FREEMAN MBOWE APOTEZA MVUTO CHADEMA NA KWA WATANZANIA KWA SASA.
Watanzania wenzangu Freeman Mbowe ni mwanasiasa aliyezaliwa tarehe 14,September mwaka 1961,na ni miongoni mwa waasisi wa Chadema chama kilichoanzishwa mwaka 1992 akiwa kijana kwa wakati huo, alichaguliwa kuongoza kurugenzi ya vijana na mshauri wa usimamizi wa fedha
"Freeman" Mbowe alipewa jina hili kwasababu alizaliwa kipindi ambacho Tanganyika ilipata Uhuru, mke wake anaitwa Liliani Mtei yani mtoto wa muasisi wa Chadema na ndo maana Mzee mtei karidhia Mbowe kuwa mwenyekiti wa Chadema, na kwa utafiti niliyoufanya kuna mkakati wa ndani unaolatibiwa na Mbowe pamoja na mkwe wake kuhakikisha baada ya Mbowe anafuatia mwenyekiti mwingine kutokea katika ukoo huo wa Mtei pamoja na Mbowe kitu kinachoanza kuzua taharuki ndani ya Chadema.
Mwaka 1995 mbowe aligombea Ubunge katika jimbo la Hai nakushindwa vibaya sana kwa asilimia 28.6 kwa wakati huo jimbo liliongozwa na mgombea wa NCCR lakini mbowe alilalamika kuwa ameibiwa kura.
Mwaka 2000 Mbowe aligombea tena ubunge katika jimbo la Hai na kushinda kwa asilimia 64.5 tena mh,mbowe japo alishinda alidai kura zake nyingine aliibiwa na chama Tawala. Mwaka 2004 mbowe alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa Chadema akichukua nafasi iliyoachwa na Mzee Bob makani.
Mwaka 2005 Mbowe alichaguliwa na chama chake kuwa mgombea Urais katika uchaguzi mkuu uliyopangwa kufanyika tarehe 30 October mwaka 2005 na mgombea mwenza alikuwa Jumbe Rajab Jumbe lakini kwa baati mbaya huyo mgombea mwenza alifariki Dunia na Tume aliamua kupanga tarehe 14december mwaka 2005 kuwa ndo siku ya uchaguzi mkuu lakini katika uchaguzi huu Mbowe alikuwa mshindi wa tatu kwa asilimia 5.88 cha ajabu Mbowe alisikika akisema ameibiwa kura na kama kawaida yake kuibiwa kura ni kama wimbo wake, lakini hakuwambia wafuasi wake je na professor Lipumba aliyepata asilimia 11 na kuwa wa pili nae alimuibia?
Mwaka 2010 Mbowe alichaguliwa kuwa mbunge wa Hai kwa asilimia 51.63 kwa wakati huu aliogopa kugombea Urais maana alikuwa amepoteza mvuto maana kama mtu jimboni kwake anapata asilimia 51.63 hakika kwenye Uraisi kwa Wakati huu angeweza kupata asilimia 0.008 lakini bado alidai kuibiwa kura zake.
Miongoni mwa vitu vingine vinavyopelekea Mbowe achokwe na wanachama wake pamoja na wananchi ni zifuatazo;
1, kufanya maamuzi ambayo hayatekelezeki na yasioleta mafanikio, mfano mnamo tarehe 13 mwezi wa nane mwaka 2006 Chadema walifanya uzinduzi wa kampeni mpya ya kuhakikisha wanashinda uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 na Mbowe aliwakikishia wananchi kuwa atahakikisha chadema wanaingia Ikulu mwaka 2010, ni hii ni mwaka mmoja baada ya mbowe kushindwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2005. Na mkutano huu ulifanyika katika ukumbi wa PTA Dar es salam,kampeni hii ilipewa jina la TUMAINI JIPYA cha ajabu wanachama na wananchi wanajiuliza mbona mwaka 2010 uchaguzi uliisha wala Chadema hatukushinda na mbowe hakutoa mlejesho kwa wananchi na kamati kuu yao ispokuwa aliendelea na wimbo wake wa kuibiwa kura na huu ni mzimu unaotafuna Chadema kuwa mazuzu wakudanganywa kila siku na wao wanafuata.
2, Mbowe ni mhoga na mtu anayependa kutanguliza watu wengine ili waumie yeye akiwa salama, mfano mwaka 2010 mbowe alitangaza maandamano makubwa pale Arusha lakini baadae wakiwa wanaandamana yeye alikimbia na kumuacha Dr.slaa na mkewe wakipigwa vibaya baada ya kukaidi amri ya polisi sisi wana chama wa Chadema sasa tumeshutuka hatutakubali tutangulizwe bila yeye kuwepo, hayo ni maneno ya mtoa taarifa wangu na kiongozi mkubwa wa Chadema.
3, katika vikao vya Chama Mbowe ni dikiteta asiyezingatia akidi ili kufanya maamuzi, mfano mwaka 2010 kamati kuu ya Chadema ilifukuza madiwani watano wa wilayani Arusha ambao ni, Estomih mallah,John Bayo, Charles Mpanda, Rehema mohamedi na Reuben Ngowi lakini taarifa za ndani za kamati kuu zinadai, kamati kuu ilikataa wasifukuzwe lakini yeye alipotoka nje katangaza kuwavua madaraka hawa madiwani kitu ambacho kinalalamikiwa mpaka leo ndani ya chama.
4,Mbowe ni kigeugeu na mtu asiyeshaurika, mnamo Sunday, September 14,2014 katika ukumbi wa mlimani city Mbowe alitangaza maandamano yasiokuwa na kikomo nchi nzima mara baada ya kuchaguliwa na kuwa mwenyekiti wao kwa kura 789 huku mpinzani wake akipata kura 20 ambae ni Gambaranyere Mwangateka, taarifa za ndani zinasema Mbowe alikurupuka kutoa kauli hiyo maana haikujadiliwa sehemu yeyote ile, kibaya zaidi baada ya Mbowe kuona hali ni mbaya kakimbia kwenda Afrika kusini huku kaacha wafuasi wake hawajui chochote na hii kupelekea maandamano hayo kufeli.
Mwezi July mwaka 2016 mbowe alitangaza maandamano makubwa nchi nzima yatakayo anza tarehe moja lakini inasemekana Mbowe hakupata baraka za kamati kuu isipokuwa yeye kalazimisha.m
Na sasa baada ya kuona hali ni mbaya habari za kina na za kuaminika zinasema tena mh,mbowe kapanga safari ya ghafula kwenda Ujerumani tarehe 28 augost mwaka huu yani siku nne kabla ya siku ambayo maandamano yamepangwa na hii ni hatari kwa vijana wenzangu tusikubali kuingia barabarani wakati mbowe akiwa Ulaya anakula kiyoyozi.
Mwisho nawashauri wanachadema hususani wabunge wasiomkubali na viongongozi wanaopinga maamuzi yake wampinge hadharani kama walivyonipa ushirikiano kupata taarifa hizi za ndani kuhusu Mbowe.
Imeandaliwa na
Comrade,
Mwita Nyarukururu
mwitanyarukururu@gmail.com