Siku za karibuni kumeibuka ntondo kwa askari Wa barabarani kutumia photo editor.. wanakubambika kesi huku unawatazama hata haya hawana ..mfano mwezi Dec nilikuwa nasafiri kutokea Dar kwenda Moshi nilipopita mto wami kwa mbele nolikuta askari polisi kikosi cha usalama barabarani wakanisimamisha nakunionyesha picha iliyokuwemo kwenye simu yake ya mkononi, kwenye picha hiyo kulikuwepo gari langu speed 58 na kibao cha 50 lakini niliwa nimekanyaga zebra ndipo hapo nikaanza kukumbuka eneo hilo la kibao cha 50 na zebra ..kwa uzoefu niliokuwa nao kwa njia Ile kipande cha msata mpaka Mandela sikumbuki kuona mazingira hayo na wala sikuwa speed katika kila kibao cha 50 nilikuwa nafuata kama maelekezo yanavyosema.. niliwalipa na wakati wakurudi nilikutana na askari wengine upande wa korogwe..ikawa vile vile picha yenye kibao cha kuimaliza 50 na speed 61 lakini hii niliing'amua kwa jinsi ilivyokuwa.. wazee ndugu zangu tuweni makini wanatumia photo editor kutumaliza.