Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,639
SEHEMU YA KWANZA
Hali ya hewa ilikuwa tulivu ingawa kulikuwa na kijua kilichochoma kwa mbali na kufanya hali ya Mwanza iwe na joto kiasi.
Anne alisimama kizimbani mbele ya jaji wa Mahakama ya Rufaa Raphael Mpoki, siku hiyo ya Januari 21, 1998 ilikuwa siku ya hukumu yake na wengi wa watu waliohudhuria mahakamani walitegemea kwa kosa alilolifanya Anne ni lazima angenyongwa.
Miongoni mwa watu waliokuwepo makahamani walikuwa watoto wake wawili, wa kike Nancy na wa kiume aliyetwa Patrick, walikuwa watoto wazuri tena mapacha na siku tano kabla ya siku hiyo walitimiza miaka kumi na mbili lakini miaka waliyoishi na mama yao katika maisha ilikuwa ni miwili tu!
Patrick na Nancy walikosa mapenzi ya mama yao na si mama tu bali pia baba yao aliyefariki dunia katika mazingira ya kutatanisha wakiwa na umri wa mwaka mmoja, yeye hawakumwona kabisa zaidi ya kuiona sura yake katika picha.
Mpaka siku hiyo Anne alikuwa amekaa mahabusu kwa takribani miaka kumi na siku thelathini na saba kamili na aliwaacha watoto wake wakiwa na miaka miwili tu! Patrick na Nancy walikuwa kama watoto wa yatima wakilelewa na mama yao mdogo, Suzanne.
Walimhurumia sana mama yao kwa sababu alikuwa amekondeana sana alivaa nguo chafu na mwili wake ulijaa vipele na ukurutu lakini pamoja na hali hiyo ya uchafu bado alionekana ni mwanamke mwenye sura nzuri na sura yake ilifanana sana na ya mtoto wake wa kike Nancy!
Tofauti pekee kati yao ilikuwa ni rangi ya ngozi zao, Nancy alikuwa mweupe zaidi ya mama yake kwa sababu baba yake Huggins alikuwa Mmarekani mweusi mwenye mchanganyiko wa damu ya kizungu ila mama yake ndiye alikuwa raia wa Sierra Leone aliyehamia Marekani miaka mingi kabla.
Anne alipowaangalia watoto wake wawili waliokuwa wamekaa miguuni kwa mama yao mdogo akiwa amewakumbatia, alilia machozi alisikia uchungu moyoni mwake kufahamu kuwa ni siku hiyo ndiyo ilikuwa ya mwisho kwake kuwaona watoto wake!
“Patrick and Nancy today I’m dying for you!”(Patrick na Nancy leo nakufa kwa ajili yenu!)
“No! Mom don’t die! Please mom we need you mom dont go!”(Hapana mama usife, tafadhali bado tunakuhitaji sana usituache) mtoto mdogo Patrick alipiga kelele mahakamani na kuchomoka mikononi kwa mama yake mdogo na kukimbia akimfuata mama yake.
Kabla hajakifikia kizimba alishikwa mkono na askari na kuanza kuvutwa akirudishwa mahali alipokaa mama yake mdogo. Mawakili waliokuwa wakiendelea na mabishano ya kisheria ndani ya mahakama na hata jaji mwenyewe walikerwa sana na kelele za mtoto Patrick aliyekuwa akilia, ikabidi hakimu aagize Patrick na Nancy pamoja na mama yao mdogo watolewe nje ya mahakama haraka ili kuruhusu mahakama iendelee na kazi yake!
“Hatutaki! Hatutaki! Hatutaki! Tuachieni tumwone mama yetu mara ya mwisho!”Patrick na Nancy walilia wakati askari akiwavuta kuwatoa nje ya mahakama.
****
Hali ilipotulia mahakama iliendelea na kazi yake kama kawaida.
“Mheshimiwa Jaji siamini hata kidogo kuwa mshtakiwa alimuua mama yake kwa sababu marehemu alikutwa nje ya nyumba yake iliyo umbali wa mita elfu moja kutoka nyumbani kwa mshtakiwa, akiwa amechomwa visu, kimoja shingoni na kingine kwenye titi la kushoto. Mheshimiwa jaji kufanyika kwa kitendo hicho haimaanishi kuwa mshtakiwa ndiye aliyefanya na hakuna ushahidi wa kutosha kulithibitisha jambo hilo uliokwishatolewa mbele ya mahakama yako tukufu!”
Mahakama ilikuwa kimya ikimsikiliza wakili Lydia Ishegoma aliyekuwa akimtetea Anne mahakamani, alikuwa ameifanya kazi hiyo kwa miaka kumi na siku hiyo ndiyo ilikuwa siku ya mwisho! Aliamua kumtetea Anne kwa sababu walisoma wote na aliyefanyiwa na mama yake mzazi yalimsikitisha sana kiasi cha kusema hata yeye asingeweza kuvumilia.
“Mheshimiwa Jaji mtu yeyote angeweza kufanya hivyo na kisha kuutupa mwili wa marehemu nje ya nyumba yake na isitoshe visu vyote vilipopimwa na wataalam wa vidole haikuonyesha alama za vidole vya aina yoyote! Jambo linalonifanya niamini muuaji alikuwa mtaalam wa kazi hiyo kuliko anavyoonekana mshtakiwa! Hivyo naiomba mahakama yako tukufu imwachie mshtakiwa huru kwa sababu ameteseka kwa muda mrefu na ni mama wa watoto wawili ambao baba yao alikufa miaka mingi!” Alimaliza wakili Lydia kutoka chama cha mawakili wanawake nchini Tanzania.
Maneno ya wakili Lydia yalionekana kumwingia jaji akilini na ndani ya moyo wake, alijikuta akiingiwa na huruma kwa sababu alishaisikia historia ya jambo lililopelekea Anne kumuua mama yake mzazi!
Alitaka sana kumwachia Anne huru lakini alishindwa atumie kifungu gani cha sheria wakati ushahidi uliokwishatolewa mahakamani uliyoonyesha wazi kuwa Anne ndiye alimuua mama yake.
Huku moyo wake ukiwa umejaa huzuni Jaji Raphael aliigonga meza iliyokuwa mbele yake kuashiria kuwa mahakama ilikuwa inapumzika kwa muda wa dakika tano na alitoka mahakamani kupitia mlango wa nyuma na alikwenda moja kwa moja hadi ofisini kwake ambako aliendelea kuwaza mambo mengi juu ya Anne.
Watu wote ndani ya mahakama baada ya Jaji kuondoka waliendelea na minong’ono kimya kimya wakimwongelea Anne aliyekuwa ndani ya kizimba akilia! Kilichomfanya Anne alie si kingine bali ni watoto wake.
“Bila Patrick na Nancy wala nisingejali kifo changu kwani kufa ni kulala! Aliwaza Isabella.
****
Mwili wake wote ulinuka na alihisi nguo zake kulowana! Inzi wengi walimzunguka na aliwapiga kwa mkono wake kuwafukuza. Anne alijua ni kitu gani kilichokuwa kimetokea, kwani mwaka mmoja kabla ya kutiwa mahabusu alipatwa na ugonjwa wa ajabu, ugonjwa uliomtesa na kumpa fedheha kubwa katika jamii iliyomzunguka, ni ugonjwa huo ndio uliomfanya mumewe na baba wa watoto wake Huggins William kijana wa kimarekani kumwacha na kuanza kuishi na mwanamke mwingine aliyeitwa Delilla.
Ni mwanamke huyo ndiye aliyempa sumu Huggins, mwanaume ambaye Anne alimpenda na kumuua! Mpaka siku hiyo ya hukumu bado Anne aliamini bila kupatwa na ugonjwa huo, Huggins asingemkimbia kwenda kwa Delilla na asingekufa.
“Mimi naona nilichomfanyia mama ni sawa tu! Kwani alichonifanyia yeye mimi yaani niwe namiminika hedhi kila siku kwa miaka kumi! Mama alistahili kifo na kama kuna maisha baada ya kunyongwa kwangu huko ahera ninakokwenda ni lazima nimuue tena! Alinifanyia ubaya mkubwa mno na ninashangaa kwanini Jaji hanihukumu ili nife, acha nihukumiwe nife niende zangu, nina thamani gani hapa duniani mie ni bora kifo!”Aliendelea kwanza Anne.
****
Dakika tano baadaye Jaji alirejea tena mahakamani na mahakama iliendelea.
“Anne!” Jaji aliita kwa huruma lakini Anne alikaa kimya bila kujibu kitu, watu mahakamani walishangaa kuona jaji Raphael Mpoki akiongea kwa upole kiasi kile siku hiyo kwani alikuwa ni jaji aliyeaminika kuwa mkali kupita majaji wote nchini Tanzania.
“Anne!”Jaji aliita tena safari hii akitabasamu, watu wote wakajua ushindi ulikuwa ni wa Anne.
“Naa..m mhe…shimi…wa!” alijibu Anne huku akilia.
“Usilie binti tafadhali niambie kwanini nisikuhukumu kifo kwa mauaji ya kikatili uliyoyafanya kwa mama yako kwa sababu kila aina ya ushahidi kuwa ulifanya tendo hilo!”Jaji alimwambia Anne huku akimwangalia kwa huruma!
Watu wote mahakamani walikaa kimya wakisubiri jibu la Anne, hata watoto wake ambao tayari walisharudishwa ndani ya mahakama pia walikuwa wakisubiri jibu la mama yao, walitaka dunia ibadilike na mama yao asihukumiwe kifo wala kifungo cha maisha, walitaka aachiwe huru ili waonje na kufaidi upendo wa mama! Walikuwa wemechoka kujisikia yatima na kushinda kutwa nzima wakiangalia picha za mama na baba yao!
Anne alijaribu kufungua mdomo ili aongee kitu lakini maneno hayakutoka kwa sababu ya kwikwi iliyokuwa imekaba kooni!
“Sema Anne, sema usiogope ongea na mimi unataka nikufanye nini maisha yako yapo mikononi mwangu?” Alisema jaji Raphael Mpoki lengo lake likiwa ni kumshawishi Anne aombe kuachiwa huru ni hicho tu alichokuwa akisubiri ili amuachie aende zake.
“Mhesh..imi...wa Ja..ji!” Anne alijikaza na kujikuta akiongea ingawa kwa shida na watu wote walikaa kimya kumsikiliza.
“Ndiyo nastahili kifo na ninaomba unihukumu kifo, ninaomba unihukumu kunyongwa lakini kabla sijafa naomba niseme maneno yafuatayo kwa watu waliopo hapa mahakamani! Ndugu zangu ni wengi wananyongwa na ni wengi wameua lakini hawakutakiwa kufanya hivyo , mimi si muuaji ila nililazimika kuua kwa sababu sikuwa na njia yoyote ya kuwalinda watoto wangu, kwa sababu mama yangu aliyenizaa mimi na kunileta duniani alitaka kuwaua wanangu ingawa tayari alikwishawaua watoto wangu wengine wawili, William na Henry!”
Mahakama ilikuwa kimya watu wote wakisikiliza kwa makini maneno ya Anne aliyoyaongea huku akilia.
“Nilipokataa kumpa watoto wangu akaniroga na kunipa ugonjwa wa kupata hedhi kila siku na hivi mnavyoniona hapa niliposimama nguo zangu zote zimeloa na nimekuwa katika hali hii kwa muda wa miaka kumi na moja! Macho yangu ni meupe kwa sababu nimepoteza damu nyingi na sili chakula kizuri gerezani! Na yote haya alinifanyia mama yangu mwenyewe ambaye bila yeye mimi nisingeifahamu dunia, mlitegemea nifanye nini wakati alitaka kuniulia watoto wangu Patrick na Nancy? Ni yeye aliyesababisha kifo cha mume wangu na kuniharibia maisha yangu kwa kweli ilibidi nimuue mama yangu ili kuokoa maisha ya watoto wangu NA SINA LA KUFANYA MHESHIMIWA JAJI NAOMBA UNIHUKUMU KIFO ILI NINYONGWE NIMFUATE MAMA HUKO ALIKO NA NIKIMKUTA NI LAZIMA NIMUUE TENA KWA SABABU AMENITESA SANA NA MARA KWA MARA NAJIULIZA NI KWANINI ALINIZAA!”
Maneno hayo ya Anne yalimfanya wakili wake aliyejua siku hiyo ushindi ulikuwa wao apigwe na butwaa na kujikuta akiziba mdomo wake kwa mikono yake yote miwili, kwa utetezi aliokuwa ametoa alifahamu wazi Anne angeachiwa huru lakini maneno aliyoyatoa Anne pale mahakamani yalimfanya wakili wake atokwe na machozi!
“ANNE WHAAAAT!”(Anne nini?) wakili wa Anne ajikuta akipiga kelele.
“Sorry Lydia I want to die! I’m very sorry for wasting your ten years time trying to defend me in court but God will pay you for me!”(Samahani Lydia nataka kufa, nasikitika kwa kukupotezea muda wako wa miaka kumi ukijaribu kunitetea mahakamani lakini Mungu atakulipia!)
Kwa historia aliyoitoa Anne watu wote mahakamani walijikuta wakimwanga machozi kumlilia Anne, maneno yake yaliwachoma watu wengi, waligundua alifanyiwa unyama mkubwa ambao binadamu yeyote mwenye akili ya kawaida asingeweza kuuvumilia, hata jaji Mpoki pia alikuwa akijifuta machozi kwa sababu ya kulia, maaskari pia walishindwa kuvumilia na kujikuta wakitokwa na machozi.
“Nimesikitishwa sana na historia aliyoitoa na sina la kufanya zaidi ya …………….!” Jaji Raphael Mpoki alijikuta akishindwa kuvumilia na kuangua kilio mbele ya watu wengi waliokuwa mahakamani, watoto wa Anne na mama yao mdogo pia waliendelea kulia machozi, mahakama nzima ilijaa vilio na maaskari walijaribu kunyamazisha mahakama bila mafanikio.
Je nini kitaendelea?
Je Anne atahukumiwa kifungo cha gerezani au atanyongwa?
Je nini kilitokea katika maisha ya mwanamke huyu?
Kuna mambo mengi ya kusisimua, tukutane baadae saa 7 kamili usiku
Hali ya hewa ilikuwa tulivu ingawa kulikuwa na kijua kilichochoma kwa mbali na kufanya hali ya Mwanza iwe na joto kiasi.
Anne alisimama kizimbani mbele ya jaji wa Mahakama ya Rufaa Raphael Mpoki, siku hiyo ya Januari 21, 1998 ilikuwa siku ya hukumu yake na wengi wa watu waliohudhuria mahakamani walitegemea kwa kosa alilolifanya Anne ni lazima angenyongwa.
Miongoni mwa watu waliokuwepo makahamani walikuwa watoto wake wawili, wa kike Nancy na wa kiume aliyetwa Patrick, walikuwa watoto wazuri tena mapacha na siku tano kabla ya siku hiyo walitimiza miaka kumi na mbili lakini miaka waliyoishi na mama yao katika maisha ilikuwa ni miwili tu!
Patrick na Nancy walikosa mapenzi ya mama yao na si mama tu bali pia baba yao aliyefariki dunia katika mazingira ya kutatanisha wakiwa na umri wa mwaka mmoja, yeye hawakumwona kabisa zaidi ya kuiona sura yake katika picha.
Mpaka siku hiyo Anne alikuwa amekaa mahabusu kwa takribani miaka kumi na siku thelathini na saba kamili na aliwaacha watoto wake wakiwa na miaka miwili tu! Patrick na Nancy walikuwa kama watoto wa yatima wakilelewa na mama yao mdogo, Suzanne.
Walimhurumia sana mama yao kwa sababu alikuwa amekondeana sana alivaa nguo chafu na mwili wake ulijaa vipele na ukurutu lakini pamoja na hali hiyo ya uchafu bado alionekana ni mwanamke mwenye sura nzuri na sura yake ilifanana sana na ya mtoto wake wa kike Nancy!
Tofauti pekee kati yao ilikuwa ni rangi ya ngozi zao, Nancy alikuwa mweupe zaidi ya mama yake kwa sababu baba yake Huggins alikuwa Mmarekani mweusi mwenye mchanganyiko wa damu ya kizungu ila mama yake ndiye alikuwa raia wa Sierra Leone aliyehamia Marekani miaka mingi kabla.
Anne alipowaangalia watoto wake wawili waliokuwa wamekaa miguuni kwa mama yao mdogo akiwa amewakumbatia, alilia machozi alisikia uchungu moyoni mwake kufahamu kuwa ni siku hiyo ndiyo ilikuwa ya mwisho kwake kuwaona watoto wake!
“Patrick and Nancy today I’m dying for you!”(Patrick na Nancy leo nakufa kwa ajili yenu!)
“No! Mom don’t die! Please mom we need you mom dont go!”(Hapana mama usife, tafadhali bado tunakuhitaji sana usituache) mtoto mdogo Patrick alipiga kelele mahakamani na kuchomoka mikononi kwa mama yake mdogo na kukimbia akimfuata mama yake.
Kabla hajakifikia kizimba alishikwa mkono na askari na kuanza kuvutwa akirudishwa mahali alipokaa mama yake mdogo. Mawakili waliokuwa wakiendelea na mabishano ya kisheria ndani ya mahakama na hata jaji mwenyewe walikerwa sana na kelele za mtoto Patrick aliyekuwa akilia, ikabidi hakimu aagize Patrick na Nancy pamoja na mama yao mdogo watolewe nje ya mahakama haraka ili kuruhusu mahakama iendelee na kazi yake!
“Hatutaki! Hatutaki! Hatutaki! Tuachieni tumwone mama yetu mara ya mwisho!”Patrick na Nancy walilia wakati askari akiwavuta kuwatoa nje ya mahakama.
****
Hali ilipotulia mahakama iliendelea na kazi yake kama kawaida.
“Mheshimiwa Jaji siamini hata kidogo kuwa mshtakiwa alimuua mama yake kwa sababu marehemu alikutwa nje ya nyumba yake iliyo umbali wa mita elfu moja kutoka nyumbani kwa mshtakiwa, akiwa amechomwa visu, kimoja shingoni na kingine kwenye titi la kushoto. Mheshimiwa jaji kufanyika kwa kitendo hicho haimaanishi kuwa mshtakiwa ndiye aliyefanya na hakuna ushahidi wa kutosha kulithibitisha jambo hilo uliokwishatolewa mbele ya mahakama yako tukufu!”
Mahakama ilikuwa kimya ikimsikiliza wakili Lydia Ishegoma aliyekuwa akimtetea Anne mahakamani, alikuwa ameifanya kazi hiyo kwa miaka kumi na siku hiyo ndiyo ilikuwa siku ya mwisho! Aliamua kumtetea Anne kwa sababu walisoma wote na aliyefanyiwa na mama yake mzazi yalimsikitisha sana kiasi cha kusema hata yeye asingeweza kuvumilia.
“Mheshimiwa Jaji mtu yeyote angeweza kufanya hivyo na kisha kuutupa mwili wa marehemu nje ya nyumba yake na isitoshe visu vyote vilipopimwa na wataalam wa vidole haikuonyesha alama za vidole vya aina yoyote! Jambo linalonifanya niamini muuaji alikuwa mtaalam wa kazi hiyo kuliko anavyoonekana mshtakiwa! Hivyo naiomba mahakama yako tukufu imwachie mshtakiwa huru kwa sababu ameteseka kwa muda mrefu na ni mama wa watoto wawili ambao baba yao alikufa miaka mingi!” Alimaliza wakili Lydia kutoka chama cha mawakili wanawake nchini Tanzania.
Maneno ya wakili Lydia yalionekana kumwingia jaji akilini na ndani ya moyo wake, alijikuta akiingiwa na huruma kwa sababu alishaisikia historia ya jambo lililopelekea Anne kumuua mama yake mzazi!
Alitaka sana kumwachia Anne huru lakini alishindwa atumie kifungu gani cha sheria wakati ushahidi uliokwishatolewa mahakamani uliyoonyesha wazi kuwa Anne ndiye alimuua mama yake.
Huku moyo wake ukiwa umejaa huzuni Jaji Raphael aliigonga meza iliyokuwa mbele yake kuashiria kuwa mahakama ilikuwa inapumzika kwa muda wa dakika tano na alitoka mahakamani kupitia mlango wa nyuma na alikwenda moja kwa moja hadi ofisini kwake ambako aliendelea kuwaza mambo mengi juu ya Anne.
Watu wote ndani ya mahakama baada ya Jaji kuondoka waliendelea na minong’ono kimya kimya wakimwongelea Anne aliyekuwa ndani ya kizimba akilia! Kilichomfanya Anne alie si kingine bali ni watoto wake.
“Bila Patrick na Nancy wala nisingejali kifo changu kwani kufa ni kulala! Aliwaza Isabella.
****
Mwili wake wote ulinuka na alihisi nguo zake kulowana! Inzi wengi walimzunguka na aliwapiga kwa mkono wake kuwafukuza. Anne alijua ni kitu gani kilichokuwa kimetokea, kwani mwaka mmoja kabla ya kutiwa mahabusu alipatwa na ugonjwa wa ajabu, ugonjwa uliomtesa na kumpa fedheha kubwa katika jamii iliyomzunguka, ni ugonjwa huo ndio uliomfanya mumewe na baba wa watoto wake Huggins William kijana wa kimarekani kumwacha na kuanza kuishi na mwanamke mwingine aliyeitwa Delilla.
Ni mwanamke huyo ndiye aliyempa sumu Huggins, mwanaume ambaye Anne alimpenda na kumuua! Mpaka siku hiyo ya hukumu bado Anne aliamini bila kupatwa na ugonjwa huo, Huggins asingemkimbia kwenda kwa Delilla na asingekufa.
“Mimi naona nilichomfanyia mama ni sawa tu! Kwani alichonifanyia yeye mimi yaani niwe namiminika hedhi kila siku kwa miaka kumi! Mama alistahili kifo na kama kuna maisha baada ya kunyongwa kwangu huko ahera ninakokwenda ni lazima nimuue tena! Alinifanyia ubaya mkubwa mno na ninashangaa kwanini Jaji hanihukumu ili nife, acha nihukumiwe nife niende zangu, nina thamani gani hapa duniani mie ni bora kifo!”Aliendelea kwanza Anne.
****
Dakika tano baadaye Jaji alirejea tena mahakamani na mahakama iliendelea.
“Anne!” Jaji aliita kwa huruma lakini Anne alikaa kimya bila kujibu kitu, watu mahakamani walishangaa kuona jaji Raphael Mpoki akiongea kwa upole kiasi kile siku hiyo kwani alikuwa ni jaji aliyeaminika kuwa mkali kupita majaji wote nchini Tanzania.
“Anne!”Jaji aliita tena safari hii akitabasamu, watu wote wakajua ushindi ulikuwa ni wa Anne.
“Naa..m mhe…shimi…wa!” alijibu Anne huku akilia.
“Usilie binti tafadhali niambie kwanini nisikuhukumu kifo kwa mauaji ya kikatili uliyoyafanya kwa mama yako kwa sababu kila aina ya ushahidi kuwa ulifanya tendo hilo!”Jaji alimwambia Anne huku akimwangalia kwa huruma!
Watu wote mahakamani walikaa kimya wakisubiri jibu la Anne, hata watoto wake ambao tayari walisharudishwa ndani ya mahakama pia walikuwa wakisubiri jibu la mama yao, walitaka dunia ibadilike na mama yao asihukumiwe kifo wala kifungo cha maisha, walitaka aachiwe huru ili waonje na kufaidi upendo wa mama! Walikuwa wemechoka kujisikia yatima na kushinda kutwa nzima wakiangalia picha za mama na baba yao!
Anne alijaribu kufungua mdomo ili aongee kitu lakini maneno hayakutoka kwa sababu ya kwikwi iliyokuwa imekaba kooni!
“Sema Anne, sema usiogope ongea na mimi unataka nikufanye nini maisha yako yapo mikononi mwangu?” Alisema jaji Raphael Mpoki lengo lake likiwa ni kumshawishi Anne aombe kuachiwa huru ni hicho tu alichokuwa akisubiri ili amuachie aende zake.
“Mhesh..imi...wa Ja..ji!” Anne alijikaza na kujikuta akiongea ingawa kwa shida na watu wote walikaa kimya kumsikiliza.
“Ndiyo nastahili kifo na ninaomba unihukumu kifo, ninaomba unihukumu kunyongwa lakini kabla sijafa naomba niseme maneno yafuatayo kwa watu waliopo hapa mahakamani! Ndugu zangu ni wengi wananyongwa na ni wengi wameua lakini hawakutakiwa kufanya hivyo , mimi si muuaji ila nililazimika kuua kwa sababu sikuwa na njia yoyote ya kuwalinda watoto wangu, kwa sababu mama yangu aliyenizaa mimi na kunileta duniani alitaka kuwaua wanangu ingawa tayari alikwishawaua watoto wangu wengine wawili, William na Henry!”
Mahakama ilikuwa kimya watu wote wakisikiliza kwa makini maneno ya Anne aliyoyaongea huku akilia.
“Nilipokataa kumpa watoto wangu akaniroga na kunipa ugonjwa wa kupata hedhi kila siku na hivi mnavyoniona hapa niliposimama nguo zangu zote zimeloa na nimekuwa katika hali hii kwa muda wa miaka kumi na moja! Macho yangu ni meupe kwa sababu nimepoteza damu nyingi na sili chakula kizuri gerezani! Na yote haya alinifanyia mama yangu mwenyewe ambaye bila yeye mimi nisingeifahamu dunia, mlitegemea nifanye nini wakati alitaka kuniulia watoto wangu Patrick na Nancy? Ni yeye aliyesababisha kifo cha mume wangu na kuniharibia maisha yangu kwa kweli ilibidi nimuue mama yangu ili kuokoa maisha ya watoto wangu NA SINA LA KUFANYA MHESHIMIWA JAJI NAOMBA UNIHUKUMU KIFO ILI NINYONGWE NIMFUATE MAMA HUKO ALIKO NA NIKIMKUTA NI LAZIMA NIMUUE TENA KWA SABABU AMENITESA SANA NA MARA KWA MARA NAJIULIZA NI KWANINI ALINIZAA!”
Maneno hayo ya Anne yalimfanya wakili wake aliyejua siku hiyo ushindi ulikuwa wao apigwe na butwaa na kujikuta akiziba mdomo wake kwa mikono yake yote miwili, kwa utetezi aliokuwa ametoa alifahamu wazi Anne angeachiwa huru lakini maneno aliyoyatoa Anne pale mahakamani yalimfanya wakili wake atokwe na machozi!
“ANNE WHAAAAT!”(Anne nini?) wakili wa Anne ajikuta akipiga kelele.
“Sorry Lydia I want to die! I’m very sorry for wasting your ten years time trying to defend me in court but God will pay you for me!”(Samahani Lydia nataka kufa, nasikitika kwa kukupotezea muda wako wa miaka kumi ukijaribu kunitetea mahakamani lakini Mungu atakulipia!)
Kwa historia aliyoitoa Anne watu wote mahakamani walijikuta wakimwanga machozi kumlilia Anne, maneno yake yaliwachoma watu wengi, waligundua alifanyiwa unyama mkubwa ambao binadamu yeyote mwenye akili ya kawaida asingeweza kuuvumilia, hata jaji Mpoki pia alikuwa akijifuta machozi kwa sababu ya kulia, maaskari pia walishindwa kuvumilia na kujikuta wakitokwa na machozi.
“Nimesikitishwa sana na historia aliyoitoa na sina la kufanya zaidi ya …………….!” Jaji Raphael Mpoki alijikuta akishindwa kuvumilia na kuangua kilio mbele ya watu wengi waliokuwa mahakamani, watoto wa Anne na mama yao mdogo pia waliendelea kulia machozi, mahakama nzima ilijaa vilio na maaskari walijaribu kunyamazisha mahakama bila mafanikio.
Je nini kitaendelea?
Je Anne atahukumiwa kifungo cha gerezani au atanyongwa?
Je nini kilitokea katika maisha ya mwanamke huyu?
Kuna mambo mengi ya kusisimua, tukutane baadae saa 7 kamili usiku