Tamthilia ya Bibi Titi Mohammed na Prof. Emmanuel Mbogo

Ahsante sana Mohamed Said
Nimekuelewa kwenye chanzo, lakini nimeshindwa kusikiliza hiyo attachment. Kwa kuwa niki ingia ina niletea vitu sivijui. Hivo nasumbuka kuipata.

Lakini ninavo jua mwisho wa siku Rais Nyerere ndio ali mfanya bibi titi atoke jela na baada ya hapo hapakuwa na maneno tena kati yao. Nadhani na Nyumba zake alimrudishia.
Pia naskia kuwa ugomvi wao hasa hasa ni ule wa azimio la arusha. Kuhusi suala la umiliki wa mali.
6fca63b9c579151e416a46da00ee1f38.jpg
point yangu kubwa ni Rais na Bi Titi walipishana baadhi ya misimamo tu ila bondi yao ilikuwa kubwa.
Hawa wazee hata uki waangalia walikuja kuelewana na waliridhia kuwa tofaut zao ndogo ndogo ziliwatenganisha kidogo. Walikuwa wana chemistry ya asili.

Nitafurahi kama uta nirekebisha nilipo kosea ahsante
Nyumba ya Bibi Titi moja iko Upanga hapa mtaa wa makao makuu ya jeshi, nafikiri ni mtaa wa Magore ule kama nakumbuka vizuri.

Mtaa unaoanzia Palm Beach unaenda kutokea mpaka Diamond Jubilee Hall/Shaaban Robert Secondary na Olympio Primary. My old stomping grounds.

Alikuja kurudishiwa ile nyumba kipindi cha Mwinyi kama sikosei.
 
Kunaweza kukawa na ukweli
Lakini ndio historia haiwez kuwasema wote walioshiriki
Kwa kumsoma muhusika mkuu ndio tutawajua na wengine
Muhusika mkuu ndiyo nani? Maana tunaona kuwa harakati za Uhuru hazikuanzia na Nyerere kama tulivyosadikishwa na kitabu cha historia cha kivukoni.

Allama Mohamed Said anaweka kumbukumbu sawa kuwa harakati zilianza zamani sana.

Unaifahamu historia ya Ikulu ya Dar na kanisa lenye "kibla" la hapo Dar?

Hutopenda kufahamu hayo?
 
Haviwezi kusambazwa na havitasambazwa vitabu kama hivyo kwa sababu wanaviandika (ukiwemo wewe) wanamalengo "mahususi" ya kuligawa Taifa kwa "udini"

Kwamba sina taarifa kamili huenda uko sahihi ama hauko sahihi kwasababu sio rahisi kila mtu awe na taarifa sahihi za kila kitu na sio kila taarifa sahihi inapaswa kuwa hadharani! Hapa ndo hamtaki kupaelewa na mtalalama sana na hamtokaa mfanikiwe!

Wakati mwingine lazima muelezwe ukweli tu!

Hawa Babu zetu waliomkaribisha Mwalimu Nyerere kujiunga nao kupigania Uhuru na hatimaye kulikomboa Taifa letu hawakuwa na fikra mgando mnazotaka vizazi vyenu virithi!

Hawa Babu zetu walipigania uhuru wa nchi yetu kwa kusukumwa na uzalendo wao wala sio dini zao hilo mnapaswa kulielewa.

Laiti kama wangesukumwa na dini zao hawa mnaowaita makafiri wasingepata nafasi ya kushiriki harakati hizi za ukombozi wa nchi yao zaidi zaidi watawala wangetumia mwanya huo kuendelea kuwagawa kwa kutumia udini maana lazima tu wangejengeana uhasama.

Ukweli utabaki kuwa ukweli, Mwalimu Nyerere aliona mbali hasa baada ya hayo makundi kuanza kutaka kujimilikisha nchi! Hakuna kiongozi mpenda haki, mpenda amani angeruhusu kitu hicho!

Mzee wangu unayajua mengi kutokana na ulivyojishughulisha kuyajua.

Hata hivyo, hunabudi kubadili mtazamo na kuacha kuhusisha dini na harakati za ukombozi kwani ni wazi wazee wetu walisukumwa na uzalendo wao wala si dini zao ndiomaana walikuwa tayari kushirikiana na watu wasio wa dini zao.

Haipingiki kwamba kwa harakati zozote zilizoanzia ukanda wa pwani ni lazima zingesheheni watu waliokwisha rithishwa dini ya kiislam kwasababu ukanda wa pwani wote ulishaenea dini hiyo hata kabla ya ukoloni!

Tanzania yetu ni ya thamani sana kuliko hizo dini zilizokuja na meli! Tanzania yetu hii ipo kwa mpango wa Mungu wala sio kwa mpango wa dini fulani!

Kwasababu hiyo ilibidi Mungu atuletee kiongozi atakayefifisha ndoto za waliotaka kujimilikisha nchi hii kama wameiumba wao!

Hayo makundi anayoyatetea Dada yetu Faiza, ni wazi yangeachiwa yajitanue, yajitape leo hii tusingekuwa hivi!

Historia nyingine iko wazi wala haijafichwa, makundi hayo yaliminywa ili tuwe na Tanzania isiyo na dini! Tumesoma darasani na watoto wanasoma hadi leo makundi kama "AMNUT" ilibidi tu yapigwe stop kwasababu yalishaanza kuonyesha dalili isiyo njema ya kutaka kueneza dini badala ya utaifa!

Sipingani na unayoyafahamu wala sina haja ya kufanya rejea ulizozitaja, napingana na mtazamo wenu wa kutaka nchi hii iwe ya kiislam eti kisa walioasisi harakati za ukombozi walikuwa waislamu! HIKI KITU HAKITAWEZEKANA!

Hao wazee wetu kina Bibi Titi, Sykes's family, na wengine wengi tunawaheshimu na tutaendelea kuenzi michango yao katika kuliletea Taifa hili uhuru, ila kwa wao kuhusika msitake nchi hii tuigawe kwa waarabu maana kuipa umiliki wa dini ya kiislam ni sawa na kuigawa kwa waarabu maana ndio waasisi wa dini hiyo!

Mimi binafsi nitampa credit mzee atakayeanzisha harakati za kutaka tuachane na hizi dini za kikoloni zilizofanikisha watu wetu kufanywa watumwa na hatimaye kutuletea ukoloni kuliko watu kama nyie ambao mnazipigia upatu kana kwamba Babu zenu walikosea kuwa na dini zao walizokuwa nazo kabla ya hizi kuja huku!

Tuachane na udini, tujenge nchi yetu! Tunapoyaendekeza haya hakika tunazidisha chuki na vinyongo ndani ya nafsi zetu kitu ambacho sidhani kama Mwenyezi Mungu anakiruhusu!

Historia nzuri ni ile inayotokana/andikwa na mtu asiyekuwa na upande! Kwa kuwa na upande ni hakika huwezi kutuletea historia yenye usahihi kama unavyodhani
Unaonesha jinsi ulivyo ghadhibika. Unaandika maandiko marefu yasiyo na mpango.

Mara vitabu. Mara babu zetu. Mara wazee wetu. Mara Waarabu. Mara Waislam.

Mara "mnataka kuifanya nchi hii ya Kiislam".

Mara hili mara lile. Umeandika mambo kibao lakini hata moja halina maana kwa kuwa unajiandikia tu na wala unachokiandika hukielewi. Ndiyo maana unaambiwa soma rejea uje na hoja.

Lile la "lecturer" wako hata baada ya kuoewa darsa umelirudisha tena kama jina tu bila hoja yoyote.

Hivi nnakuuliza, hujawahi kulazwa hospitali kwa matatizo ya kichwa?

Mara historia nzuri ni kuandikwa na "mtu asiye na upande".

Sasa Tanzania hii ni nani asiye na upande? Wote niwaonao ni wazima kamili na sijaona mtu asiye na upande akitembea. Tumtoe wapi?

Stick kwenye point moja ueleweke. Punguza ghadhab.

Wacha kubabaisha babaisha. Kujifanya unajuwa kumbe huna unalolijuwa.

Kuhusu Waarabu kugaiwa nchi sifahamu fikra hiyo potofu unaitoa wapi? Au unamaanisha WAISLAM?

Maana kama ni Uarabu hata wewe unao. Wewe si mstaarabu?
 
Unaonesha jinsi ulivyo ghadhibika. Unaandika maandiko marefu yasiyo na mpango.

Mara vitabu. Mara babu zetu. Mara wazee wetu. Mara Waarabu. Mara Waislam.

Mara "mnataka kuifanya nchi hii ya Kiislam".

Mara hili mara lile. Umeandika mambo kibao lakini hata moja halina maana kwa kuwa unajiandikia tu na wala unachokiandika hukielewi. Ndiyo maana unaambiwa soma rejea uje na hoja.

Lile la "lecturer" wako hata baada ya kuoewa darsa umelirudisha tena kama jina tu bila hoja yoyote.

Hivi nnakuuliza, hujawahi kulazwa hospitali kwa matatizo ya kichwa?

Mara historia nzuri ni kuandikwa na "mtu asiye na upande".

Sasa Tanzania hii ni nani asiye na upande? Wote niwaonao ni wazima kamili na sijaona mtu asiye na upande akitembea. Tumtoe wapi?

Stick kwenye point moja ueleweke. Punguza ghadhab.

Wacha kubabaisha babaisha. Kujifanya unajuwa kumbe huna unalolijuwa.

Kuhusu Waarabu kugaiwa nchi sifahamu fikra hiyo potofu unaitoa wapi? Au unamaanisha WAISLAM?

Maana kama ni Uarabu hata wewe unao. Wewe si mstaarabu?
Sasa kati ya maandishi haya uliyoandika na niliyoandika mimi yapi yanaonesha aliyegadhabika!?

Pole sana, sijafundishwa kujibu matusi!
 
Sasa kati ya maandishi haya uliyoandika na niliyoandika mimi yapi yanaonesha aliyegadhabika!?

Pole sana, sijafundishwa kujibu matusi!
Huna hoja tu. Tusi hujatukanwa unavunga umetukanwa, jee ukitukanwa si ndiyo mwao.

Jibu kuhusu "lecturer" wako na AMNUT ulilipata juu huko au hujalipenda au ndiyo akaae kimya kakubali.

Kiislam binti akiletewa pisa huulizwa, fulani kaleta posa umekubali?" Akikaa kimya kakubali.
 
Muhusika mkuu ndiyo nani? Maana tunaona kuwa harakati za Uhuru hazikuanzia na Nyerere kama tulivyosadikishwa na kitabu cha historia cha kivukoni.

Allama Mohamed Said anaweka kumbukumbu sawa kuwa harakati zilianza zamani sana.

Unaifahamu historia ya Ikulu ya Dar na kanisa lenye "kibla" la hapo Dar?

Hutopenda kufahamu hayo?
Hizi ni akili mgando hizi! Aliyekwambia kwamba ukianzisha jambo lazima ulimalize wewe ni nani!?

Tangu wakoloni wanaingia Afrika walipokelewa vizuri!? Je, hao waliokuwa wanawapinga wao si wapigania uhuru!?

Mandela ndiye aliyeanziasha harakati za ukombozi S. Afrika? Kwanini anajulikana yeye kwa wengi?

Timu ya mpira inakuwa na wachezaji wengi lakini mwisho wa mchezo anatajwa mchezaji bora mmoja! "Man of the match"

Mtaongea mnayoongea yote lakini kwa Tangayika ' Man of the match" katika harakati za ukombozi atabaki Nyerere leo na hata milele yote

Kuwa "man of the match" hakumaanishi alipigana peke yake, hilo kila mtu analijua! Hao wengine wapo na wataendelea kuenziwa kwa nafasi zao lakini lazima mkubali kuwa hawawezi kuwekwa kwenye "rank" moja na Nyerere! HIKI NDICHO HAMKITAKI LAKINI HAMNA NAMNA LAZIMA MKUBALI TU!

Hata kwenye familia lazima atatokea mmoja atakuwa "juu" na atatambuliwa kama alama ya familia! Hii haimaanishi familia hiyo haina watu wengine!

xxx haya endelea kutukana tena maana ndo kipaji chako xxx
 
Huna hoja tu. Tusi hujatukanwa unavunga umetukanwa, jee ukitukanwa si ndiyo mwao.

Jibu kuhusu "lecturer" wako na AMNUT ulilipata juu huko au hujalipenda au ndiyo akaae kimya kakubali.

Kiislam binti akiletewa pisa huulizwa, fulani kaleta posa umekubali?" Akikaa kimya kakubali.
AMNUT kutokana na madai yake ya longo longo kama hayo hayo ambayo kila siku mnayataka ya kutaka nchi iwe ya dini ilibidi ijifie natural death tu maana ilikutana na kisiki cha Butiama!

Au kuna jibu zaidi ya hili!
 
AMNUT kutokana na madai yake ya longo longo kama hayo hayo ambayo kila siku mnayataka ya kutaka nchi iwe ya dini ilibidi ijifie natural death tu maana ilikutana na kisiki cha Butiama!

Au kuna jibu zaidi ya hili!
"Madai yake" nani?

Mbona unakuwa muoga muoga wa kuongea?


Ooh funguka tu. Kumbe ulidanganya kuhusu "lecturer"? Yalikuwa ni yako.

Onesha rangi zako kamili wacha kujifungia ndani ya kabati.
 
Hizi ni akili mgando hizi! Aliyekwambia kwamba ukianzisha jambo lazima ulimalize wewe ni nani!?

Tangu wakoloni wanaingia Afrika walipokelewa vizuri!? Je, hao waliokuwa wanawapinga wao si wapigania uhuru!?

Mandela ndiye aliyeanziasha harakati za ukombozi S. Afrika? Kwanini anajulikana yeye kwa wengi?

Timu ya mpira inakuwa na wachezaji wengi lakini mwisho wa mchezo anatajwa mchezaji bora mmoja! "Man of the match"

Mtaongea mnayoongea yote lakini kwa Tangayika ' Man of the match" katika harakati za ukombozi atabaki Nyerere leo na hata milele yote

Kuwa "man of the match" hakumaanishi alipigana peke yake, hilo kila mtu analijua! Hao wengine wapo na wataendelea kuenziwa kwa nafasi zao lakini lazima mkubali kuwa hawawezi kuwekwa kwenye "rank" moja na Nyerere! HIKI NDICHO HAMKITAKI LAKINI HAMNA NAMNA LAZIMA MKUBALI TU!

Hata kwenye familia lazima atatokea mmoja atakuwa "juu" na atatambuliwa kama alama ya familia! Hii haimaanishi familia hiyo haina watu wengine!

xxx haya endelea kutukana tena maana ndo kipaji chako xxx
Wapi wameenziwa na wakati ulikiri juu huko hata majina hujawahi kuyasikia ndiyo kwanza umeanza kuyasikia kutoka kwa Allama Mohamed Said.

Ulikuwa una enzi hewa? Unanchekesha.
 
AMNUT kutokana na madai yake ya longo longo kama hayo hayo ambayo kila siku mnayataka ya kutaka nchi iwe ya dini ilibidi ijifie natural death tu maana ilikutana na kisiki cha Butiama!
viliku
Au kuna jibu zaidi ya hili!

Uncle...
Mimi nilipoandika kitabu cha Abdul Sykes sikufanya hivyo kwa nia ya
kushusha hadhi ya Mwalimu Nyerere katika harakati za kupigania uhuru
wa Tanganyika.

Nimeandika kitabu hiki kwa nia ya kueleza historia ya TANU na harakati
za kudai uhuru kwa kuwa vitabu vyote vilivyokuwa vimeandikwa vilikuwa
vikianza na Julius Nyerere mwaka wa 1954 TANU ilipoundwa.

Kwa kufanya hivyo historia muhimu ya African Association na TAA hadi
kufika kuundwa kwa TANU ilikuwa imepotezwa.

Nimeanza kuandika nikijua kuwa historia hii haikuwa inatakiwa kwani
kulikuwa na mradi wa TANU yenyewe wa kuandika historia yake ambao
Abdul Sykes alipewa jukumu la kuandika historia hiyo akishirikiana na
Dr. Wilbard Kleruu.

Abdul Sykes hakukamilisha kazi hii alijitoa baada ya kugundua kuwa
historia iliyokuwa inatakiwa kuandikwa si ile anayoijua yeye na Abdul
akijua mengi katika historia ya TANU kwani baba yake alikuwa muasisi
wa African Association mwaka wa 1929.

Sasa unazungumza kuhusu ''ranking,'' sijui utafanya hivyo kwa vigezo
vipi kwani ikiwa ni historia ya TANU hakuna ushahidi mahali popote
unaoonyesha kuwa Nyerere alifika kwa Abdul Sykes 1952 akiwa na
''blue print,'' ya TANU.

Harakati hizi za kuunda TANU na kudai uhuru wa Tanganyika alizikuta
kwa Abdul Sykes na kabla yake yalipita mengi na kulikuwa na wengi
katika juhudi ya kufanikisha lengo hili.

Upo ushahidi wa mchango mkubwa wa Hamza Mwapachu katika kufikia
lengo la kuunda TANU na itoshe tu kuwa mkutano wa kumtia Nyerere
katika uongozi wa TAA uliofanyika nyumbani kwake Nansio, Ukerewe
miezi ya mwanzo ya mwaka wa 1953 kati ya yeye Hamza, Abdul Sykes
na Ally Mwinyi Tambwe aliyekuwa Katibu wa Al Jamiatul Islamiyya.

Hapa sikutaka kukurejesha nyuma 1950 kwenye TAA Political Subcommittee
ambayo wajumbe wake wake walikuwa: Dr. Vedasto Kyaruzi, Abdulwahid
Sykes, Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Said Chaurembo, Steven
Mhando
na John Rupia.

Wala sijataka kukuonyesha viongozi wa TAA ambao waliingia katika
uongozina Julius Nyerere pale alipochaguliwa kuwa Rais wa TAA katika
mkutano uliofanyika Ukumbi wa Arnautoglo tarehe 17 Aprili, 1953.

Viongozi hawa ni: J.K. Nyerere, President; Abdulwahid Sykes, Vice-
President;

J.P. Kasella Bantu, General Secretary; Alexander M. Tobias and Waziri
Dossa Aziz,
Joint Minuting Secretary; John Rupia, Treasurer na Ally K.
Syke
s - Assistant Treasurer. Committee members Dr. Michael Lugazia,
Hamisi Diwani, Tewa Said, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi,
C. Ongalo
na Patrick Aoko.

Sasa huwezi kufanya ''ranking,'' ya mtu mmoja lazima wawe wengi na
unaanza juu hadi unafika chini.

Ukiwa unataka kufanya ''ranking'' inabidi sasa uanze na wajumbe wa TAA
Political Subcommittee uwachanganye na hii Halmashauri ya TAA ya 1953.

Kuna wengine wamehusika sana lakini majina yao huwezi kuyaona hapo
juu mfano Earle Seaton.

Haya ndiyo yaliyonifanya mimi niandike historia ya TANU na uhuru wa
Tanganyika kusahihisha historia iliyokuwapo.

Kuhusu AMNUT nimekwisha eleza hapa kuwa ni jina tu ''Muslim,'' ndilo
linalokufanya wewe ukiite chama cha Waislam.

Waislam chama chao kilikuwa TANU.

AMNUT iliundwa 1958 na Ramadhani Mashado Plantan, Abdulwahid
Abdulkarim, Hamisi Hunde
na Abdallah Mohamed watu ambao hawakuwa
na ushawishi mkubwa katika siasa za wakati ule ukimtoa Mashado Plantan.

Hayo mengine sijaona haja ya kukujibu.
 
Back
Top Bottom