e. Kuhakikisha kwamba hata katika mambo ambayo yanabakia
katika mamlaka ya Shirikisho, Zanzibar inakuwa na kielelezo
chake kinachotambulika, (kwa mfano (a) maaskari/majeshi
waliopo Zanzibar wawe ni Wazanzibari na hawahamishwi kikazi
kwenda upande wa pili wa muungano au kinyume chake, (b)
mtiririko wa wageni wanaongia Zanzibar uwe unadhibitiwa kwa
njia na hati zinazokubalika, n.k.),
f. Shirikisho la Tanzania liwakilishwe katika Umoja wa Mataifa kwa
viti vya Zanzibar na Tanganyika. Kwa maana hiyo, Zanzibar
irejeshe kiti chake katika umoja huo na hivyo hivyo kwa
Tanganyika, Du Mwl Nyerere alisema mtu akishaanza kusema mimi Mzanzibari na huyu Mzanzibara atajasema mimi Munguja na yule Mpemba (angalia attachment ya abdulahsf) ameshakiondoa kisiwa cha Pemba kwenye ramani ya Zanzibar
kweli hamnazo, askari walioko zanzibar wawe wazawa wa huko na wasihamishwe je hawa waliotapakaa huku bara tukiwafukuza mtaenea huko?
Kumbukeni kabla ya Uchaguzi mkuu mwaka jana katika mahojiano ITV wazanzibar waliomba wasikumbushwe Utumwa na Utwana baada ya msemaji mmoja kudai hakuna haja ya Muungano huku watazamaji kubao wakiwa wameolewa bara na wanaishi bara
Acha hayo ww vunja Muungano, na iingize hiyo ktk Katiba
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.