TALA wala rungu la TRA

TALA wala rungu la TRA

Wakuu nataka niwalipe TALA ila sio kwamba nina ela...ela niliyonayo hainitoshi kwa arakati zango so nataka niwalipe ili nikope kiasi cha juu zaidi nikamilishe mambo yangu...vipi itawezekana kweli maana ni takribani miezi mitano tangu niwakope na sijawai walipa....wamenipiga bit mpaka wamechoka sijui ndo nitawalipa wanitelekeze njiani kama na mimi nilivowatelekeza...mwenye uzoefu na ili anipe ushauri tafadhali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna jambo watz wengi hamlijui..uwe mkristo,uwe muislam,uwe mbudha,uwe huna dini.nk ukikopa mahali popote faham deni ni kifungo cha nafsi na madhara yake ni makubwa ingawa wachache ndio wanayajua.hvo we kimbia na maden ya watu na jifuraishe na kujisifia kua mjanja, but kuna mda litakubana huko na utakua ukiugulia peke ako..kwa sasa wacha tufuraishe jamvi kwa utapel wetu.
 
Binafsi sipendagi kudaiwa,ila kunawakati mambo huwa juu chini,hupelekea mtu kuonekana si mwaminifu
Kiuhalisia hakuna mtu anae penda kila kukicha kuamshwa na sms ya deni au taarifa ya kitisho kutoka kwa yule anae mdai.
Kiafya pia ni nzuri kwani hutakaa unenepe kabsa na kuwa nyama uzembe na hata kuhatarisha maisha kwa kuwa na magonjwa ya moyo kama presha.

Binafsi nimeshawahi kudaiwa na kudai pia,ila katika kudaiwa ni hali ambayo huwa ni mbaya sana pale inapofikia kupelekana mahakamani na sehemu zingine,achana na madeni madogo ya kwa mangi na kwenye bar ya mzee fulani,
Kuna haya madeni ya kuanzia 1m+
Kwa kweli kichwa huwa kinawaka moto .

Tujitahidi kulipa palipo na nafasi ya kufanya hivyo ,pia wadeni wetu wawe wanajua hali kuwa si nzuri kwa sasa kwani tulio wengi mambo ya meshabadilika ukilinganisha na kipindi cha nyuma,tusijisifu kwa kutokulipa ila tujitahidi kulipa tunapopata nafasi ya kufanya ivo.

Kila la kheri katika kupambana na changamoto za awamu hii.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi namshukuru Mungu hawa Branch wame nikopesha sana na mpaka sasa Nina kigezo cha kukopa 360,000/= kwao na Nina jitahidi sana kuwalipa na Nina omba nisije kuingiwa na shetani la udhurumati... Branch wame nisaidia sana sana naomba Mungu nizidi kuwa balozi wao mzuri...
 
ila mm naona ni bora kuwa waminifu kwa kulipa haya madeni ili kuruhusu na wenzetu wapate huduma kama tulizozpata na kujijengea heshima binafsi.
 
Habari Kutokulipa Deni la BRANCH na bado uko Kimya ni Tafsiri sahihi kabisa yakwamba umeamua kutumia Taarifa zako katika KUTAPELI FEDHA MTANDAONI. UKWELI NI KWAMBA HUVUMILIKI TENA. MAAFISA wetu Wako mitaani kwaajili ya kushughulika na WAKAIDI. hivyo endelea kukaa kimya ukakumbane na MKONO WA SHERIA
 
Mimi nimeuza simu...kitambulisho kimepotea na namba za simu pia nimetupa line....watanipata wapi ....hawawezi kunipa mkopo mdogo wakati mi nalipa pesa kubwa huo ni wizi nasema kampuni ifutwe kabisa.....

Hii tabia wanayo Airtel timiza unakopa elfu 23 unaambiwa urejeshe 30 baada ya wiki tatu ukirejesha unakopeshwa 31500 ...na wao niliwapigia nikagombezana nao siwalipi ng'ooooooo

Sent using Jamii Forums mobile app
Hawa ndiyo niliwapiga mzinga wa maana.
 
Back
Top Bottom