TAFAKARI: Kwanini Rais anaogopa kutubu?

TAFAKARI: Kwanini Rais anaogopa kutubu?

Au inawezekana alipoambiwa atubu basi anadhani ameambiwa aungame manake huyu jamaa Kiswahili kinampa taabu!

Nasikia kuungama ni kueleza uovu mtu aliofanya mbele ya Padre!

Kama ndivyo, thubutu! Labda afungwe minyororo na kuburuzwa hadi church or else, there's no way anaweza kuwa tayari kumwaga radhi mbele ya Padri hata kama mapadri wanakula kiapo cha kutotoa siri!
 
Hakuna ajuaje kama anakataa kutubu au keshatubu kwa Mungu wake kimyakimya (sio lazima akapige goti kwa Kakobe). So far yupo kimya na hizo kelele zinatoka kwa wachumia tumbo jamii ya Gambooo na Rwega-hasira
Toba yake itapokelewa kwa kwenda kumwomba msamaha Lisu na wazazi wa Saanane. Pia aweke ahadi ya kutomfanyia mtu mwingine yeyeote. Damu ya mtu huhitaji toba maalum. La sivyo huleta laana. La sivyo itakuwa ni kupoteza muda.
 
Akatubu Kwa kosa lipi alilofanya linalohitaji toba?

Akatubie wapi? Kwa Kakobe, Gwajima, mzee upako, Kwa Pengo au wapi?

Je unataka aje atuambie kila anapokutana na Mungu wake Kwa ajili ya maombi yake na toba?

Nadhani Toba ni jambo binafsi sana la kiroho kati ya mtu na Mungu wake na si kati ya mtu na MIUNGU ya watu wengine
Mkatoliki anajua
 
Akatubu Kwa kosa lipi alilofanya linalohitaji toba?

Akatubie wapi? Kwa Kakobe, Gwajima, mzee upako, Kwa Pengo au wapi?

Je unataka aje atuambie kila anapokutana na Mungu wake Kwa ajili ya maombi yake na toba?

Nadhani Toba ni jambo binafsi sana la kiroho kati ya mtu na Mungu wake na si kati ya mtu na MIUNGU ya watu wengine
Yeye ni mkatoliki, anajua namna ya kutubu. Kabla ya kusogelea kiti cha kitubio kwanza anahitajika kuwaomba msamaha wale aliowakosea, kisha ndipo asogelee kiti cha kitubio.

Akamwone Lisu, amwombe msamaha. Ben Saanane, kama hayupo hai, akawaombe msamaha wazazi wake. Makosa mengine ya bahati mbaya, ni yeye na Mungu wake. Hayahitaji toba ya wazi.

Makosa ya jumla kwa Taifa kama kukiuka katiba, anahitajika kuondoa marufuku alizoziweka kabla ya kujongea kwenye sakramenti ya kitubio.
 
Akatubu tu hakuna namba, haiwezekani katiba inaruhusu vyama vingi na mikutano ya siasa yeye anazuia, akatubu tu.
 
Hivi nyie watu mnajuaje kama Magufuli huwa hatubu? Au mnataka akutubu kwa Kakobe mbele ya waumini wake? Fanyeni kazi acheni upumbavu.
 
Biblia haisemi binadamu aende akaombe toba kwa binadamu mwenzake.
Rais hawezi kutubu kwa kakobe wala kwa kadinali Pengo hata kama ana dhambi kiasi gani kwa kuwa wote ni binadamu hivyo hawawezi kumuondolea dhambi.
Toba ya kweli ipo kwa yesu kristo mwana wa Mungu pekee wala si Kakobe. Yeye tu ndiye awezaye kufanya ondoleo la dhambi.
Nina imani kila siku anafanya toba kwa kuwa hakuna binadamu mkamilifu na kila siku tunatenda dhambi either kwa kujua au kutokujua.
Kwahiyo kufanya toba ni jukumu la binadamu wote.
 
Atubu kwa kosa gani???wanaotaka atubu waseme atubu nn ...mda mwingne watz tuachage ujinga inakua ka mtu hajui anataka nini...
 
Nimekumbuka hadith ya "Abdul and the Angel".

Abdul alijenga kibanda chake nje ya mji akisha akawaaminisha watu humo ndani kuna malaika. Lakini malaika huyo huonekana kwa wasio na dhambi tu. Kwa hiyo watu wa huo mji walikuwa wakiingia ili kumuona Malaika na hivyo kupata kujua ikiwa wana dhambi au hawana. Usipomuona means wewe una lundo la dhambi. Can you guess what happened?

Kivumbi ni pale mfalme wao nae alipoambiwa aende kumuona malaika ili wajue ikiwa ana dhambi au hana. Maskini wee, mfalme hodi mpaka kibandani. Asimuone malaika wala kivuli chake.

Unadhani alivyotoka kibandani angesemaje?
 
Wewe ulishatubu?usimuonyeshee mwenzio kidole wakati hakuna mwanadamu aliyemkamilifu
Majanga ya mkulu hayafanani na mleta mada..ukae ukijua hilo sio kilakitu cha kutubu..ila kuna point ukifikia inabidi utubu
 
Atubu kwa kosa gani???wanaotaka atubu waseme atubu nn ...mda mwingne watz tuachage ujinga inakua ka mtu hajui anataka nini...
Mauaji mengi ya yametokea kipindi cha utawala wake

Atubu kwa yale aliyotendewa Lissu na kupotea Ben Saanane.

Atubu kwa kuvunja sheria na katiba za nchi.

Atubu kwa kunyanyasa wapinzani ambao taktibani 400+ wametiwa mbaroni kwa makosa ya kubambikiziwa tu kwenye utawala wake na wengine bado wako mbaroni hawajatoka.

Atubu kwa kutukana Watanzania kila siku
 
Wito umekwishatolewa na viongozi wakubwa wa kidini kumtaka Rais aende akatubu, na mara tu kauli hiyo ilipotolewa wapambe wa Rais walilipuka kwa hasira na hamaki kuipinga kauli hiyo ili kumlinda Rais asitubu. Mpaka sasa Rais hajajitokeza hadharani na kutubu.

Pasipo kuweka uchabiki katika hili, embu tujiulize haya maswali.
1/Kwanini Rais anaogopa kutubu?
2/Kuna kosa kumwambia Rais atubu?
3/Kuna hasara gani kama Rais ataamua kutubu?
4/Nini faida ya Toba kwa nchi ikiwa Rais atatubu kwa makosa yake au makosa ya watendaji wake?
Wewe ulitaka atubu vipi? Rais wako ni mkatoliki na kitubio ni moja ya sacrament zao wakatoliki. Hivyo kutubu kwa wakatoliki ni siri kati ya padre kama mjumbe wa Mungu wake na yeye hivyo hizo kiki zenu za kusubiri mtu aanzishe na ninyi mje mtujazie server ni ujinga. Kuna mambo ya muhimu wananchi wanayahitaji kama walivyoahidi walipopita kujinadi kama milioni 50 kila kijiji. Huu ujumbe wa Kakobe tumeusikia hakuna haja kila mtu kuundia thread.
 
Back
Top Bottom