Tamaduni Music hawajawahi kufanikiwa kwenye chochote kile wanachokianzisha

Tamaduni wabadilike kifikra. Kuendelea kung'ang'ania muziki ambao hauhitajiki sokoni ndo anguko lao. Hata wanamuziki wa Congo baada ya kuona wanapotea wameamua kubadilika.. zamani walikuwa wanatoa nyimbo ndefu za hadi dakika 10 ila siku hizi na wao wanatoa nyimbo za dakika 3 hadi 4. Na yale masebene wamepunguza. Kina Pepe Kale wakifufuka watashangaa sana kuona Werrason katoa wimbo wenye verse ya Hiphop. Wacongo pia walikuwa ni wabishi mno kupiga bila vyombo lakini siku hizi nao kuna matamasha wanapiga bila vyombo ili mradi mkono uende kinywani. Kimsingi muziki una mabadiliko dunia nzima. Tamaduni wao wakubali kubadilika na kuacha UJEURI. Kujifanya unasimamia misingi ya Hiphop huku unazidi kutumbukia kwenye umaskini ni upuuzi mtupu.
Ni upuuzi wa kiwango cha SGR
 
Hawa wasanii wa tamaduni Music hapa nawazungumzia

Nikki mbishi

Stereo

One the incredible

Songa

P the Mc

Zaiid

Ghetto ambassador

Kad go

Azma

Nash mc

Wakazi

Man su lee

Dizasta

Ni wasanii wenye vipaji vikubwa sana , kitu ambacho kimenifanya niwe shabiki yao mkubwa sana , Napenda tungo zao, flows n.k.

Lakini kinachonisikitisha hii crew kifedha hawana mafanikio yoyote ukija kwa msanii mmoja mmoja ukimtoa Stereo ambaye kaajiriwa na Azma ambaye kafungua biashara zake nje ya music.

Hawa wengine wote wana maisha ya kuikitisha sana tofauti na ukubwa wa vipaji vyao

Kuna kauli yao wanaipenda sana VITENDO DHIDI YA MANENO Lakini ukiangalia uhalisia wa mambo hii kauli yenyewe inawapinga kwakua hakuna hata moja walilo lianzisha likafanikiwa kwa asilimia

Tukianza na

Kilinge

Hii ilikua tamasha ambalo ilikua kila jumamosi wanakutana pale Msasani club kwa ajili ya kufanye vitu vingi kama battles , kuuz album, mixtape na project zao mbali mbali

Lakini kutokana na kukosa kwao nidhamu walishindwa kuendeleza huu utamaduni wa kilinge

Rap City Battle
Hii ni project nyingine iliyo anzishwa na Wakazi, One the incredible, P the Mc & Man su lee
Hii ilikua inafanyika pale Micasa lounge Riverside.

Walikua wanakutanisha underground Artists kwa ajili ya freestyle battle lakini baada ya muda walishindwa kuiendeleza

Kinasa
Hii ni project ya Nash Mc inafanyikia Temeke lakini hii nayo mpaka leo hatujawahi kuona impact yoyote coz hakuna kipaji kipya (New artist) chochote alichokitoa huko ushwahilini

Kikosi kazi kazini
Hii ni project ya mwisho ambayo iliongozwa na Azma , hapa waliunda kama kundi lakini hawakua tamaduni crew wote walikua kama nane, walitoa baadhi ya nyimbo na walisema washafanya album.

Lakini ukweli ni kwamba nyimbo iliyofanya vizuri ilikua ni ile Dis truck ya WEUSI na hii ilipata media coverage kubwa kwa sababu wali diss Kundi la weusi.

Baada ya kutoa ile dis truck ngoma zilizofuata hakuna media iliyokua na mpango nazo
Taaribu wakaanza kukaa kimya mpaka leo

Ukiwauliza mmoja mmoja watakuambia bado kikosi kazi ipo lakini ukweli ni kwamba walishaona financially haikua na impact yoyote zaidi ya kujichoresha tuu

Inasikitisha sana kuona hawa jamaa wanaenda kuzeeka bila kunufaika na vipaji vyao , wameku wakiwa diss sana wasanii wengine wa HIPHOP walio main stream kuwa wanapendelewa lakini ukweli hawa jamaa wanafeli kutokana na ujinga wao wenyewe.

Bado wana mentality za kimtaa mtaa na hawajua jinsi soko la Music linavyoenda

Inashangaza sana mpaka leo bado wanaendelea na mfumo wao wa kuuza Santuri na kanda mseto kwa kuzungusha mtaani , email na whatsapp ..eti madai yao hizi plartform zinazouza music zinawaibia

Huu ulimbukeni wao ushawagharimu na utaendelea kuwa gharimu sana

Ukianza hata level ya umaarufu hawa jamaa wanafahamika na watu wanaofuatilia sana HIPHOP
Wengi uliowataja hapo watu wa kawaida hawawajui
 
Mada Nzuri sana hii,
Jamaa wanavipaji lakini sana na ni wanasanaa wazuri mno kuna tatizo lipo kati yetu wote kwa maana ya kwama
Je kati ya hao wote tamaduni crew uliowataja ni nani umenunua album yake na unayo ?

Je ni yupi kati yao ambae umeweza kustream nakusikiliza nyimbo zake katika digital platforms zenye muhimili mzuri wa malipo kama deezer , sportfy nk

Kati ya show na matamasha yote pamoja na project za arts wanazouza kama matishirt ya tamaduni logo au matamasha umekua ukiudhuria ?

Sisi ndio wa kuwapa muhimili mzuri hawa wasanii wa mziki huu pendwa naomba kumquote dizasta vina “Kama haiuzi kosa ni lako”
Natamani niandike kwa urefu sana ila sio mwandishi mzuri
Asante Vesper-valens
 
One the incredible nasikia anakula bangi na kuchangaya kila takataka ajabu wote alivuta nae wamefetuka vichwa kabaki peke yake makostamina
 
sio namwita yeye ndio anasema , kuwa hakuna underground yoyote ana jina kama yeye
Jina kimaandishi? au kufahamika mana ukimuweka HATA NACHA TU watu wanamfaham huku kijijini kwetu na sio man sulee

Au anazungumzia hapo pwani ndo ana jina?
 
Mada Nzuri sana hii,
Jamaa wanavipaji lakini sana na ni wanasanaa wazuri mno kuna tatizo lipo kati yetu wote kwa maana ya kwama
Je kati ya hao wote tamaduni crew uliowataja ni nani umenunua album yake na unayo ?

Je ni yupi kati yao ambae umeweza kustream nakusikiliza nyimbo zake katika digital platforms zenye muhimili mzuri wa malipo kama deezer , sportfy nk

Kati ya show na matamasha yote pamoja na project za arts wanazouza kama matishirt ya tamaduni logo au matamasha umekua ukiudhuria ?

Sisi ndio wa kuwapa muhimili mzuri hawa wasanii wa mziki huu pendwa naomba kumquote dizasta vina “Kama haiuzi kosa ni lako”
Natamani niandike kwa urefu sana ila sio mwandishi mzuri
Asante Vesper-valens
Short and clear..
 
Back
Top Bottom