Taifa la washabikia uzinzi - Tanzania

It is a pity kuwa nchi nzima na Rais wetu, PM, etc wanashabikia uzinzi. Huyu Marehemu (RIP) alikuwa katika matendo yasiyo mpendeza Mungu, lakini hayo yote Tanzania hawayaoni. Huyu alikuwa anafanya uzinzi, basi najua mtanipiga madongo, potelea mbali.

jitahidini kuwa wise. Rais is a parent na hata mtoto angekuwa kibaka ni wake. Beside, unuhakika gani kama Lulu na Marehemu ni wapenzi? Wakiwa wachumba je? Na tena hawafanyi ngono hadi siku ya ndoa? Mimi watu kama wewe mnayekashfu mfu nadhani hamjalelewa ki heshima. Nisamehe kama nimekukosea but mnakera. Hizo tuhuma mnazirusha kwa Marehemu atarudi lini azijibu? Kama ungekuwa karibu ningekung'ata kwa hasira mkuu wangu. Stop doing so and who knows kwako itakuwajme? Kanumba alikuwa na nidhamu ndiyo maana hakutaka watu wayaone haya na kama si kifo hakuna mtu angejua. Kwa maana hiyo ndiyo maana anaitwa kioo cha jamii. Fikiria before posting kitu ambayo nina uhakika unajua itaumiza wengine. Grow up.
 
Mkuu,
Dunia ndivyo ilivyo; si wewe wala mimi wenye uthubutu wa kuibadilisha!! Kimsingi, hata mimi nimeshangaa….lakini hapakuwa na jinsi!! Wananchi wenyewe ndio wametaka hivyo….hata kama JK na kebineti yake wasingetia mguu; bado watu wangeenda tu….ni ngumu kueleweka lakini ndivyo ilivyo!! Ni kweli, marehemu mzinzi, mhasherati na anaweza tajwa kwa kila uovu, lakini wananchi hawayajali hayo!! Binafsi, kwangu sina TV wala Redio…hebu nijuzeni wenye navyo! Je, vituo vya redio na TV vilikuwa vinawahamasisha watu kwenda huko au ilitokea tu?! Je, serikali ilitangaza kwamba msiba wa Kanumba ni wa Kitaifa au vipi?! Tangu nizaliwe, msiba wa kwanza kushuhudia ukitikisa na ule wa Marehemu Dyana (Princess of Wailes)….hata nae, kama ilivyo kwa Kanumba, msiba wake ulitokana ndani ya kichaka cha uzinzi na uasherati…lakini dunia mzima ikasisimka! Hapa kwetu, ni msiba wa wa Mwalimu Nyerere….na sasa ndio huu wa Kanumba!!! Rais na watendaji wake mtawaonea tu….public imetaka iwe ilivyokuwa, hivyo nao hawana budi bali ni kuendena na matakwa ya public! Hebu ona hapa JF palivyojaa posts kuhusu msiba wa Kanumba….tumetaka, tusitake….bado tutaendelea kuzishuhudia; ziwe zenye positive or negative perception; zitaendelea kuwepo tu!!
 
Usikute wewe mwenyewe umezaliwa nje ya ndoa hapa unasumbua watu hapa.Usihukumu kama vile we ndo mungu

Kuzaliwa nje ya ndoa si kosa la mtoto, bali la mama na baba, tunaongelea kosa la kanumba, haikukosewa ilipotamkwa "mkimfungia duniani amefungiwa na mbinguni pia"
 
Mtu akishafariki makosa yote tunamwachia Muumba wake ndiye mwenye Mamlaka ya kumwaadhibu. Kama tukimhukumu marehemu, Mungu atafanya nini ?

That being the case,Lulu aachiwe huru mapema iwezekanavyo.
 
Hayo ya uzinzi nadhani sisi wanadamu hayatuhusu kilichofanyika watu wamemzika kama kawaida hayo mengine ni yeye na mungu wake...halafu watu hawewezi kushabikia msiba.
 
Sifikiri kama ni kumhukumu marehemu, mtoa mada nadhani alikuwa na maana ya vijana tunahitaji kujifunza jambo kutokana na kifo cha Kanumba, alikuwa mtu maalufu sana, labda alikuwa bado yuko kwenye selection ya nani awe wife.
At the age of 28 alihitajika kuwa tayari anaye mke na huenda kifo chake kingekuwa chenye heshima zaidi.
Sote njia ni moja, lakini kila m2 anajaribu kuomba mwisho wake uwe ni mwema na utakaoacha heshima kwa jamii iliyobaki.
 
Kama Kanumba kuishi na mwanamke kama wachumba bila ndoa ndio UZINZI, basi umetukana wengi sana tena wenye uongozi mkubwa kwenye vyama vya siasa!
Tuombe radhi mashabiki...........

Alikua haishi na mwanamke,alikua anaishi na mtoto,under 18.
 
Mume overvalue sana, huyu ni mzinzi alikuwa azikwe kikawaida tu. Tatizo nchi yetu wananchi malimbukeni watupu, huwezi kumpa coverage ile pamoja na presidential support mwasherati kama yule. Shame on all those waliokwenda Sinza Vatican na Leadets club. Leo mutaponda comment yangu lakini after a couple of years muje mujiulize wenyewe kama mulikuwa munastahili ku invest muda wenu na raslimali fedha kwenda kumzika muigizaji aliyebaka binti wa miaka 17. Alipomchukua kwa wazazi wake alisema anamtoa kwa kipaji chake kumbe anamtia! Nanyi munashabikia uchafu huo

my dear hii ndio jamii yetu ilivyo unatakiwa kuielewa hivyo, hata leo Kanumba angesema anagombea urais tungemchagua kwa kuwa either ana mvuto au pesa, na ukiwauliza watz watakuambia tabia yake binafsi haihusiani na uongozi matokeo yake ndio tunakuwa na viongozi wabovu na tunaanza kulalamika, kuchukia majirani zetu wanaoendelea mara wazungu wabaya tunatafuta visingizio kibao wakati mchawi wetu ni sisi wenyewe! kama jamii ni nzuri lazima itatetea uovu. lakini angalia jamii yetu inashabikia maovu.
 
jitahidini kuwa wise. Rais is a parent na hata mtoto angekuwa kibaka ni wake. Beside, unuhakika gani kama Lulu na Marehemu ni wapenzi? Wakiwa wachumba je? Na tena hawafanyi ngono hadi siku ya ndoa? Mimi watu kama wewe mnayekashfu mfu nadhani hamjalelewa ki heshima. Nisamehe kama nimekukosea but mnakera. Hizo tuhuma mnazirusha kwa Marehemu atarudi lini azijibu? Kama ungekuwa karibu ningekung'ata kwa hasira mkuu wangu. Stop doing so and who knows kwako itakuwajme? Kanumba alikuwa na nidhamu ndiyo maana hakutaka watu wayaone haya na kama si kifo hakuna mtu angejua. Kwa maana hiyo ndiyo maana anaitwa kioo cha jamii. Fikiria before posting kitu ambayo nina uhakika unajua itaumiza wengine. Grow up.

Nitasema kweli fitina kwangu mwiko. Sina unafiki wa kufunika kombe mwanaharamu apite. Huyu alikuwa katika uovu na kitoto kidogo! Namwombea sana, lakini ukweli tuuseme watanzania wametia aibu.
 
my dear hii ndio jamii yetu ilivyo unatakiwa kuielewa hivyo, hata leo Kanumba angesema anagombea urais tungemchagua kwa kuwa either ana mvuto au pesa, na ukiwauliza watz watakuambia tabia yake binafsi haihusiani na uongozi matokeo yake ndio tunakuwa na viongozi wabovu na tunaanza kulalamika, kuchukia majirani zetu wanaoendelea mara wazungu wabaya tunatafuta visingizio kibao wakati mchawi wetu ni sisi wenyewe! kama jamii ni nzuri lazima itatetea uovu. lakini angalia jamii yetu inashabikia maovu.

Watu wamezimia kwaajili ya marehemu Kanumba, sidhani kama waume/wake zao wangekufa wangezimia, ninapata picha.
 
Mambo yote tis a, ishu ni kuwa tumechemsha hat a m/Jackson alivyofariki watu Wali pause kwanza wajue chanzo! Sasa uchunguzi unaendelea viongozi wote same rally behind marehemu hata bila aibu kuwa jamaa kafariki katika ugomvi tena mwanamke, what if he was violent to so many women as his behaviour? Aren't we propoting it?

Je police wakija na ushahidi unaomvua sifa warehemu watakuwa huru kuutoa na kuwaaibisha wakuu wao walioshadadia msiba?

Kama hii ni nchi ya innocent until proven guilty mbona kina mama Pinda wasipite pia kumjulia hali huyo binti ten a mwanamke mwenzetu au ndo mfumo dume umewa daka?

My conclusion ni kuwa people have rushed to ensure Chadema Hawa tumii huu msiba kuwa shine! Kweli sasa CDM inawahemesha wazee!
 
Imani ya kweli tumeiacha tumejitengenezea ndama.Akifa leo mtumishi wa Mungu wala watu hawatahuzunika ila huyu aliyewafurahisha kwa mambo ya dunia hii basi utakuta wengi wanalia.Viongoz wetu hamjatuonyesha njia ipasayo kwa hili.
 
nafikiri kuna umuhimu mkubwa sana kuwafundisha watu nini maana ya freemason, na ni watu wepi. kwasababu nimeona watz wanachanganya sana. mtu akifanya kitu cha ajabu tu wanasema freemason. try to google and knwo who they are.

freemason hawadili na mtu masikini wa chini kama kanumba, kuingia tu mle kuna umakini mkubwa na kuna madaraja. mabilionea tu ndo wanakuwa mafreemason. hivi vyama vya kichawi kama vya wachaga wa kimara (wachaga wenzangu) etc, cults kama za kinijeria etc, sio freemason.....yule mhindi wa tz ambaye ni kiongozi wa freemason miaka mingi kamwulizeni namna ya kuingia humo. pia, usilinganishe kanisa la shetani lile kule karibu na moven peak hotel (sijui kama imebadilishwa nakumbuka jina hili) wanalosali usiku uchi etc, ni tofauti na freemason pamoja na kwamba vyote ni vyama vya kishetani. freemason ni kikundi cha watu matajiri sana wanaoongoza dunia hii katika kila nchi. masikini haingii mle hata siku moja. ila kuna cults ndogondogo kama hizi za lion club pia ni za kishetani, usilinganishe na hizo.

Acha uongo wewe,..
hauwezi kuwa bilionea kama hauna milioni.

Juzi hapa tulikua tunasikia ushuhuda wa jamaa alotupwa
south africa kufanya kazi za freemason na mwishoni aka
kimbia baada ya kuumia.
 
Simu inaita halafu demu anakimbilia nje kuongea, kuna siri gani? Kuna heshima gani?

sasa hapo hakuna upendo. asiye kupenda achana nae asije umiza moyo wako.

Kimsingi inatakiwa mwanamke ampende mwanaume zaidi, hapo ndo kuna amani na furaha.

Haitakiwi mwanaume ampeeendee mwanamke saaana, halafu mwanamke ndo hivoo wala hajali... matokeo yake ni mateso na hata kifo.

RIP Kanumba - Sote binadamu ni wakosefu na tujifunze.
 
It is a pity kuwa nchi nzima na Rais wetu, PM, etc wanashabikia uzinzi. Huyu Marehemu (RIP) alikuwa katika matendo yasiyo mpendeza Mungu, lakini hayo yote Tanzania hawayaoni. Huyu alikuwa anafanya uzinzi, basi najua mtanipiga madongo, potelea mbali.

wewe ulitaka asizikwe hata angekuwa kaua m2 sembuse uzinzi walishindwa manabii (daudi) sembuse kanumba
 
Waebrania 9:27..."After death comes judgement". Ndugu zangu kinachozikwa ni mwili wa mtu, roho ambayo ndiye mtu hasa ameshawekwa sehemu anayostahili, na hii ni kulingana na state aliyokutwa nayo kabla ya kifo.

Sasa hapo haijalishi waliomzika ni akina nani, awe rais, serikali, chama au dini ya aina yoyote ile, mkanda mzima wa jinsi alivyoishi duniani upo tayari kama ushahidi. Kama ni msamaha ulitakiwa kufanyika huku duniani, tusidanganyike wanadamu.

Ezekiel 33:11. ...GOD HAS NO PLEASURE IN THE SINNER'S DEATH..." Because he knows exactly where they are heading to.
 
Mambo yote tis a, ishu ni kuwa tumechemsha hat a m/Jackson alivyofariki watu Wali pause kwanza wajue chanzo! Sasa uchunguzi unaendelea viongozi wote same rally behind marehemu hata bila aibu kuwa jamaa kafariki katika ugomvi tena mwanamke, what if he was violent to so many women as his behaviour? Aren't we propoting it?

Je police wakija na ushahidi unaomvua sifa warehemu watakuwa huru kuutoa na kuwaaibisha wakuu wao walioshadadia msiba?

Kama hii ni nchi ya innocent until proven guilty mbona kina mama Pinda wasipite pia kumjulia hali huyo binti ten a mwanamke mwenzetu au ndo mfumo dume umewa daka?

My conclusion ni kuwa people have rushed to ensure Chadema Hawa tumii huu msiba kuwa shine! Kweli sasa CDM inawahemesha wazee!

Hizi siasa sasa zitatumaliza na kutuondolea utu....mbona hii issue ni wananchi wa kawaida ndio ambao waliitikia zaidi?! Sasa suala la CHADEMA (na labda la CCM) linatoka wapi hapo?!
 
Back
Top Bottom