Taifa liadhimishe Komba day

Taifa liadhimishe Komba day

Bora hata Mubarak Mwinshehe, au Marijani Rajabu
 
Mmh kwanza nahitaji kujua uyu komba ameifanyia nn nchi hii?maana hapa TBC wanarusha kipndi cha kuagwa uyu komba hii ni television ya taifa na cyo ya ccm how wanampa uyu komba air time iv...na hapo kuna pesa zetu za walipa Kodi zinatumika kuendesha hii shughuli..mbona wanakufa mawaziri ila hawafanyiwi ivo..au kuna yoyote kazi yoyote kafanya kwa taifa hili cyo kwa ccm

Mimi mwenyewe nimechoka kabisa! toka asubuhi mpk sasa ni Komba wamemaliza kuaga sasa ni nyimbo zake zinarindima TBC1... haya wee na yule mbunge wa Zbar yeye mbona haikua hivi au ubunge unatofautiana viwango?
 
Ila kiukweli tutazimis tungo zake.
Fikiria leo tupate msiba mkubwa wa kitaifa(Mungu na apishilie mbali),nani atahanikiza kwa nyimbo zenye hisia kali za majonzi kama ilivyokuwa enzi za Capteiiiin!!.

Msiba wa kitaifa!!! Kama akifa nani kwa mfano? Mana hata mwenye kaya akifa bado hautakuwa msiba wa kitaifa bali wa mafisadi
 
Salam wakuu,

Baada ya Msiba mzito wa Capt J Komba, niliamua kusikiliza kazi mbalimbali alizozifanya. Nimegundua jamaa alikuwa na uwezo mkubwa sana, Yaani alikuwa na uwezo wa kutunga wimbo na kurekodi ndani ya nusu saa. Pia tofauti na nyimbo za akina Diamond, Nyimbo za capt Komba hazichuji kabisa. Halafu zina ushawishi sana.

Kwa kweli kuna kila sababu ya kumuenzi. Tuteue siku 1 ya mapumziko tuwe tunasikiliza track zake. Japo mimi sio CCM, ila kuna wimbo unaitwa Arambee ulikuwa unanishawishi sana, hasa kwenye yale maneno "Wapinzani tuwalete tuwachanechane tuwatupee" dah... huyu jamaa alikuwa hatare sana.

Komba day ni muhimu aisee.


Ni kweli Capt KOMBA kafanya mengi hasa kwenye tasnia ya sanaa ya muziki,lakini si dhani kama kumuenzi ni lazima tutenge siku ya mapumziko,nadhani kama tutaipa kipaumbele tasnia hii itakuwa ni namna bora ya kumuenzi kuliko kutenga siku ya kukaa tu bila kazi,na hata tukifanya hivyo bila kuzienzi kazi zake ni bure.
 
Jamani tuwekezeni katika kumcha Molah Hakika ckutegemea kama na huyu Mpendwa du! Mungu kavuna kama alitenda mama peponi kama hakutenda mema Ndiyo hivo tena sisi hatuwezi kumwamuru Molah
 
Labda ccm ambayo inazaliwa weekend siku hizi kwa ajili ya kukusanya watu.
 
kweli,kafanya mengi KWENYE TASNIA YA UZINZI NA UZINIFU, Watoto Nje Ya Ndoa Tena Siyo Mmoja, Huyu Hakusitahili Hata Kusomewa Ibada Kanisani,kanisa Katoriki Waache Unafiki,mbona Akifa Mtu Asiyemaarufu Ambae Amezaa Nje Ya Ndoa Hazikwi Na Kanisa Kwanini Kwa Komba?
 
Kwa lipi jema alifanya kumtukana warioba
 
Salam wakuu,

Baada ya Msiba mzito wa Capt J Komba, niliamua kusikiliza kazi mbalimbali alizozifanya. Nimegundua jamaa alikuwa na uwezo mkubwa sana, Yaani alikuwa na uwezo wa kutunga wimbo na kurekodi ndani ya nusu saa. Pia tofauti na nyimbo za akina Diamond, Nyimbo za capt Komba hazichuji kabisa. Halafu zina ushawishi sana.

Kwa kweli kuna kila sababu ya kumuenzi. Tuteue siku 1 ya mapumziko tuwe tunasikiliza track zake. Japo mimi sio CCM, ila kuna wimbo unaitwa Arambee ulikuwa unanishawishi sana, hasa kwenye yale maneno "Wapinzani tuwalete tuwachanechane tuwatupee" dah... huyu jamaa alikuwa hatare sana.

Komba day ni muhimu aisee.

Huu ni msiba mzito kwa mke wa marehemu, watoto wa mrehemu, mama wa marehemu, baba wa marehemu na jamaa zake wa karibu, kwa sisi wengine ukijumlisha na kauli yake (marehemu) eti kuingia mstuni kupambana na matakwa ya wananchi tunajionea heri kwetu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom