Ni muda mrefu jamii yetu imekuwa ikiwaheshimu na kuwaamini viongozi wa dini katika masuala mbalimbali ya kiroho na ustawi wa familia.
Ni jambo la kawaida sana kwa waumini wa dini zote kupeleka matatizo yao mbalimbali ya kifamilia kwa viongozi wa dini.
Ni dhahiri kwamba wengi wetu hupeleka masuala mbalimbali hata yale ya unyumba na siri nzito nzito za chumbani na familia kwa ujumla kwa kuwa tuna imani viongozi wa dini wana hulka ya kutunza siri na kusaidia kutatua matatizo yetu ya kiroho au kifamilia.
Hii ni tofauti kwa Gwajima ambaye ni mtomvu wa heshima ya kiongozi wa dini kwa kueleza siri za familia aliyoipa huduma za kiroho kisa tu kachokozwa kisiasa na yeye kajibu kwa kutoa siri za familia ya Slaa.
Angekuwa daktari angeweza kufutiwa cheti na kudaiwa fidia.
Lakini tukumbuke ni Gwajima huyu huyu aliyeshutumiwa kuvuruga ndoa ya Mbasha badala ya kutatua mgogoro wa familia hiyo.
Hii ni trend ya Gwajima anayejiita Bishop ambayo inatakiwa kuangaliwa kwa jicho la Tahadhari hasa hasa na waumini wake wanaompelekea siri za ndani.
Isitoshe naamini UKAWA itashindwa vibaya, japo sijafanya utafiti, kwa sababu zifuatazo:
1) waumini wa kweli wa dini, aliyoyasema Ngwajima, kwenye kivuli cha UKAWA, kama
ulivodokeza, kinawaondolea imani na umoja huo.
2) kutofautiana kwa Gwajima na Slaa, kunawaondoa wafuasi wa Slaa CHADEMA.
3) wananchi makini, wanaopenda mabadiliko nje ya CCM, wanajiuliza tena kama viongozi wa
UKAWA wanaweza kukidhi hilo.
4) UKAWA inategemea kundi la vijana kwa kuchochea chuki dhidi ya CCM, kwa mfano alio utoe
Mgombea mwenza kwenye kampeni kuhusu kilichotokea Misri na mambo mengine
yanayongelewa kujikomba kwa vijana. Lakini ikumbukwe ni vijana haohao wanarudi nyumbani
na njaa zao baada ya kukesha na kushinda kwenye hiyo mikusanyiko. Naamini, wachache
kama siyo wengi, nwisho wa siku watajitambua.
5) uadilifu wa viongozi wa UKAWA waliohama CCM, haujatetewa na haohao waliowaita mafisadi
zaidi ya maneno yasiyo na tija kwa kukubali kwamba kweli ni fisadi. Ati shetani akingia
nyumba ya malaika anakuwa malaika. Huwezi kuondolewa dhambi bila kutubu.
Watubu kwanza.