Michael Amon
JF-Expert Member
- Dec 22, 2008
- 8,775
- 3,610
Wapendwa wana JF wenzangu, ninapenda kuwatahadharisha watumiaji wote wa facebook waliopo katika jamvi hili hata wale ambao hawapo katika jamvi hili kuwa makini pale mtumiapo facebook maana leo yamemkuta dada yetu mmoja ambaye alipostiwa status na mtu asiyemfahamu katika account yake bila ya yeye kufahamu. na mbaya zaidi hali hiyo ilitokea wakati yupo katika jitihada za kuingia katika chumba cha mtihani. Status hiyo ilisema hivi, " Nina hamu ya ******* na mwanaume mwenye **** ***** ******* hadi ***** ****".
Ni vyema ndugu zangu tukawa makini katika kutumia hizi social network hasa facebook ili kuepuka fedheha kama hizi. Na ili kuepuka hii hali ni vyema mkazingatia mambo yafuatayo:-
Ni vyema ndugu zangu tukawa makini katika kutumia hizi social network hasa facebook ili kuepuka fedheha kama hizi. Na ili kuepuka hii hali ni vyema mkazingatia mambo yafuatayo:-
- Kwanza kabisa nisingependa kushauri kutoa password ya account yako kwa mtu yoyote hasa yule unayemuita laazizi wako, wa ubani, your sakafu etc. kwani matatizo kama haya yanaweza kutokea endapo mtaachana.
- Pili nashauri msipende kuweka e-mail address na namba zenu za simu katika profile zenu kwa namba contact details hizo zinatumika sana katika kuhack account ya mtu.
- Tatu msipende kuaccept request za mtu usiyemfahamu au kufungua link au application usizozifahamu kwani njia hizo huwa zinatumika sana katika kuhack.
- Nne usisahau kulog out mara baada ya kutumia facebook hata kama ni kwenye simu au laptop yako kwani mtu mwingine anaweza akafungua facebook na kuikuta account yako na kuifanyia vyvoyote atakavyo.