Kwanza,
taifa halipo salama katika kila nyanja iwe uchumi, elimu, afya, siasa, nk nk nk nk
Pili,
walalahoi yaani watu wa kipato cha chini na kati wasitegemee chochote kutoka kwa viongozi wao walio chini ya CCM,
viongozi hao wameapa kwa damu na nyama, kwa mwili na roho chafu kuhakikisha kuwa hakuna hata mlalahoi atakaeibuka na kunawiri kiafya, kielimu, kiuchumi, kisiasa, nk nk badala yake km kuibuka ni kufikia ngazi ya kuweza kununua gari la mitumba(used) na mafuta yakuzingue kila kukicha. Mifano ipo hai wote wanaona.
Tatu,
yeyote yule anaepinga CHADEMA nadiriki kusema ni shetani tena yule mwovu mbaya, maana kwa jinsi serikali, ccm, usalama wa taifa wanavyowafanyia umafia CHADEMA sasa nazidi kuipenda CHADEMA na kuiamini kuliko hata hapo mwanzo, naoan kweli CHADEMA ni mpango wa Mungu alie hai
Nne,
njia pekee ya kukabiliana na huu umafia unaofanywa kwa walalahoi ni kuasi njia zote kuu za CCM; zipi, kwa jinsi gani kila mtu atajua kwa nafasi yake mwenyewe!!!!
Kila la kheri!!!!!