Tamko la Chama Cha Walimu(CWT)

Tamko la Chama Cha Walimu(CWT)

Walimu wanatakiwa ajira zao zipitiwe upya, kuna mtu aliwahi kushauri wanafunzi wakifanya mtihani walimu nao wafanye mtihani huohuo pia!!"kwa ishu seriou kama hii" hilo neno sikulielewa
Naunga mkono hoja mkuu........
 
Kwa maoni yangu, rais wa chama cha waalimu ndg. Gratias Mkoba na kaimu katibu mkuu mwl. Oluoch wanapaswa kujihuzuru kwa kuandaa mgomo ambao kwa tafsiri yangu ulikuwa ni kiini macho, hawakuwa na dhamira ya dhati ya kuwataka waalimu wagome kwa kuishinikiza serikali kuwapa waalimu madai yao. Nina sababu zifuatazo kwa kusema haya: 1. kama viongozi waandaji wa mgomo, sikutegemea kukiukwa kwa masharti ya mgomo na hivyo kuufanya mgomo ni halari kisheria. Kitendo cha kutoa masaa 48 siku ambazo si za kazi, upigaji kura bila kuwepo afisa wa kazi, na makosa mengine yaliyoufanya mgomo uwe batili binafsi siamini kama hawakujuwa sheria ila walifanya makusudi kwa sababu zao binafsi. Naamini kabisa wanasheria wapo, wangeweza kuwatumia kwa ishu seriou kama hii kama wao ni wajinga wa sheria. Wametuzalilisha waalimu kwa kutafsiriwa kuwa mambo yetu ni ya ovyo ovyo. 2. kuwadanganya na kuwaaminisha waalim, ambao ni wanachama wao kuwa mgomo ni halari, umefuata misingi na taratibu zote za kisheri, na kwamba wasiwe na wasi wasi, kila wakati walipohojiwa katika vyombo vya habari unaonyesha kuwa viongozi hawa ni waongo na si watendaji. Waalimu watashindwa tena kuitikia matamko yao ya migomo kwa kuwa hawatakuwa na uhakika na maneno yao. wakiendelea kutuongoza kamwe mgomo wowote utakaotangazwa hautafanikiwa. 3. Uongozi wa juu wa CWT chini ya mr. Mkoba haukufanya maandalizi ya mgomo ipasavyo kwa kuwashirikisha wanachama wake wote ambao ndio wagomaji. Hakuna elimu ya uamusho iliyotolewa kwa wanachama na ndiyo maana mwitikio wa mgomo haujaweza kutikisa sana. Najuwa wadau wa elimu, hasa waalimu wenzangu mnasababu nyingine nyingi za kumfanya huyu mtu ajihuzuru. Naomba tuziweke zitusaidie kumtoa huu jamaa, hana lolote juu ya maslahi ya waalimu.
Nilikuwa najiuliza inakuwaje watoto wetu wanamaliza shule hawajui kuandika na kusoma, kumbe jibu ndio hili! Mwalimu unakosa umakini mdogo tu wa kuandika kitu rahisi kama hiki je likija swala la taaluma la kutumia akili na weledi inakuwaje??kama kweli wewe ni mwalimu rudi darasani haraka kajifunze tena kuandika na kiswahili kwa ujumla! pole sana kumbe ndio maana hata migomo haifanikiwi kutokana na kuwa na walimu wa aina hii!!
 
Mkuu, that was meant to be a joke!

Thanks very much for clarification maana nilishaanza kupiga mahesabu niuze ng'ombe wangu niwahamishie watoto wangu wakasome hata somalia kuna nafuu!!
 
Thanks very much for clarification maana nilishaanza kupiga mahesabu niuze ng'ombe wangu niwahamishie watoto wangu wakasome hata somalia kuna nafuu!!

Hahahahahahahahahahahah mkuu umenichekesha sana! Idea siyo mbaya aisee, kama vipi wapeleke madogo wakapige shule ughaibuni...
 
walimu ni disgrace na disappointment kwa kada ya academicians wa Tanzania! hawajui wanachokifanya!
 
JUMAMOSI, AGOSTI 04, 2012 05:38

NA GABRIEL MUSHI


*CWT yatangaza rasmi kurudi darasani
*Yakusudia kukata rufaa ngazi za juu
* Mukoba asisitiza madai yao yako palepale
*Alia na polisi wanaotisha walimu waliogoma

HATIMAYE Chama cha Walimu Tanzania (CWT), kimesalimu amri na kutangaza kusitisha mgomo wa walimu uliodumu kwa siku kadhaa nchi nzima.

Kutokana na kauli hiyo, CWT imewataka walimu wote kurudi kazini ili kutekeleza agizo la Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi, lililotolewa juzi mjini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana, Rais wa CWT, Gratian Mukoba, alisema pamoja na mambo mengine, hukumu hiyo imewakatisha tamaa kwa kiasi kikubwa, hivyo wanajipanga kwa ajili ya kukata rufaa.

Alisema maagizo yaliyotolewa na mahakama yatekelezwa na CWT, baada ya kuipitia kwa umakini hukumu hiyo.

"Leo (jana), nimewaita kwa ajili ya kutekeleza sehemu ya maagizo ya Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi, yaliyotolewa na Jaji Sophia Wambura kwenye Shauri Na. 96 ya mwaka 2012. Katika hukumu hii, mahakama imeagiza chama kitoe maelekezo kwa wanachama wake kurudi kazini kuanzia leo (jana) Agosti 3, mwaka huu.

"Kwa maelekezo hayo, chama kinawaagiza wanachama wake kurudi kazini kuanzia leo (jana) kutekeleza majukumu yao ya kila siku, maagizo mengine ya mahakama yatatolewa maelekezo, baada ya kupitia hukumu kwa makini na kupata ushauri wa wakili wetu na wanachama watajulishwa," alisema.

Alisema kuhusu kulipa fidia ya hasara waliyoipata wanafunzi, chama kinasubiri taarifa rasmi ya Serikali, kwa kuwa CWT haina uwezo wa kufahamu hasara waliyopata wanafunzi.

Alisema mwenye uwezo wa kuwasilisha hasara hiyo, ni mlalamikaji katika kesi hiyo, ambaye ni Serikali.

"Kwa kuwa hukumu hii, imewakatisha tamaa walimu wanarudi kazini, huku mwajiri wao akionyesha kutowajali kutokana na madai yao kutopewa kipaumbele katika kuboresha maslahi yao.

"Walimu wanamwangalia mwajiri wao ambaye ni Serikali amewapuuza akifahamu kuwa kwa vyovyote vile atakimbilia mahakamani…hii haijafuta cheti cha kutopatikana kwa suluhu ya mgogoro wa Julai 25, mwaka huu, haiondoi ukweli kwamba maslahi ya walimu ni duni.

"Pamoja na walimu kuendelea kupuuzwa na mwajiri wao kwa kuwapa maslahi duni, chama kitaendelea na majadiliano na Serikali kuhusu nyongeza ya mishahara na posho kama kilivyowasilisha. Chama kina imani hukumu hii imetoa somo kwa mwajiri ili atambue umuhimu wa kuzungumza na walimu wote nchini," alisema.




KUKATA RUFAA
Kuhusu kukata rufaa, alisema chama hicho kinawasiliana na wakili wake ili kuona uwezekano wa kukata rufaa.

"Baadhi ya vipengle vya hukumu, vinahitaji ufafanuzi wa Mahakama ya Rufaa ili kuondoa utata wa kisheria, wanachama wanaombwa kuwa wavumilivu wakati huu.

"Kwa sababu mahakama, imetuonea kwa kipengele wanachodai tulitoa muda kwa Serikali kabla ya kuitisha mgomo katika siku za mapumziko, wakati wao wenyewe walishawahi kutoa saa 3:48 usiku," alisema.



WATAKA KULINDWA
Kuhusu usalama wao, Mukoba alisema katika kipindi cha mgomo baadhi ya wakuu wa mikoa na wilaya, waliamuru wanachama wa CWT na viongozi wake kukamatwa bila na sababu za msingi.

"Baadhi yao, wamefikishwa mahakamani kwa kuhamasisha mgomo wa walimu, chama kina wasiwasi kuhusu usalama wa viongozi na wanachama walioshiriki na kuhamasisha mgomo wa walimu.

"Chama kinatoa rai, kwa Serikali na vyombo vya dola, wakiwamo maofisa usalama na makamanda wa polisi wa mikoa na wilaya, kuhakikisha viongozi wa chama na wanachama waliohamasisha mgomo wanakuwa salama bila kudhurika.



MAZUNGUMZO NA SERIKALI
Alisema walimu wanarudi kazini bila kuwa na mawazo yaliyotulia, juu ya utendaji wao wa kazi.

"Chama kinatoa wito kwa Serikali, kukutana na CWT haraka kuendeleza majadiliano ya madai ya walimu, msimamo wetu tangu mwanzo ulikuwa ni kujadiliana na Serikali kupitia kwa msuluhishi, aliyeteuliwa na Tume ya usuluhishi na uamuzi.

"Tatizo lilikuwa ni serikali ambayo haikuwa tayari kuzungumza na CWT, ushahidi umeonekana kuwa muda wa siku 50 za mgogoro huu, hakuna mwakilishi wa Serikali aliona umuhimu wa kukutana na viongozi wa CWT kuzungumza nao, badala yake waliamua kutumia vyombo vya habari kukishambulia chama.

"Chama kinashauri Serikali ichukue hatua za haraka kutibu majeraha ya walimu kwa kujadiliana na CWT kuhusu madai yao na kufuta barua zote zilizosambazwa kwa walimu kujieleza kwa nini wasichukuliwe hatua za kinidhamu," alisema.

Julai 30, mwaka huu, CWT kiliitisha mgomo wa walimu nchi nzima ili kuishinikiza Serikali kutekeleza madai yao ambayo ni nyongeza ya mshahara kwa asilimia 100, posho ya walimu wanaofundisha masomo ya sayansi asilimia 55, walimu wa sanaa 50 na mazingira magumu 30. Lakini Rais Jakaya Kikwete akihutubia taifa katika utaratibu wake aliojipangia, alisema Serikali haina uwezo wa kulipa madai ya walimu kutokana na bajeti ndogo iliyopo
.
 

Waalimu Wangejaribu Style Nyingine... Wangefikiria kwanza kuna shule NYINGI PRIVATE; WATOTO WA WAKUBWA WOTE

Wanasome NJE YA NCHI; SIO KAMA ZAMANI ENZI ZETU... Kwahiyo Matakwa yao yawe Madogo sio Nyumba ya Ghorofa...

Hata Kama Mama Kikwete alikuwa Mwalimu ni enzi hizo sasa hivi ana dunda ile shule ya UTURUKI; hatoki Jasho tena

Waalimu Mfukuzeni Kiongozi wenu wa Chama Cha Waalimu hafai...
 
Back
Top Bottom