whitehorse
JF-Expert Member
- Aug 29, 2009
- 2,570
- 4,455
WanaJF wenzangu, napenda kuchukua nafasi hii kuwatahadharisha na usalama wa magari yenu mnapoyapaki pale quality centre hali ya usalama inazidi kupotea. Sasa imekuwa sawa na mlimani city ya zama zile. Wale wezi wa kubomoa vioo na kukomba vilivyomo wamehamia rasmi kule nyerere road kwa sasa. Waambie ndugu jamaa zako na rafiki zako mimi ni muhanga nimeibiwa kabegi kana nguo za mtoto walidhani labda ni vitu vya maana. Nikaenda pale police chang'ombe kureport nikaambiwa kwa sasa kesi kuhusu wizi wa vitu kwenye magari mahali pale zinamwagika kila iitwayo siku. Na sijawahi kuhizi hivyo kutokana na ulinzi kabambe uliopo pale. Naomba mwenye kusoma habari hii awaambie na wengine.
Sent from Samsung tablet
Sent from Samsung tablet