Jurrasic Park
JF-Expert Member
- Sep 13, 2013
- 3,831
- 6,878
Kaka yangu mshana umekuwa hopeless hivyo
Bora ungebakia kupiga ramli tu haya mengine achana nayo
Bora ungebakia kupiga ramli tu haya mengine achana nayo
MKUU KATIKA HILI KILA MWENYE MAMLAKA AKAJIFUNZE KWA MH.KIKWETE.Umeona mbali sna kikwete alikuwa zaidi ya kiongozi zaidi ya Baba ktk maisha hkn kitu kigumu km kuvumilia kuelezwa mapungufu yko wakt ww ndio una power na usitumie power yko kumuazibu anae kueleza ukweli maana binadam tumeubwa kuchukia ukweli...
Nikishakuwa kaka yako siwezi kuwa hopeless labda unibadilishie title.... By the way umeniita hopeless kitu ambacho ni mtazamo wako na sina tatizo kabisa na hilo.... Sasa hebu nijibu kwa hoja ukionyesha huo u hopeless! Ukishindwa basi wewe ndio utakuwa zaidi ya hopelessKaka yangu mshana umekuwa hopeless hivyo
Bora ungebakia kupiga ramli tu haya mengine achana nayo
Naona uko kwenye kichwa cha JK!
hahahhaaahaha... Bavicha mna hali mbaya kweli!
Umepaelewa pale nilipoandika tafakuri ya Kikwete kwa mtazamo wangu?
Sometimes wanachosha kweli hawa wadudu sijui wamelishwa nini?Tatizo la wanaCCM wanapenda kusifu na kutukuza tu,ndiyo ahwa waliomsifu JK enzi zake mpaka JK akaona taabu lakini nafikiria leo JK anashangaa wale waliomshangilia na kumpa big up ndiyo wale leo wanaomtukana matusi yote.Hakika anaona bora upinzani uliomzodoa pale pale yakaisha kuliko hawa wanafiki wapiga makofi mwisho wa kipindi wanakutukana mpaka basi.
Miezi michache iliyopita kukawa na amsha amsha kubwa sana ya vita dhidi ya madawa ya kulevya... Vita ikaishia njiani kwa aibu kubwa baada ya kubainika kinara wa mapambano hayo alikuwa na agenda zake binafsi na alifaidika kwa hali na mali... Kama ni kitanzi kilipaswa kianzie kwa huyu bwana... Ile haikuwa vita bali geresha....!!!!
Paskali Kikwete hakutaka kunuka damu... Hakutaka kumwaga damu isiyo ha hatia.. Huku damu yenye hatia ikiendelea kutamba na kutamalaki....
Walioidhinishwa kunyongwa ni wa wa awamu zilizopita! Je awamu hii sisi hatuna????
Nimelizungumzia hili ndani ya mada kuu,labda tu kwakuwa sikutoa mifano dhahiri kama wewemshana jr hatuwezi sema kikwete was good sababu sasa hivi tuna magufuli ambaye hatukubaliani naye. it is wrong na ndo hapo kwa upande wa wapinzani wanaonekana kuwa wanaendesha siasa kwa mihemko na matukio. mnamkumbuka mwangosi?mnamkumbuka dr ulimboka? dr mvungi?ab kibanda kumwagiwa tindikali?kubenea? mimi nakumbuka. nakumbuka hya mambo yalitokeaje na nini kilikuja kutokea baadaye. aliyemhusika na mauaji ya mwangosi alipata adhabu gani? alipandishwa cheo. aliye taka kumuua dr ulimboka alikuwa wapi ?kwa maelezo ya kubenea ni mtu wa ikulu. nini kilifanyika? haya mambo kuna watu wanakosea sana kuanza kumsafisha kikwete hivi sasa kwa uovu alioufanya simply kwa sababu kuna maguful. mi nlidhani tunapaswa kukemea uovu uliopita,uliopo na ujao. huo ni mtizamo wangu.
Nimelizungumzia hili ndani ya mada kuu,labda tu kwakuwa sikutoa mifano dhahiri kama wewe
Leo unamwambia kikwete.mnyongeni?Mzee wa mafumbo na vijembe vya kiaina
Sometimes wanachosha kweli hawa wadudu sijui wamelishwa nini?
Una mashetani wewe, wangapi wameuliwa na kuteswa enzi za Kikwete.Kikwete alikuwa na busara,mstahimilivu na muungwana. Ni wangapi wamepotea awamu hii bila miili yao kuonekana? Ni wangapi wamepigwa risasi kwa kuonesha udhaifu kwenye taasisi za serikali!? Ni wangapi wameuawa kwa kujeruhiwa na risasi za polisi kabla hawafikishwa mahakamani kutekeleza agizo lakunyang'anya silaha? Ni wangapi wako magerezani kwa kutekeleza haki yao ya kikatiba ya kuchagua na kuchaguliwa,kutoa maoni na kukutana?
Mdhaifu ni yule anayetumia nguvu pasipo busara na akili huku yeye akiwa baba wa familia. Akigawa familia kwa misingi ya kikanda, kidini,kisiasa na kiitikadi. Asiyejua nafasi yake kwa familia kwa kuficha ukweli na kutokuwa na uhakika na ukigeu geu kwa kile anachosema na kutenda. Wapi wenye vyeti feki!?Wakati Bashite analindwa huku kukiwa na tuhuma za wazi za kutumia cheti kisicho chake.
Kuacha kusaini hati ile ya kifo ilikuwa na maana yake kubwa sana nyuma ya pazia....!!!! Nampongeza Kikwete kwenye hili pamoja na udhaifu wake wote....
Miezi michache iliyopita kukawa na amsha amsha kubwa sana ya vita dhidi ya madawa ya kulevya... Vita ikaishia njiani kwa aibu kubwa baada ya kubainika kinara wa mapambano hayo alikuwa na agenda zake binafsi na alifaidika kwa hali na mali... Kama ni kitanzi kilipaswa kianzie kwa huyu bwana... Ile haikuwa vita bali geresha....!!!!
Paskali Kikwete hakutaka kunuka damu... Hakutaka kumwaga damu isiyo ha hatia.. Huku damu yenye hatia ikiendelea kutamba na kutamalaki....
Walioidhinishwa kunyongwa ni wa wa awamu zilizopita! Je awamu hii sisi hatuna????
MKuu Mshana,Namnukuu Paskali.... "Kikwete alikuwa dhaifu sana ndio maana hakutaka wanyongwe.... " Sikubaliani kwa asilimia zote na Paskali.... Ni kweli JK alikuwa dhaifu!? Lenient! Lakini kwa ishu ya kunyongwa aliongozwa na tafakuri na mtazamo binafsi wenye kuacha maswali yenye majibu ya wazi kabisa...
Kikwete hakutokea porini mpaka kuupata urais hata Mkapa Mwinyi .... Ni watu waliokulia kwenye system, kwenye chama... Maisha yao kwa sehemu kubwa yalikuwa siasa... Walifanya siasa tangu wakiwa vijana.. Hawa hawakusukumiziwa urais, hawakuwa wanajaribu bali walikuwa ni wanasiasa walioiva...
Sipingani na hoja ya kuwanyonga waliokamatwa na madawa ya kulevya... Napingana na Paskali kwa kumuita JK dhaifu kwenye hili.... Mnyonge mnyongenj lakini haki yake mpeni....
Tafakuri ya kikwete kwa mtazamo wangu ni hii.... Hakutaka kutoa idhini ya kunyonga... Hii ni official hata kama PENGINE kwenye shughuli za kisiasa na uongozi wa nchi kuna watu walikufa kupitia yeye, lakini akikiangalia chama akiiangalia serikali aliona wazi kabisa kuna watu wabaya zaidi waliojificha kwenye koti la ngozi ya kondoo waliofanya mabaya zaidi kuliko hao vijana waliokamatwa ambao hata hivyo hawajui zaidi ya kutumika kama punda huku wazungu wa unga wenyewe wakiachwa salama salimini....
Tafakuri ya kikwete ni hii... Tazama kama yule kiongozi mkubwa kabisa ndani ya jumuiya ya chama aliyeaminiwa kutengeneza dawa za kupunguza makali ya ukimwi., lakini ndugu yule kwa kukosa UTU, kwa kukosa UZALENDO kwa kukosa HEKIMA, AKILI na WELEDI na ukizingatia analipwa pesa nzuri tu kwa kazi ile akaamua kutengeneza dawa bandia.. Huu ni zaidi ya uuaji, huu ni zaidi ya uhujumu uchumi.. Huu ni sawa na uhaini... Dawa zile zingeuzwa nje ya nchi na zikakamatwa tungeweka wapi nyuso zetu kama TAIFA? lakini Je dawa zile bandia zimeteketeza roho ngapi zilizokuwa na matumaini makubwa ya kupata nafuu huku wakiamini wanakunywa dawa sahihi?
Uuaji na ukatili huu mkubwa haujaonekana wameonekana vijana wetu, jiulize ndani ya chama na serikali kuna wenye madaraka wangapi wamefanya madudu ya kutisha yaliyoangamiza roho nyingi? Kikwete aliyafahamu yote haya... Kuacha kusaini hati ile ya kifo ilikuwa na maana yake kubwa sana nyuma ya pazia....!!!! Nampongeza Kikwete kwenye hili pamoja na udhaifu wake wote....
Miezi michache iliyopita kukawa na amsha amsha kubwa sana ya vita dhidi ya madawa ya kulevya... Vita ikaishia njiani kwa aibu kubwa baada ya kubainika kinara wa mapambano hayo alikuwa na agenda zake binafsi na alifaidika kwa hali na mali... Kama ni kitanzi kilipaswa kianzie kwa huyu bwana... Ile haikuwa vita bali geresha....!!!!
Paskali Kikwete hakutaka kunuka damu... Hakutaka kumwaga damu isiyo ha hatia.. Huku damu yenye hatia ikiendelea kutamba na kutamalaki....
Walioidhinishwa kunyongwa ni wa wa awamu zilizopita! Je awamu hii sisi hatuna????