Grand Master Dulla
JF-Expert Member
- Jul 20, 2012
- 411
- 146
Nilisikitishwa sana jana wakati nasikiliza redio moja ya kenya ambapo jamaa mmoja mkalenjini kwa kabila anayeanzia na jina la Joseph (ubin wake nimeusahau) alipokuwa akielezea kwa uchungu mazira yaliyomkuta alipokwenda kufanya kazi katika nchi moja ya kiarabu,kisa chake kinaanza kwamba mnamo mwishoni mwa mwaka jana alipata kazi ya uhouse boy katika nchi mojawapo za huko uarabuni,anadai kwamba kazi iliendelea vizuri sana mpaka miezi ya mwanzoni mwa mwak huu pale alipogundua kwamba mood ya bosi wake mzee mwenye nyumba imebadilika sana juu yake bila ya yeye kujua sabab hasa ya msingi.Anadai kuwa kuna siku bosi wake alimwita chumbani na kuanza kutaka kulala naye na alipokataa bosi akaanza kumlazimisha wakati huo mke wa bosi alikuwa hayupo katoka toka asubuhi,kumlazimisha kuliendelea na madai hasa si kwamba bosi alikuwa anataka alalwe bali alikuwa anataka kumlalia joseph alipoona anakataa sana bosi akatoa pendekezo kwamba joseph kama anaona hatari sana basi aanze kumlala yeye bosi yaani bosi alaliwe kwanza kisha bosi amlale josephy kitendo ambacho pia josephy alikataa pia. Basi si muda mkewe akarudi na bosi akatulia lakini akaanza kuonyesha mateso kama vile kutompa chakula ila kila siku jamaa alikuwa akimsisitizia kuhusu hilo suala.Alipoona ankonda sana alifanikiwa kutoroka akenda ubalozini kwao nao wakamrudisha kenya sasa anaishi jijini Nairobi na wala hana mpango wa kurudi tena uarabuni.
Je hiki ni kisa ch ajabu kwako? hivyo kaeni chonjo kwa wenye mpango wa kwenda nchi hizo zilizobarikiwa kwa utajiri wa mafuta.
Je kuna mkasa wowote ule wa kusikitisha unaofanana na huu unaoujua? FUNGUKENI WADAU!!!!
Je hiki ni kisa ch ajabu kwako? hivyo kaeni chonjo kwa wenye mpango wa kwenda nchi hizo zilizobarikiwa kwa utajiri wa mafuta.
Je kuna mkasa wowote ule wa kusikitisha unaofanana na huu unaoujua? FUNGUKENI WADAU!!!!