mtu aliyeonyesha kuguswa kwani wote waliamini kifo cha ndugu yao sababu ni yeye kwani tangu Sophia aondoke baba yake alizohofika kidogokidogo mpaka kufikia umauti wake. Laki Elizabeth aliwaomba angalau wampeleke kwa wakwe zake na Sophia lakini ndugu wa Sophia walimwambia Elizabeth usijalibu kwasababu mama yake Joseph akijua kijana wake amefariki bhasi hata huyo Sophia atamfuata Joseph alipo hivyo wewe cha msingi lala hapa asubuhi anza safari ya kurudi huko mjini na huyo Sophia ukiona vipi mtelekeze hospitalini kwani hayo ndo malipo ya mambo aliyo tufanyia sisi pamoja na ndugu yetu. Elizabeth hakuwa na jinsi hivyo alipumzika ili awahi kuanza safari yake mapema kwani aligundua Sophia ni ndugu yake yeye hakuna ndugu mwingine anaweza kuwa nae karibu na kumsaidia kwakipindi anachopitia Sophia kwa sasa zaidi yake.
Asubuhi na mapema katika ufalme wa wetu Mfalme alikuwa bado anawaza jinsi ya kumsaidia zawadi aweze kupona lakini hakuweza kupata jibu lolote kila alipojitahidi kuwaza. Upande wa malkia nae alichukua kibakuli cha dhahabu na kumtilia maziwa zawadi kisha akaelekea katika chumba alicholala zawadi nakuanza kumywesha maziwa hivyo hivyo akiwa amepoteza fahamu kisha akamsafisha na kumvalisha mavazi mazuri yaliyokuwa yametengenezwa kwa magamba ya miti na ngozi za wanyama kisha malkia alianza kufikilia Wazo la mganga la kuwa uso wa zawadi ndo unaweza kumfanya kila mtu amuombee na kuachana na mawazo ya kumuua wakati huohuo wazee wa ufalme walitangaza mitaani kuwa katika ufalme kuna mtoto shetani anayelelewa na Mfalme pamoja na malkia hata hivyo waliwaambia wananchi wa ufalme wa Wetu waungane nao ili waweze kumfanya Mfalme akose nguvu ya kuweza kumtetea binti huyo.
Upande mwingine baada ya kupambazuka Elizabeth alirudi mjini na kuelekea hospitalini moja kwa moja Elizabeth alimuangalia Sophia kwa huzuni sana kisha akawa anakwambia wewe ni dada yangu lakini Sophia hakuwa anaelewa chochote kile kinacho endelea na hapo ndo Elizabeth alishauriwa kumpeleka Sophia marekani kwani kuna madaktari wazuri ambao wanaweza kumtibia sophia tatizo alilo kuwa nalo. Elizabeth alikuwa ni binti wa kipekee wa tajili mmoja aliyejulikana kwa jina la Mr.Thomas hivyo haikuwa shida kwa yeye kumpeleka Sophia marekeni kwani aliongea na Mr.Thomas na Mr.Thomas aliweka pesa ya kutosha kwenye ya Elizabeth na kumwambia nyie wote ni binti zangu kuweni makini na ntakuja kuwatembelea mara kwa mara mpaka matibabu ya dada yako yatakapo kuwa yamekamilika. Elizabeth alimkumbatia na kumuahidi baba yake watarudi salama lakini pia alimwambia baba yake awe makini kwani kuondoka kwake baba yake atakuwa mwenyewe kwani mama yake Elizabeth alikufa yeye alipo maliza elimu yake ya sekondari .
Siku iliyo fuata katika ufalme Mfalme na malkia waliamshwa na kelele za watu zilizokuwa zikisikika nnje ya ufalme zikimwambia Mfalme na malkia wamtoe huyo binti mchawi auwawe asije akasababisha laana katika ufalme wao. Malkia alichukia sana na kumchukua mtoto kisha akatoka nae nnje akiwa kambeba na kuanza kushuka nae kwenyengazi huku akielekea mahali ambapo watu wamesimama wakiwa na mawe,wengine fimbo na vitu mbalimbali wakihitaji kumuua binti huyo wakati malkia anakimbia na mtoto kuelekea mahali ambapo watu wote wapo walinzi pamoja na Mfalme walikuwa wakimfuata kwa nyuma na walipofika mahali watu walipo Malkia alienda katikati yao na kuwageuzia zawadi kisha akawaambia 'haya muueni huyo hapa', baada ya malaika kuwaambia hivyo malkia alishangaa sana kwani baada tu ya watu kuuona uso wa zawadi wote walikuwa kama wamewekwa kwenye barafu kwani ni kimya tu kilitawala katika eneo hilo.

USIKOSE SEHEMU YA 4 $ 5.
 
TAMTHILIA : ZAWADI .

MUANDISHI :WINIFRIDA FRANCIS THOBIAS.

SEHEMU : 4 $ 5.

WHATSAPP NO : 0746115688.

Baada ya watu wote kumuona zawadi walishusha silaha zao chini na kubaki kumshangaa tu zawadi. Mfalme nae akatumia mshangao wao kusogea mbele na kuwauliza je mpo tayari kutoa maisha ya huyo binti mdogo ambaye hakuwahi kuwafanyia ubaya wowote ? tokea amefika hapa ni amelala tu lakini bado Hamna huruma naye kabisa. bhasi sawa inatosha sasa nitawapa mnachokitaka, mfalme akawaambia walinzi mchukueni binti huyo na mumuangamize kwani nikiwaangalia wote nyie mmejiandaa kabisa hata kuwa waasi kwajiili ya binti huyu mdogo mana mlibeba hadi silaha kama mmekuja kutoa maisha yangu pia pamoja na malkia wangu yaani mmesahau kabisa sheria na taratibu tulizojiwekea sindio. watu wote walinyamaza kimya na kupiga magoti huku wakimuomba mfalme awasamehe kwani walichofanya ni dhambi.
Lakini Mfalme aliwaambia nimewasamehe wote lakini pia msijali kwasababu leo ntatimiza ahadi yangu binti huyu ata uwawa. Walinzi walimpokonya mtoto malkia na moja kwa moja wakampeleka sehemu ambayo watu hunyongwa mpaka kufa pale wanapo kutwa na hatia . Malkia alishtuka sana na kuzimia palepale kisha walinzi wake wakamchukua na kumpeleka ndani na Wazo lakumnyonga zawadi bado lilikuwa kichwani mwa Mfalme hata baada ya malkia kuzimia Mfalme alisimamisha kidogo zoezi hilo lakini baada ya Mfalme kuletewa jibu la kuwa malkia ni Mzima kabisa amepatwa tu na mshtuko mdogo ataamka baada ya muda kidogo, Mfalme aliwaambia walinzi waiingize shingo ya zawadi katika kitanzi ili watu wapate amani na waache uasi.
Lakini Wakati walinzi wanaiingiza shingo ya zawadi katika kitanzi watu wote wa ufalme wa Wetu walilia wakimuomba msamaha Mfalme na kumwambia tunaomba binti huyu apone na awe mmoja wetu hata hivyo tunaona kabisa ni jinsi gani wewe na malkia mnavyo mpenda na sisi pia tunampenda . Mfalme aliwaambia sawa lakini kama kweli mnahitaji uwepo wake kuna sharti kwani mganga amesema inapaswa ifanyike ibada kubwa ya kumuombea binti huyu ili apone na aweze kuishi nasisi kama watu wengine na wote mnahitajika katika ibada hiyo asikosekane hata mmoja wenu kama mtakuwa tayari lakini kama hampo tayari inabidi tu binti huyu auwawe ili aishi kwa amani mbinguni. Watu wote walimwambia Mfalme ni bora ibada ifanyike leo vipi kama kesho mtoto akifa, Mfalme alishangaa sana lakini hakujali aliwaambia watu kwa pamoja washirikiane kuandaa ibada na wazee wa ufalme ndo wakamwambia Mfalme wao watasimamia maandalizi hayo, malkia alipo amka alishangaa kumuona binti pembeni yake alimkumbatia sana huku machozi ya yakimtoka, Mfalme nae alimuomba msamaha na kumpa taarifa nzuri kuwa kila mtu yupo tayari kwaajili ya ibada , Malkia alifurahi sana na kumkumbatia mumewe. Baada ya muda maandalizi yalikamilika na malkia na Mfalme walitoka nnje kwaajili ya ibada na wazee wa jadi ndo walisimamia ibada hiyo na wakati ibada ilipo kuwa ikiendelea wazee wa jadi walimuomba malkia pamoja na Mfalme wasimame kama wazazi wa binti huyo mpaka ibada itakapo isha na Malkia pamoja na Mfalme hawakukataa wote walisimama kama wazazi wa zawadi mpaka pale ambapo zawadi alipiga chafya na kusimama kisha akaanza kucheka sana baada ya kuona mazingira ya eneo lile yalivyo kuwa mazuri lakini cha ajabu baada ya furaha zawadi alisogea mpaka mahali ambapo Mfalme alikuwa amekaa kisha akamwambia Mfalme wewe ndo baba yangu Mfalme akamwambia kwanini unaulizia hivyo lakini zawadi alimjibu ni kwasababu nna njaa sana yaani nna njaa ya kutosha naweza pata chakula kweli , Mfalme alibakia anacheka pamoja na watu wengine lakini malkia alimwambia usijali chochote utakacho utakula, zawadi alimwambia bila shaka wewe ni mama yangu malkia alimwambia ndio mwanangu kisha Malkia akamshika mkono zawadi ili waelekee ndani zawadi akapate chakula, Mfalme aliwashukuru watu wote kwakuhudhulia katika maombi lakini watu waliiinamisha vichwa vyao chini na kumtakia Mfalme maisha mrefu kisha baada ya Mfalme kuingia katika ufalme na watu wengine wote walitawanyika.
Ilipo fila usiku malkia alimwambia Mfalme binti hakumbuki chochote na kwa umri alio nao hata tumwambie nini hawezi tuelewa anachojua yeye mimi na wewe ndo wazazi wake, Mfalme alimwambia malkia nimeona hilo na cha zaidi ni kuwa hajui hata jina lake na sijui hata nimpe jina gani zuri binti huyu wa maajabu, malkia akapendekeza wamuite zawadi kwani ni binti alie patikana katika mazingira magumu akiwa aelewi chochote na kila mtu alitamani kumfanyia jambo baya aliposikia tu kuhusu yeye kabla hajamuona, lakini baada ya kumuona kila aliemfikilia vibaya alifurahia Kana kwamba ameona zawadi nzuri iliyo pelekea yeye kurejesha utu wake aliokuwa ameupoteza kwa muda mrefu hivyo huyu binti ni zawadi hata kwangu na kwako pia Mfalme wangu na kwasababu yake kwasasa wote tunafuraha . Mfalme alikubaliana na malkia kuwa binti huyo ataitwa zawadi bila ya wao kujua kweli hilo ndo jina halisi la mtoto huyo hata kabla hajapata ajali iliyopelekea yeye kufika mikononi mwao .
Zawadi alikuwa msumbufu kidogo kwasababu hakuwa anatambua sheria za ufalme yeye alipo amka asubuhi alienda moja kwa moja kwa mfalme na bila ya kugonga hodi aliingia ndani na kwenda kulala katikati ya Mfalme na malkia jambo ambalo lilikuwa likimfurahisha sana malkia bila kujali kuwa ni sheria anavunja . Malkia na Mfalme walichukua maamuzi ya kumtangaza zawadi kama binti Mfalme wa ufalme wa Wetu na kila mtu alikubaliana nao.
Zawadi aliheshimika sana na kilamtu lakini pia alipokea upendo kwa kila mtu yaani kwa wazazi wake pamoja na watu wote wanaoishi katika himaya ya Wetu.
Baada ya miaka miwili wakati zawadi amelala alisikia sauti ya mwanamke mmoja akilia sana kwasababu mume wake aliadhibiwa kifo baada ya kuiba samaki katika jiko la ufalme , kelele za mwanamke huyo zilimfanya zawadi aamke na kutoka nnje ili akapate kujua nini hasa kinaendelea. Baada ya zawadi kutoka nnje alishangaa kuona shingo ya mtu huyo imeshawekwa katika kitanzi na kiti alicho simamia kimepigwa teke haraka bila hata ya kuuliza zawadi alikata kamba kwa upanga wake na kumuuliza Mfalme kwani baba huyu ameuwa watu wangapi mpaka akahukumiwa kufa pia, Mfalme akamuangalia tu zawadi na hakumjibu chochote lakini mzee mmoja alimwambia zawadi kwa heshima binti Mfalme bwana huyo unae muona ameiba samaki aliyekuwa mahususi kabisa kwaajili ya familia ya Mfalme na kutokana na dhambi hiyo aliyo ifanya anahukumiwa kufa ili asitokee mtu mwingine atakae jifananisha yeye na Familia ya Mfalme.
Zawadi alicheka sana lakini ghafla alishangaa kuona wakati yeye anacheka hakuna mtu anae cheka na yeye watu wote walikuwa wanahasira na yeye kwanza kwasababu ya kusitisha hukumu ya Mfalme, lakini pili kwa yeye kucheka sababu ya hukumu ya Mfalme. Mfalme alimuangalia zawadi na kumwambia vip mbona unacheka sana ina maana adhabu niliyompa ni ndogo sana ?, zawadi alimwambia Mfalme ,baba yangu katika ufalme wetu samaki ni moja kati ya chakula ambacho kinapatikana kiurahisi sana lakini kutokana na hali ya hewa ya sasa imekuwa ni ngumu kwa baadhi ya familia kupata samaki, kwasababu ili kupata samaki inabidi uwe na mtumbwi na mtumbwi upo mmoja tu ambao unatumiwa na wavuvi wa ufalme na wazee wa ufalme, lakini pia samaki ndo chakula tegemezi kwakila mtu anaeishi katika ufalme wetu kwa sasa hivyo tukisema kila anaeiba samaki auwawe basi kalibia wakazi wote wa ufalme wa Wetu watauwawa kwani wanategemea samaki na upatikanaji wa samaki kwa sasa unahitaji watu kwenda kina kirefu sana cha maji na watu wetu hawawezi kwenda huko kwasababu hawana mitumbwi hivyo kama hakuta kuwa na mtumbwi kwaajili yao bhasi kila siku wata uwawa kwani samaki ni kitumuhimu kwao na bila ya samaki watu watakufa njaa kwani matunda kwa sasa hakuna kabisa je watafanyaje,
mzee mmoja alimwambia binti Mfalme vyovyote vile ila kila atakaekutwa ameiba xamaki wa ufalme atauwawa kwasababu nikinyume na taratibu tulizo jiwekea na nidhambi pia. zawadi alimuangalia kwa hasira mzee huyo na kumwambia unaweza kuapa kichwani kwangu kuwa hujawahi kuchukua samaki katika ufalme tokea samaki wawe washida katika ufalme huu wa Wetu ? mzee huyo aliinama tu na kukaa kimya na kuinamisha kichwa chini , zawadi aliwaambia nadhani wote mmepata jibu kuwa samaki ni muhimu kwasasa na sio kwa watu wakawaida tu bali yeyote yule akipata nafasi ya kuiba samaki ataiba kwasababu ni muhimu kwasasa kwasababu matunda hakuna na hapa tukisema kwa uaminifu mlio kwisha kufanikiwa kuiba samaki bila kukamatwa muuwawe basi ni wote nyie, hivyo ni bora muwe waungwana na njia itafutwe ya kuweza kujenga mtumbwi kwaajili ya kuhakikisha familia zote za ufalme wetu hazilali njaaa.
Mfalme alimuelewa sana binti yake na wakazi wa ufalme wa Wetu walizidi kuvutiwa na zawadi kwani alikuwa binti mdogo lakini anahekima kuliko hata wazee wanao heshimika katika ufalme huo. Malkia alitabasamu tu nakuzidi kumpenda zawadi lakini baadhi ya wazee wa jadi walimchukia sana kwani walimuona nimvunjaji tu wa kanuni na sheria zilizo wekwa katika ufalme wao . Lakini Mfalme alitoa amri baba yule aachiwe lakini pia kwaushirikiano mtubwi ujengwe na zawadi asimamie hilo kwa sababu Wazo ni lake, lakini pia kwakipindi ambacho mtumbwi unatengenezwa samaki zinazo letwa kwaajili ya ufalme zigawanye na katika familia za watu ambao hawana mitimbwi kisha Mfalme akasimama na malkia wakaingia katika ufalme na baada tu ya Mfalme kuingia ndani ya ufalme wakazi wa ufalme wa Wetu wasiojiweza wakambeba zawadi juujuu huku wakiwa na furaha sana na kumuona zawadi kama mungu wao kwani sikuzote zawadi amekuwa akiwawazia tu wao.
lakini wakati zawadi amebebwa juujuu yeye alikuwa akiwaza ni jinsi gani watu wao wanaweza kupata chakula kitakacho wafaa katika maisha yao yote ya kila siku ili kusiwepo na tabu ya chakula kipindi ambacho matunda hamna na samaki wanasumbua .
Lakini pia kwa upande wa pili mama yake zawadi alishafika marekani na matibabu yake yalikuwa ya kiendelea na taratibu mabadiliko ya afya yake yalikuwa yakijidhihilisha .

USIKOSE SEHEMU YA 6 $ 7.
 
TAMTHILIA : ZAWADI.

MUANDISHI:WINIFRIDA FRANCIS THOBIAS.

WHATSAPP NO: 0746115688.

SEHEMU : 6 $ 7.

Kwapamoja watu walisheherekea sana maamuzi ya Mfalme kwasababu chakula pekee wanacho tegemea ni samaki, na imekua ngumu sana kwa watu kwasasa kupata samaki hali inayopelekea familia nyingi kuingia kwa siri katika ufalme na kuiba samaki ili familia zao ziweze kuishi . hivyo kama Mfalme angeendelea kusimamia msimamo wake wa kuua kila anaekutwa na hatia ya kuiba samaki basi hakika angemaliza watu wake wote na ndio maana zawadi aliamua kuwa muwazi kwa baba yake juu ya kipindi kigumu watu wao wanachopitia.
Baada ya masaa machache baada ya kesi ya mtu yule alieiba samaki kuachiliwa huru Mfalme, Malkia pamoja na binti yao zawadi walienda kutembelea mizimu na lengo kuu la wao kutembelea mizimu yao ilikuwa ni kuomba mizimu hiyo iwasaidie watu wao juu ya hali wanayo pitia kwasasa. mfalme aliiomba mizimu iwape njia ya kuweza kuwasaidia watu wao waweze kupata chakula kisha akachukua samaki mmoja mkubwa sana pamoja na matunda akaweka katika mti aliokuwa akiabudu mizimu hiyo kama sadaka ambayo itaifanya mizimu hiyo iweze kumjibu kwa haraka.
Lakini wakati Mfalme , Malkia pamoja na Zawadi wanarudi nyumbani Zawadi alimuomba Mfalme aangalie Miti imara ambayo yeye pamoja na watu wao wataitumia kutengenezea ngalawa, Mfalme alimkubalia Zawadi katika hilo lakini Malkia alikuwa na hofu sana hivyo alimwambia Zawadi kuwa makini sana na hakikisha unarudi katika ufalme mapema. Baada ya Mfalme kuondoka zawadi alikuwa akikagua ni miti gani mizuri zaidi na mirefu itakayo wasaidia wao kupata ngalawa kubwa sana kwaajili ya uvuvi na alipokuwa akikagua ghafla alianguka sehemu iliyokuwa na miti mingi ya mihogo, zawadi aliiangalia sana lakini hakuwa anajua nikitu gani hivyo aliiangalia huku akiwaza ni miti ya namna gani yenye mizizi minne hivi na laini lakini zawadi akapotezea kwani miti hiyo aliona cio imara kwa yeye kutengenezea ngalawa hivyo aliipita na kuendelea na ukaguzi wake na kwabahati nzuri kweli alipata miti mizuri na kuiwekea alama kwa kuikwangua alama ya ex kisha akaelekea katika ufalme na kuwaambia walinzi waende eneo ambalo yeye ameona miti hiyo ili wakaikate na kesho asubuhi watu wataifuata na ujenzi wa ngalawa utaanza.
Walinzi walifanya kama walivyo ambiwa walienda na kuikata miti hiyo na kuifunga lakini wakati wanarudi katika ufalme moja kati ya wazee wa ufalme aliwauliza mnatoka wapi vijana ? , walinzi wakamwambia ukweli kuwa wanatoka kukata miti kwaajili ya ngalawa, mzee huyo alionekana kuchukizwa lakini hakutaka kuonyesha mbele ya walinzi hao hivyo aliwapongeza na kuendelea na safari yake na walinzi nao walienda katika ufalme na kumjulisha binti Mfalme kuwa miti tayari na wamesha hiifadhi .Zawadi alienda moja kwa moja kwa Mfalme nakumjulisha Mfalme kuwa tayari alipata miti kwaajili ya ngalawa na tayari walinzi wamekataa hivyo hivi karibuni tatizo la chakula litatatulika , Malkia alifurahi sana lakini alimshauri Mfalme itakuwa vizuri kama atakwenda kukagua miti hiyo kabla ya wazee wa jadi mana kama zawadi atakuwa amekata miti ya tiba itakuwa ni tabu nyingine katika ufalme. Mfalme alikubaliana na Malkia na kumwambia zawadi usiku wataenda kukagua miti hiyo kwani Mfalme alikuwa na kazi ya kufanya lakini pia usiku ni muda mzuri kama kutakuwa na miti ya tiba walinzi watakuwa hawana kazi yeyote mida hiyo hivyo wataichukua na kuitupa majini .
Upande wa pili mzee yule aliepewa habari kuhusiana na miti, Alienda moja kwa moja na kuwaeleza wazee wenzie wa jadi kuwa zawadi tayari amesha amuru watu wakakate miti ya ngalawa yaan yule mtoto cjui anataka kuonekana nani, wazee walimchukia sana na kumuona zawadi kama mtu anataka kuwabebea heshima yao na kuwafanya vituko mbele ya kila mtu na hapo ndo wazee wakaamua kupanga mpango wa kuharibu kabisa mpango wa zawadi na kumfanya kila mtu amuone zawadi kama mtu anaye jali mipango yake tu na sio watu walio mzunguka kama wao wanacho fikilia, hivyo wazee wakawatuma vijana wanao waamini wakakate miti ya dawa na kuweka mahali miti ya zawadi ilipo na kisha miti ya zawadi ifichwe mahali ambapo hata ikitokea zawadi anataka kujitetea ashindwe kufanya hivyo.
Vijana waliotumwa na wazee hao wa jadi waliingia msituni na kukata miti kama walivyo agizwa na kisha wakaificha sehemu ili itakapofika usiku wakaanze kuibadilisha chini ya uongozi wa vikongwe hivyo vya jadi.
Giza lilipoingia mida kama ya saa mbili hivi Mfalme, Malkia, Zawadi pamoja na walinzi walielekea msituni ili Mfalme pamoja na malkia wakahakikishe kama miti ambayo zawadi amewatuma walinzi wakakate kweli cio ya dawa ? , na kweli malkia alipo kagua miti pamoja na Mfalme waligundua kweli miti zawadi aliyo watuma walinzi wakakate sio ya dawa, na baada ya kukaguliwa Mfalme aliwaamuru walinzi waifunge vizuri ili kesho watu watakapofika mahali hapo penye miti wabebe tu wasipate tabu yakuanza kufunga tena, walinzi walifunga na baada ya kumaliza tu kufunga safari ya kurudi katika ufalme ilianza lakini wakati wakina Zawadi wako njiani kuelekea katika ufalme kwambali Mfalme waliona watu wanao kuja katika eneo walipo wao hivyo Mfalme akamwambia zawadi,Malkia pamoja na walinzi wazime mwenge uliokuwa ukiwasaidia katika matembezi yao ili watu wanaokuja wasiwaone na kweli Mfalme pamoja na watu wake walijificha na kumbe wazee na wale vijana ndio walikuwa wakielekea katika eneo lile lenye miti ya zawadi huku vijana hao wakiwa wamebeba miti ya dawa kisha walipofika eneo kwenye miti ya zawadi wakaichukua miti hiyo ya zawadi na kuweka miti ya dawa na kisha wakaichukua miti ya zawadi na kuipeleka pembeni ya bahari bila ya wao kujua Mfalme alikuwa akiwaangalia kwa hasira sana. Baada ya Mfalme kushuhudia yote hayo alimwambia zawadi mambo mengine tutapanga nyumbani cha umuhimu ni kuwa tumejua kunawatu wamejipanga kukuangusha na kuwafanya watu wote wa ufalme huu wa Wetu wakuchukie hivyo turudini katika ufalme.
Mfalme alirudi na kumchukua zawadi na kuongea nae kwasiri kisha akamwambia zawadi akalale. Asubuhi na mapema watu wote walikuwa tayari mbele ya nyumba ya Mfalme ili wakaanze ujenzi wa ngalawa na hapo ndo zawadi aliwapa habari kwanza twendeni tukachukue miti kwaajili ya ujenzi wa ngalawa, hapohapo ndo wazee wa jadi walijifanya kama wanajali sana kuhusu ngalawa kwani walikuwa wakiwaambia watu haraka tukabebe miti ili kazi iishe haraka, jambo lililomfanya zawadi kucheka sana .
Zawadi aliwaambia watu waelekee mahali ambapo miti ipo lakini cha ajabu wazee wajadi ndo wakawa wanaongoza njia , zawadi aliwaangalia sana na kucheka kwani aliwaona kama hawana akili ya kuwaza mbali hivi, kisha walipofika eneo ambalo wao walibadilisha miti ya zawadi ya kujenga ngalawa na kuweka miti ya dawa ili kumchonganisha zawadi pamoja na watu ghafla zawadi alipoona miti ile ya dawa aliwaambia wazee wajadi mbona kama miti yenu mnayo taka kuchangia kwenye ujenzi wa ngalawa niya dawa ?, wazee wakamwambia hii ndo sehemu ambayo wewe umeweka miti yako na sio sisi na wala sisi hatukutoa ahadi ya kutoa miti kwaajili ya ngalawa iweje tuhusike na miti hii , zawadi aliwaambia kama na kumbuka miti yangu ya ngalawa ilipo ni siri yangu mimi na walinzi wangu pamoja na Mfalme sasa nyie mmejuaje miti yangu ilipo maana mimi sikuwaambia mje huku nimekuwa nikiwafuata tu nyie njia mnayo tuongoza bila ya kutoa neno lolote kwetu . Wazee walibakia wanamuangalia sana zawadi lakini zawadi aliwaambia walinzi wachache wapeleke miti hiyo katika ufalme na baada ya ujenzi wangalawa lazima muhusika wa kitendo hicho apatikane. Zawadi aliwaambia watu wamfuate na wakaelekea mpaka mahala ambapo wazee walificha miti ya zawadi kisha zawadi akawaambia watu waanze kubeba miti na ujenzi wa ngalawa uanze, wazee walibakia kushangaa tu lakini zawadi yeye alionekana kuwa busy tu na ujenzi wa ngalawa na kweli baada ya muda kidogo ujenzi wa ngalawa ulikamilika na zawadi aliwapongeza watu wake kwa hilo na usiku wa siku ileile ngalawa iliingia majini pamoja na wavuvi ili kuweza kupata samaki na kweli siku ya kwanza samaki walipatikana wengi na watu walifurahia sana, lakini siku ya pili upatikanaji wa samaki ulikuwa mchache sana na hapo ndo zawadi alikosa amani kabisa kwani aligundua watu hawapati chakula kinacho watoshea na siku ya tatu samaki ndo walikosekana kabisa hivyo ikabidi watu watumie samaki waliokuwa nao majumbani mwao.
Baada ya muda kidogo njaa ilizidi sana na hapo ndo wazee wa jadi walikubaliana kutumia njia hiyo ilikumuangamiza zawadi kwani waliwaambia watu kuwa yote hayo yamesababoshwa na ukataji wa miti ya dawa kwaajili ya ngalawa, zawadi alipoyasikia maneno hayo alimwambia baba yake basi inatosha baba itisha mkutano maana wazee wamezidi sasa ,na hapo ndo Mfalme akaitisha mkutano na baada ya watu kufika tu katika mkutano huo , wazee wa jadi pamoja na watu wakamwambia Mfalme tunaangamia kwasababu ya makosa ya zawadi, tunaomba aazibiwe kwa makosa yake aliyoyatenda, tunaomba auwawe kwasababu kitendo cha yeye kukata miti ya dawa ndio kinapelekea sisi tuna kufa njaa.
Kwahasira zawadi alitoka mbele mpaka kwenye sehemu ya kitanzi kisha akawaambia watu wake 'mnauhakika aliekata miti akifa njaa itaisha' ? watu walimwambia zawadi ndio na zawadi aliwaambia msijali basi kwasababu leo wahusika wa kukata miti ya dawa wataazibiwa nasio zawadi asie kuwa na hatia na tokea hapo naamini chakula kitakuwepo kama kawaida. Zawadi aliwapaishara walinzi na walinzi wakaenda kuwapandisha mbele vijana wote waliotumiwa na wazee wajadi kukata miti hiyo, kisha akawauliza nani aliwatuma mkate miti hiyo mana siku ile mimi nilishughudia kila kitu. vijana walinyamaza kimya lakini zawadi akawapa tena ishara walinzi na walinzi hakawachukua watoto, wake, na wazazi wa vijana hao kisha wakawaambia msipo kuwa wa kweli watu wenu wakaribu watakufa kwaajili yenu.
wazee wa jadi waliogopa sana na kuanza kutia maneno yasiyo eleweka lakini Mfalme akawaambia kaeni kimya leo, kwasababu hata mimi nilishughudia nikaamua kunyamaza lakini inaonekana kuna watu wanataka kujua zaidi kuhusu jambo hili na ndio maana taarifa zinapaa kwa haraka sana, Kisha Mfalme akamwambia zawadi unaweza kuendelea. Zawadi akachukua panga na nakumyooshea mama wa mmoja kati ya vijana hao na palepale kijana huyo aliogopa sana na kumwambia zawadi binti Mfalme sisi tuliagizwa tu na wazee wa jadi kufanya hivyo haikuwa lengo letu , zawadi alicheka sana na kuwaambia wanakijiji leo inabidi haki itendeke sindio, wanakijiji wote kimya lakini moja kati ya mtoto wa wazee hao wa jadi alimwambia zawadi wauwawe bila huruma.

USIKOSE SEHEMU YA 8 $ 9.
 
Back
Top Bottom