TAHLISO waionya Chadema

TAHLISO waionya Chadema

..kuwa msikivu kwanza.

..Chadema wanatetea hoja zilizowasilishwa na Tume ya Warioba ambaye ni mwana-Ccm.

..Sasa wewe na wana-Ccm wenzako mngetueleza kwanini mnaipinga Tume ya Warioba ambaye ni mwana-Ccm mwenzenu.
Kwani time hiyo uliyoitaja ambayo chadema mnaheshim maoni yake, umeambiwa ni msahafu au biblia? Hamnaa mtu au kikundi chenye kutaja kisikosolewe kwani sio Malaika wa mbinguni.
Kwani kuwa mwanasisiemu maaana yake nikua malaika ambaye hawezi kukosea? Hapa duniani hakunamkamilifu Kwa jambo lolote lile. Hivyoo mawazo ya Kila mtu lazima yadadafuliwe na wenzake na pia naye akubali mawazo huru mengine juu yakile anachokiamini.
 
Kwani time hiyo uliyoitaja ambayo chadema mnaheshim maoni yake, umeambiwa ni msahafu au biblia? Hamnaa mtu au kikundi chenye kutaja kisikosolewe kwani sio Malaika wa mbinguni.
Kwani kuwa mwanasisiemu maaana yake nikua malaika ambaye hawezi kukosea? Hapa duniani hakunamkamilifu Kwa jambo lolote lile. Hivyoo mawazo ya Kila mtu lazima yadadafuliwe na wenzake na pia naye akubali mawazo huru mengine juu yakile anachokiamini.

..Ccm wasikilize mawazo ya Chadema.

..Chadema wasikilize mawazo ya Ccm.

..Tanzania sio miliki ya chama kimoja.
 
Jumuiya ya Wanafunzi Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO) wamekionya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kutokana na tabia yake ya kupinga mambo mbalimbali yanayofanywa na Serikali hata kama yana manufaa kwa wananchi na Taifa kwa jumla.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, leo, Rais wa Jumuiya hiyo Frank Nkinda amesema kwa kipindi kirefu, chama hicho kimejijengea tabia mbaya ya kutafuta uungwaji mkono hata katika masuala yasiyo na maslahi kwa Taifa na kupinga mapendekezo yenye dhamira ya kuwaweka watanzania pamoja.

Akitolea mfano wa baadhi ya mambo hayo ikiwemo ripoti ya kikosi kazi iliyokabidhiwa juzi kwa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ikiwa imesheheni mapendekezo mbali mbali yenye tija kwa taifa letu. Nkinda alisema wao kama wasomi wa Elimu ya juu hawaoni sababu yeyote ya Chadema kuipinga ripoti hiyo

“Sote tulisikia muhtasari wa kile kilichowasilishwa na Mwenyekiti wa Kikosi kazi, Prof. Rwekaza Mukandala kwa Mhe. Rais, kwakweli dhamira yake ni njema. Sasa tumeshangaa kakikundi kamoja kamekuja juu na kusema mapendekezo haya hayafai na kwamba ni matumizi mabaya ya fedha za umma, lakini ikumbukwe kwamba watu hawa waliitwa kutoa maoni yao wakakataa, sasa wanataka hata yale yaliyotolewa na watanzania wengine kwa uhuru na haki watu wayapinge ”alisema Nkinda

Aliongeza kuwa TAHLISO kama Taasisi inayolea nguvu kazi ya Taifa, kimsingi wana mamlaka ya Kuonya, kukemea na kushauri mambo mbalimbali katika Kuchochea maendeleo ya Taifa.

" Tumesikitishwa na kauli ya Katibu mkuu wa Chadema John Mnyika ya kuita ripoti hiyo kuwa ni matumizi mabaya ya fedha za umma kwa kuwa tu wao walikataa kuwasilisha maoni kwenye kikosi kazi cha Rais" alisema Nkinda

Alisema mtu au taasisi yoyote ya kiungwana ilipaswa kupongeza dhamira iliyoonyeshwa na Rais Samia Suluhu Hassan ya kutafuta maridhiano ya kitaifa kwa kupata maoni ya wadau juu ya njia gani za kupita kabla ya kufikia hitimisho na siyo kulalamika mbele ya vyombo vya habari suala alilosema halina msingi wowote.

Aliongeza kuwa Watanzania wameipokea ripoti hiyo kwa mikono miwili na wanawapongeza wadau wote walioshiriki kutoa maoni kwenye kikos...
Unawasemea waTanzania we umetumwa na Nani? Yaonekana huko Darasani unakaa Dawati la Mwisho kabisa!
 
Kwahiyo na nyiee mumekubali kuridhi madhaifu yetu? Sasa ni lini mtatofautiana na sisi ilijamiii iwaone umakini wenu?? Kubalini mlivyokosolewa na TAHILSO hiyo ndio demokrasia, msilithi udhaifu wa mtu nyinyi jipambanueni Kwa kukubali kupokea na kujitafakari pale mnapo ambiwa madhaifu yenu na mwingine. Tena mheshim mawazo ya mtu huyo kabisa
Ebu anza wewe na wenzio wa ccm huko kuheshimu maoni na mapendekezo ya umma kupitia Rasimu ya Katiba ya Warioba
 
Jumuiya ya Wanafunzi Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO) wamekionya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kutokana na tabia yake ya kupinga mambo mbalimbali yanayofanywa na Serikali hata kama yana manufaa kwa wananchi na Taifa kwa jumla.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, leo, Rais wa Jumuiya hiyo Frank Nkinda amesema kwa kipindi kirefu, chama hicho kimejijengea tabia mbaya ya kutafuta uungwaji mkono hata katika masuala yasiyo na maslahi kwa Taifa na kupinga mapendekezo yenye dhamira ya kuwaweka watanzania pamoja.

Akitolea mfano wa baadhi ya mambo hayo ikiwemo ripoti ya kikosi kazi iliyokabidhiwa juzi kwa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ikiwa imesheheni mapendekezo mbali mbali yenye tija kwa taifa letu. Nkinda alisema wao kama wasomi wa Elimu ya juu hawaoni sababu yeyote ya Chadema kuipinga ripoti hiyo

“Sote tulisikia muhtasari wa kile kilichowasilishwa na Mwenyekiti wa Kikosi kazi, Prof. Rwekaza Mukandala kwa Mhe. Rais, kwakweli dhamira yake ni njema. Sasa tumeshangaa kakikundi kamoja kamekuja juu na kusema mapendekezo haya hayafai na kwamba ni matumizi mabaya ya fedha za umma, lakini ikumbukwe kwamba watu hawa waliitwa kutoa maoni yao wakakataa, sasa wanataka hata yale yaliyotolewa na watanzania wengine kwa uhuru na haki watu wayapinge ”alisema Nkinda

Aliongeza kuwa TAHLISO kama Taasisi inayolea nguvu kazi ya Taifa, kimsingi wana mamlaka ya Kuonya, kukemea na kushauri mambo mbalimbali katika Kuchochea maendeleo ya Taifa.

" Tumesikitishwa na kauli ya Katibu mkuu wa Chadema John Mnyika ya kuita ripoti hiyo kuwa ni matumizi mabaya ya fedha za umma kwa kuwa tu wao walikataa kuwasilisha maoni kwenye kikosi kazi cha Rais" alisema Nkinda

Alisema mtu au taasisi yoyote ya kiungwana ilipaswa kupongeza dhamira iliyoonyeshwa na Rais Samia Suluhu Hassan ya kutafuta maridhiano ya kitaifa kwa kupata maoni ya wadau juu ya njia gani za kupita kabla ya kufikia hitimisho na siyo kulalamika mbele ya vyombo vya habari suala alilosema halina msingi wowote.

Aliongeza kuwa Watanzania wameipokea ripoti hiyo kwa mikono miwili na wanawapongeza wadau wote walioshiriki kutoa maoni kwenye kikos...
Chadema ni mufilisi mkuu,imagine inaongozwa na wafuatao ;Mbowe(elimu ndogo saaana),Lema kimsingi hajaenda shule,Asenga yule wa Segerea anakesha mitandaoni kutukana,John Mrema (ana kabelimu ingawa anaishi kwa mke wake ,John Mnyika nae pia Elimu yake hijakamilika inavyostahili (hana degree),John henche (alikosa kujiunga na UDSM ankaenda soma chuo cha hadhi yake , the list goes on ,ndio muone ni chama cha aiana gani hiki
 
Chadema ni mufilisi mkuu,imagine inaongozwa na wafuatao ;Mbowe(elimu ndogo saaana),Lema kimsingi hajaenda shule,Asenga yule wa Segerea anakesha mitandaoni kutukana,John Mrema (ana kabelimu ingawa anaishi kwa mke wake ,John Mnyika nae pia Elimu yake hijakamilika inavyostahili (hana degree),John henche (alikosa kujiunga na UDSM ankaenda soma chuo cha hadhi yake , the list goes on ,ndio muone ni chama cha aiana gani hiki
Kwenye hiyo list yako, kwa hicho kigezo kimoja tu cha elimu ya darasani, kuna wa kumlinganisha na musukuma, kibajaji, majimarefu (RIP), Kawawa (RIP - Tena mwalimu Nyerere alisema, huko CCM hana wa kumlinganisha na Kawawa kwa ubora).

Uongozi bora ni mwunganiko wa qualities nyingi, la sivyo Marais wote Duniani, na mawaziri wangekuwa maprofesa. Hebu niambie, miongoni mwa hao maprofesa jalala/njaa waliojazana huko CCM, ni yupi unaweza kumtaja ana msimamo thabiti. Sifa kuu ya msomi wa kweli ni kuongozwa na kanuni ya ukweli.

Wengi wa hao wanaoitwa wasomi wa CCM, ni aheri ya Musukuma ana positive impact kwa jamii kuliko hao wasomi wanafiki na fuata upepo.
 
..TAHLISO kama wasomi walipaswa kupangua hoja za Chadema kwa kutumia vielelezo mbalimbali na sio kuwatishia na kuwaonya wasitoe maoni yao.

..Wakati Mnyika akitoa maelezo kukosoa ripoti ya kikosi kazi alikuwa akifanya rejea ktk kazi na utafiti uliofanywa na Tume ya Warioba.
Kwenye hiyo list yako, kwa hicho kigezo kimoja tu cha elimu ya darasani, kuna wa kumlinganisha na musukuma, kibajaji, majimarefu (RIP), Kawawa (RIP - Tena mwalimu Nyerere alisema, huko CCM hana wa kumlinganisha na Kawawa kwa ubora).

Uongozi bora ni mwunganiko wa qualities nyingi, la sivyo Marais wote Duniani, na mawaziri wangekuwa maprofesa. Hebu niambie, miongoni mwa hao maprofesa jalala/njaa waliojazana huko CCM, ni yupi unaweza kumtaja ana msimamo thabiti. Sifa kuu ya msomi wa kweli ni kuongozwa na kanuni ya ukweli.

Wengi wa hao wanaoitwa wasomi wa CCM, ni aheri ya Musukuma ana positive impact kwa jamii kuliko hao wasomi wanafiki na fuata upepo.
Hao uliowataja sio viongozi wa chama wewe
 
Kwenye hiyo list yako, kwa hicho kigezo kimoja tu cha elimu ya darasani, kuna wa kumlinganisha na musukuma, kibajaji, majimarefu (RIP), Kawawa (RIP - Tena mwalimu Nyerere alisema, huko CCM hana wa kumlinganisha na Kawawa kwa ubora).

Uongozi bora ni mwunganiko wa qualities nyingi, la sivyo Marais wote Duniani, na mawaziri wangekuwa maprofesa. Hebu niambie, miongoni mwa hao maprofesa jalala/njaa waliojazana huko CCM, ni yupi unaweza kumtaja ana msimamo thabiti. Sifa kuu ya msomi wa kweli ni kuongozwa na kanuni ya ukweli.

Wengi wa hao wanaoitwa wasomi wa CCM, ni aheri ya Musukuma ana positive impact kwa jamii kuliko hao wasomi wanafiki na fuata upepo.
Chadema wangekuwa na msimamo Lowasi asingeweza kuwa mgombea urais wao ,zaidi ya miaka kumi walituaminisha kuwa alikuwa ni fisadi
 
Vijana wa aina hii wangekuwepo miaka ya 1940-1960 hakika tusingepata uhuru, pengine wangeipa "press conference" kumpa onyo Nyerere.
 
Wasomi kufata ubwana mabwana na uelekeo wa ufisadi ,unatufikisha hapa yaani mwanafunzi wa chuo kikuu Tena Udsm anasema hayo.

Sent from my Infinix X688C using JamiiForums mobile app
 
lakini ikumbukwe kwamba watu hawa waliitwa kutoa maoni yao wakakataa, sasa wanataka hata yale yaliyotolewa na watanzania wengine kwa uhuru na haki watu wayapinge ”alisema Nkinda Retired Tindo
Inahitajika afya ya akili kuwaelewa chadema, maoni ya chawa yasiyo na umuhimu kwa taifa yanayoenda kinyume na katiba bali maslahi binafsi kupewa nafasi
 
Kama hata mpumbavu atakukosoa bila uzito wa hoja basi tutakuwa na taifa la wajinga wasiokuwa critical thinkers tukikubali ujinga wao, na demokrasia siyo kukubali kila upumbavu.

Kosa kubwaa la chadema ni hii yakujiona watakatifu mda wote, na ndio hawahawa chadema kuchakutwa nikutaka eti kuwepo na uhuru wa mawazo. Wao wanataka uhuru wa mawazo iwe kukosoa chama kinginee ila Kwa wao chadema iwenikusifiwa tuuu. Chadema kubalini kukosolewa ndio demokrasia inataka hivyoo. Pokeeni na mawazo kinzani kwenu, kwani yapo yanayowajenga na nyiee pia.
 
Chadema kubalini kusikia na mawazo kinzani kwenu pia, hiii ndio demokrasia sahihi. Nyinyi ndio vinala wa kutaja uhuru wa mawazo na kukosoa, Kwa Nini nyinyi hampendi kukosolewa??. Au nyinyi furaha yenu kikosolewe chama kinginee tuuu Kwa kuwa nyinyi ni malaika? La hasha, pokeeni kukosolewa ndio itakuwa sababuu ya kukua kwenu chadema
Lini nyie wapambe wa CCM mliishauri CCM ikubaliane na uwanja sawa wa kufanyia siasa?
Mmeacha kuiba kura na kukubali tume huru ya uchaguzi kufuata ushauri mnaopewa?
 
Back
Top Bottom