Tahadhari kwa waumini wa Gwajima

Tahadhari kwa waumini wa Gwajima

Ukitaka kufaidi thread Kama hii, tafuta computer yenye screen kubwa yenye mwanga usioumiza macho pamoja na kopo kuubwa la bisi na bilauli moja ya juisi ya pensheni. Hapo ndio utajua utamu wa JF !🙂🙂
 
Si busara kuzumzia maisha ya ndoa ya mtu, ni mambo mapana na kila mmoja yanamsibu ila yanatofautiana.
 
Teh teh teh jamani laha sana ebu waacheni hawa watumishi wa bwana watupe raha .padri vs.askofu inanogaje?
 
Gwajima aliwarekodi watu aliokuwa anaenda kuwapa ushauri wa kiroho.
Halafu anatangaza ushauri huo na matatizo yao hadharani.
Ole wako...ukimwambia siri zako utajuta.

Yaani kama kumsihi Josephine amruhusu Slaa aendelee na siasa ni suala la kiroho basi huyo mama ni kweli Atakuwa na mashetwani kwa roho!
 
Wauminiwake kuweni waangalifu huyo asije kuwapiga kibiriti kama Kibwetere
 
Gwjima hana kosa apo mwenye makosa apo ni uyo padli msaliti sababu nae analiju neno akuanzae mmalize
 
Yaani wewe na Gwajima nyote mu wanadamu...

Lakini unataka sisi tukuamini zaidi mwanadamu wewe kuliko Gwajima...

Sasa kama Gwajima ni mwanadamu na kakosea, iweje wewe uliye mwanadamu usiwe umekosea kutoa tahadhari hii...?
 
Gwajima kamuweza kweli mzee wa mihogo ambae ni mbeya na mwongo na mwenye tamaa za kimwili kama shetani.
 
Gwajima mtumishi anaetia mashaka sana!! hasa ukwasi alionao na ufukara wa waumini wake!! achilia mbali kuzaa na mke wa mtu..!"
 
Huwezi kusema hadharani siri za maisha binafsi ya mtu kama umeaminiwa. Gwajima anajiita au kujitangaza kwamba ni askofu,Dr akamwamini kwa kumtaka ushauri(kama ni kweli) kwa mambo ya ndani sana ya familia,lakini Gwajima ametumia nafasi hiyo kushambulia familia ya Dr Slaa. Mapovu yamemtoka kujibu hoja za kisiasa kuweka wazi mazungumzo ya siri(kama yalikuwepo). Hili si sahihi. Kama aliyozungumza kuhusu Dr Slaa ni ya kweli,Gwajima amekiuka wajibu wake kama kiongozi wa dini.Haaminiki,hana kifua cha kubeba siri za watu. Dr Slaa huwa anakija na nondo nzito za serikali,lakini sikuwahi kumsikia akitaja vyanzo vya taarifa zake. Dr ni Padre wa Kanisa Katoliki,amefundishwa kutunza siri za watu,hata kutoa maisha yake.
 
Ukitaka kufaidi thread Kama hii, tafuta computer yenye screen kubwa yenye mwanga usioumiza macho pamoja na kopo kuubwa la bisi na bilauli moja ya juisi ya pensheni. Hapo ndio utajua utamu wa JF !🙂🙂

..hiyo juice ya 'pensheni' kuinunua mpk uwe umestaafu sio.!
 
Dr Slaa kaambiwa akijibu,Gwajima atarusha hiroshima yaani ni ma atoms tu hadi hawataona tena..Kazi ipo
 
Ni muda mrefu jamii yetu imekuwa ikiwaheshimu na kuwaamini viongozi wa dini katika masuala mbalimbali ya kiroho na ustawi wa familia.

Ni jambo la kawaida sana kwa waumini wa dini zote kupeleka matatizo yao mbalimbali ya kifamilia kwa viongozi wa dini.

Ni dhahiri kwamba wengi wetu hupeleka masuala mbalimbali hata yale ya unyumba na siri nzito nzito za chumbani na familia kwa ujumla kwa kuwa tuna imani viongozi wa dini wana hulka ya kutunza siri na kusaidia kutatua matatizo yetu ya kiroho au kifamilia.

Hii ni tofauti kwa Gwajima ambaye ni mtomvu wa heshima ya kiongozi wa dini kwa kueleza siri za familia aliyoipa huduma za kiroho kisa tu kachokozwa kisiasa na yeye kajibu kwa kutoa siri za familia ya Slaa.

Angekuwa daktari angeweza kufutiwa cheti na kudaiwa fidia.

Lakini tukumbuke ni Gwajima huyu huyu aliyeshutumiwa kuvuruga ndoa ya Mbasha badala ya kutatua mgogoro wa familia hiyo.

Hii ni trend ya Gwajima anayejiita Bishop ambayo inatakiwa kuangaliwa kwa jicho la Tahadhari hasa hasa na waumini wake wanaompelekea siri za ndani.


KWA HISANI YA MTU WA TANZANI!!

Haya mambo mbona huwa hamsemi hadi leo gwajima kawapeni za uso
 
Back
Top Bottom