Namnukuu Paskali.... "Kikwete alikuwa dhaifu sana ndio maana hakutaka wanyongwe.... " Sikubaliani kwa asilimia zote na Paskali.... Ni kweli JK alikuwa dhaifu!? Lenient! Lakini kwa ishu ya kunyongwa aliongozwa na tafakuri na mtazamo binafsi wenye kuacha maswali yenye majibu ya wazi kabisa...
Kikwete hakutokea porini mpaka kuupata urais hata Mkapa Mwinyi .... Ni watu waliokulia kwenye system, kwenye chama... Maisha yao kwa sehemu kubwa yalikuwa siasa... Walifanya siasa tangu wakiwa vijana.. Hawa hawakusukumiziwa urais, hawakuwa wanajaribu bali walikuwa ni wanasiasa walioiva...
Sipingani na hoja ya kuwanyonga waliokamatwa na madawa ya kulevya... Napingana na Paskali kwa kumuita JK dhaifu kwenye hili.... Mnyonge mnyongenj lakini haki yake mpeni....
Tafakuri ya kikwete kwa mtazamo wangu ni hii.... Hakutaka kutoa idhini ya kunyonga... Hii ni official hata kama PENGINE kwenye shughuli za kisiasa na uongozi wa nchi kuna watu walikufa kupitia yeye, lakini akikiangalia chama akiiangalia serikali aliona wazi kabisa kuna watu wabaya zaidi waliojificha kwenye koti la ngozi ya kondoo waliofanya mabaya zaidi kuliko hao vijana waliokamatwa ambao hata hivyo hawajui zaidi ya kutumika kama punda huku wazungu wa unga wenyewe wakiachwa salama salimini....
Tafakuri ya kikwete ni hii... Tazama kama yule kiongozi mkubwa kabisa ndani ya jumuiya ya chama aliyeaminiwa kutengeneza dawa za kupunguza makali ya ukimwi., lakini ndugu yule kwa kukosa UTU, kwa kukosa UZALENDO kwa kukosa HEKIMA, AKILI na WELEDI na ukizingatia analipwa pesa nzuri tu kwa kazi ile akaamua kutengeneza dawa bandia.. Huu ni zaidi ya uuaji, huu ni zaidi ya uhujumu uchumi.. Huu ni sawa na uhaini... Dawa zile zingeuzwa nje ya nchi na zikakamatwa tungeweka wapi nyuso zetu kama TAIFA? lakini Je dawa zile bandia zimeteketeza roho ngapi zilizokuwa na matumaini makubwa ya kupata nafuu huku wakiamini wanakunywa dawa sahihi?
Uuaji na ukatili huu mkubwa haujaonekana wameonekana vijana wetu, jiulize ndani ya chama na serikali kuna wenye madaraka wangapi wamefanya madudu ya kutisha yaliyoangamiza roho nyingi? Kikwete aliyafahamu yote haya... Kuacha kusaini hati ile ya kifo ilikuwa na maana yake kubwa sana nyuma ya pazia....!!!! Nampongeza Kikwete kwenye hili pamoja na udhaifu wake wote....
Miezi michache iliyopita kukawa na amsha amsha kubwa sana ya vita dhidi ya madawa ya kulevya... Vita ikaishia njiani kwa aibu kubwa baada ya kubainika kinara wa mapambano hayo alikuwa na agenda zake binafsi na alifaidika kwa hali na mali... Kama ni kitanzi kilipaswa kianzie kwa huyu bwana... Ile haikuwa vita bali geresha....!!!!
Paskali Kikwete hakutaka kunuka damu... Hakutaka kumwaga damu isiyo ha hatia.. Huku damu yenye hatia ikiendelea kutamba na kutamalaki....
Walioidhinishwa kunyongwa ni wa wa awamu zilizopita! Je awamu hii sisi hatuna????