Kweli kabisaaaKwa ufupi tu MWANAMKE ni mbinafsi sana... Hivyo yahitaji akili sana, busara, hekima na ubabe kidogo ili uishi nao vyema... la sivyo... Ni maumivu
Sent using Jamii Forums mobile app
Ukitaka raha ya uzee ni kweli unapaswa kujiandaa kipindi cha ujana,
Na wengi wetu huwa tunakosea sana wakati wa kuoa tu!
Ila ukitaka raha ya uzee, usikubali kutofautiana sana na mwanamke angalau mpishane miaka miwili au mitatu uzee wako utafaidi sana!
Lakini unakuta mwanaume una miaka 35 unaoa binti wa miaka 25 au 23 hapo jua tu utapata tabu sana!
Mama ni mama!!Imenitoa gizani huwa namjali sana mama kuliko baba! Nimetambua makosa yangu nitajirekebisha kuanzia leo
Sent using Jamii Forums mobile app
Huto msikia utaona matendo,mm n mja wa watu ambao hua namsikiliza mama na baba kwa tahadhari sana na hua natoa chochote kwa kupima situation,nyimbo za kusema nani Kama mama sijawahi zielewasiku mtoto wangu nikimsikia anasema anampenda mama kuliko baba, aise hakuna rangi ataacha kuiona.
Pamoja na huu ushauri mzuri nimemwelewa mtoa mada but pia itategemeana na akili ya mtu,watoto wa kike ni rahisi sana kulishwa sumu na mama kuliko wanaume but tatizo la wanaume ni kuegemea familia zaoKwanza kabisa niombe radhi kwa kuingia uwanja huu pasipo ruksa ya mtoa uzi.
********************************************
Matokeo ya leo ni maamuzi mliyoyaishi wazazi tangu mwanzo wa kuiunda NDOA yenu.
Tusipandikize sumu kwa baba watarajiwa waamini hiki kilichowasilishwa hapa na pindi waingiapo katika ndoa waishi maisha yaliyojaa hofu (NDOA haitakuwa yenye furaha kamwe).
Siku zote malezi ya watoto hujengwa katika msingi ulio bora baina ya wazazi wote wawili (Baba na mama).
Watoto wakilelewa katika familia zenye mahusiano mazuri, majibizano yenye kuheshimiana, na kauli zisizokatisha tamaa ni dhahiri watoto pia watajengewa hulka ya kuwaheshimu na kuwathamini wazazi wao pasipo kuwa na chembe chembe za ubaguzi.
Vilevile kutokana na msingi bora waliojiwekea kama familia mama pia hatakuwa na chembe chembe za roho mbaya, visasi + kumsiliba mumewe kwa uozo wa aina yoyote. Nao watadumu katka UPENDO uliotukuka na mwisho wa siku kuzeeka pamoja pasipo kuumizana hisia wala kuleteana maradhi yatokanayo na msongo wa mawazo.
Mara nyingi baba zetu wamekuwa wakifikiri malezi ya watoto huegemea zaidi kwa mama kuliko baba (Tukumbuke malezi si kula, kunywa, kulala na kuvaa pekee). Wanaume walio wengi wamejijengea kasumba ya kuhakikisha tu anatoa pesa ya kukidhi mahitaji ya familia, na pesa hii mara zote hupitia kwa mama.
Tatizo huanza pale mama atakapokuwa na roho ya choyo, ubinafsi, upendo wa kinafiki ndipo darasa la kuwapandikiza watoto wake tabia alizonazo litakapoanza.
Watoto nao wataamini maneno ya mama yao kwani mara zote mama ndo huwa rafiki wa karibu sana kuliko baba. Hali hii itapelekea matatizo yote wayaelekeze kwa mama, mama nae kutokana na kukosa msingi mzuri wa familia hushindwa kumshirikisha baba.
Mwisho wa siku watoto humuona mama ndo kila kitu katka maisha yao, na hata watakapofanikiwa bado mama atakuwa rafiki wa karibu sana kuliko baba yao, hii hupelekea mama kula hadi vilivyofichwa uvunguni wakati huo baba akiambulia tabasamu pekee kutoka kwa wanawe.
Sent using Jamii Forums mobile app
Unakosea wanawake ni watu wenye ego na wabinafsi,wafitini sana nimekuja kujua ukubwaniImenitoa gizani huwa namjali sana mama kuliko baba! Nimetambua makosa yangu nitajirekebisha kuanzia leo
Sent using Jamii Forums mobile app
Mtetezi wa wanawake JF!!Kwanza kabisa niombe radhi kwa kuingia uwanja huu pasipo ruksa ya mtoa uzi.
********************************************
Matokeo ya leo ni maamuzi mliyoyaishi wazazi tangu mwanzo wa kuiunda NDOA yenu.
Tusipandikize sumu kwa baba watarajiwa waamini hiki kilichowasilishwa hapa na pindi waingiapo katika ndoa waishi maisha yaliyojaa hofu (NDOA haitakuwa yenye furaha kamwe).
Siku zote malezi ya watoto hujengwa katika msingi ulio bora baina ya wazazi wote wawili (Baba na mama).
Mwisho wa siku watoto humuona mama ndo kila kitu katka maisha yao, na hata watakapofanikiwa bado mama atakuwa rafiki wa karibu sana kuliko baba yao, hii hupelekea mama kula hadi vilivyofichwa uvunguni wakati huo baba akiambulia tabasamu pekee kutoka kwa wanawe.
Sent using Jamii Forums mobile app