Table manners


Adabu za kuanza kula chakula kwa Muislam ni:-
1. Kunawa mikono yako yote miwili kabla ya kuanza kula.
2. Kumtaja Mwenyezi Mungu kwa kusema ‘BismiLlaah’ (Jina la Allaah Subhanau Wa taala).
3. Kula kwa mkono wa kulia na kula kilicho mbele ya sahani upande wako kama mnakula kwa pamoja.
4. Inapendekezwa kukaa chini ( kwenye mkeka/ jamvi) ukiwa umekunja miguu.
5. Kuacha kuongea / mazungumzo wakati wa mlo.
6. Kumshukuru Mwenyezi Mungu baada ya kula na utamshukuru mwenyeji wako/ aliyeandaa chakula na kumwombea dua.

Nimewalilisha. Ahsanteni
 
sijawai alikwa lunch au dinner kwa mtu maishani
sijui ni huu usenior bachelor?
napelekwa tu kwenye michemsho,viti moto haramu nk
 
kile kitambaa cha kama mtoto anaetoa udenda kile mimi siwezi kujifunga kamwe
bora waninyime msosi wao
 
Hii ni kwa akina mboga saba. huku kwetu ni mwendo wa mduara, sinia la ugali/wali kati na vibakuli vya mboga, ukishanawa mikono (tena mara nyingi mkono wa kulia tu) unakula, ukishiba unanawa mkono unasepa. Kushukuru pia ni majaliwa.
 
hizo wine zatia hamu .. okey na wale wanao ongea na chakula mdomoni halafu unaona mchakula wake jamani jamani uwiiiii uwii... halafu tatizo hilo wanalo masista du wale wanaojifanya kila mada anajua .. basi sawa kujua si kosa meza kwanza ndiyo uongeee ..
 
Kuna siku nlikua mahali, nlikua na njaa nikapewa kuku (kidali) ilibidi nimle kwa mkono watu wakipita najifanya nimeshika umma na kisu, wakiondoka naendeleza kwa mkono
Hahaha umenifurahisha sana mm pia napenda kumla kuku kwa mkono
Cku moja nlkuwa mahala akaja dada mmja na jamaa akaagiza wali samaki alikuwa anapata shida kumla samaki hadi huruma,nkajisemea c amle kwa mkono tu?
 
Nyama zote zinabaki kweny mfupa.

Halafu hivi ni haki kweli kula wali kwa uma???? Unautani wa kichina kula wali kwa vijiti eeeh???
Wali kwa umma tena?..Hizo mbwembwe za kichina siziwezi..Hata kisu na uma natumia pale inapobidi kulingana na mazingira niliyopo
 
Kila jamii itabaki kuwa na tamaduni zake but kikubwa ni kutafuna na kumeza tu, zingine mbwembwe tu.
 
Looks delicious!, calories zake sasa..
Sure ni Delicious... Wajua beef iliyokatwa katwa kidogo kwenye Burger au pizza always huwa bomba sana... kuliko iliyosagwa.

Hii kitu ukiletewa lazima uombe Sahani na Uma midomo size hiyo hatuna... labda yule comedian Kazoa wa jambo na vijambo
 
Reactions: kui
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…