Tafadhali CAG usijiuzulu

Ni kweli. Ila soma hii
The 10 Worst Accounting Scandals of All Time

Kuna wkt auditors wanakuwa intimadated kuficha ukweli ila baada ya miaka ukweli unakuja hadharani
 
Ukweli mtupu...
 
Mimi namfahamu huyu CAG, ni credible sana. Angalau kwa yeye kuwepo pale tutakuwa tunajua upigaji unaofanywa na Rais/Serikali kuu. Kwa wasiojua hili la CAG linampasua kichwa jiwe. Anatamani aweke mtu wake pale.

Sote tumsihi tafadhali CAG usijiuzulu na jiwe hawezi kukuondoa kwani hana mamlaka labda aku pyu pyu...
 
Yaan tatizo la Tanzania ni moja tu kwamba CCM ni wengi mnooo... Na wengi wao hawajui kuchambua au kupembua mambo... Iwe kwa makusudi au isiwe kwa makusud....

Kwa maana hiyo.. Hakuna au kuna wazelendo wachache sana ndani ya CCM
Na CCM wamejipa kazi ya kusambaza ulaghai... Ukweli una kazi sana kupenya katikati ya MaCCM
 
Sikh hizi kila hafla anaita wakuu wa vyombo vya usalama, ili kutisha watu, kulikuwa na ulazima gani CAG kuwepo pale??

kulikuwa na ulazima gani kuongelea mambo yanashugulukiwa na bungeni
Yeye anajiona yupo sahihi..
 
Mungu atatuvusha. Haya majizi ipo siku yao
 
Kwann ajiuzulu huu ni wakati wa mpito acha mambo yajiendee.Ukitaka kuishi na chongo ziba moja,ukishafika mbele unaliachia kama kawa.
 
Mi ninachoona CAG kasimamamia msimamo wake ule ule asingeweza kupinga andishi lake.
Kwenye ripoti CAG amesema 1.5t hazijulikani ziliko na ndo wazalendo wanahoji ziko wapi.
Hakuna kwenye ripoti CAG aliposema zimeibiwa sijasikia. Hata alipoulizwa na Azam Tv alijibu hivi hivi kua hela hazijaibiwa ila 1.5t hazionekani ziliko hadi akasema bunge lihoji hizo 1.5 t zimetumika wapi. Sasa Raisi kauliza swali kua eti CAG kuna hela zimeibiwa? Na kwa sababu CAG kwenye ripoti hakuna aliposema zimeibiwa ndo mana akajibu hapana mheshimiwa.
Na Mimi kwa uelewa wangu kama CAG angejibu ndio ningekua na mashaka na CAG na kusema ni muongo.
Sasa watanzania tujiulize kwa nini Raisi aliigeuza hoja ya CAG kua hela hazijulikani matumizi yake na hazionekani zilipo na kusema eti CAG kuna hela zimeibiwa? Kwa nini asingemuuliza CAG kua eti CAG kuna hela hazionekani zilipo na wala matumizi yake hayapo?
Nilichoelewa ni kwamba upande wa serikali wanajua kabsa kua CAG amesema 1.5t hazijulikani zilipo na hajasema zimeibiwa ila kinachofanyika ni kuugeuza ukweli wa hoja ya CAG.
Alichofanya Raisi ni kumuingiza kwenye mtego CAG na kwa vile CAG alielewa mchezo ndo mana alijibu vile kua hamna zilizoimbiwa. Namini Kama CAG angejibu ndio angegeuziwa kibao kua CAG ni muongo kwenye maandishi kasema hazionekani zilipo afu uku anajibu zimeibiwa.
Kwa sababu evidence za hoja ya kuibiwa ni tofauti na evidence ya hoja ya kutoonekana.
Asante CAG kwa kukwepa mtego wa Raisi.
Hata sisi watanzania hatusemi mmeiba ila tunahoji hizo 1.5t zetu mmezipeleka wapi.kama mmetumia tuambieni mmetumia kwenye nini?
 
Lumumba sipajui. Anyway hata kama kateuliwa na mtangulizi wake kwa hiyo anawajibika kwa nani sasa. Aende kwa mkwere basi. Zero digits kabisa mkuu
Bado unajitekenya masabuli na kucheka empty set
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…