Wewe Mzee hebu tuheshimiane hiyo ruhusa nani katoa na lini??? Mr Rocky nataka maelezo ya kina hapa kumbe ndo ulikuwa hulali kumbe ndo unafanya madudu yako huku today no "Morning Groly"
sitamani kuyaona haya yakuvunjiwa ndoa ndoa.madame B
Nakushauri kama unampenda mumeo wa zamani rudi.kama humpendi vunja ukimya dai chako talaka ni haki yawote kuomba kikatiba
Umenena vema mkiva , hata kama ndoa inavunjika lazima iwe kwa utaratibu maalum unaokubalika kisheria
Kichwa cha habari Chahusika.
UTANGULIZI
Takribani wiki mbili zilizopita nilileta kwenu taarifa ya kutengua uhusiano batili kati cha Chimbuvu na mke wa mtu Madame B. Kathka taarifa ile niliwataka Madame B na Chimbuvu kusitisha maramoja uhusiano wao batili au la waurasmishe kwa sheria na taratibu halali za hapa chit chat.Hatua hiyo ilifikiwa baada ya kujitokeza yafuatayo
i.Malalamiko yaliyofikishwa mbele ya tume yangu na ndugu Ruttashobolwa ambae ndie mume halali wa Madame B
ii.Malalamiko yaliyoletwa kwangu na wanachit chat wengi tu juu ya tabia inayokera ya Madame B na Chimbuvu ya kutoheshimu ndoa hivyo kulipaka matope jukwaa tukufu la chit chat.
iii.Barua rasmi iliyoletwa kwangu na shemeji zake Madame B ambao ni ndugu zake Ruttashobolwa wakitaka hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya wahusika. ndugu hao ni Judgement, Bishanga na nitonye.
iv.Hali ya sintofahamu iliyotokea hapa jamvini baada ya Madame B kudaiwa kuwatapeli kimapenzi wadau tedo na chilli.
Baada ya taarifa ile wahusika hawakuonyesha utayari wa kutekeleza maelekezo HALALI ya tume na kuendelea na uhusiano wao unaotia kinyaa.
Tangu jana tarehe 28/11/2012 nilikuwa napitia ripoti za kamati ya SCREENING ,SHERIA na ile ya MAADILI, na baada ya kujiridhisha natoa maazimio yafuatayo
i Madame B akiri kuwa yeye ni mke halali wa Ruttashobolwa kama inavyofahamika hapa na aombe msamaha kwa wana chit chat wote kwa usumbufu aliousababisha.
ii Chimbuvu atoe tamko rasmi la kuachana na Madame B na aombe msamaha kwa usumbufu aliowasababishia wana chit chat wote.
Hayo yote yafanyike kabla ya siku ya ijumaa tarehe 30/11/2012 saa tano asubuhi. Kushindwa kufanya hivyo kutapelekea hatua zifuatazo kwa wahusika zikiwa kama ni hatua za awali.
i Madame B na Chimbuvu kutopewa LIKE na mwana chit chat yeyote katika post zao.
ii.Kuto QUOTE post yoyote ya Madame B au Chimbuvu.
iii.Kuwekwa hadharani kwa picha zao ZA AIBU walizopigwa bila wao kujua.Kazi hii itafanywa na Asprin na Mtambuzi.
iv.Kusutwa hadharani wote wawili wakiwa wamevishwa kanga na kupakwa majivu. Kazi hii itafanywa na gfsonwin cacico snowhite ,FP lara 1 Ciello na Zinduna chini ya usimamizi wa malafyale watu8 huku ikifadhiliwa na Arushaone na Bishanga.
Aidha tume inampongeza sana ndugu Ruttashobolwa kwa kuonyesha busara na utulivu wakati tume ikishughulikia suala lake.
Mwisho natoa wito kwa wadau wote kusimamia utekelezaji wa maazimio na kusimamia taratibu halali zilizowekwa.
Baba V
MWENYEKITI WA TUME ZA KURATIBU MAHUSIANO NA NDOA CHIT CHAT 2012
Baba V,siwezi toa uamuzi wowote.
Kwani mpenzi wangu wa sasa Chimbuvu sijui aliko mpaka muda huu.
Anaweza akawa ametekwa na mume wa zamani Ruttashobolwa au la.
Hvyo nataka nijue usalama wake kwanza.
Ngoja nikacheki na kile kikundi cha matarumbeta na ngoma ya kibao kata kwa ajili ya shughului hii adhimu..
Unanipigia makelele, nimelala.
Nimekuja mama wala usihofu
Baba V,siwezi toa uamuzi wowote.
Kwani mpenzi wangu wa sasa Chimbuvu sijui aliko mpaka muda huu.
Anaweza akawa ametekwa na mume wa zamani Ruttashobolwa au la.
Hvyo nataka nijue usalama wake kwanza.
Unahitaji busara sana kujadili maamuzi haya. Ukikurupuka utaharibu zaidi!
Nimerudi mamaa,ingawa jana wakati nadrive usiku nilibadilishana gari na rafiki yangu ila tulipofika njiani gari langu lililokuwa mbele lililushiwa vitu vyenye ncha kali na kumjeruhi rafiki yangu,katika purukushani wale watu walikimbia na tulimpeleka hospitali na cm yangu ilipotea ktk mazingira ya kutatanisha ila sasa suala lipo polisi,