Tamko la Foreign Affairs kuhusu kesi ya Radar

Ngambo Ngali

JF-Expert Member
Apr 17, 2009
3,517
1,359
Taarifa kwa vyombo vya Habari

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa inafuatilia kwa ukaribu taarifa kuhusu uamuzi wa Mahakama ya Southwark mjini London, Uingereza kuiamuru Kampuni ya BAE Systems ya Uingereza kulipa faini ya Paundi za kiingereza laki tano 500,000 kwa kushindwa kuweka kumbukumbu sahihi za kihasibu kuhusu fedha zilizolipwa na kampuni ya BAE Systems kwa Mfanyabiashara Shailesh Vithlani wa Tanzania miaka mitano iliyopita.

Serikali ya Tanzania,kupitia Ubalozi wetu nchini Uingereza imeomba taarifa rasmi kutoka Serikali ya Uingereza kuhusu uamuzi huo. Serikali inasubiri kwa hamu kubwa kurejeshwa kwa bakaa ya Dola Milioni 30 za Kimarekani kama ilivyokuwa katika makubaliano kati ya Idara ya Serious Fraud (SFO) na Kampuni ya BAE Systems baada ya kuondoa faini ya kiasi cha Paundi Laki tano za Kiingereza ambazo kampuni ya BAE Systems imeamuriwa kuilipa Mahakama ya Southwark mjini London.

Mara baada ya kupata taarifa rasmi, Serikali ta Tanzania itachukua hatua muafaka ikiwa ni pamoja ni pamoja na urejeshwaji wa kiasi cha fedha kinachotakiwa kurejeshwa Tanzania kulingana na makubaliano kati ya SFO na Kampuni ya BAE Systems.

Imetolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

22 Desemba, 2010

Source: issamichuzi.blogspot.com

Taarifa ya foreign affairs kuhusu chenji ya radar, nimependa hapo kwenye red, swali wanasuburi kwa hamu kwa nia njema na manufaa ya walalahoi au zitarudi tena kulekule???????

Mbona mambo ya ndani wako kimya kuhusu hili pamoja na kuwa BAE wamekiri kosa la Rushwa lilikuwa merinated kutoka kosa la rushwa na kwenda mwenye kosa la kutoweka kumbukumbu sahihi huku kwetu wahusika mustakabali wao unakuwaje????
 
mkuu, hiyo chenji inarudi kwenye mzunguko wa ufisadi mwingine , si unajua tena 2015 siyo mbali?.......................
 
grrrrrr...sometimes hili linchi bana... miviongozi inatupayukia kuhusu rejesho la hela, hali wengi wetu usongo wetu ni kuona wahusika wa huu uhujumu uchumi wanaozea jela!!

Sijui, labda tusubirie tamko la wizara ya mambo ya ndani na la polisi wetu... ukiachilia huyo Vithlani aliyekimbia, lazima kuna viongozi waliohusika...
 
We jamaa yangu wee, hivi unataka serikali yetu ichukue hatua gani tena zaidi ya kutoa tamko kwa vyombo vya habari, na wakubwa kukaa mkao wa kula?
 
hahahahha yaaaaani hawa watu eti inafuatilia kwa karibu.
Karibu si wanaye chenge mbona wameshamsafisha.

Hizi sanaa nyingine zinatia kinyaa.
Na vipi kuhusu Ule UFISADI wa jengo na Ubalozi wa Italy
 
hivi jamani kuna mtu anajua makadirio ya ujenzi wa daraja la kigamboni? Badala ya serikali kupitisha bakuli kwanini isipeleke pesa hiyo yote either kwenye ujenzi wa daraja la kigamboni au hata kutatua tatizo la umeme Kigoma au pengine pesa hiyo ikatumika kuweka mtandao wa maji toka kimbiji kuja temeke,kitunda,pugu na maeneo mengine ambayo yana uhaba mkubwa wa maji safi na salama?
 
wizara iseme pia Watanzani waliosababisha aibu hiyo watachukuliwa hatua gani?
 
hivi jamani kuna mtu anajua makadirio ya ujenzi wa daraja la kigamboni? Badala ya serikali kupitisha bakuli kwanini isipeleke pesa hiyo yote either kwenye ujenzi wa daraja la kigamboni au hata kutatua tatizo la umeme Kigoma au pengine pesa hiyo ikatumika kuweka mtandao wa maji toka kimbiji kuja temeke,kitunda,pugu na maeneo mengine ambayo yana uhaba mkubwa wa maji safi na salama?

Utaambiwa hizi pesa zilishapelekwa kwenye mfuko maalumu tumboni kwa mtu...hakuna mtu/kiongozi mwenye mawazo kama yako...
sometime nikifikiria hii nchi...ni kama mwanamke kahaba ambaye amekataa tamaa na yeye haangalii nani analala naye na wala hadai pesa wala chochote....
 
Taarifa kwa vyombo vya Habari

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa inafuatilia kwa ukaribu taarifa kuhusu uamuzi wa Mahakama ya Southwark mjini London, Uingereza kuiamuru Kampuni ya BAE Systems ya Uingereza kulipa faini ya Paundi za kiingereza laki tano 500,000 kwa kushindwa kuweka kumbukumbu sahihi za kihasibu kuhusu fedha zilizolipwa na kampuni ya BAE Systems kwa Mfanyabiashara Shailesh Vithlani wa Tanzania miaka mitano iliyopita.

Serikali ya Tanzania,kupitia Ubalozi wetu nchini Uingereza imeomba taarifa rasmi kutoka Serikali ya Uingereza kuhusu uamuzi huo. Serikali inasubiri kwa hamu kubwa kurejeshwa kwa bakaa ya Dola Milioni 30 za Kimarekani kama ilivyokuwa katika makubaliano kati ya Idara ya Serious Fraud (SFO) na Kampuni ya BAE Systems baada ya kuondoa faini ya kiasi cha Paundi Laki tano za Kiingereza ambazo kampuni ya BAE Systems imeamuriwa kuilipa Mahakama ya Southwark mjini London.

Mara baada ya kupata taarifa rasmi, Serikali ta Tanzania itachukua hatua muafaka ikiwa ni pamoja ni pamoja na urejeshwaji wa kiasi cha fedha kinachotakiwa kurejeshwa Tanzania kulingana na makubaliano kati ya SFO na Kampuni ya BAE Systems.

Imetolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

22 Desemba, 2010

Source: issamichuzi.blogspot.com

Taarifa ya foreign affairs kuhusu chenji ya radar, nimependa hapo kwenye red, swali wanasuburi kwa hamu kwa nia njema na manufaa ya walalahoi au zitarudi tena kulekule???????

Mbona mambo ya ndani wako kimya kuhusu hili pamoja na kuwa BAE wamekiri kosa la Rushwa lilikuwa merinated kutoka kosa la rushwa na kwenda mwenye kosa la kutoweka kumbukumbu sahihi huku kwetu wahusika mustakabali wao unakuwaje????

Sisi tunstaka waliohusika huku kwetu wanashughulikiwa ipasavyo si issue ya kudai fidia.
 
Kweli nchi hii ina majuha wa kupitiliza. Hivi serikali ya CCM wan akimbilia hizo pesa huku kuna kesi dhidi ya Chenge na wengine ambayo upelelezi wake uliisha na kungojea tu kufika mahakamani kama inavyoeleza dokezo la Wikileaks hapa chini akinukuliwa si mwingione bali Hosea mwenyewe?

Mimi naona serikali ya UK iweke sharti kwamba isilipe fidia hiyo hadi watuhumiwa wa rada hapa TZ wafikishwe mahakamani na kuhukumiwa, kama vile serikali ya UK ilivyofanya kwa BAE (mtuhumiwa waliotoa rushwa) -- walifikishwa mahakamani na kutozwa faini. Ni lazima serikali yetu huku nayo ionekana inalishughulikia suala hili la radar. Kweli JK na timu yake hawafai kuongoza nchi hii ki-uadilifu.





PCB: Ready to Prosecute the BAE Radar Deal
------------------------------------------
¶2. (C) Edward Hoseah, Director General of the Prevention of
Corruption Bureau (PCB) told the DCM that the PCB was almost
finished with its investigation of the U.K.- Tanzanian BAE
radar deal and that it intended to prosecute the case. "We
are focused on the 31 percent commission paid to BAE. We
understand that businessmen need commissions but the question
is whether 31 percent is lawful or not," Hoseah said. He
called the deal "dirty" and said it involved officials from
the Ministry of Defence and at least one or two senior level
military officers.

¶3. (C) Hoseah said that the two primary suspects, XXXXXXXXXXXX and Shailesh Vithlani, CEO of
Merlin International, were currently out of the country but
that when they returned the GOT would begin to prosecute. "I
have obtained President Kikwete's support to prosecute the
culprits once they return to Tanzania," he said, stressing
that prosecution of the case would mark an important
milestone in the PCB's struggle. "The real signal of the
GOT's political commitment will be when we take this radar
case to court," Hoseah said.

¶4. (C) Note: Shailesh Vithlani is a British citizen who
reportedly grew up in Tanzania. He heads Merlin
International, a Dar es Salaam based company. Merlin
International has been implicated as the agent for Britain's
BAE Systems which sold a USD 40 million military radar system
to the GOT in 2002. Beyond the BAE radar deal, Merlin has
been linked in the media to a range of other high profile
government deals including the sale of a Gulfstream
presidential jet to former President Benjamin Mkapa.
According to a July 13 report in This Day, a local newspaper,
at the time of the BAE deal, Vithlani's local partner was
Tanil Somaiya of Shivacom Tanzania Ltd.
 
Kweli nchi hii ina majuha wa kupitiliza. Hivi serikali ya CCM wan akimbilia hizo pesa huku kuna kesi dhidi ya Chenge na wengine ambayo upelelezi wake uliisha na kungojea tu kufika mahakamani kama inavyoeleza dokezo la Wikileaks hapa chini akinukuliwa si mwingione bali Hosea mwenyewe?

Mimi naona serikali ya UK iweke sharti kwamba isilipe fidia hiyo hadi watuhumiwa wa rada hapa TZ wafikishwe mahakamani na kuhukumiwa, kama vile serikali ya UK ilivyofanya kwa BAE (mtuhumiwa waliotoa rushwa) -- walifikishwa mahakamani na kutozwa faini. Ni lazima serikali yetu huku nayo ionekana inalishughulikia suala hili la radar. Kweli JK na timu yake hawafai kuongoza nchi hii ki-uadilifu.





PCB: Ready to Prosecute the BAE Radar Deal
------------------------------------------
¶2. (C) Edward Hoseah, Director General of the Prevention of
Corruption Bureau (PCB) told the DCM that the PCB was almost
finished with its investigation of the U.K.- Tanzanian BAE
radar deal and that it intended to prosecute the case. “We
are focused on the 31 percent commission paid to BAE. We
understand that businessmen need commissions but the question
is whether 31 percent is lawful or not,” Hoseah said. He
called the deal “dirty” and said it involved officials from
the Ministry of Defence and at least one or two senior level
military officers.

¶3. (C) Hoseah said that the two primary suspects, XXXXXXXXXXXX and Shailesh Vithlani, CEO of
Merlin International, were currently out of the country but
that when they returned the GOT would begin to prosecute. “I
have obtained President Kikwete’s support to prosecute the
culprits once they return to Tanzania,” he said, stressing
that prosecution of the case would mark an important
milestone in the PCB’s struggle. “The real signal of the
GOT’s political commitment will be when we take this radar
case to court,” Hoseah said.

¶4. (C) Note: Shailesh Vithlani is a British citizen who
reportedly grew up in Tanzania. He heads Merlin
International, a Dar es Salaam based company. Merlin
International has been implicated as the agent for Britain’s
BAE Systems which sold a USD 40 million military radar system
to the GOT in 2002. Beyond the BAE radar deal, Merlin has
been linked in the media to a range of other high profile
government deals including the sale of a Gulfstream
presidential jet to former President Benjamin Mkapa.
According to a July 13 report in This Day, a local newspaper,
at the time of the BAE deal, Vithlani’s local partner was
Tanil Somaiya of Shivacom Tanzania Ltd.






Mi naona viongozi wetu wanalaaana...Ishu kama hii haiitaji mjadala....shame on them.
 
haya mafisi na mabweha yanasubiri pesa irudi! yani hayana muda wa kuzitafuta ila wakichakarika wengine wao wanatoa macho kama manguruwe. Hawa uingereza wangeingiza hizo pesa kwenye taasisi zao za maendeleo ka ilivyo USAID- Danida Nk. kuliko kuwarudishia haya majambazi. Kwani zilizorudi BOT kwa msaada wa Dr,. Slaa kufichu wakasingizia zinapelekwa Rukwa kwa ajili ya kilimo kwanza si wamezitafuna. Tunaongozwa na mafisi. shiit.
 
Serikali inasubiri kwa hamu kubwa kurejeshwa kwa bakaa ya Dola Milioni 30 za Kimarekani

Kwa mwendo huu jamaa wanajipongeza na kujiona wajanja, pesa uweke mfukoni, halafu wazungu wanakulipa tena kama zawadi ya matendo yako machafu!!!, hizi dili chafu hazitaisha inji hii.
 
hivi jamani kuna mtu anajua makadirio ya ujenzi wa daraja la kigamboni? Badala ya serikali kupitisha bakuli kwanini isipeleke pesa hiyo yote either kwenye ujenzi wa daraja la kigamboni au hata kutatua tatizo la umeme Kigoma au pengine pesa hiyo ikatumika kuweka mtandao wa maji toka kimbiji kuja temeke,kitunda,pugu na maeneo mengine ambayo yana uhaba mkubwa wa maji safi na salama?

Good idea! Lakini serikali ikubali waingereza wenyewe ndio watekeleze na kuisimamia miradi hiyo nchini mwetu kwa kutumia wananchi wetu wanaowaamini. Nisiulizwe kuhusu sovereignty au kama nao (waingereza) hawatakula. Hadi hapo tumeshapoteza uhuru wa kusimamia maslahi yetu na hata kama wakijimegea kiasi sio tatizo; kwani sie tulidai tumeibiwa? Kuna chochote tulichotegemea zaidi ya kuwatetemekea na kuwaenzi wezi wetu?
 
Taarifa kwa vyombo vya Habari

... Serikali inasubiri kwa hamu kubwa kurejeshwa kwa bakaa ya Dola Milioni 30 za Kimarekani kama ilivyokuwa katika makubaliano kati ya Idara ya Serious Fraud (SFO) na Kampuni ya BAE Systems baada ya kuondoa faini ya kiasi cha Paundi Laki tano za Kiingereza ambazo kampuni ya BAE Systems imeamuriwa kuilipa Mahakama ya Southwark mjini London.

Mara baada ya kupata taarifa rasmi, Serikali ta Tanzania itachukua hatua muafaka ikiwa ni pamoja ni pamoja na urejeshwaji wa kiasi cha fedha kinachotakiwa kurejeshwa Tanzania kulingana na makubaliano kati ya SFO na Kampuni ya BAE Systems. ...

[/SIZE]


Bila shaka kuwa kiongozi serikalini inabidi usiwe na soni wala haya!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom