TAHLISO waionya Chadema

TAHLISO waionya Chadema

Mbona wakati Ndugai anafurumushwa hukutoa huu ushauri kwa mwenyekiti wa CCM apokee maoni kinzani ya Spika ndugai.?
Kwahiyo na nyiee mumekubali kutembelea hayo madhaifu ya CCM?? Lini watanzania wataona utofauti kati yenu na CCM? Au mumekubali kuwa kama CCM??
 
Kwahiyo na nyiee wapigania demokrasia tunaowamini mnatembelea nyao za CCM?? Lini tutaona utofauti wenu na CCM??
..iko hivi.

..Kikosi kazi kimewasilisha mapendekezo kwa Raisi.

..Je, unaridhika na mapendekezo ya kikosi kazi? Sababu zako ni zipi?

..Je, haujaridhika na mapendekezo ya kikosi kazi? Hoja zako ni zipi?

..Tujielekeze kwenye mapendekezo ya kikosi kazi.

..Vyama na taasisi mbalimbali vipime na kuyachambua mapendekezo hayo badala ya kushambuliana.

..Wajumbe wa Kikosi kazi wajitokeze kutoa ufafanuzi na kuyatetea mapendekezo waliyoyatoa.
 
Kosa kubwaa la chadema ni hii yakujiona watakatifu mda wote, na ndio hawahawa chadema kuchakutwa nikutaka eti kuwepo na uhuru wa mawazo. Wao wanataka uhuru wa mawazo iwe kukosoa chama kinginee ila Kwa wao chadema iwenikusifiwa tuuu. Chadema kubalini kukosolewa ndio demokrasia inataka hivyoo. Pokeeni na mawazo kinzani kwenu, kwani yapo yanayowajenga na nyiee pia.
Nakubaliana na wewe ila nilitaka kujua TAHLSO ni kinanani na CHADEMA ni kina nani? je hao TAHLSO ulishawahi kusikia wakihoji juu ya nani hasa walimshambulia TUNDU LISU? au tuseme wakati ule hawakuwepo?
kwamba kwenye vyuo vikuu kuna degree inaitwa political science kisha anatokea mpuuzi mmoja anakataza wanafunzi kujihusisha na siasa.... TAHLSO walikuwepo uliskia wakimkosaa kiongozi yule?
sasa tutawaamini vipi?
 
Jumuiya ya Wanafunzi Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO) wamekionya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kutokana na tabia yake ya kupinga mambo mbalimbali yanayofanywa na Serikali hata kama yana manufaa kwa wananchi na Taifa kwa jumla.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, leo, Rais wa Jumuiya hiyo Frank Nkinda amesema kwa kipindi kirefu, chama hicho kimejijengea tabia mbaya ya kutafuta uungwaji mkono hata katika masuala yasiyo na maslahi kwa Taifa na kupinga mapendekezo yenye dhamira ya kuwaweka watanzania pamoja.

Akitolea mfano wa baadhi ya mambo hayo ikiwemo ripoti ya kikosi kazi iliyokabidhiwa juzi kwa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ikiwa imesheheni mapendekezo mbali mbali yenye tija kwa taifa letu. Nkinda alisema wao kama wasomi wa Elimu ya juu hawaoni sababu yeyote ya Chadema kuipinga ripoti hiyo

“Sote tulisikia muhtasari wa kile kilichowasilishwa na Mwenyekiti wa Kikosi kazi, Prof. Rwekaza Mukandala kwa Mhe. Rais, kwakweli dhamira yake ni njema. Sasa tumeshangaa kakikundi kamoja kamekuja juu na kusema mapendekezo haya hayafai na kwamba ni matumizi mabaya ya fedha za umma, lakini ikumbukwe kwamba watu hawa waliitwa kutoa maoni yao wakakataa, sasa wanataka hata yale yaliyotolewa na watanzania wengine kwa uhuru na haki watu wayapinge ”alisema Nkinda

Aliongeza kuwa TAHLISO kama Taasisi inayolea nguvu kazi ya Taifa, kimsingi wana mamlaka ya Kuonya, kukemea na kushauri mambo mbalimbali katika Kuchochea maendeleo ya Taifa.

" Tumesikitishwa na kauli ya Katibu mkuu wa Chadema John Mnyika ya kuita ripoti hiyo kuwa ni matumizi mabaya ya fedha za umma kwa kuwa tu wao walikataa kuwasilisha maoni kwenye kikosi kazi cha Rais" alisema Nkinda

Alisema mtu au taasisi yoyote ya kiungwana ilipaswa kupongeza dhamira iliyoonyeshwa na Rais Samia Suluhu Hassan ya kutafuta maridhiano ya kitaifa kwa kupata maoni ya wadau juu ya njia gani za kupita kabla ya kufikia hitimisho na siyo kulalamika mbele ya vyombo vya habari suala alilosema halina msingi wowote.

Aliongeza kuwa Watanzania wameipokea ripoti hiyo kwa mikono miwili na wanawapongeza wadau wote walioshiriki kutoa maoni kwenye kikos...
Educated fools
Hakuna uteuzi siku za karibuni
 
Jumuiya ya Wanafunzi Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO) wamekionya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kutokana na tabia yake ya kupinga mambo mbalimbali yanayofanywa na Serikali hata kama yana manufaa kwa wananchi na Taifa kwa jumla.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, leo, Rais wa Jumuiya hiyo Frank Nkinda amesema kwa kipindi kirefu, chama hicho kimejijengea tabia mbaya ya kutafuta uungwaji mkono hata katika masuala yasiyo na maslahi kwa Taifa na kupinga mapendekezo yenye dhamira ya kuwaweka watanzania pamoja.

Akitolea mfano wa baadhi ya mambo hayo ikiwemo ripoti ya kikosi kazi iliyokabidhiwa juzi kwa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ikiwa imesheheni mapendekezo mbali mbali yenye tija kwa taifa letu. Nkinda alisema wao kama wasomi wa Elimu ya juu hawaoni sababu yeyote ya Chadema kuipinga ripoti hiyo

“Sote tulisikia muhtasari wa kile kilichowasilishwa na Mwenyekiti wa Kikosi kazi, Prof. Rwekaza Mukandala kwa Mhe. Rais, kwakweli dhamira yake ni njema. Sasa tumeshangaa kakikundi kamoja kamekuja juu na kusema mapendekezo haya hayafai na kwamba ni matumizi mabaya ya fedha za umma, lakini ikumbukwe kwamba watu hawa waliitwa kutoa maoni yao wakakataa, sasa wanataka hata yale yaliyotolewa na watanzania wengine kwa uhuru na haki watu wayapinge ”alisema Nkinda

Aliongeza kuwa TAHLISO kama Taasisi inayolea nguvu kazi ya Taifa, kimsingi wana mamlaka ya Kuonya, kukemea na kushauri mambo mbalimbali katika Kuchochea maendeleo ya Taifa.

" Tumesikitishwa na kauli ya Katibu mkuu wa Chadema John Mnyika ya kuita ripoti hiyo kuwa ni matumizi mabaya ya fedha za umma kwa kuwa tu wao walikataa kuwasilisha maoni kwenye kikosi kazi cha Rais" alisema Nkinda

Alisema mtu au taasisi yoyote ya kiungwana ilipaswa kupongeza dhamira iliyoonyeshwa na Rais Samia Suluhu Hassan ya kutafuta maridhiano ya kitaifa kwa kupata maoni ya wadau juu ya njia gani za kupita kabla ya kufikia hitimisho na siyo kulalamika mbele ya vyombo vya habari suala alilosema halina msingi wowote.

Aliongeza kuwa Watanzania wameipokea ripoti hiyo kwa mikono miwili na wanawapongeza wadau wote walioshiriki kutoa maoni kwenye kikos...
Huyu kilaza ana gpa ya ngapi kwanza?
 
Nakubaliana na wewe ila nilitaka kujua TAHLSO ni kinanani na CHADEMA ni kina nani? je hao TAHLSO ulishawahi kusikia wakihoji juu ya nani hasa walimshambulia TUNDU LISU? au tuseme wakati ule hawakuwepo?
kwamba kwenye vyuo vikuu kuna degree inaitwa political science kisha anatokea mpuuzi mmoja anakataza wanafunzi kujihusisha na siasa.... TAHLSO walikuwepo uliskia wakimkosaa kiongozi yule?
sasa tutawaamini vipi?
Kwani nyiee chadema mnaposema uhuru wa kutoa mawazo Kwa Kila mtu au kikundi, mnamanisha mtu kusema Kila ambacho na nyiee mnakipendaa?? Kama hawajazungumzia juuu ya shambulio la lisu, wewe kusema. Uhuru wa maoni siomtu kumpangia aseme kitu unachokipenda wewe, hawajasema kuhusu shambulio la lisu Leo, maaana yake Hilo halipoo mioyoni mwao, kikubwa kubalini Kwa hili walilolisema juu ya chadema. Kama mnataka Kila mtu aseme mnachotaka nyinyi basi hapo hakuna uhuru wa mawazo ya mtu au kikundi kama chadema mnavyodai. Kubalini mawazo kinzani na nyiee ILI na nyiee mawazo yenu yaonekane kuwa mko sahihi kukosoa wenzenu. Kumbukeni chadema sio malaika wa mbinguni.
 
Chadema kubalini kusikia na mawazo kinzani kwenu pia, hiii ndio demokrasia sahihi. Nyinyi ndio vinala wa kutaja uhuru wa mawazo na kukosoa, Kwa Nini nyinyi hampendi kukosolewa??. Au nyinyi furaha yenu kikosolewe chama kinginee tuuu Kwa kuwa nyinyi ni malaika? La hasha, pokeeni kukosolewa ndio itakuwa sababuu ya kukua kwenu chadema

Ni wapi CDM wamekuzuia kukosoa, au umekariri ukisikia CDM hawataki kukosolewa na ww unarukia hilo neno ili uende na fashion?
 
..iko hivi.

..Kikosi kazi kimewasilisha mapendekezo kwa Raisi.

..Je, unaridhika na mapendekezo ya kikosi kazi? Sababu zako ni zipi?

..Je, haujaridhika na mapendekezo ya kikosi kazi? Hoja zako ni zipi?

..Tujielekeze kwenye mapendekezo ya kikosi kazi.

..Vyama na taasisi mbalimbali vipime na kuyachambua mapendekezo hayo badala ya kushambuliana.

..Wajumbe wa Kikosi kazi wajitokeze kutoa ufafanuzi na kuyatetea mapendekezo waliyoyatoa.
Kama hamjaridhika na jicho kikosi kazii, endeleeni kupaza sauti, ila mkumbuke kwamba, sio lazima mawazo yenu ndio yasikolizwe tuu, sikilizeni na mawazo ya wenzenu. Hamjaridhika wekeni mjadala Mpana, ilakumbukeni sio lazima napendekeza yenu yakubaliwe kwani na nyiee sio Malaika wa mbinguni, kubalini na mawazo mbadala. Na kama hamuamini mawazo na kile wakionacho wenzenu, hiyo sio demokrasia Bali itakua ubishi na kelele tuu.
 
Ni wapi CDM wamekuzuia kukosoa, au umekariri ukisikia CDM hawataki kukosolewa na ww unarukia hilo neno ili uende na fashion?
Mbona mnawafokea TAHILSO? Wamekanya na kuwataka msiwe mnakosoa Kila kitu. Sasa naona imewauma saana
 
Ni wapi CDM wamekuzuia kukosoa, au umekariri ukisikia CDM hawataki kukosolewa na ww unarukia hilo neno ili uende na fashion?
Chadema si walikataa kushirikiana na hicho kikosi kazi basi walitakiwa kukaa pembeni waawachie vyama waliokubaliana na kikosi kazi sio wajitokeze na kuanza kutoa mapovu Yao na matamko kama ya waimba taarabu
 
Kama hamjaridhika na jicho kikosi kazii, endeleeni kupaza sauti, ila mkumbuke kwamba, sio lazima mawazo yenu ndio yasikolizwe tuu, sikilizeni na mawazo ya wenzenu. Hamjaridhika wekeni mjadala Mpana, ilakumbukeni sio lazima napendekeza yenu yakubaliwe kwani na nyiee sio Malaika wa mbinguni, kubalini na mawazo mbadala. Na kama hamuamini mawazo na kile wakionacho wenzenu, hiyo sio demokrasia Bali itakua ubishi na kelele tuu.

..kauli njema zaidi ingekuwa ni mawazo ya kila upande yatasikilizwa.

..kwamba juhudi zitafanyika kuzingatia mawazo, mapendekezo, na mitizamo, ya makundi mbalimbali.

..Watz tunapaswa kujifunza kusikilizana na kutafuta maelewano.

..Raisi Ssh amenukuliwa akisema kuwa mapendekezo ya kikosi kazi sio amri kwa serikali yake.

..Kwa maoni yangu Rais hakupaswa kutoa kauli ile kwasababu yeye ndiye aliyeunda na kukipa hadidu za rejea kikosi kazi.

..Kwa hiyo utaona hata Rais Ssh sio msikivu na sio mkomavu ktk masuala ya siasa na demokrasia.
 
Siku hizi wasomi ni weupe sana tofauti na enzi zetu! Natilia sana shaka elimu wanayopewa vijana wetu siku hizi huku vyuoni.
 
Back
Top Bottom