Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,011
- 9,879
Serikali kupitia Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Ummy Mwalimu imesema imetenga Shilingi Bilioni 50 kwenye Bajeti ya mwaka 2021/22 kwa ajili ya kununua Vitabu vya Kiada kwa wanafunzi wote wa msingi na Sekondari Nchini.
.
Mhe. Ummy Mwalimu ameyasema hayo leo alipokua akizungumza na wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Bugumbikiso Kata ya Chifunfu Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema walipolalamikia uhaba wa vitabu shuleni hapo, ambapo amesema kupatikana kwa vitabu hivyo kutasaidia kila mwanafunzi kupata kitabu chake mwenyewe sawa na muongozo unavyotaka wa kitabu kimoja kwa Mwanafunzi mmoja yaani 1:1.
.
Mhe. Ummy Mwalimu ameyasema hayo leo alipokua akizungumza na wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Bugumbikiso Kata ya Chifunfu Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema walipolalamikia uhaba wa vitabu shuleni hapo, ambapo amesema kupatikana kwa vitabu hivyo kutasaidia kila mwanafunzi kupata kitabu chake mwenyewe sawa na muongozo unavyotaka wa kitabu kimoja kwa Mwanafunzi mmoja yaani 1:1.