makoye2009
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,638
- 1,219
Rais Chama cha Walimu nchini (CWT) Mwl. Gratian Mukoba akitoa taarifa ya chama hicho
--
UONGOZI wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT), umesitisha mgomo uliokuwa unaendelea nchini, hivyo kuwataka walimu kurejea kazini.
Rais wa chama hicho, Mukoba amesema wameamua kusitisha mgomo, baada ya kuingiwa na hofu ya viongozi wao wa juu kuhofiwa kukamatwa.
Pole sana na Hongera Mukoba kwa uamuzi mwafaka.
Rais Kiwete ni kama mwendawazimu kwa hiyo kushindana naye na wewe unaweza kuonekana kama mwendawazimu. Wazungu wanasema, "Never argue with a fool,people may not notice the difference" .
Watanzania tumeshajua kwamba Serikali ya CCM inayoongozwa na Rais Kiwete HAITAWAHI KUSIKILIZA MADAI YA WAFANYAKAZI WA IDARA YOYOTE HAPA TANZANIA. Tumeona hivyo kwa Madaktari na sasa kwa Waalimu! Kila siku wimbo ni uleule wa serikali haina pesa na madai ya wafanyakazi hayatekelezeki! Lakini Pesa ya KULIPA WABUNGE POSHO ZAO NA MISHAHARA MINONO IPO!PESA YA KULIPA MAFISADI IPO! PESA YA KUNULILIA MASHINGINGI IPO,PESA YA KULIPA WAFANYAKAZI HEWA IPO!!!
MIMI NIWAOMBE WAALIMU WOTE KWA UMOJA WAO,KWAMBA MWAKA 2015 HAUKO MBALI SANA. KAZI ILIYOBAKI NI KUIADHIBU SERIKALI YA CCM KWENYE SANDUKU LA KURA,FULL STOP! NAJUA WAALIMU MUNA USHAWISHI MKUBWA NA MNAWEZA KUHAMASISHA WAPIGA KURA KUKIKATAA CCM KWENYE SANDUKU LA KURA!
Wasalaam.