Tamko la Ikulu juu ya Richmond

hapa nadhani viongozi wetu wamekosa uelewa....Richmond ina mkono wa rais maana kashindwa kuwachukulia hatua wote waliotajwa kwenye riport!!!
 


Mambo Aliyofanya Rais
Katika suala zima la kukodisha mitambo ya kuzalisha umeme, Rais alihusika katika mambo manne. Kwanza, katika kuamua TANESCO itumie mitambo ya kukodi kuzalisha umeme na Serikali igharamie ukodishaji huo. Suala hilo lilikuwa lazima liamuliwe na yeye kwa sababu lilikuwa linahitaji Serikali kugharamia ukodishaji. Kama si hivyo lisingefikishwa kwake kwani ni jambo ambalo lingekuwa juu ya TANESCO kuamua kukodisha na kulipia. Gharama hizo hazikuwa zimepangwa katika bajeti ya serikali hivyo ilikuwa ni lazima kupata idhini ya Rais ya kutafuta hizo pesa na kuzitumia kwa ajili hiyo.


Pili, Rais alihusika katika kuzungumza na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kuwaomba wakubali sehemu ya pesa waliyopanga kuipa Tanzania kama msaada kutokana na mpango wa msamaha wa madeni itumike kugharamia ukodishaji wa mitambo ya kuzalisha umeme. Walikubali, na USD 225 milioni zilitumika kukodisha mitambo ya Kampuni za Aggreko, Alstom na Richmond (ambayo baadae ikawa Dowans) na matumizi mengine ya dharura za umeme. Matumizi hayo mengine yalijumuisha pia ununuzi wa mitambo ya aina ya Watsilla ya kuzalisha megawati 100 za umeme pale Ubungo kwa kutumia gesi asilia. Mitambo hiyo imeshanunuliwa, kufungwa na tayari inazalisha umeme.


Tatu, Rais alihusika katika vikao vya Baraza la Mawaziri vilivyojadili matatizo ya upungufu mkubwa wa umeme nchini na kuamua hatua mbalimbali za kukabiliana na tatizo hilo. Moja ya hatua zilizoamuliwa kuchukuliwa, ni hii ya kukodisha mitambo ya kuzalisha umeme. Katika vikao hivyo vya Baraza la Mawaziri alitoa maelekezo ya mambo ya kuzingatiwa katika zoezi zima la kupata makampuni au watu watakaotoa huduma hiyo. Hususan, Rais alisisitiza kuwa pamoja na udharura uliokuwepo Kanuni na Sheria ya Ununuzi wa Umma zizingatiwe.


Nne, Rais alikataa Kampuni ya Richmond isipewe malipo ya awali (down payment) ya USD 10 milioni na kutaka ukweli kuhusu uaminifu na ukamilifu (integrity) wa kampuni hiyo ujulikane. Rais alikataa maombi yaliyopelekwa kwake na Wizara ya Nishati na Madini ya kumuomba aagize Wizara ya Fedha, iilipe kampuni hiyo fedha hizo. Rais aliagiza Wizara ya Fedha ibaki na msimamo wake na kuitaka Wizara ya Nishati na Madini pamoja na TANESCO wafanye mambo mawili. Kwanza, wafanye utafiti zaidi kujua undani wa Kampuni ya Richmond. Isije kuwa ni kampuni bandia wakapewa fedha wakatokomea nazo na mitambo isipatikane na hukuna namna ya kuipata kampuni wala wahusika wake. Pili aliagiza wawatake viongozi wa Kampuni ya Richmond kwanza walete mitambo, ikishafika, ndipo walipwe. Maagizo hayo ya Rais yalizingatiwa na Kampuni ya Richmond ikapewa sharti hilo. Lakini, ikashindwa kulitekeleza na kuishia kuingia mkataba na Kampuni ya Dowans iliyokuja kuleta hiyo mitambo badala yake.


Wakuu zangu, mimi nimetatizwa na mtililiko wa mambo alofanya rais kiasi kwamba inaonyesha kuwa mwandishi kaaza na mambo ya mwisho kurudia mwanzo. Ukisoma kwa makini utagundua kwamba haiwezekani swala la Tanesco kutumia mitambo ya kukodisha liwe la kwanza kabla ya baraza la mawaziri kukaa kujasdili matatizo ya Umeme nchini na udharura wake..Hivyo maagizo yake ya kuzingatia kanuni na sheria yanatangulia maamuzi ya Tanesco kununua mitambo toka mashirika hayo na serikali igharamie..
Hivyo nambari tatu inatakiwa kuwa jambo la kwanza kwa mtazamo wangu.. Sasa utata unakuja pale rais alipokwenda kuomba fedha IMF..isingewezekana yeye kwenda omba fedha IMF kama report ya mashirika hayo ina utata..na alitakiwa kuzisoma na kuzielewa kabla hajawakilisha majina yao IMF.. mambo yote aliyosema yazingatiwe hayakuzingatiwa, iweje yeye kama rais wa nchi awakilishe jumla ya fedha zinazohitajiwa kwa ununuzi wa mitambo ambayo yeye hafahamu breakdown yake. Nikiwa na maana JK alifahamu fika Richmond wapo ktk hesabu na wanahitaji kiasi gani kulingana na taarifa ya Luhanjo.. amesema hivi:- Pili, Rais alihusika katika kuzungumza na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kuwaomba wakubali sehemu ya pesa waliyopanga kuipa Tanzania kama msaada kutokana na mpango wa msamaha wa madeni itumike kugharamia ukodishaji wa mitambo ya kuzalisha umeme. Walikubali, na USD 225 milioni zilitumika kukodisha mitambo ya Kampuni za Aggreko, Alstom na Richmond (ambayo baadae ikawa Dowans) na matumizi mengine ya dharura za umeme.

Kwa hiyo JK aliwakilisha maombi yetu IMF, Richmond ikiwa ktk hesabu ya mashirika amabyo yatafua umeme na ndio maana wakawa ktk fungu la fedha zilizotolewa..
Jambo la mwisho ambalo sijui kama Lusanjo anafikria sisi wananchi wajinga sana..Richmond ilianza kudai kuzalisha na generator moja kabla mkataba haujahamia Dowans.

Tunakumbuka vizuri kuwa generator ya kwanza (moja) ilipoingia nchini chini ya jina la Richmond na hata meneja wa shirika hilo alizungumza ktk magazeti yetu akidai uzalishaji utaanza mara moja...nakumbuka vizuri hata Michuzi alituonyesha mtambo huo ktk Blog yake pindi ilipowasili nchini chini ya jina la Richmond na sii Dowans, sasa iweje leo tunaambiwa rais alikataa BoT kuwapa Richmond down payment wakati swala hilo liliibuka baada ya wananchi kugundua kwamba Richmond ilikuwa shirika feki..
Hiyo kazi au niseme jambo la mwisho alofanya rais ni baada ya kugundua kuwa Richmond ni shirika feki ndipo alipokataa na kuomba uchunguzi ufanyike kinyume cha hapo aidha rais alifahamu mchezo mzima au hakufahamu jambo ambalo linamweka ktk udhaifu wa uongozi..


Haiwezekani kabisa kuwa rais hakuhusika kwa sababu yeye ndiye muidhini wa gharama zote za matumizi hayo, hivyo yawezekana kabisa hata yeye hakufahamu alichokuwa akikubali kama alivyodai Mama Meghji ktk fedha za BoT, zilizochotwa na Balali au alifahamu sana isipokuwa bomu limelipuka.. Na kibaya zaidi ni kwamba kama alikuwa hafahamu iweje hadi leo hii kashindwa kabisa kuchukua hatua zinazotakiwa wakati swala zima liko wazi kabisa na ushahidi umejianika wenyewe..


































 
Last edited:
Raisi alihusika moja kwa moja na swala la richmondi kwa nini alimkata Idrisa asijiuzuru alipotishia kujiuzuru pale angesimamisha mipango yoye ya manunuzi lakini kwa sababu aliruhusu idrisa arudi kazini naakaidhinisha malipo ya awali inathibitisha jinsi na yeye alivyouvaa ufisadi
 
watanzania wakipata uhuru wa kuongea, wanautumia vibaya. Siyo uungwana hata kidogo kumuita rais wetu 'idiot'. Kamwe siwezi kukubaliana na utovu huu wa nidhamu uliokithiri. Rais ni 'head of state' ndiyo 'baba' yetu. Sasa wewe unaweza ukamuita baba yako mzazi 'idiot'? HAPANA, tusifikishwe huko. Kinachotakiwa katika 'blog' hii ni hoja zenye mantiki kwa faida ya nchi yetu na siyo matusi yasiyo na tija.

Ni kweli JK ana mapungufu, kwani yeye ni binadamu kama sisi. Lakini pamoja na mapungufu hayo JK 'has this country at heart". Hana utajiri, ni 'mlalahoi' mwenzetu; hana makuu. JK ni mchukia rushwa na ufisadi, hana uroho wa kujilimbikizia mali. Amefananafana na Mwalimu Nyerere kwa upande wa tabia na kuipenda nchi yake na watu wake.

Lakini ni kweli tamko hilo la IKulu kuhusu Richmond lina kasoro. Hakukuwa na sababu ya kutoa tamko hilo. Maelezo hayo yangeweza kutolewa katika namna nyingine lakini siyo kutolewa na IKULU. Kwa maoni yangu kuna kasoro na mapungufu mengi kuhusiana na baadhi ya watendaji wa IKULU. Tukumbuke IKULU ni 'taasisi' nyeti. Inapaswa iwe na watu makini na waadilifu. Sina hakika sana kama kweli baadhi ya watu ndani ya IKULU ni makini na waadilifu kwa kiwango cha kutotiliwa shaka. Sina hakika na hili, kama kweli baadhi wanaipenda nchi na ni watendaji wazuri.

Suala hili la Richmond lisipofanyiwa kazi kwa umakini linaweza likaigawa nchi yetu. Mjadala ndani ya Bunge kwa hakika haukuwa mzuri kwa umoja wetu. Nina hofu ya kitakachotokea mjadala huu ukianza tena na kuendelea zaidi.


Duuu....

Natumai huyu ni mtengeneza kura na sio mpiga kura anayetegemewa kuleta 'mabadiliko' 2010....

Yaani uhuni huu wa RICHMOND ugawe nchi na sio yale ya Waraka wa Wakatoliki na Mahakama ya Kadhi ya waislamu.....

omarilyas
 
Kikwete makamasi yanamtoka, anachukua shati lake chafu alilovaaa na kujipangusa makamasi hayo, katika kujipangusa huko anayatapakaza zaidi kutoka puani kwenda uso wote sasa...

Yaani hawa jokers hata kuandika wameshindwa!
 
1954,
Unaposema JK anafananafanana na Mwalimu unasema uwongo. Yeye mwenyewe kwa kauli yake amejiweka katikati ya Mwinyi na Mpaka. Na hawa tunawajua kuwa ndio magwiji wa ufisadi. Conclusion: therefore hata Kikwete mwenyewe ni fisadi.
 
This is stupid & wrong move

sasa msemaji wa ikulu ni nani? Luhanjo, salva au wale ma mediocres wengine?


Ikulu imekuwa kama chaka la incompetents...yaani media wanaset Agenda halafu wao wanafuata

hiii issue as far as i know uchunguzi haujakamilika nau liko mikononi mwa vyombo vya sheria sasa whats this kujibizana na media...sometimes i dont understand those ******...tangu juzi naona wanatoa statements kila kukicha

why pick a fight wanajua clearly they cant win? Just wehn tunataka kujua kwa nini miradi ya Milleium Challenge Account ina delay wao wanataka kufufua mambo ambayo yatawatoa from main agenda ya kuwahudumia wananchi

sasa sijui nani kawaambia kuwa its better kujibizana kuhusu mambo haya..ukweli ni kuwa wakishatoa statement next week nzima wataandamwa mpaka mwiki mbili...sasa wakishatoa hii whats next? watajibu na Meremeta ? then baada ya hiyo watajibu na kwa nini kamati ya mauaji ya Mwembechai haijaundwa mpaka leo?

hawa jamaa wanatia kinyaa sana

I guess the only person than can save JK's presidency ni Mama Salma maana husikii wao kujibizana na media..huu ni mtego na i am not sure they will get themselves out of it

Sasa kama watafuata ushauri wako ni lini tutakuwa na serikali inayowajibika kwa wananchi.

Nadhani aliyekosea hapa ni Salva kwa kutoa taarifu isiyokamilika na kitendo cha taarifa ya pili kutolewa na Luhanjo kunaamaanisha kuwa taarifa ya mwanzo ilikosa uwazi, ukweli na umakini....Uncle Ben Nkapa angeita ya ujanjaujanja...

Heko Ikulu kwa kuonyesha kuwa RESPONSIVE and DECISIVE angalao kwa hili ingawa mengine naona bado kuna kusuasua kwa sana.

omarilyas
 
Kwamba Raisi Jakaya Mrisho Kikwete hakuhusika kabisa katika sakata la Richmond, ni kichekesho cha mwaka na kama ni kweli basi ni dalili mbaya sana kwa hatma ya taifa. Mbona iko hatari ya taifa kuuzwa na wajanja na Raisi asiwe na habari ingawa Waziri Mkuu, mawaziri kadhaa na maofisa wengine wa serikali aliowateua yeye mwenyewe wanahusika - huyo Raisi hatufai, period.

Kutoka Richmond hadi shemeji Dowans na sasa shangazi Noor oil, tunarudi kule kule ! Watanzania tutalia sana lakini mzimu wa Babu Kagoda utatutafuna bila huruma. Hapo hapo kamanda CCM anazidi kukusanya nguvu, majeshi yake yakijitayarisha kutoa pigo lingine 2010 huku wananchi tukizidi kuuchapa usingizi. Ikulu yamtetea JK, Bunge lamtetea SS, tumpate wapi wa kututetea !
 
Yaani this thing is simple na nashangaa kwanini wanatumia nguvu nyingi na kuita wahariri,kupoteza muda na kutusumbua tu.

Ndiyo Jk hausiki nani anahusika sasa,kwanini wasimtaje jina?na kama walipuuzia maagizo ya Mkulu walichukuliwa hatua gani?

Navyojua Rais ana uwezo wa kutengua uteuzi wa mtu yeyote,alifanya aliutenguza uteuzi wa balali(usanii flani).Hata hili linawezekana kabisa na afanye sana.

Hili suala la RDC ni siasa za maji taka ambazo wamezipiika wao wenyewe.tatizo ni uwaziri mkuu na hawana lolote.Tokea six alipokosa U-PM basi imekuwa vuru vuru mechi tu..

sasa watamalizana wao kwa wao na mie naona tuangalie 2010..tunampa nani Nchi,Je tunaamua kumsuport Mkwere au tunaunganisha nguvu na kuchagua Chaguo La Mungu.

- Mkulu Gembe, yaani imekuchukua all this years kuona mwanga, wellcome to the club, ndio maana tunasema JF ni shule nzito sana, hata wewe duh1 ubarikiwe na Mungu wa Mbinguni mazee.

Respect.

Field Marshall Es!
 
The only thing that shall save us ni sisi wenyewe kubadilika,mnaonaje mwaka 2010 tupeleke wapinzani wengi bungeni maana italeta changamoto bungeni na hata mambo ya kifisadi yatakemewa kwa nguvu zote,naomba mnipe habari juu ya majaji waliochaguliwa siku za karibuni na bwana JK,wana vigezo au tuseme ndo ule msemo wa kupeana shavu unatimizwa.
 
Ni watanzania wenyewe watakaojiletea maendeleo. Zimwi la Richmond linatajwa kila wakati ili kufukia madudu mengine yanayotokea kwa sasa. Suala la kuua watu North Mara halafu Mkuu wa Mkoa alishasema hakuna tatizo na pia waka mislead Kagasheki alipotembelea siyo issue kubwa? Wanataka watu wangapi na wanyama kiasi gani na bionuwai kiasi gani iharibike ili hatua ichukuliwe? Swala la Richmond ni la ubishi ubishi tu lakini hili la watu kufa... linahitaji attention ya haraka sana, lakini govt is becoming deaf...
 
.............................. Watendaji wa IKULU wawe makini sana na masuala nyeti kama haya.

Yatakiwa wawe hivyo! Tatizo ni kwamba, ili wawe makini ni lazima wawe na uwezo huo. Na muhimu zaidi wawe na ufahamu kwamba wasipokuwa makini matatizo haya au yale yatawapata.

Kwa hali ya hapo Ikulu, nani ni makini? kwa sababu hata aliye juu kabisa si makini na mana hiyo hakuna atakayewapa taabu wasio makini.

Tukubali kwamba, wazembe wa kufikiri, ni ktk nyanja zooote! Na hata wakiamua kujinyonga, usishangae kuwakuta kwenye jani la mgomba. Hawawezi hata kuchangua tawi imara!
 
Nuilidhani mwisho wa mwezi uliopita mukulu mwenye we angeliongelea hili kwa undani kwenye hotuba zake za kila mwisho wa mweZi.... oh! hivi zilifutwa vile eh????
 
Nuilidhani mwisho wa mwezi uliopita mukulu mwenye we angeliongelea hili kwa undani kwenye hotuba zake za kila mwisho wa mweZi.... oh! hivi zilifutwa vile eh????
Mwenyewe nikadhani labda huwa nachelewa kuangalia Tv. Alifuta utaratibu wake wa kuongea na Taifa kila mwisho wa mwezi? Sababu ni nini hasa?

Dah, kazi ipo!
 
Let me breakdown this thing:

a. Baada ya Lowassa kuuzira Uwaziri Mkuu kamwe hakumsamehe Kikwete. Na wakati Kikwete alipopata nafasi ya kumsafisha (kwenye ule mkutano na wazee Dar) hakufanya hivyo hasa bali alimtengenezea godoro la kuangukia pale aliposema Lowassa kujiuzulu ilikuwa ni ajali ya kisiasa.

Watu wengi hawakumbuki maneno yaliyotangulia hilo la "ajali ya kisiasa". Hivyo ikumbukwe kuwa Kikwete hakuwa na jinsi isipokuwa kukubali kujiuzulu kwa Lowassa.

b. Mawaziri wote watatu (Lowassa, Karamagi na Msabaha) hakuna hata mmoja wao aliyekubali kufanya makosa. Karamagi alisema hakuwa Waziri wakati huo, Msabaha alisema yeye Bangusilo na Lowassa alisema hakupewa nafasi kujitetea. Wote walitaka Watanzania waamini kuwa Richmond ilitoka hewani na ikafanikiwa kuingia na kupewa tenda na mizimu!


c. Baada ya wao kujiuzulu chaguo la Waziri Mkuu mpya lilikuwa la nani anaweza kuwasafisha wakuu hao na hasa Lowassa? Pinda. Kama mnavyojua Pinda alikuwa ni Waziri chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Hivyo, Pinda alipoingia alikuwa na mission moja kubwa nayo ni kumsafiisha Lowassa na watu wote waliotajwa kwenye ile ripoti.

d. Lowassa asingeweza kusafishika bila ya kuwasafisha watendaji wengine. Kama Lowassa alijiuzulu kwa sababu ya makosa ya watu walio chini yake na kama kina Karamagi na Msabaha nao walijiuzulu kwa sababu ya makosa ya watu walio chini yao je itakuwaje kama tutawaonesha kuwa walio chini hawakufanya makosa wanayodaiwa kuyafanya?

e. Hapo ndipo kwa kukiuka Katiba Pinda akaruhusu uchunguzi mwingine nje ya ule wa Bunge. Katika hili alifanya makosa mawili ambayo ingekuwa nchi nyingine angetakiwa kujiuzulu. Kwanza, alivunja Katiba kwa kutotii maagizo ya Watanzania juu ya Richmond. Bunge lina madaraka ya kuisimamia serikali na Bunge limefanya uchunguzi na kutoa maelekezo ya nini kifanyike. The ONLY response ya serikali ilitakiwa kutii. Kosa la pili, linatokana na hilo la kwanza nalo ni Pinda ameonesha dharau kwa Bunge (contempt of parliament).

Baada ya Lowassa, Karamagi na Msabaha kujiuzulu na baraza la mawaziri kujiuzulu na kuundwa kwa baraza jipya kilichotakiwa kufanyika ni mwanyika, Hosea na watumishi wote waliotajwa kwenye ile ripoti kuwa wawajibishwe waalitakiwa kuandika barua zao za kujiuzulu vile vile. Hawakutakiwa kuomba kutoa maelezo ya ziada n.k Walitakiwa kulitii Bunge.


f. Hapa ndipo penye tatizo. Tangu Februari mwaka jana Bunge limekubali kudharauliwa na kupuuzwa. Bunge limeshindwa kuidhibiti serikali na kuipa nafasi ya kuendelea kulipuuza. Matokeo yake ni hili la sasa ambapo Bunge limesema aidha maelekezo ya Bunge yatekelezwe au Rais alivunje watu warudi kuomba kura upya.

Huu ni msimamo wenye nguvu na dhaifu kwa wakati mmoja. Ni wenye nguvu kwa sababu Bunge linadai haki yake ya kuisimamia serikali na kuishauri. Serikali haina uchaguzi juu ya hilo. ni dhaifu kwa sababu wakisema warudi kwenye kupiga kura sasa hivi ni wangapi waliopo sasa watarudi tena? Je wako tayari kupoteza viti vyao sasa hivi?

So what we are waiting is the looming showdown between the executive and the legislature. Matokeo yake mwamuzi atakuwa the Judiciary! and that my friends is democracy at work!
 
JK kama hakuhusika ameshindwa nini kuwawajibisha waliofanya uozo? Nae mwizi tu. Yote majizi.
 
Back
Top Bottom