Ngambo Ngali
JF-Expert Member
- Apr 17, 2009
- 3,517
- 1,360
Taarifa kwa vyombo vya Habari
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa inafuatilia kwa ukaribu taarifa kuhusu uamuzi wa Mahakama ya Southwark mjini London, Uingereza kuiamuru Kampuni ya BAE Systems ya Uingereza kulipa faini ya Paundi za kiingereza laki tano 500,000 kwa kushindwa kuweka kumbukumbu sahihi za kihasibu kuhusu fedha zilizolipwa na kampuni ya BAE Systems kwa Mfanyabiashara Shailesh Vithlani wa Tanzania miaka mitano iliyopita.
Serikali ya Tanzania,kupitia Ubalozi wetu nchini Uingereza imeomba taarifa rasmi kutoka Serikali ya Uingereza kuhusu uamuzi huo. Serikali inasubiri kwa hamu kubwa kurejeshwa kwa bakaa ya Dola Milioni 30 za Kimarekani kama ilivyokuwa katika makubaliano kati ya Idara ya Serious Fraud (SFO) na Kampuni ya BAE Systems baada ya kuondoa faini ya kiasi cha Paundi Laki tano za Kiingereza ambazo kampuni ya BAE Systems imeamuriwa kuilipa Mahakama ya Southwark mjini London.
Mara baada ya kupata taarifa rasmi, Serikali ta Tanzania itachukua hatua muafaka ikiwa ni pamoja ni pamoja na urejeshwaji wa kiasi cha fedha kinachotakiwa kurejeshwa Tanzania kulingana na makubaliano kati ya SFO na Kampuni ya BAE Systems.
Imetolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
22 Desemba, 2010
Source: issamichuzi.blogspot.com
Taarifa ya foreign affairs kuhusu chenji ya radar, nimependa hapo kwenye red, swali wanasuburi kwa hamu kwa nia njema na manufaa ya walalahoi au zitarudi tena kulekule???????
Mbona mambo ya ndani wako kimya kuhusu hili pamoja na kuwa BAE wamekiri kosa la Rushwa lilikuwa merinated kutoka kosa la rushwa na kwenda mwenye kosa la kutoweka kumbukumbu sahihi huku kwetu wahusika mustakabali wao unakuwaje????
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa inafuatilia kwa ukaribu taarifa kuhusu uamuzi wa Mahakama ya Southwark mjini London, Uingereza kuiamuru Kampuni ya BAE Systems ya Uingereza kulipa faini ya Paundi za kiingereza laki tano 500,000 kwa kushindwa kuweka kumbukumbu sahihi za kihasibu kuhusu fedha zilizolipwa na kampuni ya BAE Systems kwa Mfanyabiashara Shailesh Vithlani wa Tanzania miaka mitano iliyopita.
Serikali ya Tanzania,kupitia Ubalozi wetu nchini Uingereza imeomba taarifa rasmi kutoka Serikali ya Uingereza kuhusu uamuzi huo. Serikali inasubiri kwa hamu kubwa kurejeshwa kwa bakaa ya Dola Milioni 30 za Kimarekani kama ilivyokuwa katika makubaliano kati ya Idara ya Serious Fraud (SFO) na Kampuni ya BAE Systems baada ya kuondoa faini ya kiasi cha Paundi Laki tano za Kiingereza ambazo kampuni ya BAE Systems imeamuriwa kuilipa Mahakama ya Southwark mjini London.
Mara baada ya kupata taarifa rasmi, Serikali ta Tanzania itachukua hatua muafaka ikiwa ni pamoja ni pamoja na urejeshwaji wa kiasi cha fedha kinachotakiwa kurejeshwa Tanzania kulingana na makubaliano kati ya SFO na Kampuni ya BAE Systems.
Imetolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
22 Desemba, 2010
Source: issamichuzi.blogspot.com
Taarifa ya foreign affairs kuhusu chenji ya radar, nimependa hapo kwenye red, swali wanasuburi kwa hamu kwa nia njema na manufaa ya walalahoi au zitarudi tena kulekule???????
Mbona mambo ya ndani wako kimya kuhusu hili pamoja na kuwa BAE wamekiri kosa la Rushwa lilikuwa merinated kutoka kosa la rushwa na kwenda mwenye kosa la kutoweka kumbukumbu sahihi huku kwetu wahusika mustakabali wao unakuwaje????