TAHADHARI: Wizi kwa unaempa lift

TAHADHARI: Wizi kwa unaempa lift

Dreamliner

JF-Expert Member
Joined
Jan 17, 2010
Posts
2,034
Reaction score
215
Wadau.. Mfanyakazi mwenzangu, ameibiwa LAPTOP baada ya kuwapa lift watu watatu, mmoja akiwa ni mwanafunzi FAKE. Alikuwa anatoka maeneo ya MAJOHE asubuhi kuelekea maeneo ya Gongolamboto halafu kibaruani. Alipofika Relini, Watu wawili na mwanafunzi FAKE wakaomba lift. Jamaa alipoona na mwanafunzi yupo. akasimama na kuwapa lift.

Wale watu, walilaza kiti cha nyuma na kupata ACCESS kwenye buti ambako alikuwa ameweka Laptop. Wakaitoa kwenye BAG lake, na kuupitisha chini ya kiti cha abiria aliyeko upande wa kushoto wa gari mbele, (Mwanafunzi fake) kwani alipoingia garini, aliweka madaftari yake chini. Hivyo basi, alipofika Pugu Sec, akatelemka, na kuchukua madaftari (Counters) yake na kuunganisha na laptop ya jamaa.

Jamaa alikuja kushtuka baada ya kufika kibaruani na kuona hana laptop na alijua kaibiwa kwani zile shughuli aliziona zikifanyika, lakini hakuhisi kama ni wizi ulikuwa unaendelea. Wale wezi wawili wakatelemkia Gongo la Mboto..

Hivyo hata nyuma ya BUTI la gari sio salama tena. Dawa ni kutompa mtu yeyote lift.
 
Usinikumbushe kwa kuwa nishaibiwa simu hivi hivi na mtu niliyempa msaada wa usafiri na huwa nishasema simpi mtu nisiyemfaham msaada kama huo tena maana asilimia kubwa sio watu wema awe mwanafunzi au mama mtu mzima au dada
 
Watu sio wastaarabu kabisa...lift upewe na bado uibe...kweli ni somo kwetu sote
 
Sasa kama Wababa wanafanyiwa hivi, wamama itakuwaje? hii ni moja ya sababu wanawake wengi hawatoi lift kwa yeyote njiani, potelea mbali acha tuonekane tuna roho mbaya tumechoka kuibiwa mapochi na vipodozi vyetu kila siku!
 
Sasa kama Wababa wanafanyiwa hivi, wamama itakuwaje? hii ni moja ya sababu wanawake wengi hawatoi lift kwa yeyote njiani, potelea mbali acha tuonekane tuna roho mbaya tumechoka kuibiwa mapochi na vipodozi vyetu kila siku!

Utoe lift una gari wewe? Kujishaua tu kama FaizaFox.
 
Say ni bahati mbaya lakini abiria tena stranger analaza kiti cha gari yako wewe owner hustuki tu?????

Kioo cha ndani "rear driving mirror" kama nakumbuka vizuri alikuwa hatumii!!!!?????

Tunatofautiana sana

Ndiyo maana nimesema hilo jamaa ni liboya la kufa mtu.
 
Say ni bahati mbaya lakini abiria tena stranger analaza kiti cha gari yako wewe owner hustuki tu?????

Kioo cha ndani "rear driving mirror" kama nakumbuka vizuri alikuwa hatumii!!!!?????

Tunatofautiana sana

Kuna ndugu yangu naye kaibiwa simu ya blackberry,alikuwa amewapatia lift jamaa wawili maeneo ya Stop over Kimara.
 
kwa sababu hizohizo nilishaacha kuwapa watu lifti na nilishamuomba Mungu anisamehe kwa hilo
 
Mi niliibiwa simu hivyo lift sitoi ovyo!!!
Wadau.. Mfanyakazi mwenzangu, ameibiwa LAPTOP baada ya kuwapa lift watu watatu, mmoja akiwa ni mwanafunzi FAKE. Alikuwa anatoka maeneo ya MAJOHE asubuhi kuelekea maeneo ya Gongolamboto halafu kibaruani. Alipofika Relini, Watu wawili na mwanafunzi FAKE wakaomba lift. Jamaa alipoona na mwanafunzi yupo. akasimama na kuwapa lift.

Wale watu, walilaza kiti cha nyuma na kupata ACCESS kwenye buti ambako alikuwa ameweka Laptop. Wakaitoa kwenye BAG lake, na kuupitisha chini ya kiti cha abiria aliyeko upande wa kushoto wa gari mbele, (Mwanafunzi fake) kwani alipoingia garini, aliweka madaftari yake chini. Hivyo basi, alipofika Pugu Sec, akatelemka, na kuchukua madaftari (Counters) yake na kuunganisha na laptop ya jamaa.

Jamaa alikuja kushtuka baada ya kufika kibaruani na kuona hana laptop na alijua kaibiwa kwani zile shughuli aliziona zikifanyika, lakini hakuhisi kama ni wizi ulikuwa unaendelea. Wale wezi wawili wakatelemkia Gongo la Mboto..

Hivyo hata nyuma ya BUTI la gari sio salama tena. Dawa ni kutompa mtu yeyote lift.
 
Kuna ndugu yangu naye kaibiwa simu ya blackberry,alikuwa amewapatia lift jamaa wawili maeneo ya Stop over Kimara.

Mika minne iliyopita jamaa yangu naye kaweka pesa kwenye begi la laptop halafu kaliweka siti ya nyuma kwenye saloon kawapa jamaa lifti buguruni wakawa busy kumpigisha story njia nzima nonstop kufika tabata wakashuka kumbe wamelamba 2.5 M....

Binadamu ndio wanaosababisha binadamu wengine kuwa na roho mbaya...huko maporini ukimpa mtu Lifti huna hakika kama mbele ya safari hatakuonesha AK47 na kujimilikisha gari, Huku mijini simu na lap top ni majanga kila uchao.......acha tuishi kama ulaya, hakuna huruma, hakuna kuaminiana!
 
Hebu lakini niwaulize? unampaje lift mtu usiyemfahamu?? tena kwa ulimwengu huu ulioharibika?? tujifunze kuchukua tahadhari jamani!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom