Tafakari kabla ya kutenda: somo la maisha

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,640
697,940
Hivi ni vifaranga vya ndege vilivyofariki kwa njaa vikiwa ndani ya kiota baada ya kumsubiri kwa muda mama yao awaletee chakula lakini kumbe mama yao alikuwa ameuawa na mtu asiyejua umuhimu wa uhai wake kwa watoto wake na watu wengine wanaomheshimu na kumtegemea.

Mambo ya kujifunza:
1.
Kila unapopigana na mtu, jua unapigana na wategemezi wake pia.

2. Ukiua roho umeua ndoto za watu wengi zaidi.

3. Usiue ndoto ya mtu mwingine kwa sababu tu haukubaliani na mawazo yake.

4. Msaidie aelimike kama wewe ili aone mwanga zaidi, baadae atakushukuru na kukuombea mema.

5. Ukishindwa kumpa mtu manufaa basi usimpe mtihani.

6. Usipoweza kumnusuru basi usimdhuru.

7. Kama huna la kumfurahisha basi usimuhuzunishe.

8. Ukiwa hukubaliani nae basi usimfanyie uadui.

9. Usipofurahia neema zake basi usimuonee wivu.

10. Ukiwa humkubali basi usimuharibie kwa kumfanyia fitna.

11. Ukiwa huna la kumsifu basi usimkejeli.

12. Ukiona amekuzidi maarifa au maisha, basi usimchukie au kumchafua.

13. Usiwe sababu ya watu kuacha ndoto zao.

14. Kila unayemuona mdogo, pamoja na udogo wake naye pia ana watu wanaomtegemea kama wewe.

IMG-20240216-WA0008.jpg
 
Mwaka 1977 Vincent Simmons alihukumiwa kifungo cha miaka 100 jela nchini Marekani baada ya kupatikana na hatia ya jaribio la kuwabaka watoto pacha, Karen na Sharon waliokuwa na miaka 14, wakati huo yeye akiwa na miaka 25.

Simmons alisisitiza kuwa hana hatia. Kufikia mwaka 2022, jaji alibaini kuwa hakuwa na hatia na kuachiwa huru baada ya kutumikia adhabu hiyo kwa miaka 44.
FB_IMG_1708100218363.jpg
 
Hivi ni vifaranga vya ndege vilivyofariki kwa njaa vikiwa ndani ya kiota baada ya kumsubiri kwa muda mama yao awaletee chakula lakini kumbe mama yao alikuwa ameuawa na mtu asiyejua umuhimu wa uhai wake kwa watoto wake na watu wengine wanaomheshimu na kumtegemea.

Mambo ya kujifunza:
1.
Kila unapopigana na mtu, jua unapigana na wategemezi wake pia.

2. Ukiua roho umeua ndoto za watu wengi zaidi.

3. Usiue ndoto ya mtu mwingine kwa sababu tu haukubaliani na mawazo yake.

4. Msaidie aelimike kama wewe ili aone mwanga zaidi, baadae atakushukuru na kukuombea mema.

5. Ukishindwa kumpa mtu manufaa basi usimpe mtihani.

6. Usipoweza kumnusuru basi usimdhuru.

7. Kama huna la kumfurahisha basi usimuhuzunishe.

8. Ukiwa hukubaliani nae basi usimfanyie uadui.

9. Usipofurahia neema zake basi usimuonee wivu.

10. Ukiwa humkubali basi usimuharibie kwa kumfanyia fitna.

11. Ukiwa huna la kumsifu basi usimkejeli.

12. Ukiona amekuzidi maarifa au maisha, basi usimchukie au kumchafua.

13. Usiwe sababu ya watu kuacha ndoto zao.

14. Kila unayemuona mdogo, pamoja na udogo wake naye pia ana watu wanaomtegemea kama wewe.

View attachment 2906065
This just came in time.

Kudos mshana
 
Mwaka 1977 Vincent Simmons alihukumiwa kifungo cha miaka 100 jela nchini Marekani baada ya kupatikana na hatia ya jaribio la kuwabaka watoto pacha, Karen na Sharon waliokuwa na miaka 14, wakati huo yeye akiwa na miaka 25.

Simmons alisisitiza kuwa hana hatia. Kufikia mwaka 2022, jaji alibaini kuwa hakuwa na hatia na kuachiwa huru baada ya kutumikia adhabu hiyo kwa miaka 44.View attachment 2906140
Nita fatilia kesi yake, nione Kama wali mlipa😆
 
Back
Top Bottom