Zakaria Lang'o
JF-Expert Member
- Apr 2, 2012
- 2,593
- 2,767
Naamini kuwa Chadema wako sawa kwa sababu iwapo wao ndio washukiwa kwa mujbu wa hoja yako, basi watakuwa wanashangaa kwanini hawahojiwi na mamlaka husika. Hivyo nakuomba uishauri mamlaka inayohusika kumtafuta Ben iwahoji Chadema.Mamlaka husika ya kumtafuta Saanane na watekaji wake ni jeshi la polisi. Kazi hiyo walishaianza tangia taarifa ya kupotea kwake ifikishwe polisi takribani wiki 3 zilizopita. Chadema ni washukiwa wa sakata hilo. Sasa chadema wanapotoa amri ya kwamba mtekwaji awe amepatikana ndani ya masaa 72, si inadhihirisha kwamba wanafahamu aliko au walikomficha?