Tai hapigani na nyoka ardhini

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,461
Reaction score
829,861
Atamchukua juu angani na kubadilisha uwanja wa vita, na kisha atamwachilia nyoka angani.

Nyoka hana stamina, hana nguvu na hana usawa hewani. Hivyo kushindwa mapigano ni hakika kwa asilimia 100

lakini haina maana kwamba nyoka ni mdhaifu la hasha. Udhaifu wake unatokana na uwanja wa vita usio wake tofauti na ardhini ambapo ana nguvu ya kujeruhi kuumiza na hata kusababisha mauti.

Chukua vita yako katika ulimwengu wa roho kwa kuomba na ukiwa katika ulimwengu wa roho Mungu anachukua vita vyako.

Usipigane na adui katika eneo lake la faraja, badilisha uwanja wa vita kama Tai na Mungu akusimamie kwa maombi yako ya bidii na ya dhati ya moyo wako.

Utakuwa na uhakika wa ushindi safi!



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duuh kweli.....
 
Hakika
 
Mara nyingi sana huwa nakwambia usiwe muongo kwenye mitandao ya kijamii. Jionee:


View: https://youtu.be/zEkOCE525Pk?si=LS6cpLjJSk8JJVEa
Nyoka anafatwa na kutandikwa hapo hapo chini na tai.


Hivi uongo huwa unakusaidia nini?
 
Sasa Kaka mchawi (Mshana Jr), binafsi kuna jimama limoja hivi lichawi sana hapa mtaani kwetu anataka kunimaliza kwa kuniroga na mimi si mchawi, napambana naye kivipi?
 
Mara nyingi sana huwa nakwambia usiwe muongo kwenye mitandao ya kijamii. Jionee:


View: https://youtu.be/zEkOCE525Pk?si=LS6cpLjJSk8JJVEa
Nyoka anafatwa na kutandikwa hapo hapo chini na tai.


Hivi uongo huwa unakusaidia nini?
wewe bibi unamatatizo.
short video hiyo ndio unaleta ushahidi hapa..?

Nyoka hujaona kakamatwaje clip imekatwakatwa ndio unatuletea hapa ???

wewe ndio wale mtu akisema fisi wanaushilikiano sana wanasaidiana kwenye vita.
Unaenda kutafuta clip ya fisi mmoja katelekezwa kwenye vita na mwenzio kuja kupinga hoja 🀣🀣🀣🀣
 
Dah Bonge la ujumbe πŸ’― certified....

Usipigane na adui katika eneo lake la faraja,
badilisha uwanja wa vita kama Tai
na Mungu akusimamie kwa maombi yako ya bidii na ya dhati ya moyo wako πŸ“ŒπŸ“ŒπŸ“ŒπŸ“Œ

Na ndio maana huwa namshangaa yule anayerogwa badala ya kujinasua kwa nguvu zingine na yeye anakimbilia kwenye kujiingiza kwenye uchawi eti na yeye kuMroga aliye mroga..

Kongole Mkuu leo hii ni fungu lenye maneno ya Faraja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…